David Kafulila ahutubia Dunia kupitia Africa Energy Summit M300

David Kafulila ahutubia Dunia kupitia Africa Energy Summit M300

Ki-inglishi bwana asikwambie kuwa Fluent 100%, cha kuongea, kwa sisi wengi ni ngumu hata kama ni PhDs: swangish inatuharibia: huwa najiona kama niko vema, siku moja nilikuwa mazingira fulani na watu fulani tukiongea kwa lugha hii ya malkia, loh ndani ya Lisaa limoja misamiati ikakata, taya zikaanza kuuma! Jasho jingi! Matumizi ya viungo na mwili vikaongezeka: kusikiliza zaidi kukaongezeka: aaah we Acha kabisa, pamoja na kufahamu lugha hii, ila ukitaka kuwa Fluent vema kujitengenezea mazingira ya kuongea ongea kila wakati na kusoma kwa sauti na kimya kimya, hasa Novels! Wataalam wa lugha ongezeni tufanyeje
 
View attachment 3217060
View attachment 3217061

Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Ubia kati ya Sekta ya Umma na Sekta binafsi (PPPC), David Kafulila, amesema tangu serikali ya Tanzania ifanye marekesho ya sheria na miongozo yake mbalimbali sasa kiwango cha wawekezaji kuja kuwekeza nchini Tanzania kimeongezeka.

Kafulila ameyasema hayo wakati akihitimisha siku ya kwanza ya Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika unaohusu Nishati unaofanyika kwa siku mbili nchi Tanzania kuanzia Januari 27 na 28, 2025 katika kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Mwl Julius Nyerere (JNICC) jijini Dar es Salaam.

Aidha Kafulila ameongeza kuwa, serikali ya Tanzania itaendelea kufanya marekebisho ya sheria na miongozo ambayo bado inaleta changamoto kwa wawekezaji na hatimaye kutimiza ajenda M300 ya kuwafikishia nishati ya umeme waafrika milioni 300 ifikapo mwaka 2030.

Mhe Kafulila amesema ni lazima sekta binafsi Africa yote zihusishwe katika mchakato huo kwa sababu ndio wadau wakubwa wa maendeleo ulimwenguni kote.

Ameongeza kuwa ajenda hiyo haipaswi kuwa ya mipango pekee bali iwe ya kiutendaji zaidi na hatimaye iweze kuleta manufaa barani Afrika kwa waafrica.

Ukiacha Mhe Rais Dkt Samia Suluhu Hassan aliyekuwa mgeni rasmi kuhutubia mkutano huo wa M300 wengine ni Naibu Waziri Mkuu Mhe Dkt Dotto Biteko, Waziri wa Fedha Mhe Dkt Mwigulu Nchemba na Mhe David Kafulila Mkurugenzi wa kituo cha Ubia nchini PPPC.
Kiingereza cha Iringa hicho. …wi nidi praiveti patinashipu…
 
Kwani kwenye hiyo hotuba si anaisoma?

Utasemaje ni fluent kwenye kuongea ili hali sote tunaona hapo anasoma

Nilichojifunza Kafulila tangu apewe hicho kitengo, amejua kujiongeza Kwa kuweka machawa hapa JF wakikesha kumuandikia threads humu na kumpamba

Kuna wengine wanafika mbali hadi kumuona a President to be

Sawa mpambeni tu, lakini mkumbuke huko CCM yeye ni kama ng'ombe aliyekatwa mkia

Bado wajumbe wanamwona wa kuja

Ndiyo maana hata alipoacha URAS na kwenda kugombea Ubunge kule kwao, wajumbe walimnyima Kura
 
