Pre GE2025 DC Longido: Mazingira ya 2020 na yale yaliyofanyika kwenye mapori yalitengenezwa na serikali ili tupite bila kupingwa!

Pre GE2025 DC Longido: Mazingira ya 2020 na yale yaliyofanyika kwenye mapori yalitengenezwa na serikali ili tupite bila kupingwa!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Afukuzwe na aseheme alifanya nini kwenye mapori,huenda aliuua,poor Tanzania!!
Siyo yeye ni Serikali ndio ilifanya hayo mambo huko maporini.
Inabidi serikali itoe tamko mambo gani yalifanyika huko maporini?
 
Kwani Rais hawapendi wasema kweli?
Sura kama hizi ndizo zilizojaa kwenye nafasi za utawala na uongozi. Isivyokuwa bahati hata watumishi wa Serikali kwenye nafasi zao wanafanana na huyo jamaa hapo juu kwa kauli na matendo yao. Wale wanaoingia mara kwa mara kwenye ofisi za Serikali wanaelewa hali ilivyo.
 
Hivi hawa viongozi wa CCM huwa wanajiuliza madhara ya maneno Yao kwa wananchi yatapokelewaje?

Luka 12:2-4

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Hakuna jambo lililofunikwa ambalo halitafunuliwa au siri iliyofichwa ambayo haitajulikana. 3 Kwa hiyo, yote mliyosema gizani yatasikiwa mchana: na yote mliyonong’onezana mkiwa mmeji fungia chumbani, yatatangazwa hadharani.
4 “Nawambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, na halafu basi.
 
Kuna chama kimebaki na mipini tu majembe yote yashajitafutia mahala Sasa,nawahakikishieni kunakucha soon.

Luka 12:2-4

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Hakuna jambo lililofunikwa ambalo halitafunuliwa au siri iliyofichwa ambayo haitajulikana. 3 Kwa hiyo, yote mliyosema gizani yatasikiwa mchana: na yote mliyonong’onezana mkiwa mmeji fungia chumbani, yatatangazwa hadharani.
4 “Nawambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, na halafu basi.
 
Siamini kama haya maneno yanatoka kinywani mwa kiongozi mkubwa.

Naomba tumsikilize kwa makini anavyo wadharau wapiga kura na anavyo jimwambafai kushiriki kwenye uchaguzi wa 2020.

Kama viongozi wetu wapo hivi sioni kama uadilifu unaoimbwa na wenzake utakuja kutimia.

Asante sana CCM, idumu.

"Na mimi naomba niwahakikishie, mimi niko very tough, kama kuna mtu ambaye siyo mwoga ni mimi! Wote hapa madiwani mwaka 2020 hayuko diwani aliyepiga kampeni hapa nyumba kwa nyumba, hakuna!

"Sasa yale mazingira ya mwaka 2020 siyo kwamba yalikuja yenyewe automatically kwasababu ninyi mlikuwa wagombea bora sana, ni mazingira ambayo yalikuwa, yametengenezwa na serikali ndio iliyofanya kazi ile ya wewe kupita bila kupingwa.

"Na kuna watu mnafahamu kilichotokea kwenye mapori huko na sehemu zingine na mimi nilihusika kwenye majimbo fulani fulani, sasa mazingira yale ni serikali ndiyo iliyofanya ile kazi, diwani huna ujanja wowote kwenye kata yako ya kwamba utashinda bila serikali, HAKUNA.

"Na usije ukajidanganya ndio maana sisi sasa hivi tumeshafanya kazi huko kubwa sana, ya kuchakata huko kwenye kata, vijiji, vitongoji vyote, taarifa zile zote tunazo, hali ya mambo jinsi ilivyo, tunaendaje.."



Pia soma:

Haya wanaosemaga kwamba hakuna ushirikina, nini hicho? Huyu jamaa karogwa hapo na wale ndugu wa marehemu aliowaua.

Hayupo sawa huyu kaanza kuchanganyikiwa. Damu za watu zinamsumbua huyu. Na hata anaweza kupelekwa porini na yeye!

Mfuatilieni miaka kadhaa atakuwa chizi tayari wa kuvua nguo.
 
Siamini kama haya maneno yanatoka kinywani mwa kiongozi mkubwa.

Naomba tumsikilize kwa makini anavyo wadharau wapiga kura na anavyo jimwambafai kushiriki kwenye uchaguzi wa 2020.

Kama viongozi wetu wapo hivi sioni kama uadilifu unaoimbwa na wenzake utakuja kutimia.

Asante sana CCM, idumu.

"Na mimi naomba niwahakikishie, mimi niko very tough, kama kuna mtu ambaye siyo mwoga ni mimi! Wote hapa madiwani mwaka 2020 hayuko diwani aliyepiga kampeni hapa nyumba kwa nyumba, hakuna!

"Sasa yale mazingira ya mwaka 2020 siyo kwamba yalikuja yenyewe automatically kwasababu ninyi mlikuwa wagombea bora sana, ni mazingira ambayo yalikuwa, yametengenezwa na serikali ndio iliyofanya kazi ile ya wewe kupita bila kupingwa.

"Na kuna watu mnafahamu kilichotokea kwenye mapori huko na sehemu zingine na mimi nilihusika kwenye majimbo fulani fulani, sasa mazingira yale ni serikali ndiyo iliyofanya ile kazi, diwani huna ujanja wowote kwenye kata yako ya kwamba utashinda bila serikali, HAKUNA.

"Na usije ukajidanganya ndio maana sisi sasa hivi tumeshafanya kazi huko kubwa sana, ya kuchakata huko kwenye kata, vijiji, vitongoji vyote, taarifa zile zote tunazo, hali ya mambo jinsi ilivyo, tunaendaje.."



Pia soma:

Mazingira ya kwenye mapori ndio yapi au ndio Yale ya watu kutekwa na kutupwa porini na kama ndio hivyo kumbe Sasa mpaka Sasa wanahusika na watu kupotea
 
Hata kama mmetengua uteuzi wake lakini Marco Ng’umbi kasema ukweli mchungu.

Kauthibitishia Umma mambo matatu-;

1. Kathibitisha kuwa Maccm hatakubaliki,

2. Kathibitisha kuwa maccm huwa yanaiba Kura,

3. Kathibitisha kuwa Serikali huwa inateka watu na kuwatupa kwenye mapori.View attachment 3084434
Mkuu

Luka 12:2-4

Neno: Bibilia Takatifu

2 “Hakuna jambo lililofunikwa ambalo halitafunuliwa au siri iliyofichwa ambayo haitajulikana. 3 Kwa hiyo, yote mliyosema gizani yatasikiwa mchana: na yote mliyonong’onezana mkiwa mmeji fungia chumbani, yatatangazwa hadharani.
4 “Nawambieni rafiki zangu, msiwaogope wale wauao mwili, na halafu basi.
 
Kuna haja ya kuanzisha shule Ya kukuza uelewa Kwa viongozi wapuuzi kama huyu DC,anaongea ambayo mama hayataki,akiwemo ofisini kufikia kesho itakuwa ni doa Kwa serikali yetu.
Hoja sio kuwa mama hataki kusia hayo, ila huu ni ushahidi kuwa uchaguzi ni maigizo tu mara nyingi kuna uchakachuaji. Ilianzia kwa Nape sasa imekuja kwa huyu, hii ndio sababu kila mara watu wanataka Tume huru ya Uchaguzi ili wakushinda ashinde na wakushindwa ashindwe.
 
Back
Top Bottom