David Kafulila anakumbukwa na wakulima wa Simiyu kwa kupaisha bei ya Pamba kufikia Tsh. 2200 kwa kilo katika historia ya Taifa letu alipokuwa RC

David Kafulila anakumbukwa na wakulima wa Simiyu kwa kupaisha bei ya Pamba kufikia Tsh. 2200 kwa kilo katika historia ya Taifa letu alipokuwa RC

Fuatilia kilichokuwa kinaendelea kabla, wakati na baada ya kutumbuliwa kwa Kafulila.
Kafulila alitumbuliwa na kutolewa kuwa RC wa Simayu, akawekwa benchi, akasugua makalio, akaanza uchawa mitandaoni, akakumbukwa na kupewa cheo cha mchongo kwenye uwekezaji. Ni kacheo fulani hivi ka ovyo, sasa jamaa naona hajaridhika nako maana hakampi upigaji wa kingedere, ndio maana kaswaga machawa kibao hapa JF wakumpa promo ili kuboost uteuzi mwingine.
Kwanini unadhalilisha watu wewe,

Kusugua makalio ndio nini?

Kama mliweza kumfanyia fitna mtu aliyeleta neema kwa wakulima kisa maslahi yenu basi shame on you.

Najua Mama hatakuja kurudia kosa kama hilo kwa Kafulila.

Najua Mama anasoma sana humu Jf namtahadharisha kuna baadhi ya watu kazi kwao ni uongo na fitina tu Wala hakuna kazi wanafanya.

Mtu kama Kafulila anasaidia hata Rais atawale kwa raha kwani ni mtu anajua kuzikabili hoja zote toka ndani na nje ya Serikali,

Lakini pia ni mtu ukimpatia elfu 5 itafika kwenye mradi elfu 5 kama ilivyo.

Vijana tuache kufitiniana sio sawa na Mungu hakubaliani na mtu Mwongo na Mchawi.
 
Soma hii itakusaidia,
👇👇👇

Kafulila alianzisha kitu kinaitwa "Simiyu model" .

Nia ya hii Model ni kutaka Ushirika kushindana na watu binafsi katika ununuzi wa Pamba.

Lakini pia Kafulila alianzisha kamati za pamba kudhibiti Kila hujuma ya walanguzi wa Pamba.

Matokeo ndio hayo bei ikafika mpaka 2200 wakati miaka yote bei ya pamba haijawahi kuzidi 1,200 kwa mkulima.

Ndio Wapo watu kama wewe mnaoweza kusema sababu ni kupanda kwa bei ya pamba katika soko la dunia dine,

Ukweli ni kwamba haukuwa mwaka wa kwanza bei kupanda katika soko la dunia na bado bei haikuzidi 1200/.

Mfano wa miaka ambayo Pamba ilipanda sana katika Soko la dunia ni Mwaka 2011, 2012, 2018 katika miaka hii bei ya pamba katika soko la dunia ilipanda na bado mkulima hakupata zaidi ya 1200/=.

Sasa huyu Kafulila alidhibiti chain ya wapigaji eneo la pamba ndani ya Mkoa mpaka kwenye mfumo wa wanunuzi.

Mimi naombeni watu waje wafanye utafiti alichofanya Kafulila na kilichotokea kwenye bei ya pamba ili kitumike kama mwongozo wa Serikali Kwa manufaa ya Sasa na kizazi kijacho.

Ukiongea na wazee wa pamba hapa Simiyu au mchambuzi wa miaka kama Mzee Joseph Mihangwa watakwambia yule kijana alikata mtandao wote wanaokula jasho la mkulima wa pamba.

Tunaweza kuzungumza mengi lakini Kafulila bado ni mtu mwenye uthubutu na ujasiri mkubwa wa kiuongozi.
Napenda sana mtu anayetumia hoja kama wewe ili kujifunza wote. Sasa naomba unisaidie kidogo kile umesema nisome japo ni maelezo yako.
Je Kafulila alianzisha Ushirika au alianzisha mfumo wa Ushirika kushindana na Kampuni binafsi? Kwamba Ushirika ununue na watu binafsi wanunue?
U.esema kamati ya kuthibiti walanguzi. Je kipi ni kipi mfumo wa watu binafsi kununua kama aliuruhusu unautofautishaje na ulanguzi?
Yeye na Mtaka nani alianzisha nini? Kwa Simiyu kama hupajui Mtaka ndio mkuu wa Mkoa alikubalika, bado hajapatikana mwingine.
Ova. Noya du. Iyingi bulongo guke
 
Kwanini unadhalilisha watu wewe,

Kusugua makalio ndio nini?

