Debate: Kuajiriwa Vs Kujiajiri

Debate: Kuajiriwa Vs Kujiajiri

Good wish to all

Moja ya definition ya maisha ni mapambano na moja ya definition ya mafanikio ni ushindi,

Nilikuwa natafakari kitu nikasema ngoja nishare na home of great thinker. Dunia ya sasa watu wengi sana tunahimizwa kujiajiri hasa kipindi hiki cha tatizo la kidunia la ajira.

Hoja yangu, wapo watu wameajiriwa serikalini na sekta binafsi na wanalipwa mshahara mzuri tu may be 3m ambao kwa tz unaweza ukaishi vizuri sana wanahimizwa wajiajiri ambapo kwenye upande wa kujiajiri ni biashara chache sana zinaweza kukupa pato hilo kwa mwezi kama faida na tena sio uhakika. Na kwa nn mtu akiamua kuajiriwa na akatumia sehemu ya kipato chake kujiajiri wengi wao huwa wanapitwa mafanikio na watu waliocha ajira na wakajiajiri completely. Kuna siri gani katika ulimwengu wa kujiajiri ambao unamtaka mhusika awe direct involve kwenye hicho alichojiajiri na mafanikio yake.

Au kujiajiri ni overarated?
Au kuajiriwa ni underated? or it depend with month salary?
Kuna siri gani iliyojificha nyuma ya kujiajiri ambayo ni msingi wa mafanikio. Kuna mtu aliacha kazi yenye mshahara wa 6m plus bonus akaenda kujiajiri.
Je mishahara ya kwa mwezi na faida za kwenye biashara zote zikiwa sawa nini kitatokea Nani atakuwa amewin na nani atakuwa amelose.
Mlioacha kazi na mkajiajiri tupeni hizo siri na sisi tufanikiwe.

Help me guyz
Kujiajiri ingekuwa rahisi maccm yasingekuwa yanaiba kura na kuua watu ili yatangazwe mashindi.
 
Ni vizuri sana kujiweka kwenye position ya KUYAWEZA YOTE kwa wakati mmoja au tofauti,
Zote ni mbinu za utafutaji na zote zina mafanikio tegemea hali yako, mazingira husika, uwezo husika n,k

HAKUNA TOFAUTI ZA MSINGI KATI YA KUAJIRIWA NA KUJIAJIRI
Kama hakuna tofauti ya kuajiriwa na kujiajiri kwa nini watu wengi wenye mafanikio makubwa ni walio upande wa kujiajiri???
 
Good wish to all

Moja ya definition ya maisha ni mapambano na moja ya definition ya mafanikio ni ushindi,

Nilikuwa natafakari kitu nikasema ngoja nishare na home of great thinker. Dunia ya sasa watu wengi sana tunahimizwa kujiajiri hasa kipindi hiki cha tatizo la kidunia la ajira.

Hoja yangu, wapo watu wameajiriwa serikalini na sekta binafsi na wanalipwa mshahara mzuri tu may be 3m ambao kwa tz unaweza ukaishi vizuri sana wanahimizwa wajiajiri ambapo kwenye upande wa kujiajiri ni biashara chache sana zinaweza kukupa pato hilo kwa mwezi kama faida na tena sio uhakika. Na kwa nn mtu akiamua kuajiriwa na akatumia sehemu ya kipato chake kujiajiri wengi wao huwa wanapitwa mafanikio na watu waliocha ajira na wakajiajiri completely. Kuna siri gani katika ulimwengu wa kujiajiri ambao unamtaka mhusika awe direct involve kwenye hicho alichojiajiri na mafanikio yake.

Au kujiajiri ni overarated?
Au kuajiriwa ni underated? or it depend with month salary?
Kuna siri gani iliyojificha nyuma ya kujiajiri ambayo ni msingi wa mafanikio. Kuna mtu aliacha kazi yenye mshahara wa 6m plus bonus akaenda kujiajiri.
Je mishahara ya kwa mwezi na faida za kwenye biashara zote zikiwa sawa nini kitatokea Nani atakuwa amewin na nani atakuwa amelose.
Mlioacha kazi na mkajiajiri tupeni hizo siri na sisi tufanikiwe.

Help me guyz

Usitenganishe wala kutofautisha kati ya kujiajiri na kuajiriwa vyote vinategemeana, na vyote ni muhimu, pia elimu ya chuo ya kuhitimu haikufanyi uchague ajira au uchague utavuna kipato kwa njia gani elimu ni msingi na ufunuo wa mambo mengi knowledge is power,

Ni vyema uajiriwe then ujiajiri yani ufanye vitu hivi kwa wakati mmoja au pia umalize kimoja uje kingine elimu yako iwe ya kuongeza ubunifu juu ya mambo hayo mawili,

Ukiajiriwa utapata mengi ili uje kujiajiri, ajira itakupa exposure, utapata mtaji na pia utafahamiana na wengi yani utajenga network ya watu, utajiri namba moja duniani ni kuwa na network, kwahiyo msidharau kuajiriwa ni vyema kutambua mambo haya ni yanakujengea kuja kuwa tajiri kama una malengo tu
 
Sasa kama elimu ni msingi kuwa mfanyabiashara mbona wapo watu wengi tu hawana elimu na ni wafanyabiashara waliofanikiwa.
Mbona hata hao wasomi wa biashara bado hatuwaoni kwenye kurasa za mbele za mafanikio.

