DC Jerry Muro amfokea DED kama mtoto mdogo kwa kuchelewa dakika 10 kwenye msafara

DC Jerry Muro amfokea DED kama mtoto mdogo kwa kuchelewa dakika 10 kwenye msafara

Fafanua basi kama wote wako sawa kivipi...?
Mkuu wako tofauti,Dc ni zaidi ya Mkurugenzi.Kuna kitu hapa kinaleta mvurugano ni kwa awamu hii ya tano wizara ya TAMISEMI kuwa china ya ofisi ya Rais hivyo Rais anapotamka na kuwatangaza Wakurugenzi imejengeka dhana ya wakurugenzi kujiona nao wana ngazi sawa na wakuu wa wilaya jambo ambalo sio.Mkuu wa wilaya ni kiongozi wa kisiasa na wakurugenzi ni watendaji, aidha, mfano rahisi tu ni kwamba unaweza kukuta kuna wilaya inazo halmashauri zaidi ya tatu zenye wakurugenzi lakini Mkuu wa wilaya anayeongoza wilaya hiyo ni mmoja tu.Ikumbukwe kwamba kuna wilaya na mamlaka za serikali za mitaa au halmashauri za wilaya,miji,manispaa na majiji.(rejea sheria ya tawala za mikoa 19,1998 na sheria namba 8-9/1984 za serikali za mitaa)
Tukirudi kwenye tukio,Kiitifaki Mkurugenzi alitakiwa awepo eneo la tukio hata kabla ya Dc na Rc,tukubaliane tu kwamba alikosea na kama kulikuwa na dharula angetoa taarifa.Upande wa pili Dc alikuwa sahihi kukemea jambo hilo ila namna alivyotoa karipio lake labda ndio linazua utata, ila ilibidi afanye hivyo ili kuonyesha mamlaka yake( ambalo ni hulka ya kibinadamu) na kumuonyesha bosi wa RC kwamba anasimamia watu walio chini.
Wasalam.
 
my conviction, kila upande una makosa, mkurugenzi alitakiwa ampigie simu dc kumwambia kwamba atachelewa kufika kwa sababu zilizomfanya achelewe, lakini it was not necessary kwa dc kuropoka especially kama lilikuwa kosa la kwanza
 
DC mpya wa Arumeru, Jerry leo ameonekana kwenye video fupi akimfokea mkurugenzi wa manispaa kama mtoto mdogo kwa kuchelewa dakika 10 tu, tukio hilo limetokea mbele ya RC ( Gambo ) na baadhi ya viongozi wa Arusha, huku Gambo akionesha dhahiri kutofurahiswa na tukio lile



Huu ndio mfano wa maudhui wa kale kawimbo kanakoitwa 'Madaraka ya Kukevya'

tena anamyooshea kidole sisi kwetu mtu akikunyooshea kidole bi dharau sana,km alishindwa kuwa msemaji wa klabu unampa ukuu wa wilaya eti kisa alitukana wapinzani daaah nonsense
 
DC mpya wa Arumeru, Jerry leo ameonekana kwenye video fupi akimfokea mkurugenzi wa manispaa kama mtoto mdogo kwa kuchelewa dakika 10 tu, tukio hilo limetokea mbele ya RC ( Gambo ) na baadhi ya viongozi wa Arusha, huku Gambo akionesha dhahiri kutofurahiswa na tukio lile



Huu ndio mfano wa maudhui wa kale kawimbo kanakoitwa 'Madaraka ya Kukevya'


Hivi kwa nini anajihisi kuwa anadharauliwa? Anatumia nguvu nyingi na anaonekana kuwa na jazba kila anapoongea, sasa anahisi kunamtu anataka kuchukua nafasi yake?
Tunuafahamu kuwa yeye ndiye mkuu wa wilaya , sasa kwa nini anajitangaza sana kuwa yeye ndiye mkuu wa wilaya?

Kama anahisi hafahamiki, basi ingekuwa vizuri afanye ziara ya kujitambulisha katika vijiji, kata natarafa zote za wilaya hiyo.
 