Kama mliweza kumfanyia fitna mtu aliyeleta neema kwa wakulima kisa maslahi yenu basi shame on you.

Najua Mama hatakuja kurudia kosa kama hilo kwa Kafulila.

Najua Mama anasoma sana humu Jf namtahadharisha kuna baadhi ya watu kazi kwao ni uongo na fitina tu Wala hakuna kazi wanafanya.

Mtu kama Kafulila anasaidia hata Rais atawale kwa raha kwani ni mtu anajua kuzikabili hoja zote toka ndani na nje ya Serikali,

Lakini pia ni mtu ukimpatia elfu 5 itafika kwenye mradi elfu 5 kama ilivyo.

Vijana tuache kufitiniana sio sawa na Mungu hakubaliani na mtu Mwongo na Mchawi.
Asante sana mkuu kwa ujio wako humu,
Hawa vijana wa Mtaka naona ni kama wabifu
Kafulila kitu pekee kitambeba kwenye maisha yake ni Zero corruption status.
 
Acha uzushi.
Mama akimzawadia Kafulila uRC wa Simiyu kwenda kuendelea kuwaunganisha wakulima wa Pamba kazi ambayo Mtaka alikuwa amekwisha kuifanya kwa 100%. Kilikuwa ni kipimo cha kwanza kabla ya kuja kumhamishia mkoa mkubwa kama Arusha nk. Lakini Kafulila akafeli kwa 100% akaishia kutumbuliwa usiku usiku.

Kafulila aliharibu mnooo kule Simiyu, akawagawa wananchi na kumkosanisha mama Samia na wanachi wa Simiyu, leo Samia anatukanwa ovyo na wanaSimiyu kwa kumuondoa Mtaka na kuleta kile Kibuyu cha kiha kutoka Kigoma.
Kila kitu Mtaka Mtaka Mtaka, 🤣🤣

Sasa kama MNEC alikuwa anamiliki Soko la madini na Sheria ziko wazi Soko la madini lazima iwe mali ya Serikali Mtaka alikuwa wapi?

Kama wachina wa CHICCO walikuwa wamebumba barabara zaidi ya KM20 MWIGUMBI -MASWA ndio Kafulila kuwaambia warudie kwa gharama zao na wakafanya hivo kwa zaidi ya 40bl huyu Mtaka alikuwa wapi?

Wakati wakulima hao masikini wanalanguliwa Pamba yao na kuiza kwa TSH 800 au 1000 huyu Mtaka wako alikuwa wapi?

Nimesoma ulichoandika nikacheka sana aisee.🤣🤣🤣

Nikusahihishe tu ndg yangu wanamchukia Kafulila sio masikini na wanyonge ila ni hawa wamiliki wa Masoko ya madini na wazee wa 10% kwa Wachina pamoja na wachuuzi wa Pamba hawa ni kweli wanamchukia sana nakubaliana na wewe 100%✓
 
Napenda sana mtu anayetumia hoja kama wewe ili kujifunza wote. Sasa naomba unisaidie kidogo kile umesema nisome japo ni maelezo yako.
Je Kafulila alianzisha Ushirika au alianzisha mfumo wa Ushirika kushindana na Kampuni binafsi? Kwamba Ushirika ununue na watu binafsi wanunue?
U.esema kamati ya kuthibiti walanguzi. Je kipi ni kipi mfumo wa watu binafsi kununua kama aliuruhusu unautofautishaje na ulanguzi?
Yeye na Mtaka nani alianzisha nini? Kwa Simiyu kama hupajui Mtaka ndio mkuu wa Mkoa alikubalika, bado hajapatikana mwingine.
Ova. Noya du. Iyingi bulongo guke
Huku juu umeanza vizuri sana ila chini umeharibu Kila kitu kuanza kumtaja taja huyo mtakatifu.

