Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Taarifa nilizopata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika ni kwamba, Mwenyekiti wa CHADEMA, FREEMAN MBOWE ametiwa nguvuni na Jeshi la Polisi baada ya jitihada za kukimbia na kujificha kushindikana.

Mbowe amekamatwa maeneo ya Mikocheni ambako alienda kujificha ili asikamatwe na Jeshi la Polisi.

Kwa sasa wapo njiani kuelekea Central ambako atahojiwa kutokana na tuhuma za kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya pamoja na kulisababishia usumbufu na gharama jeshi la polisi.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Mbowe amekamatwa akitolewa kwenye Appartment Moja kwenda nyingine akitumia gari Nyeusi, Tinted yenye namba za usajili T 830 DEW aina ya VX. Wamemkamata akiwa nje ya geti ya Appartment hiyo ambayo ni miongoni mwa majengo ya siri ( Safe House) yanayomilikiwa na CHADEMA


unless my brain is playing me up, nimeona na kusikia kwenye taarifa ya habari saa 2 usiku huu ITV wamesema Mbowe amekutana na mapolisi njiani wakati akielekea mwenyewe kituoni. baadae wakarudi naye nyumbani kumpekua - huyu mleta thread hii ni dhahiri kaanzia story yake ya "kukamatwa Mbowe" walipomaliza kumpekua.

mods tafadhali ondoeni hii distortion ya kwenye hii thread.
 
Polisi wenyewe ndio hawa...
6805908648ced3d1f2a73f205a0f2e33.jpg
mkuu hii ni photoshop
 
Hajaenda mwenyewe, usipotoshe, ukweli tuukubali mengine baadae.
Mkuu, leo chadema wamechanganyikiwa sana. Yaani kukamatwa kwa Mbowe ni kama chama kimedhalilika. Henry Kilewo, Tumaini Makene na John Mrema wamesimamia propaganda ya kuwa Mbowe kajipeleka mwenyewe polisi. Sijui kwa nini hawakutoa mapema taarifa hiyo mpaka Lizaboni alipoumbua kukamatwa kwake. Yamechanganyikiwa
 
unless my brain is playing me up, nimeona na kusikia kwenye taarifa ya habari saa 2 usiku huu ITV wamesema Mbowe amekutana na mapolisi njiani wakati akielekea mwenyewe kituoni. baadae wakarudi naye nyumbani kumpekua - huyu mleta thread hii ni dhahiri kaanzia story yake ya "kukamatwa Mbowe" walipomaliza kumpekua.

mods tafadhali ondoeni hii distortion ya kwenye hii thread.
Hahahahahahahaaaaaa! Chadema kwa kupindua maneno nyie! Ina maana walienda kumpekua hata kabla hajaripoti kituo cha polisi? Ina maana walipokutana naye tu njiani ndo wakamwambia haya twende nyumbani kwako tukakupekue? By the way je Mbowe anaishi Mikocheni?
 
Watasachi nyumba zake zote au.. upuuzi kwenye hii nchi sijui utaisha lini
 
Mbowe huyu aliyeita press conference? Nilisema huwezi kucheza na Serikali, hilo ni somo, wapinzani mna wakati mgumu sana kuelewa maana ya Serikali. Mtanyooka tu, mnafikiri nchi hii ni yenu peke yenu. Tupo Watanzania lukuki ambao tupo nyuma ya uongozi imara wa JPM.
 
Kuna uwezekano mkubwa yaliyomkuta Manji yanaweza kumkuta pia Mbowe, kwa style hii ni vigumu sana kupambana na vita vya madawa ya kulevya.
umepata like yangu kwa mala ya kwanza! Nimekushangaa haushangilii kama wenzio akina Lizaboni and company! At least umekuwa sio shabiki wa Dracula Leo! Umeutoa utu wapi jamaani! Endelea hivyohivyo
 
Back
Top Bottom