Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
Eneo la Malamba Mawili ambalo lipo kata ya msigani linahudumiwa kupitia mtambo wa Maji Ruvu Juu.
Kutokana na maeneo hayo kuzungukwa na vilima vikali na hupata maji siku ya Jumanne, Alhamis na Jumapili, lakini baadhi ya maeneo kushindwa kupata maji pindi msukumo wa maji unapokuwa mdogo.
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) inaendelea na jitihada mbalimbali za kufanya maboresho ya huduma za Maji katika eneo hili kwa kufanya mradi wa kuongeza msukumo wa maji kwa kulaza bomba lenye kipenyo cha inchi 8 kwa umbali wa KM 3.5 katika maeneo hayo lengo ni kuboresha huduma.
Kwa sasa utekelezaji wa mradi huo umefikia 48% na kazi inaendelea. Hata hivyo wakati tukiendelea na utekelezaji huo tutaendelea kuratibu upatikanaji wa uhakika wa huduma za Maji ili kuhakikisha maeneo yote yanapata huduma ya maji.
Everlasting Lyaro
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
DAWASA
Malalamiko ya awali - KERO Maji Malamba Mawili ni mgao mkali, baadhi ya Wakazi walio kwenye miinuko wana miezi hawapati maji kutokana na kasi ndogo ya maji yanayotoka
Kutokana na maeneo hayo kuzungukwa na vilima vikali na hupata maji siku ya Jumanne, Alhamis na Jumapili, lakini baadhi ya maeneo kushindwa kupata maji pindi msukumo wa maji unapokuwa mdogo.
Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es salaam (DAWASA) inaendelea na jitihada mbalimbali za kufanya maboresho ya huduma za Maji katika eneo hili kwa kufanya mradi wa kuongeza msukumo wa maji kwa kulaza bomba lenye kipenyo cha inchi 8 kwa umbali wa KM 3.5 katika maeneo hayo lengo ni kuboresha huduma.
Everlasting Lyaro
Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano
DAWASA
Malalamiko ya awali - KERO Maji Malamba Mawili ni mgao mkali, baadhi ya Wakazi walio kwenye miinuko wana miezi hawapati maji kutokana na kasi ndogo ya maji yanayotoka