Hii ni Kampeni ya kuzidi kumuumiza mtanzania na kuendelea kujipinga wao wenyewe na serikali Yao.
Wakati mama Yao kina Mwashambwa anapiga kelele kuhusu matumizi ya Nishati safi Kwa ajili ya utunzaji wa mazingira na afya za watu wa bara la Africa, Kafulila anakuja kupunguza watumiaji wa umeme ambao ni nishati safi.
Ndio anapunguza kwa kujenga mazingira umeme uonekane ni anasa kwa sababu ukiacha mapendekezo ya January ya Kuomba 1Tri. Kwa ajili ya kuboresha miundo mbinu pamoja na kuwapa tenda wahindi. Sasa Kafulila amekuja kutoa mapendekezo kwa mabepari wengine kuhusu suala la usambazaji. Ccm inajinasibu kwamba imesambaza umeme vijijini kwa asilimia kubwa sana kuliko wakati wowote (availability)
Kinachokuja kutokea ni kuongeza gharama za umeme kwa mlaji Ili kifidia hizo gharama za kiuwekezaji anazoweka mwekezaji. Subsequently umeme unakua tena sio huduma kwa wananchi bali anasa. Angalia kutoka 5000 unit 17 mpaka sasa unit 4 . Kutokana na utitiri wa Kodi na tozo. Tanzania is a fallen states where politicians seeks personal benefits and popularity.