Deal ya Ali Kiba na Sony: Makosa yanayojirudia..

Deal ya Ali Kiba na Sony: Makosa yanayojirudia..

Na wewe kwa akili yako hivi unaamini akina Nakaya,Rose Muhando wamechuja kisa walisaini mikataba na Sony au mtu kama D'banj kaisha kisanii kisa yupo lebo ya Kanye West? Tusiwe tunakariri kuwa msanini ataendelea kuwa juu milele na hawezi chuja kisanii yani zama zako kisanii zikipita huwa hazijirudii tena

Hebu ajiulize tu Vanilla Ice/ Mc Hammer/ Ja Rule/ DMX na wengineo wako wapi hivi sasa na wanafanya nini...
 
Na wewe kwa akili yako hivi unaamini akina Nakaya,Rose Muhando wamechuja kisa walisaini mikataba na Sony au mtu kama D'banj kaisha kisanii kisa yupo lebo ya Kanye West? Tusiwe tunakariri kuwa msanini ataendelea kuwa juu milele na hawezi chuja kisanii yani zama zako kisanii zikipita huwa hazijirudii tena


yale yale ukiwa na management mbovu lazima uteleze tu nakaya alikuwa na muda gani ktk game? unawezeje kusema zama zake zimekwisha? sugu na afande sele utawaitaje?
 
Mtafikiri hiyo mikataba mnaionaga hahahhahah....mnajua kilichoandikwa ndani?? Hivi ali kiba mnawafananisha na akina nakaaya ...ku sign contract inategemea na wewe juhud zako sasa kama ume sign lebo kubwa halaf umekalisha makalio yako bila juhud binafs kuendelea kua juu unafikr utaacha kutokuangukaaa....tumien le akiliz kubwaaz ...alaaah
Mkuu nakusamehe bure kwakuwa hujui ulisemalo
 
e6fdb0fb2ac23a2d50fef18dd0bd2e36.jpg



Soma hii wewe
 
Kumuona ambae haumpendi akipiga hatua mbele hua inaleta maumivu sana ndio maana sishangai vijana waliotoboa tunawatangazia kua ni drug dealers,Freemasons nk mara nyingi sisi wenye chuki hatukosi sababu za kumkosoa tusiempenda hasa akiwa anasonga mbele ndio faraja pekee kwetu tumejaa chuki,wivu na umaskini.
Nikutakie kila la heri kijana mpambanaji kwenye kusaka mafanikio na kamwe usiogope haters maana wapo kibao,Ali K walianza na menagement yako wakasema sana na leo watakomaa na ishu ya Sony ilimradi tu ukate tamaa acha kuangalia walioanguka wewe songa mbele Mungu akufanyie wepesi kwenye hustle zako na jitihada zako ndio njia ya mafanikio.
 
Huko kwenye mitandao ya kijamii kumechafuka habari ya Ali kusign deal na Sony wengi wakiamini huo ndio utakuwa mwanya wa msanii huyo kutoboa kimataifa.. Jambo ambalo mashabiki wake wanashindwa kuelewa ni kuwa huo unaweza kuwa anguko la King Kiba badala ya kuwa neema..

Kwanza kabisa kitu ambacho hawakielewi ni kuwa Ali hajasaini na Sony Music Ent. BMG (ishu yake sio 'global deal') bali amesaini na Sony Music Africa ambayo ni subsidiary ya Sony Music Entertainment!! Kwa ninavyoelewa Sony Music Africa wana sambaza mziki na kumanage wanamuziki ndani ya Africa pekee.. Sasa eidha Ali hajui alichosaini au chumvi inaongezwa kunogesha habari..

Kingine watu wanaona hii ni kama Bahati Ali amepata wanachoshindwa kuelewa ni kwamba wasanii wakubwa Africa huwa wanakataa kusign na hizi kampuni zenye asili ya marekani na ulaya kutokana na kampuni hizi kushindwa kutimiza malengo na kutoelewa mazingira ya soko la mziki Africa! Kwa mfano wasanii wote ambao wamewahi kusign na Sony karibia wote walikuja kufa kimuziki kutokana na Sony kushindwa kuwa market kutokana na kutoelewa mziki wa Africa; mfano wasanii kama Nakaaya Sumari, Nneke Egbuna (Nigeria), Luncvile (SA), Nathan Ro (SA) wote hawa wamepotea kwenye mziki..

Mfano mwingine ni msanii D'banj ambaye aliondoka Mavins na kujiunga na label ya GodLife chini ya kanye west, mpaka sasa D'banj anasafiria jina lake tu lakini kimuziki ameshuka vibaya sana!! Kampuni za kimarekani hazina record ya kuwatoa wasanii wa kiafrika na hii inatokana na kutoelewa industry yetu na ndio maana Psquare walikataa mabilioni waliyotaka kupewa ili wasign Convict records..

