DC Jokate, huu ni muda sasa wa kubadili aina ya mavazi yako

DC Jokate, huu ni muda sasa wa kubadili aina ya mavazi yako

Mawazo ya aina hii ndio yaliyokijaza kichwa chako, unaukagua mwili wa mtoto wa kike ukitafuta nini?

Ewe mnafiki, huwa mnalaumu Magufuli alikuwa dikteta, ila wewe na haya mawazo yako ya kuingilia mavazi ya mwingine hujioni kama u-dikteta pia, sijui mtaamka lini nyie viumbe.
Siyo mimi, bali kwa mila zetu si heshima kwa mwanamke kuacha kifua chake wazi.

Na pia muongozo wa mavazi wa watumishi wa umma unaelekeza kuwa wanawake wasiache vifua vyao wazi
 
Mawazo ya aina hii ndio yaliyokijaza kichwa chako, unaukagua mwili wa mtoto wa kike ukitafuta nini?

Ewe mnafiki, huwa mnalaumu Magufuli alikuwa dikteta, ila wewe na haya mawazo yako ya kuingilia mavazi ya mwingine hujioni kama u-dikteta pia, sijui mtaamka lini nyie viumbe.
Hatujaingilia mavazi yake bali tumehoji kile ambacho amekiacha wazi, yaani kifua nje!
 
Mkuu, mbona Jokate hajavaa vibaya katika mavazi yote uliyoweka hapa? Usije kuleta ushamba wa dini hapa na kulazimisha mtoto wa watu avae magunia kukuridhisha wewe na itikadi zako za kidini.
Hajavaa vibaya huko chini, ila juu kwenye kifua hajavaa kabisa, kakiacha wazi kinyume cha muongozo wa mavazi ya watumishi wa umma
 
Hatuna Shida na Mavazi, ni Muda sasa wa yeye kufanywa kazi!! Temeke ni chafu kama dampo!! Na muda Muafaka wa kuachana na siasa za kusifiwa na kurudi kwenye siasa za taratibu na sheria!! Na kusimamia utendaji!! Wananchi tunategemea maelekezo ya viongozi kuelekeza wafanyabiashara watafutiwe maeneo rafiki ya kufanya biashara yatekelezwe na barabara ziachwe kwa kusudio stahiki!! Fikiria unatoka Mjini kwenda Mkuranga unamaliza masaa mawili Mbagala Mwisho!! Ndio kusema hakuna uongozi!?
 
Unajua maana ya "kuacha kifua wazi"?
images (18).jpeg


Huoni kifua njenje hapo?

Suti yake siyo tatizo, atafute kivazi kifunike hicho kifua kisiwe nje
 
Iweje kifua kiwe wazi kama kilichopo kifuani hakionekani? au wewe unakiona? wacha hayo mawazo ya vijana wewe ni mtu mzima unaonekana.
Kama kifua hukioni hapo basi utakuwa kipofu.

Anyway, kwenye muongozo wa mavazi ya watumishi wa umma nilioweka hapo kwenye kipengele cha MAVAZI YASIYOFAA KWA WANAWAKE nukta ya tatu imesema wazi kuwa moja yamavazi yasiyofaa ni yale yanayoacha kifua nje
 
Kama kifua hukioni hapo basi utakuwa kipofu.

Anyway, kwenye muongozo wa mavazi ya watumishi wa umma nilioweka hapo kwenye kipengele cha MAVAZI YASIYOFAA KWA WANAWAKE nukta ya tatu imesema wazi kywa moja yamavazi yasiyofaa ni yale yanayoacha kifua nje
Ok, kama unawaamini hao waliosema hivyo basi nenda kawaulize, inawezekana vipi kifua kiwe wazi kama kile kilichopo kifuani hakionekani?
 
Kwako DC Jokate

Kwanza nikupongeze kwa kazi nzuri unayofanya, binafsi nakukubali sana aina ya uongozi wako, umefanya kazi nzuri sana huko Kisarawe.

Pia, sina wasiwasi kuwa hata hapa Dar ulipohamishiwa katika wilaya ya Temeke utafanya vizuri.

Naamini kabisa kuwa kwa jinsi unavyochapa kazi ukiendelea hivi basi una future ya kuwa kiongozi mkubwa nchini.

Ila kuna kitu nataka nikwambie, Mavazi yako hasa yale yanayoacha kifua chako wazi si muafaka kwa mwanamama mwenye hadhi ya ofisi ya umma unayoishikilia.

Nafahamu kuwa una bsckground ya mambo ya mitindo na ulimbwende, lakini naomba ufahamu sasa kuwa sasa wewe ni mkubwa kuliko hayo, wewe ni mtumishi na kioo cha jamii, ni kioo cha mabinti nchini, nakuomba basi hilo vazi linaloacha kifua chako nje uliache na badala yake tafuta vazi zuri tu linaloendana na hadhi ya ofisi ya Umma.

Ndugu DC hii nchi imejaa marijali, wanaume shababi, ambao kiukweli wakiona kifua kizuri kama hicho wanaweza kupatwa mfadhaiko, kwa hiyo ili kuepusha hayo yote nakuomba ndugu DC kwa unyenyekevu mkubwa utuonee huruma kwa kuvaa mavazi muafaka zaidi.

Mheshimiwa wewe una potential ya kuwa kiongozi mkubwa huko mbeleni, naomba uanze kujiweka katika hali ya mtu aliyetayari kupokea majukumu makubwa kwa kujinasabisha na majukumu hayo kitabia na kiutendaji.

Natanguliza shukrani, na samahani sana kama nimekukwaza

View attachment 1829430View attachment 1829432View attachment 1829433View attachment 1829434
Dereva wa Jokate, ujumbe umefika, najua madereva wa hawa ma-viongozi vijana wasio olewa [SUKARI -MAMMY] mnapata shida sana, ujumbe umefika , Jei-wa-insta-mwaga-maa atamfunda, ni mama yake mdogo.
 
unalinganisha chuchu mbili na nywele zisizo na idadi?
Huo ni mfano tu nimekupa ili kutambulisha uwepo wa kitu mahala pake, anyway, hapa ulitakiwa useme "sehemu ya juu ya kifua" sio kifua chenyewe, imaginations zako ndio zimeku cost hapa.
 
Back
Top Bottom