Debate: Kuajiriwa Vs Kujiajiri

Debate: Kuajiriwa Vs Kujiajiri

hapana fafanua mkuu
Nilimaanisha hivi wewe kuisaidia elimu ni wewe kama zao la waliopata elimu basi ukalete chachu ya maendeleo

Kuna elimu ambayo ni informal na elimu formal... Informal ni elimu ya kuzaliwa, na formal elimu ni elimu ya darasani.... Sasa mafanikio hayategemei sana uwe na elimu bali elimu inakutegemea wewe kupata mafanikio unayoyataka... Dunia ina kila kitu fursa, changamoto ni wewe tu inakufanya sasa kuvitumia na kuleta mafanikio.
 
Safari com ni corporate mzee

Jamii wakati mwingine inadanganywa sana na hawa watu wanaitwa "Motivation speakers"
Mkuu point yako ni kuwa Hakuna Wafanyabiashara wanaotengeneza faida ya mshahara wa CEO wa safaricom au ?

Kuna Wafanyabiashara ninawajua hapo kariakoo wanatengeneza zaidi ya milion 200 Kama faida kwa mwezi mmoja.
 
Usiongelee kwa nadharia tu fikirisha pia wazo lako kivitendo.. Ni kwanini ajira yako ionekane inakuja kuwaandalia watoto wako urithi kwaninj urithi umeweka hapa katika kuchugua mkondo wa kipato yani uchague kujiajiri hata kama mambo yamegoma ili tu watoto waje kurithi,fanya na zalisha kitu unachoona utaweza kukujengea utajiri, swala la watoto wekeza snaa kwenye elimu yani fanya elimu iwe mrithi wa kwanza, tafuta shule zitakazo wajenga watoto wako waje kujitegemea na sio tegemezi kwenye mirathi yako, wazazi wengi tunaanguka hapa zaidi.
Huo ndio ukweli mchungu, ajiriwa ufe uone familia yako itarithi nini. Na fanya biashara ufe uone familia yako itarithi nini.


Tuongelee kwa muktadha wa mazingira ya kitanzania. Kuna familia kadhaa tunazijua baba au mama walikuwa Ni watumishi wa ajira nzuri ila baada ya vifo vyao familia zimebaki hohe hahe.

Elimu pekee kwa mtoto kwa TANZANIA sio sababu ya yeye kufanikiwa.
 
Nilimaanisha hivi wewe kuisaidia elimu ni wewe kama zao la waliopata elimu basi ukalete chachu ya maendeleo

Kuna elimu ambayo ni informal na elimu formal... Informal ni elimu ya kuzaliwa, na formal elimu ni elimu ya darasani.... Sasa mafanikio hayategemei sana uwe na elimu bali elimu inakutegemea wewe kupata mafanikio unayoyataka... Dunia ina kila kitu fursa, changamoto ni wewe tu inakufanya sasa kuvitumia na kuleta mafanikio.
Uko too theoretical jamaa, elimu bila other supportive means za kujikomboa hutusui.
 
Nikiwa rais wa tanzania , kuna vitu ntavifanya ili kila mtu aelewe nini maana ya kuajiliwa na kujiajili maana kuna watu wanaongea maneno tu ila hawaelewi.
1 kustaafu kwa lazima iwe serikalini au private itakuwa miaka 45
2 hakuna ukoo utakayoruhusiwa kupata ajira serikalini kwa zaidi ya watu 10, kwa wakati mmoja, waliopata ajira muwasaidie wengne mitaji.
3 Ntafuta elimu ya theory sana, practical sana.
4 Ntaanzia real practical field, kama unasoma biashara uende sokoni ufanye biashara na ulete faida. Usipopata faida unacarry , kilimo waende mashambani huko walime na wapate, wao wasivune, na wengine wote kulingana na kada zao.
 
Tatizo ni utayari na uthubutu wengi tunaona nikifanya kazi hii fulani atanionaje so inshort uthubutu na utayari ndo unatukwamisha wengi
Yes lazima kuwa na sehemu ya kuanzia bila kuchagua asili au aina ya kazi
 
Uko too theoretical jamaa, elimu bila other supportive means za kujikomboa hutusui.
Umesoma post yangu lakini bado hujanielewa... Mimi sijaweka elimu kuwa chombo kitakacho mpatia mtu utajiri. Bali nimeweka makundi ya elimu na namna kila moja yanavyoleta mchango kwenye kupiga hatua....
 
Good wish to all

Moja ya definition ya maisha ni mapambano na moja ya definition ya mafanikio ni ushindi,

Nilikuwa natafakari kitu nikasema ngoja nishare na home of great thinker. Dunia ya sasa watu wengi sana tunahimizwa kujiajiri hasa kipindi hiki cha tatizo la kidunia la ajira.