Binafsi nahisi shida kubwa ya Simiyu ni huyo huyo Mtakatifu.

So endelea ku-enjoy Jf

 
Fuatilia kilichokuwa kinaendelea kabla, wakati na baada ya kutumbuliwa kwa Kafulila.
Kafulila alitumbuliwa na kutolewa kuwa RC wa Simayu, akawekwa benchi, akasugua makalio, akaanza uchawa mitandaoni, akakumbukwa na kupewa cheo cha mchongo kwenye uwekezaji. Ni kacheo fulani hivi ka ovyo, sasa jamaa naona hajaridhika nako maana hakampi upigaji wa kingedere, ndio maana kaswaga machawa kibao hapa JF wakumpa promo ili kuboost uteuzi mwingine.
Kinachokusumbua wewe ni wivu na chuki binafsi tu. Kwanza ungekuwa na akili sawasawa ungejiuliza wapo watanzania wangapi ambao wangeweza kuteuliwa na Mheshimiwa Rais?kwanini hawakufikiriwa hao na badala yake akapewa heshima hiyo ya kuwa mkurugenzi wa PPP? Kwanini hukuteuliwa hata wewe tu au mimi na badala yake akapewa heshima hiyo Mhessimiwa Kafulila? Kufikiriwa tu na Mheshimiwa Rais na kupewa nafasi ni heshima kubwa sana.

Mimi nitaendelea kumuunga mkono Mheshimiwa Rais kwa sababu ni kiongozi na mtu safi, mzalendo,mchapa kazi na mbunifu kazini. Ni kiongozi asiyeyumba kiuongozi.
 
Kila kitu Mtaka Mtaka Mtaka, 🤣🤣

Sasa kama MNEC alikuwa anamiliki Soko la madini na Sheria ziko wazi Soko la madini lazima iwe mali ya Serikali Mtaka alikuwa wapi?

Kama wachina wa CHICCO walikuwa wamebumba barabara zaidi ya KM20 MWIGUMBI -MASWA ndio Kafulila kuwaambia warudie kwa gharama zao na wakafanya hivo kwa zaidi ya 40bl huyu Mtaka alikuwa wapi?

Wakati wakulima hao masikini wanalanguliwa Pamba yao na kuiza kwa TSH 800 au 1000 huyu Mtaka wako alikuwa wapi?

Nimesoma ulichoandika nikacheka sana aisee.🤣🤣🤣

Nikusahihishe tu ndg yangu wanamchukia Kafulila sio masikini na wanyonge ila ni hawa wamiliki wa Masoko ya madini na wazee wa 10% kwa Wachina pamoja na wachuuzi wa Pamba hawa ni kweli wanamchukia sana nakubaliana na wewe 100%✓
Kwa hoja hizi nzito ulizomjibu huyo asiye elewa kitu chochote kile na mwenye wivu na chuki binafsi na Mheshimiwa Kafulila ,itakuwa huko aliko anatafuta panadol ili anywe kupunguza maumivu ya kichwa na kuishiwa nguvu.
 
Huku juu umeanza vizuri sana ila chini umeharibu Kila kitu kuanza kumtaja taja huyo mtakatifu.

Binafsi nahisi shida kubwa ya Simiyu ni huyo huyo Mtakatifu.

So endelea ku-enjoy Jf

Wana Simiyu wanaelewa vyema sana kuwa Mhessimiwa Kafulila ni jembe na chuma kilichowainua na kuwapatia bei kubwa sana katika Historia ya Nchi yetu
 
Nakumbuka tangazo lilipotolewa kuwa Kafulila sio Mkuu wa Mkoa wa Simiyu tena,

Kulikuwa na mnada pale Sakasaka watu walipiga mwano utafikili wamefiwa kisa Kafulila.
Simiyu madalali wa Pamba wanamchukia sana Kafulila aliwatia hasara wakanunua Pamba kwa 2200 badala 1000 au mia nae.
Ila nasikia hahongeki huyu muha ndio maana anapigwaga vita sana sio mtu ya dili.
Mheshimiwa Kafulila ni mzalendo wa kweli kwa Taifa letu.aligona kupokea ma Million kwa mamillioni ili aachane na sakata la Escrow ,Lakini kwa uzalendo wake aligoma kabisa kupokea na kukubali pesa chafu na badala yake akaongeza moto zaidi kwamafisadi na wala rushwa wote.
 