Eeeehhhh... Jamani Jerry anakoelekea sio kabisa.. Eeeeeh..!!😡😡😡😳😳😳😳 Mh Rais wangu tengua huyu mtu, plz plz plz...!!! Yaani nasema kweli kabisa ingekuwa ni mm ananinyooshea kidole hivyo napiga ngumi hadi atakimbia atasahau kila kitu hapo..hatarudia tena kabisa..!!
KICHAA HUWA HAPANGIWI, SANA SANA ATAMPANDISHA CHEO KICHAA MWENZAKE
 
Baba yako au mama yako angekuwa DED halafu anafokewa unaona kama hivi ungejiskiaje? Acha upuuzi wa kuandika ujinga ujinga
Usiingize mambo udugu katika kazi. Sheria msumeno haijalishi kama ni baba, mama au mtoto. Pole kwa ufinyu wako wa kufikiri
 
  • Thanks
Reactions: BRN
Kwani angemuitaa baada ya ziara hiyo na kumuonya kiofisi angekosea wapi? Au ndio promo za camera? Anajenga chuki kati yake na walio chini. Apunguze jazba, uongozi ni kucheza na saikoloji za watu tuuu
 
Hivi alishindwa nini kusubiri na kumwuliza in closed door?

Je anefahamu kilichomfanya akachelewa?

Je kulikuwa nai ulazima wa kutoa maneno ya matusi?

Kulikua na sababu ya kumdhalilisha mbele ya subordinate wake?

Wilaya ya Meru haina DC ipo wazi ni suala la Muda tu.
 
That is not how we are supposed to serve.

Kama mwanachama mtiifu wa CCM ambayo inajukumu la kuisimamia Serikali.

Naomba mheshimiwa D.C. aonywe na mamlaka ya uteuzi.
Huyo muro hatokemewa wala kuitwa kwenye kamati ya maadili sana sana atambiwa achape kazi!

Ova
 
Wilson Mahela ni PhD holder. Amefundisha chuo kikuu UDSM muda mrefu wakati wewe ukifanya ukanjanja kwenye media. Amekuzidi umri, amekuzidi elimu, amekuzidi busara. Kama umeshindwa kumheshimu kwa nafasi yake basi ungemheshimu hata kwa umri wake tu.

Halafu kichekesho unamlaumu DED kwa kuchelewa dakika 10, lakini wewe umepoteza dakika nyingi zaidi kumtukana. Hivi lengo lako lilikua kuokoa muda kweli?
Huyu Dr.Wilson Mahela ni PhD holder. Amefundisha chuo kikuu UDSM muda mrefu wakati wewe ukifanya ukanjanja kwenye media. Amekuzidi umri, amekuzidi elimu, amekuzidi busara. Kama umeshindwa kumheshimu kwa nafasi yake basi ungemheshimu hata kwa umri wake tu.

Then huyo DED unayemdhalilisha ndo anayekuweka mjini. Tunajua maDC hamna budget. Mnalelewa na ofisi za DED kwa kila kitu. Hadi mafuta ya gari mnaomba kwao. Sasa how comes unamdhalilisha mtu anayekufanya usurvive? Kesho ukimuomba mafuta akikunyima utamfanya nini? Au ndo utaita tena macamera uanze kumtukana? Growup na uache sifa za kijinga. Uongozi ni kujifunza. Take time to learn from your elders kabla ya kukurupuka. Unajidhalilisha na kumdhalilisha aliyekuteua.!


Nani kakopi hapa ama wewe ndo Malisa JF BWAANA! Kama siyo yeye ujifunze kueleza ulipopata habari hii
 
Baadhi ya viongozi ni wanajiona wao miungu hawana mapungufu wamekamilika, watawaliwa ndio wenye mapungu ya kibinadamu. Hawajui wanatenda kama mafarisayo kuwapa wengine sheria ngumu wakati wao hawawezi kuzitekeleza
 
NINGEMKATA KIBAO,PAAAAAAAAAAAAAAAAAP!
MBELE YA HIZO HIZO KAMERA ANAZOTAKA KUCHUKULIA UJIKO!
 
Eeeehhhh... Jamani Jerry anakoelekea sio kabisa.. Eeeeeh..!!😡😡😡😳😳😳😳 Mh Rais wangu tengua huyu mtu, plz plz plz...!!! Yaani nasema kweli kabisa ingekuwa ni mm ananinyooshea kidole hivyo napiga ngumi hadi atakimbia atasahau kila kitu hapo..hatarudia tena kabisa..!!
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kwani DC hana ofisi wakakaa wakosoana kwa utaratibu mzuri wa heshima na adabu, heshima iko pande zote mtawala na mtawaliwa.
 
Back
Top Bottom