DC Nzega aagiza kukamatwa kwa mkuu wa chuo cha madini kwa kumdharau RC Tabora

DC Nzega aagiza kukamatwa kwa mkuu wa chuo cha madini kwa kumdharau RC Tabora

The Watchman

JF-Expert Member
Joined
Nov 7, 2023
Posts
896
Reaction score
1,427
Mkuu wa Wilaya ya Nzega Naitwapwaki Tukai ameliagiza Jeshi la polisi kumkamata na kumuweka ndani Abraham Lwakajunguti ambaye ni mkuu wa chuo cha mmDadini Lusu kilichopo wilayani Nzega kwa madai ya utovu wa nidhamu akishindwa kutoa majibu mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora wakati walipokua kwenye mkutano wa hadhara alipotakiwa kutoa maelezo juu ya kikundi cha watu wanaoingia kuchimba madini ya dhahabu kwenye eneo la chuo hicho bila kuwa na leseni halali.

Kufuatia hali hiyo mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe Paul Chacha akaagiza mkuu huyo wa chuo aondolewe kwenye nafasi ya ukuu wa chuo hicho cha madini kutokana na utovu huo wa nidhamu.

 
Mkuu wa Wilaya ya Nzega Naitwapwaki Tukai ameliagiza Jeshi la polisi kumkamata na kumuweka ndani Abraham Lwakajunguti ambaye ni mkuu wa chuo cha mmDadini Lusu kilichopo wilayani Nzega kwa madai ya utovu wa nidhamu akishindwa kutoa majibu mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora wakati walipokua kwenye mkutano wa hadhara alipotakiwa kutoa maelezo juu ya kikundi cha watu wanaoingia kuchimba madini ya dhahabu kwenye eneo la chuo hicho bila kuwa na leseni halali.

Kufuatia hali hiyo mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe Paul Chacha akaagiza mkuu huyo wa chuo aondolewe kwenye nafasi ya ukuu wa chuo hicho cha madini kutokana na utovu huo wa nidhamu.

View attachment 3242769
Hivi hawa wataalamu wa madini wanaokotwa majalalani au mkuu wa Mkoa au Wilaya anaweza kuwa MTU yeyote
 
Hahahaha unamuweka lockup kwa Sheria ipo?
Kwahiyo ukimdharau RC au DC basi wanabaki kisheria yakukuweka lockup?

Zipo taratibu za kumuadhibu mtumishi mtovu wa nidhamu, hizo ndio taratibu?
Hajamdharau,ni kwamba jamaa alikosa majibu eti hilo ni kosa la kumuweka ndani,mi nazan la kumtoa kwenye ukuu wa chuo lilitosha
 
Mkuu wa Wilaya ya Nzega Naitwapwaki Tukai ameliagiza Jeshi la polisi kumkamata na kumuweka ndani Abraham Lwakajunguti ambaye ni mkuu wa chuo cha mmDadini Lusu kilichopo wilayani Nzega kwa madai ya utovu wa nidhamu akishindwa kutoa majibu mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora wakati walipokua kwenye mkutano wa hadhara alipotakiwa kutoa maelezo juu ya kikundi cha watu wanaoingia kuchimba madini ya dhahabu kwenye eneo la chuo hicho bila kuwa na leseni halali.

Kufuatia hali hiyo mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe Paul Chacha akaagiza mkuu huyo wa chuo aondolewe kwenye nafasi ya ukuu wa chuo hicho cha madini kutokana na utovu huo wa nidhamu.

View attachment 3242769
Hizo kima zinaturudisha miaka 100 nyuma, hawajui utawala Bora, wala utawala wa sheria.
 
Kuna kitu hakipo sawa pale mboka-manyema, matukio yamekua mengi.
 
Mkuu wa Mkoa Naona ni tatizo , huyu ni Mtendaji ambaye hata kabla ya kuja kwa wananchi angeeza kuongea naye Ili yasitokee . Ila huyu mkuu wa Mkoa kafanya haya
1. Kagombana na kapuya foundation
2. Meneja Gpsa
3.chuo Cha madini

Hapa nafikiri Ras ataliweka sawa
 
Ma DC na Ma RC sijui wanajionaga wao ni nani!

Mnajitutumua na vyeo vya kuteuliwa kwa sababu ya ukada! Na huku wananchi tukiwa tumeshavikataa kitambo kwenye Rasimu ya Katiba ya Jaji Warioba, kutokana na ukweli kwamba hivyo vyeo vimepitwa na wakati!
 
Hajamdharau,ni kwamba jamaa alikosa majibu eti hilo ni kosa la kumuweka ndani,mi nazan la kumtoa kwenye ukuu wa chuo lilitosha
Nijuavyo uteuzi wa mkuu wa chuo (kama ni cha seriali) unafanywa na Rais. Inashangaza mkuu wa mkoa/wilaya kumuagiza Rais atengue uteuzi wake. Nafikiri wa kutenguliwa ni wao kwa kosa la ‘insubordination’
 
Back
Top Bottom