Kwa hoja hizi nzito ulizomjibu huyo asiye elewa kitu chochote kile na mwenye wivu na chuki binafsi na Mheshimiwa Kafulila ,itakuwa huko aliko anatafuta panadol ili anywe kupunguza maumivu ya kichwa na kuishiwa nguvu.
Jamaa anatumika vibaya na huyo Mtakatifu ambae bila huruma anatesa Wanawake wasio na hatia.

Hajui Kama nyota ya mtu inang'aa inang'aa tu.
 
Naona machawa mnapongezana.
Bora hata ile misukule ya Lumumba iliyokuwa inalipwa buku mbili na bundle kuja kupost upupu, kuliko hii michawa ya sasa.
Poor CCM.
Kama umeumia basi wewe kunywa hata sumu tu ndugu yangu ili UFE tu maana huna faida zaidi ya wivu na chuki.
 
Bei ya pamba haipangwi na Mkuu wa Mkoa wewe chawa mchafu
Uko sahihi

Simiyu akiwa mkuu wa mkoa Kafulila aliumiza sana watu huyo Kafulila alizuia magari ya abiria Kwa jina maarafu michomoko yasifanye hiyo biashara siji msahau Usafiri ulikuwa taabu hatari

Baada ya malalamiko ya wananchi na wauzaji vituo vya mafuta kuwa biashara zao zinadoda Raisi akamwondoa ukuu wa mkoa Simiyu haraka haikuchukua hata muda

Mpuuzi huyo alileta mateso sana Kwa wananchi wa Simiyu
 
Jamaa anatumika vibaya na huyo Mtakatifu ambae bila huruma anatesa Wanawake wasio na hatia.

Hajui Kama nyota ya mtu inang'aa inang'aa tu.
Ni ngumu sana kuizima au kuifikisha nyota ya Mheshimiwa Kafulila katika mioyo na akili za watanzania,kwa sababu wanakumbuka na kuziona alama alizoziacha na kazi kubwa aliyoifanya katika taifa letu.
 
Uko sahihi

Simiyu akiwa mkuu wa mkoa Kafulila aliumiza sana watu huyo Kafulila alizuia magari ya abiria Kwa jina maarafu michomoko yasifanye hiyo biashara siji msahau Usafiri ulikuwa taabu hatari

Baada ya malalamiko ya wananchi na wauzaji vituo vya mafuta kuwa biashara zao zinadoda Raisi akamwondoa ukuu wa mkoa Simiyu haraka haikuchukua hata muda

Mpuuzi huyo alileta mateso sana Kwa wananchi wa Simiyu
Wewe ni liongo sana na mzushi sana.
 
Ndugu zangu Watanzania,

Uongozi ni kuacha alama zinazoishi katika Maisha na mioyo ya watu, ni kuacha kitu kitakacho simuliwa vizazi kwa vizazi,ni kuacha rekodi ambayo itaimbwa na kuzungumzwa na watu kwa miaka mingi hata kama wewe utakuwa haupo uongozini au Duniani lakini utaendelea kuishi na watu japo hupo Duniani au madarakani.

Uongozi siyo habari ya umeongoza miaka mingapi au umekaa miaka mingapi. kinachomfanya mtu akakumbukwa na watu ni kazi alizozifanya kwa muda alipokuwa na madaraka au hai na faida ya uhai wake kwa watu na uongozi wake ulivyogusa maisha ya watu.

Ndio maana leo hii viongozi na watu kama John F Kennedy, Dr Martin Luther King Junior, BoB Marely, Abraham Lincolin wanaendelea kukumbukwa na watu wengi sana Duniani kwote licha ya kwamba walikufa miaka mingi na waliishi miaka michache Duniani kabla ya kufikia uzee wao. Ndio maana pia viongozi kama Edward Moringe Sokoine wanakumbukwa na Taifa letu japo walikaa madarakani kwa Muda mfupi lakini historia zao na majina yao yameganda na kunasa katika mioyo ya watanzania kutokana na mikono yao na kazi zao kugusa maisha ya watu na kuleta matokeo Chanya.

