DC mpya Gairo una kazi kubwa ya kurejesha tabasamu kwa wananchi

DC mpya Gairo una kazi kubwa ya kurejesha tabasamu kwa wananchi

DustBin

JF-Expert Member
Joined
Jun 3, 2021
Posts
609
Reaction score
604
Nawasalimu kwa jina JMT

Napenda nielekeze maoni yangu kwa DC mpya wa Gairo, mdogo wangu Jabiri M. Omari na nimzindushe kwamba wana gairo walinyanyaswa sana na yule dada. Nimepata kuzungumza na baadhi ya wananchi wa Gairo wakanieleza hili, kwamba yule dada hakuwa mstaarabu na wala hakua na mahusiano mema na wananchi, hivyo katika kazi uliyonayo mdogo wangu ni kurejesha imani ya wananchi kwa ofisi ya mkuu wa wilaya.

Nimeambiwa mtangulizi wako zilikua haziivi hata na MP wa hapo, hivyo hili lilikua ni tatizo kubwa. Nakuomba uyarekebishe hayo ili Gairo yetu ipige hatua kimaendeleo. Bado wana Gairo wanahitaji hospitali kubwa hako ka zahanati kalichopo hakakidhi haja za wananchi. Lakini pia suala la Administrative Block za utawala na nyumba maalumu ya DC lipewe kipaumbele.

Nakutakia utekelezaji mwema!

Kaka yako
DustBin
 
Huyo DC ni yule tunaambiwa alikuwa anapika na kupakulia wakubwa? Nasikia alikuwa nyodo kwenda mbele
 
Huyo DC ni yule tunaambiwa alikuwa anapika na kupakulia wakubwa!? Nasikia alikuwa nyodo kwenda mbele
Nimeambiwa wananchi wengi wamefurahi waliposikia ameondoshwa. Mwisho wa yote tujifunze kuwa wapole na wananchi tunaowaongoza!
 
Binafsi nishawahi kuonja joto kwa mbali ya huyo

Dc aliyetoka hapo gairo.

Ova
 
Nimeambiwa wananchi wengi wamefurahi waliposikia ameondoshwa. Mwisho wa yote tujifunze kuwa wapole na wananchi tunaowaongoza..!
Alikuwa kiburi, dharau sana

Ova
 
Kwani aliyekua DC wa pale si alikua yule mmama na ni mlokole flani. Kila kukicha naona Facebook kule anaweka mijipicha mafanikio yake pale Gairo. Au wewe ni mpinzani wake?
 
Sio arudishe furaha tu ya kicheko but aendane na kasi ya yule dada..maana furaha lazima iendane na maendeleo
 
kwani aliyekua DC wa pale si alikua Yule mmama na ni mlokole flan. Kila kukicha naona Facebook kule anaweka mijipicha mafanikio yake pale Gairo. Au wewe ni mpinzani wake?!!
Sinaga mambo ya chuki binafsi na mtu. Haya niliyoyasema nimeyatoa field. Wananchi wenyewe ndio wameyasema hayo. Na hilo lipo wazi kwa ambae amekaa Gairo ktk utawala wa huyo former DC
 
Sio arudishe furaha tu ya kicheko but aendane na kasi ya yule dada..maana furaha lazima iendane na maendeleo
Gairo ni wilaya changa ambayo inahitaji msukumo wa viongozi wake kujituma na kusimamia kuleta maendeleo. Kimaendeleo bado ipo nyuma hasa kwenye miundombinu. Suala la kutoelewana baina ya Mhe. Mbunge na DC halikua na afya kwa Gairo kimkakati
 
Sasa shida hapo ni nani,Mbunge mwenye jimbo au DC!ukumbuke DC ni mteule wa Rais kwenye utawala,kwa hiyo mwenye jimbo ndio alipaswa awe na uhusiano mzuri na DC ili alipatie maendeleo jimbo lake,na ujuwe pia DC anaweza hamishwa siku yoyote kwenda wilaya nyingine lakini sio mbunge,au mi ndio sielewi...
 
Back
Top Bottom