Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Dawa za Kulevya: Freeman Mbowe akamatwa na Polisi; ahojiwa na kuachiwa

Taarifa nilizopata kutoka kwenye chanzo changu cha kuaminika ni kwamba, Mwenyekiti wa CHADEMA, FREEMAN MBOWE ametiwa nguvuni na Jeshi la Polisi baada ya jitihada za kukimbia na kujificha kushindikana.

Mbowe amekamatwa maeneo ya Mikocheni ambako alienda kujificha ili asikamatwe na Jeshi la Polisi.

Kwa sasa wapo njiani kuelekea Central ambako atahojiwa kutokana na tuhuma za kujihusisha na biashara ya madawa ya kulevya pamoja na kulisababishia usumbufu na gharama jeshi la polisi.

Taarifa zaidi zinasema kuwa Mbowe amekamatwa akitolewa kwenye Appartment Moja kwenda nyingine akitumia gari Nyeusi, Tinted yenye namba za usajili T 830 DEW aina ya VX. Wamemkamata akiwa nje ya geti ya Appartment hiyo ambayo ni miongoni mwa majengo ya siri ( Safe House) yanayomilikiwa na CHADEMA

=====
UPDATES:

Apekuliwa nyumbani, arejeshwa Central...


Aachiwa:
Safi sana. Hakuna aliye juu ya Sheria. Awamu hii siyo ya kuogopa MTU.
 
Tunasafari ndefu ya kupambana na vita ya madawa ya kulevya.Naomba serekali iache siasa kwenye jambo hili na ijikite kwenye dhamira ya kweli ya kupambana na vita ya ukweli ya madawa ya kulevya.
 
Kila siku tunaambiwa CDM hawana nyumba hivi hii appertment imenunuliwa na CCM?? Ni ajabu na kweli.

Ila Lizabon achene sana kwa sasa,maana atakuja kulia kilio kisicho na mwenyewe.
 
Kwa hiyo hizo nyaraka ndio vielelezo vya madawa ya kulevya? Hii ni aibu ya mwaka kwa watawala hawa waliopo. JK na wastaafu wengine toeni semina elekezi jinsi ya kurun nchi
 
Pole mkuu naona umenena kwa hisia kali sana!kibaba unachowapimia wenzako na wewe utapimiwa hichohicho!
***
kila tendo au chochote ukionacho leo hii kiko katika rotations / hata sisi hupita pia, endapo kilitendwa chema kitakuja chema endapo kilitendwa kibaya kitakuja kibaya ~amini niyasemayo...main karma principles..
it may take time,but it must happen...
 
Kwa hiyo hizo nyaraka ndio vielelezo vya madawa ya kulevya? Hii ni aibu ya mwaka kwa watawala hawa waliopo. JK na wastaafu wengine toeni semina elekezi jinsi ya kurun nchi

Hawawezi maana walimpa huyu ili anyanyase Wapinzani. Ukimsikiliza Makamba snr alisema sasa Wapinzani watabatizwa kwa moto na moto ndiyo huu tunaouona.

Hawawezi kujitoa maana ndicho wali chini subiri a kwa hamu bila kujua Upinzani ukishaingia kutoa si rahisi.

Wanachofanya ni kuhamasisha Wapinzani wafanye fujo wawe na lakusema.Mpaka sasa naona Serikali imelala Zorro kwa 4G.

Congratulations CDM.
 
Back
Top Bottom