Niende kwenye mada wanyamwezi ni nyoko si mwanaume si mwanamke mapenzi yao wote ya kichawi, mvuto na wito wa kutumia dawq kumuita unaemtaka.
Hivi mkoa wa tabora sikonge wanyamwezi huu upuuzi wameutoa wapi.
Kizinde changu kimewashinda kila walichojaribu wapi mwamba nimeiva.
Leteni visa vyenu vya mapenzi ya dawa na ulozi wa mapenzi.
Lete lete visa hivyo.
Wadiz.
Mkuu umesahau ule mti wa 'kalilalila' wenye vimajani vidogo vidogo unaootaga visuguuni.
Pamoja na ujanja wako unaojisifu kuwa nao, ukija kuchomewa hiyo utakuja kujidharau mwenyewe baadaye, hautakuja kutoa ushuhuda Jf maana utajiona hufai na hivi unavyojisifia ovyo ovyo namna hii!
Hata sasa hivi ukichomewa, kesho utakata tiketi kwa dharula ili uende, ukifika Morogoro dem anaweza anakizima kibatari ili kukuzingua uhangaike.
Akikizima upendo unashuka, unarudiwa na hali yako ya kawaida unajiona mjinga unaahirisha safari, unarudi.
Ukifika kwako anachoma tena unaanza safari, ukifika huko sasa unaandaliwa chakula ambacho ni wali mboga yake ni nsansa ya kansolele ya Lwanzali, ama kisamvu chenye tui la karanga ya kushiba.
Chakula cha asili ya Tbr, kina ladha tamu sana.
Hata ungelikuwa Waziri utapiga simu ya dharula kwa Majaliwa kuomba udhuru nakwambia.
Kitakachokunasua hapo mpaka yeye mpenzi wako ajiridhishe kuwa mfukoni mwako umeishiwa huna kitu, siyo ile kuishiwa kwa kuigiza, umeishiwa kabisa hata senti tano huna na account bank inasoma sifuri ndiyo unafukuzwa.
Visa vya kukufukuza ataanza kuigiza kukushangaa kukaa siku zote hizo bila kumkumbuka mkeo, unalazimishwa sasa uende kuwaona familia yako kisha utakuja rejea tena safari nyingine.
Wewe ulivyokolezwa lazima utakataa katakata kuondoka kwa kudai huoni umuhimu.
Ndiyo hapo utaanza kupangiwa majukumu ya kwenda shamba kulima majaruba kule Mguluko ama Kasela na utatii kumridhisha mama na ujanja wako huo utauweka mfukoni.
Na hivi sasa utakuwa hauna hela umeishiwa, utatengenezwa msukule wa ridhaa, kwa sababu haupotezwi kwa viini macho, utaendelea kujiona na kujitambua na watu wengine wataendelea kukuona kama kawaida, lakini unakuwa umezama sanaaa, yaani huoni wala husikii.
Na kulimishwa jarubani baba ndiyo kipimo halisi cha kuona kama dawa imeshika😁😁😝😜.
Nimewaona kwa macho jinsi waheshimiwa pamoja na wajanja kama wewe wakipelekwa shamba kuvuruga majaruba na kupanda mpunga kama kawaida bila ubishi wala lawama.
Kuzinduliwa hapo ni kwa jitihada za ndugu ama mkeo.
Vinginevyo hainaga ujanja hiyo, ni kuzamia mazima.
Ndiyo maana Tabora inaitwa 'mboka', ogopa sana.