Kingine kinachosemwa na watu ni kwamba hizi kampuni zina mambo mengine makubwa zaidi kwahiyo inakuwa nguvu kwao kuwa serious sana na mwanamuziki mmoja mmoja; kwa mfano kampuni mama ya Sony Music Africa (Sony Entertainment BMG) ina zaidi ya label 25 ndogo ndogo kama hii aliyosign kiba na ina wasanii karibia katika kila nnchi ya ulaya, Asia na Amerika ya kusini. Wana zaidi ya wasanii elfu moja wanaowasimamia so inakuwa ngumu kwao kutoa macho kwa msanii mmoja mmoja na ndio maana wasanii wengi wakubwa wa Africa wanakataa kusign chini yao wanaona ni afadhali watengeneze timu zao wenyewe za management ambazo macho yao na attention yote itakuwa kwao wao kama wasanii..

Anyways, let me just assume management ya Ali inafahamu vitu ambavyo mimi sivifahamu na wamefanya research ya kutosha kabla ya kusign na hatimaye watatuprove wrong wote ambao tuko sceptical about this deal.!!
Kama kijana mwenzangu namtakia kilala kheri na mafanikio katika safari yake mpya...

Una hakika?
uploadfromtaptalk1463670821137.png
 
Wabongo tumezoea kukurupuka hasa kwenye kusaini mikataba....wengi hawasomi mikataba na pia hawaielewi!!
 
Huko kwenye mitandao ya kijamii kumechafuka habari ya Ali kusign deal na Sony wengi wakiamini huo ndio utakuwa mwanya wa msanii huyo kutoboa kimataifa.. Jambo ambalo mashabiki wake wanashindwa kuelewa ni kuwa huo unaweza kuwa anguko la King Kiba badala ya kuwa neema..

Kwanza kabisa kitu ambacho hawakielewi ni kuwa Ali hajasaini na Sony Music Ent. BMG (ishu yake sio 'global deal') bali amesaini na Sony Music Africa ambayo ni subsidiary ya Sony Music Entertainment!! Kwa ninavyoelewa Sony Music Africa wana sambaza mziki na kumanage wanamuziki ndani ya Africa pekee.. Sasa eidha Ali hajui alichosaini au chumvi inaongezwa kunogesha habari..

Kingine watu wanaona hii ni kama Bahati Ali amepata wanachoshindwa kuelewa ni kwamba wasanii wakubwa Africa huwa wanakataa kusign na hizi kampuni zenye asili ya marekani na ulaya kutokana na kampuni hizi kushindwa kutimiza malengo na kutoelewa mazingira ya soko la mziki Africa! Kwa mfano wasanii wote ambao wamewahi kusign na Sony karibia wote walikuja kufa kimuziki kutokana na Sony kushindwa kuwa market kutokana na kutoelewa mziki wa Africa; mfano wasanii kama Nakaaya Sumari, Nneke Egbuna (Nigeria), Luncvile (SA), Nathan Ro (SA) wote hawa wamepotea kwenye mziki..

Mfano mwingine ni msanii D'banj ambaye aliondoka Mavins na kujiunga na label ya GodLife chini ya kanye west, mpaka sasa D'banj anasafiria jina lake tu lakini kimuziki ameshuka vibaya sana!! Kampuni za kimarekani hazina record ya kuwatoa wasanii wa kiafrika na hii inatokana na kutoelewa industry yetu na ndio maana Psquare walikataa mabilioni waliyotaka kupewa ili wasign Convict records..

Kingine kinachosemwa na watu ni kwamba hizi kampuni zina mambo mengine makubwa zaidi kwahiyo inakuwa nguvu kwao kuwa serious sana na mwanamuziki mmoja mmoja; kwa mfano kampuni mama ya Sony Music Africa (Sony Entertainment BMG) ina zaidi ya label 25 ndogo ndogo kama hii aliyosign kiba na ina wasanii karibia katika kila nnchi ya ulaya, Asia na Amerika ya kusini. Wana zaidi ya wasanii elfu moja wanaowasimamia so inakuwa ngumu kwao kutoa macho kwa msanii mmoja mmoja na ndio maana wasanii wengi wakubwa wa Africa wanakataa kusign chini yao wanaona ni afadhali watengeneze timu zao wenyewe za management ambazo macho yao na attention yote itakuwa kwao wao kama wasanii..

Anyways, let me just assume management ya Ali inafahamu vitu ambavyo mimi sivifahamu na wamefanya research ya kutosha kabla ya kusign na hatimaye watatuprove wrong wote ambao tuko sceptical about this deal.!!
Kama kijana mwenzangu namtakia kilala kheri na mafanikio katika safari yake mpya...
Kaka najua unaongea ukweli sana ila sijajua kama hakuna msanii aliyefanikiwa akiwa na sony....kufanikiwa kwa mtu hakutokani na matokeo taliyopita ila ni kufanya kazi kwa bidiii.....ulichoongea kina ukweli sana sana ila huyu ni ali kiba nikumuombea kwa mungu afanikiwe ili wengine nao wafuate nyayo zake....ali kiba atatakiwa kufanya kazi bora sana sana....jambo la kuwa na sony ni its easy kufanya kolabo maana una status tayari na sony watakuunganisha vizuri.....hili deal linaweza kuwa na distribution ya kazi zake tu,videos na mauzo ya album
Dili bado halijajulikana sana so lets wait n see mambo yaliyopo sony navyojua hawa manage msanii. Msanii itakuwa bado yupo na management yake ila wao wanakukuza zaidi tu
 