Ki-inglishi bwana asikwambie kuwa Fluent 100%, cha kuongea, kwa sisi wengi ni ngumu hata kama ni PhDs: swangish inatuharibia: huwa najiona kama niko vema, siku moja nilikuwa mazingira fulani na watu fulani tukiongea kwa lugha hii ya malkia, loh ndani ya Lisaa limoja misamiati ikakata, taya zikaanza kuuma! Jasho jingi! Matumizi ya viungo na mwili vikaongezeka: kusikiliza zaidi kukaongezeka: aaah we Acha kabisa, pamoja na kufahamu lugha hii, ila ukitaka kuwa Fluent vema kujitengenezea mazingira ya kuongea ongea kila wakati na kusoma kwa sauti na kimya kimya, hasa Novels! Wataalam wa lugha ongezeni tufanyeje
Daaah pole sana 🤣🤣
 
Nimejaribu kumlinganisha na Mkapa, kuna kitu nilitaka kusema, sijui ni masikio yangu 🙉


View: https://youtu.be/XN19XsgU9Es?feature=shared

A VERY INTELLIGENT AND SIGNIFICANT SPEECH ON ASSORTED SOCIETAL ISSUES BY LATE MZEE MKAPA

Hiyo khotoba ina mengi ambayo yanaakili, mantiki na ufasaha wa muktadha wa uono na uchambuzi wake.

Labda mbali kuzidi wazungumzaji wengi--wazungumzaji katika majukwaa ya aina zile za makutano ya mafungamano ya (1) Washirika wa Maendeleo na (2) Wanajamii wanaobadilishana mashauri juu ya kadhia zao za 'Kimaendeleo ya Vitu/Upungufu wa Pesa za Kuendesha Miradi/Uhitaji'.

Dakika ya kumi (dk 10 - dk 15) ya hiyo media, video, mzee Mkapa anazungumza jambo lenyewe khasa kuhusiana na dhamira na azma ya 'Maendeleo Endelevu' na mikingamano ijayo na urazini wenye kukosa fasaha ya ukweli khasa wa mambo; mambo ya uono wa juu juu wa mambo na kutengenezea mashauri mushkeli juu ya jitihada, mifumo na utendaji...

Mzee Mkapa, anatumia Uono na Ufikirifu Mifumo katika mashauri yake na uandishi wake wa Khotuba... Ni nadra sana kwa viongozi wengi katika jamii yetu kuwa mahiri katika Uono na Ufikififu mifumo; huu huja na uzoefu na busara binafsi ya mtu katika ku-JUA mambo ilivyobora. Hii ndiyo inafanya Mzee Mkapa anaonekana ni mbora katika khotuba zake kwa kuwa 'Zina Akili Khasa'--namna ya hizo kuweza kuwa na 'Mbegu za u-JUA-ji' na siyo tu 'hoja shindanishi' ama vipi...

Kwa hivyo Mzee Mkapa, siku alipozungumza kwenye huo mualiko katika shule ya Siasa ya John F Kennedy, Septemba 15, 1999, alitoa khotuba iliyotayarishwa vizuri kwa mapana na marefu ya mbegu za u-JUA-ji na tena kwa mashauri yanayowasilishwa kwa haiba ya Uono na Ufikirifu Mifumo....

Kwa hivyo, yeye katika dakika ya kumi, kuzungumza kuhusu Azimio la Copenhagen, Copenhagen Social Development Summit, kama kitovu cha 'Shauri Uono' kulandanishia 'Uono Mifumo' na basi kukazia Udhamirifu unaokwenda juu wa Upeo na Hadhi wa nia/matendo jamii ulio na misingi ya Ukuu Kiroho, Maadili na Miiko... Halafu anachukua muktadha mushkeli wa tafsiri za mambo, "stereotyping"--mambo ya kubatizana majina na kasumba, kukontrasti mashauri yenye kuzingatia 'Utata' wa uono bora kwa mambo yanayopimika na mambo yasiyopimika kwa vigezo vya 'fedha za misaada'...

