DAWASA Special thread: Tupe maoni, maswali, malalamiko na ushauri

Wanakata maji bila taarifa siku ya pili leo . This is too much na wiki kadhaa walitufanyia hivyo hivyo kinondoni. Nadhani kuna haja ya kuanza kuwasemea sasa wamekuweka kama shirika la baba yao.
 
Nilitegemea kuona tangazo la tatizo la kukosekana kwa maji hivi sasa kwenye ukurasa wao huu lakini kimya, sijui huu ukurasa ni wa kupata taarifa kutoka kwa wananchi tu na sio wao kuwapa wananchi taarifa.
 
DAWASA ivi hapa kimara mwisho njia ya matosa mmechimba kutengeneza bomba letu alaf mkaacha ivo ivo bila kufukia mnasabisha hadha magari yanapita njia moja alaf ni kilimani mnategemea nini siku ya nne leo
 
Tunashukur sana kwa maelezo mazuri.

Lakin tunasikitika kwa Dana Dana zinazofanywa na wanao pokea malalamiko yetu.

Mpokezi nao wanataka kujua tatizo badala ya kuelekea kwa wahusika wa kutatua tatizo.

Ofisi za Tabata Kero tupu.

Tumelalamikia kuhus bili kuleta kubwa tafauti na matumizi... Mpaka tukaandika barua ya malalamiko Lakin ni kuahidiwa watakuja mafundi... Mara tumeletewa barua ya kujibu kero... Mara kero itatuliwa... Huku bili za makosa zina endelea kutuma.

Tukaenda wenyewe kuwaona wahusika Lakin ni Dana Dana... Ukishafika mapokezi Unaambiwa mhusika ashaondoka ofisini... Ajab ni kua hao wahusika hawana namba za simu ili wawasiliane na wateja?

Ina maana mteja utamsubiri mhusika ambae hujui atakuja saa ngapi?

Alafu lugha zao mbaya.

Hao wasomaji mita utafikir I hawajapewa kozi maalum ya namna ya kuongea nao wateja.
Lugha za kihuni zumeenea/kushamiri.

Afisa amefikia na mafundi wa bomba kuja angalia tatizo la mita... Mita mbovu wameona... Wakaahidi itabadilishwa wamefika ofisini wanasema mita ni nzima.

Hizi ni lugha za wafanyakazi kweli Waliopata mafunzo?

Alafu gharama za bili zina endelea kusoma... Ilhali miezi mitatu sasa malalamiko ya mita hiyo yameripotiwa kwenu.

Baada ya kupitia huku na kule ndipo tu naambiwa Afisa alikuja na mafundi bomba hahusimi na matatizo ya mita.

Huu ni unyanyasaji kwa wateja wenu.

Watu wa mapokezi muwaweke wanapokua weledi kwa kuhudumia wateja wenu na kuwaelekeza vzuri.

Hiyo ni ofisi ya serikali si ofisi ya mtu binafsi ambae anafanya anavyojisikia.

Ahsanteni.

Kazi njema.
 
pre paid meters ndio suluhisho la matatizo yote na pia serikali itajihakikishia kukusanya mapato yake bila kupotea hata shilingi 1
Kama una leakage
Cdhan kama hilo litakuwa ni suluhisho
 
Madereva wa majitaka wanakula rushwa wakifanya trip ya pili ofisi haijui wanatia mfukoni wekeni monitoring system za kisasa
 
Tuwekeeni maji tabata yanamwaggika bure.

Dsm hii tunahangaika je huko vijijini watafanya nini
 
Nashauri Maji msisubiri atokee mwarabu achukue hii idea. Maji taka tengenezeni system watu wasichimbe mashimo ya vyoo, ninyi Muwe na main system maeneo maeneo mkusanye Kodi ya huduma maji taka tu kila mwezi...watu tumechoka kuishi na Vinyesi nyumban...hamjifunzi kwa wenzetu! Khaa!!

"Vyoo vyote viunganishwe na mfumo wa maji taka. Kusiwe na mambo ya kuchimba shimo la choo. Wewe ukijenga nyumba yako utawaita watu wa maji taka ili waje wakupe ramani ya kuunganisha choo chako na mfumo au bomba la maji taka"(konda msafi,2021)
 
Mimi ni mteja mpya nipo kibaha, surveyor amefika site, nimepata control no na nimelipia 340, 000 kama gharama ilivyokuja.

Cha ajabu ni wiki y pili sasa nikiuliza naambiwa mita hazipo hii litu siielewi.
Kama pesa imelipwa ya mita kwanini zichukue zaidi ya wiki mbili?

Mi nazani ofisini mngeku na mita za kutosha tu mtu akilipia afungiwe sasa kila nikiuliza naambiwa mita hakuna utapigiwa simu zikija hii sio poa kabisa
Jazeni mita ofisini mtu alioe apewe sio kutupangisha foleni kama vile tunapewa bure.

Nawasilisha japo hata sijui zitakuja lini
 
Miradi kadhaa inaendelea, hivyo hilo litakwisha
 
NIPO NDANI YA META 50 .... NATAKA NIVUTE MAJI YA DAWASA. JE GHARAMA YAKE NI KIASI GANI?

NIPO MAENEO YA PUGU_ MWAKANGA DAR ES SALAAM
 
NIPO NDANI YA META 50 .... NATAKA NIVUTE MAJI YA DAWASA. JE GHARAMA YAKE NI KIASI GANI?

NIPO MAENEO YA PUGU_ MWAKANGA DAR ES SALAAM
Mimi nipo Kibaha nimelipia 340, 000 sasa sijui kwako ila nimelipia mwezi wa 7 mwanzoni mpaka leo bado vifaa havijaja niko foleni
 
Baada ya kulipia new connection na kusubiri kwa miezi miwili hatimae leo nimepigiwa simu niende kuchukua vifaa kesho tayari kwa kuungnishiwa huduma
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…