Na wewe kwa akili yako hivi unaamini akina Nakaya,Rose Muhando wamechuja kisa walisaini mikataba na Sony au mtu kama D'banj kaisha kisanii kisa yupo lebo ya Kanye West? Tusiwe tunakariri kuwa msanini ataendelea kuwa juu milele na hawezi chuja kisanii yani zama zako kisanii zikipita huwa hazijirudii tena
Asante mkuu
 
Mi hata sikutegemea kukutana na haya!!!!! Mbona mpo ivyo nyie binadamu lakini? Hatakiwi afanye chochote yeye? Kila afanyalo anavutwa kurudishwa nyuma!? Kinawaumae? Basi riziki hupanga Mungu... Muacheni na maisha yake...
 
Hata Rose Muhando siku hizi avumi tena na ni baada ya kuingia mkataba na hao so called Sony...
Sijui alibweteka au ndio anavyosema mdau...hawana ujuzi wa ku market kama kina Babu Tale (kwi kwi kwi)
 
.......Kwanza kabisa kitu ambacho hawakielewi ni kuwa Ali hajasaini na Sony Music Ent. BMG (ishu yake sio 'global deal') bali amesaini na Sony Music Africa ambayo ni subsidiary ya Sony Music Entertainment!! Kwa ninavyoelewa Sony Music Africa wana sambaza mziki na kumanage wanamuziki ndani ya Africa pekee.. Sasa eidha Ali hajui alichosaini au chumvi inaongezwa kunogesha habari......
...

Mkuu "The Bold" kwa taarifa tu ni kwamba Sony BMG ilikuwa ni kampuni ya muziki (Music and Entertainment company) ambayo ilikuwa ikimilikiwa kwa ubia wa asilimia 50-50 kati ya Sony Corporation of America (SCA) na Bertelsmann AG (BMG). Kampuni hiyo ya Sony BMG ilianzishwa March 3, 2004 (Miaka 12 Iliyopita) lakini ilipofika tarehe 1/October/2008 (Miaka 7 iliyopita) Sony Corporation walinunua asilimia 50 ya hisa zilizokuwa zikimilikiwa awali na Bertelsmann AG (BMG) na hivyo kuifanya Sony BMG kuwa chini ya Sony Coporation of America kwa asilimia 100 na jina lake kubadilika na kuwa Sony Music Entertainment (SME).

Ikumbukwe ya kwamba kampuni ya Sony BMG ilikuwa mmiliki wa recording labels mbalimbali kama vile Arista Records, Columbia Records, Epic Records, J Records, Mchenry Records, Jive Records, RCA Victor Records, RCA Records, Legacy Recordings, Sonic Wave America, na nyinginezo nyingi na hivyo, mabadiliko haya (Ya mwaka 2008) yaliathiri matawi yote ya Sony BMG duniani kote isipokuwa kwa Japan ambapo waliona kuwa mabadiliko ya aina hiyo yangepelekea kupunguza kwa kiasi kikubwa ushindani katika sekta ya muziki wa nchi hiyo. Kwa maana hiyo Sony Music Entertainment Japan (SMEJ) ni tawi la Sony Music Entertainment (Iliyokuwa awali Sony BMG) lakini hufanya shughuli zake bila kuathiriwa na sera za Sony Music Entertainment of America ambayo ndiyo kampuni mama....

Hata ukiangalia kwenye list ya wasanii waliosainishwa chini ya Sony Music (fuata link hii https://en.wikipedia.org/wiki/List_of_Sony_Music_artists yapo majina ya wasanii wote ulimwenguni (e.g. Beyonce, Britney spears, Bow Wow, Avicii, drake, Alikiba na wengine wengi) ambao wako chini ya Sony Music.

Kwa mantiki hiyo, dili alilosaini Alikiba siyo kwa Africa pekee bali it’s a Global deal. MUNGU AMTANGULIE.
 
Kwanza sijasema eti nakaaya, rose n.k wamesaini Sony ambayo ni based Africa!! Nakaaya, rose, davido n.k walisaini na Sony Music Ent. BMG na kiba amesaini na Sony Music Africa ambayo ndio ina manage Keko n.k ( notice the difference) lakini all in all Sony zote hizi hazina reputation nzuri katika kumanage wasanii wa Africa..

Tuje kwenye hoja yako, ofcoz sijauona mkataba lakini waswahili wanasema 'hatakama kusoma hujui lakini macho ya kuona umepewa', kwa kifupi niko karibu sana na music industry kwasababu za kibiashara so I know all the sh*t that's in there and I know the rules.. So sijauona mkataba lakini naweza kuimagine skeleton yake ikoje!!
"So sijauona mkataba lakini naweza kuimagine skeleton yake ikoje" hapa ndo umeprove failure huwezi kuimagine kitu kilichokuzidi uwezo afu unasema upo karibu na music industry ukiwa kama nani producer,manager,dj,distributor,au una dili na mikataba ya wasanii? Si lazima kuweka ujuaji kwenye kila kitu
 
Back
Top Bottom