Mkutano wa Nishati Afrika M300, kiuono na ufikirifu mifumo, mashauri yake mengi yaliyoibuka yamekuwa ni yenye kutabirika kwa mtu yeyote mwenye uono na ufikirifu mifumo. Majukwaa haya, kiufundi, ni utundu wa kujenga ushawishi kwa muelekeo fulani wa mambo unaoweza kuwa umeshapangwa waziwazi ama isivyo waziwazi. Hili ndilo linaweza kutoa viashirifu vya tathmini ya viongozi/uongozi na watendaji/utendaji wanaojifahamu ama wanaoicheza Sikinde ngoma ya Ukae...

Hmmm​
 
Wana vibao wanasoma kama hujui ,kuhutubia ni kipaji kama yule pastor Tonny ana kipaji... Viongozi wengi hawana hicho kipaji ila sio kesi.

Wazungu Wana vibao wanasoma hata umuone anaangalia mbele.
Zinaitwa "TELEPROMPTER". Ukimuona mtu ni kama anautubia au hotuba yake anaitoa kutoka kichwani kumbe mwenzenu anasoma
 
Huwezi kusema "we need government" bali sahihi ni "we need the government".
Amesema " We need governments" ndio maana ninamsifu Kafulila kwa content na lugha iliyonyooka,

Huwezi kusema " We need the governments"🤣🤣


Phrase "the" inatumiwa kwenye majina ambayo yanajulikana,

Mfano "the government of Tanzania,"


Lakini ukiwa unamzungumzia nchi mbalimbali yaani "governments" lazima uondoe Phrase "the"

Ndio maana Kafulila akasema,

"We need governments "huwezi kusema We need the governments hii ni kosa
 
Amesema " We need governments" ndio maana ninamsifu Kafulila kwa content na lugha iliyonyooka,

Huwezi kusema " We need the governments"🤣🤣


Phrase "the" inatumiwa kwenye majina ambayo yanajulikana,

Mfano "the government of Tanzania,"


Lakini ukiwa unamzungumzia nchi mbalimbali yaani "governments" lazima uondoe Phrase "the"

Ndio maana Kafulila akasema,

"We need governments "huwezi kusema We need the governments hii ni kosa
Hajasema governments wewe acha unazi hewa. Sikiliza vizuri clip yako ya kwanza. Anasema "we nee government (sio governments) to align with private sector"

Hakuna kiingereza anachojua amekariri tu.
 
Kiingereza chake kibovu
Align align kibao ameshindwa kutengeneza sentence au paragraph iliyonyooka yenye align moja tu na subtitles zinazohusu align bila kurudia rudia align

Kingereza zero
Hujawahi kumsifu Kafulila kwa lolote,
aligh zinaonesha msisitizo wa jambo acha wivu wa kishamba, Kafulila sio levels zako hata hivyo
Kwani kwenye hiyo hotuba si anaisoma?

Utasemaje ni fluent kwenye kuongea ili hali sote tunaona hapo anasoma

Nilichojifunza Kafulila tangu apewe hicho kitengo, amejua kujiongeza Kwa kuweka machawa hapa JF wakikesha kumuandikia threads humu na kumpamba

Kuna wengine wanafika mbali hadi kumuona a President to be

Sawa mpambeni tu, lakini mkumbuke huko CCM yeye ni kama ng'ombe aliyekatwa mkia

Bado wajumbe wanamwona wa kuja

Ndiyo maana hata alipoacha URAS na kwenda kugombea Ubunge kule kwao, wajumbe walimnyima Kura
Kafulila kapambwa wapi hapo kwanini hamtaki tuseme mazuri ya watu wakiwa hai?
 
Mimi sijasema nataka kusiki s wala x au z. Nimekuambia unaemsifia kuwa anajua kiingereza hajua amekariri tu.

Ila nimegundua kuwa hata wewe hujui kiingereza ndio maana unaona yupo sahihi wakati amekosea.
Mimi sijui ndio maana nimekusahihisha kuwa huwe kusema

"We need the governments "

Ila usahihi ni,

"We need governments" kama alivyosema Kafulila
 
Back
Top Bottom