Moja ya speech ya Steve Jobs ni kuwa anajuta kusoma college kwani imempotezea muda so it means haijamsaidia kitu.

Ni mfumo upi wa elimu utumike uzalishe wajasiriamali??
Nachojua ni kuwa mfumo wetu wa elimu tumeuchukua kwa hao waliofanikiwa so whats wrong??
Elimu sio lazima ikusadie, bali wewe ndiyo uisadie elimu sijui kama unanielewa lakini...
 
mjadala mzuri lakn wachangiaji wako kwenye zile nyuzi zetu pemdwa za ulishwahi kula tunda kimasiara... huku hawana habar nako..
Waache banah kila mmoja wetu ana vipaumbele vyake katika maisha, usifikie hatua kuwalazimisha watu waje kuchangia, mwingine yupo jf hapa akipata likes nyingi tu yeye kwake ni faraja, so wewe uliekuwepo hapa jadili mada,
 
Kuajiriwa ni Hulka ya mtu muoga na mvivu kimwili na kiakili na kujiajiri ni Hulka ya mtu mchapakazi na mwenye uwezo mkubwa kiakili na uthubutu wa kuona na kuzitumia fursa ipasavyo.. PERIOD!!

Kuajiriwa ni hulka ya mtu muoga? Mbona unapotosha watu, hivi mtu kamaliza chuo hana hata mtaji anaanzaje kujiajiri, na pia ni biashara chache sana nimeona zikifanikiwa mtu akope anaanza biashara, mikopo iwe ya kuongeza nguvu tu kwenye biashara
 
Kama hakuna tofauti ya kuajiriwa na kujiajiri kwa nini watu wengi wenye mafanikio makubwa ni walio upande wa kujiajiri???
Ni vile huwajui au sbb nchi yetu ni dhaifu sana kwenye UJASIRIAKAZI, hata UJASIRIAMALI nidhaifu

Nikupe mfano mmoja tu uliza mshahara wa CEO wa Safaricom then utafute matajiri wafanyabiashara wa kitanzania wenye kipato hicho,
 
Ni vile huwajui au sbb nchi yetu ni dhaifu sana kwenye UJASIRIAKAZI, hata UJASIRIAMALI nidhaifu

Nikupe mfano mmoja tu uliza mshahara wa CEO wa Safaricom then utafute matajiri wafanyabiashara wa kitanzania wenye kipato hicho,
Nimekuelewa mzee
 
Ni vile huwajui au sbb nchi yetu ni dhaifu sana kwenye UJASIRIAKAZI, hata UJASIRIAMALI nidhaifu

Nikupe mfano mmoja tu uliza mshahara wa CEO wa Safaricom then utafute matajiri wafanyabiashara wa kitanzania wenye kipato hicho,
Umewahi kujiuliza mwenye hiyo safaricom anaingiza shilingi ngapi kwa mwezi? Au unadhani safaricom haina mmiliki ?
 
Mfanyabiashara anayepata Faida TZS 1,500,000/- na mwajiriwa anayepata mshahara TZS 1,500,000/- hawana tofauti ya mapato kwa mwezi. Issue ni matumizi ya Faida wanayopata kwa mwezi. Hilo Moja!

Jambo la pili namna kila mmoja anajiongeza kujazia kipato. Mfanyabiashara kukuza biashara yake na mwajiriwa kuwa na kipato Cha ziada. Then tunarejea pale pale, matumizi yakoje?

Ima tuweke Hili jedwali yaishe!
______&&&&&:&&Kipato. Matumizi
Mfanyabiashara
Mwajiriwa
Hapa kwa kuongezea nyama umeongelea discipline ya pesa katika jambo la matumizi, pia ni nguzo ya mafanikio, pesa unayotumia zaidi pasipo utunza na kuzalisha ni bure kutegemea kuona ni yenye tija
 
Kumbuka hili

Ukifa umeajiriwa watoto wako hawatarithi ajira yako ila ukifa una biashara watoto wako watarithi biashara zako.
Usiongelee kwa nadharia tu fikirisha pia wazo lako kivitendo.. Ni kwanini ajira yako ionekane inakuja kuwaandalia watoto wako urithi kwaninj urithi umeweka hapa katika kuchugua mkondo wa kipato yani uchague kujiajiri hata kama mambo yamegoma ili tu watoto waje kurithi,fanya na zalisha kitu unachoona utaweza kukujengea utajiri, swala la watoto wekeza snaa kwenye elimu yani fanya elimu iwe mrithi wa kwanza, tafuta shule zitakazo wajenga watoto wako waje kujitegemea na sio tegemezi kwenye mirathi yako, wazazi wengi tunaanguka hapa zaidi.
 
Back
Top Bottom