DC Temeke: Mtu akipiga Picha na hela akamatwe

Wild Flower

JF-Expert Member
Joined
Jul 20, 2023
Posts
378
Reaction score
766
Mkuu wa Wilaya ya Temeke, Sixtus Mapunda amelagiza Jeshi la Polisi la Wilaya ya Temeke kukamata Watu wote ndani ya Wilaya hiyo ambao wanapiga picha na kujirekodi video wakiwa na hela kwenye mitandao ya kijamii waseme hizo hela wametoa wapi na kodi wamelipa kiasi gani.

Amesema "Mtu akipiga picha na mahela mengi kuonesha maisha ni rahisi namna hii kama ni wa Temeke kamata, hakuna hela uliyoitolea jasho ina majigambo, hela uliyotolea jasho inafichwa kama ambavyo Mtu hasemi nimepata mshahara"

Amesema hayo Julai 10, 2024 akiongea na wakazi wa Mbagala juu ya mmomonyoko wa maadili na matukio ya kiuhalifu. Akisistiza kuwa wanaopost za hela huwashawishi vijana kujihusisha na madawa ya kulevya au ushirikina.

Your browser is not able to display this video.
 
Hii ndio Taarifa mpya kutoka kwa DC wa Temeke Sixtus Mapunda, aliyoitoa kwa Wakazi wa Wilaya hiyo, bado hatujajua kama hicho nacho ni Kipaumbele cha maendeleo na wala hatujajua pia Sheria ambayo inavunjwa na vibopa hao wa mitandaoni, Pia hatukuambiwa kupost mwisho sh ngap ama hata kupost elfu 5 pia ni kosa.

Bali tunatoa wito kwa wote wenye kiherehere cha kufanya hivyo, akiwemo DOTTO MAGARI kwamba wasithubutu kuja Temeke, watadakwa kama kuku mwenye mdondo

Taarifa kamili hii hapa

 
Siungi mkono haya mambo ya kupiga picha na fedha, ila sasa wakamatwe kwa kosa gani? Pesa yangu nimeitoa bank nikapiga nayo picha wakati nikienda fanya nilichokusudia sasa unikamate kwa kosa gani? Haya masuala ya viongozi kutoa matamko ambayo hata hayaendani na sheria na polisi wakayatekeleza yamekuwa mazoea tu.
 
Mkubwa akishasema ni amri
 
Mbona kama vile kwa mbaaaaali hapa analengwa Dotto Magari na Wenzake wengine Wazee wa Kuringishia Watu Pesa?
 
uhuru unazidi kuminywa.yani ni chore picha ya chura alafu niambiwe ni raisi kweli
 
Wakamatwe kwa sheria gani?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…