Hii maana yake nini? Unaweza kuongoza kwa miaka mingi, kukaa madarakani au kwenye cheo fulani kwa miaka mingi na bado usikumbukwe na yeyote yule pale ambapo utaondoka leo. Unaweza kuondoka leo kwenye ukuu wa mkoa au uwaziri au uwaziri mkuu au uspika au ukurugenzi wa taasisi fulani halafu kesho watu wakasahau kabisa kama ulikuwepo kwenye nafasi fulani. Kwanini? Kwa sababu uongozi wako na uwepo wako kwenye kiti haukugusa wala kubadilisha maisha ya watu au mtu yeyote yule, kwa hiyo ulikuwa kama mvuke au moshi tu ambao umekuja na kupita.

Mheshimiwa David Kafulila licha ya kukaa katika nafasi ya Ukuu wa mkoa Wa Simiyu kwa muda mfupi lakini bado anaendelea kukumbukwa na wana Simiyu kama mkuu wa mkoa aliyeleta tabasamu, furaha, matumaini na kuwainua kiuchumi kwa kupaisha Bei ya pamba yao ambayo kwa karibu 70% ya pamba yote Tanzania inatokea Simiyu kufikia bei ya 2200 kwa kilo, bei ambayo haikuwa kutokea tangia Nchi yetu ipate uhuru. Leo anakumbukwa na kusemwa kuwa hapa Simiyu kilipita na kulipita CHUMA David Kafulila aliyeleta Nuru kwa wakulima na maendeleo kwa kaya za wanasimiyu.

Jiulize wewe kiongozi uliyepo kwenye cheo fulani au wadhifa fulani ukiondoka leo kwenye nafasi uliyopo watu watakukumbuka kwa lipi? Umegusa maisha ya watu wangapi? Umeleta tabasamu kwa kaya ngapi? Wangapi wamepata nuru kutoka gizani? Wangapi wamepata matumaini kupitia mikono yako? Wangapi wanatamani urejee au urudishwe au uongezewe muda au kukuombea dua na maombi mema ya kurejea au kupata cheo kikubwa au nafasi fulani? Utakumbukwa kwa lipi ndugu yangu? Au unaisha na kufanya kazi ilimradi tu watoto wako wapate ugali mezani? Umebadilisha maisha ya wangapi?

Wangapi wanaona uwepo wako hapo ulipo ni baraka na mlango wa wao kutokea kimaisha na kuinuka kiuchumi? Wangapi wanakukumbuka kwa mema?

Gusa maisha ya watu, Leta tabasamu kwa watu,washa taa kwenye mioyo ya watu,inua watu,shika mikono ya watu uwainue juu,wape matumaini watu ili siku moja Ukumbukwe kama ilivyo kwa Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere,Nelson Mandela,kwame Nkrumah, Keneth Kaunda, Winnie Mandela na wengine wengi sana. Lakini pia ukifanya vyema utaungwa mkono ukiwa bado hai kama ilivyo kwa Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Thread moja bei gani
 
Nenda hata leo kule Simiyu halafu tamka neno Kafulila au mama Samia kama hutatukanwa.

Lakini fika hapo hapo Simiyu halafu tamko Magufuli au Mtaka uone namna utakavyoshangiliwa.

Kwa wana Simiyu, kwa sasa Kafulila ni neno la kulaaniwa.
Mheshimiwa Rais pamoja na Mheshimiwa Kafulila wanakumbukwa sana na wana Simiyu.
 
Thread moja bei gani
Haina bei bali ni uzalendo katika kuwatetea na kuwaunga mkono WAZALENDO,wachapakazi na watu safi aina ya Mheshimiwa David Kafulila Kama ilivyo kwa Mhessimiwa Daktari Samia Suluhu Hasssan.
 
Haina bei bali ni uzalendo katika kuwatetea na kuwaunga mkono WAZALENDO,wachapakazi na watu safi aina ya Mheshimiwa David Kafulila Kama ilivyo kwa Mhessimiwa Daktari Samia Suluhu Hasssan.
Nimeona umetoa single za kafulila za kutosha
 
Back
Top Bottom