Hoja yangu, wapo watu wameajiriwa serikalini na sekta binafsi na wanalipwa mshahara mzuri tu may be 3m ambao kwa tz unaweza ukaishi vizuri sana wanahimizwa wajiajiri ambapo kwenye upande wa kujiajiri ni biashara chache sana zinaweza kukupa pato hilo kwa mwezi kama faida na tena sio uhakika. Na kwa nn mtu akiamua kuajiriwa na akatumia sehemu ya kipato chake kujiajiri wengi wao huwa wanapitwa mafanikio na watu waliocha ajira na wakajiajiri completely. Kuna siri gani katika ulimwengu wa kujiajiri ambao unamtaka mhusika awe direct involve kwenye hicho alichojiajiri na mafanikio yake.

Au kujiajiri ni overarated?
Au kuajiriwa ni underated? or it depend with month salary?
Kuna siri gani iliyojificha nyuma ya kujiajiri ambayo ni msingi wa mafanikio. Kuna mtu aliacha kazi yenye mshahara wa 6m plus bonus akaenda kujiajiri.
Je mishahara ya kwa mwezi na faida za kwenye biashara zote zikiwa sawa nini kitatokea Nani atakuwa amewin na nani atakuwa amelose.
Mlioacha kazi na mkajiajiri tupeni hizo siri na sisi tufanikiwe.

Help me guyz
Ajira inaweza kutumika kukupa mtaji kuanzisha mradi,cha msingi uwe makini katika kusimamia mradi ,tathmini ya Mara kwa mara ni muhimu kubuni njia mbalimbali kukuza mauzo na kuboresha bidhaa,matangazo ya bidhaa bila kuchoka vipeperushi ,business cards,feedback toka kwa wateja na kufanyia kazi maoni,maintain database ya wateja namba za simu,email nk,matumizi ya social media, bonu na offer kwa wateja,ndizo njia ninazo tumia kuzalisha faida ya 250,000/= kwa siku.
Jambo muhimu sana kuliko yote ni kuajiri mtu makini sana meneja wa mradi hakikisha unapata mda wa kutosha kumtathimini andaa machaguo mawili hadi mataa.
Tumia watu wenye elimu ya chini sana,darasa la saba au form 4
 
Mkuu point yako ni kuwa Hakuna Wafanyabiashara wanaotengeneza faida ya mshahara wa CEO wa safaricom au ?

Kuna Wafanyabiashara ninawajua hapo kariakoo wanatengeneza zaidi ya milion 200 Kama faida kwa mwezi mmoja.
CEO Safari com mshahara wake kwa mwezi ni Tsh 330 mln ni sawa na Tsh 11 mln kwa kila siku moja
haya sasa ni wafanya biashara wantanzania wana kipato kama hicho ? ni kutoelewa tu HAKUNA TOFAUTI YA KUAJIRIWA NA KUJIAJIRI ni preferences tu

Gideon Muriuki

Gideon Muriuki, CEO Cooperative Bank: He is the highest paid CEO in Kenya. Last year, his annual pay increased to Sh. 376.4 million.7 Ago 2020

 
CEO Safari com mshahara wake kwa mwezi ni Tsh 330 mln ni sawa na Tsh 11 mln kwa kila siku moja
haya sasa ni wafanya biashara wantanzania wana kipato kama hicho ? ni kutoelewa tu HAKUNA TOFAUTI YA KUAJIRIWA NA KUJIAJIRI ni preferences tu

Gideon Muriuki

Gideon Muriuki, CEO Cooperative Bank: He is the highest paid CEO in Kenya. Last year, his annual pay increased to Sh. 376.4 million.7 Ago 2020

Kama pointi yako ni Wafanyabiashara wangapi wanaweza kutengeneza huo mshahara na mimi nakuuliza Ni waajiriwa wanangapi wanalipwa huo mshahara.


Halafu nenda katembelee Ile kampuni ya Marehemu Patel aliefariki wiki kadhaa zilizopita uone huwa anatengeneza Kiasi gani kwenye kampuni ... Yani milion 300 Wafanyabiashara washindwe kutengeneza kwa mwezi ??!!! Acha dharau
 
Usitenganishe wala kutofautisha kati ya kujiajiri na kuajiriwa vyote vinategemeana, na vyote ni muhimu, pia elimu ya chuo ya kuhitimu haikufanyi uchague ajira au uchague utavuna kipato kwa njia gani elimu ni msingi na ufunuo wa mambo mengi knowledge is power,

Ni vyema uajiriwe then ujiajiri yani ufanye vitu hivi kwa wakati mmoja au pia umalize kimoja uje kingine elimu yako iwe ya kuongeza ubunifu juu ya mambo hayo mawili,

Ukiajiriwa utapata mengi ili uje kujiajiri, ajira itakupa exposure, utapata mtaji na pia utafahamiana na wengi yani utajenga network ya watu, utajiri namba moja duniani ni kuwa na network, kwahiyo msidharau kuajiriwa ni vyema kutambua mambo haya ni yanakujengea kuja kuwa tajiri kama una malengo tu
Inategemeana na ajira au nafasi uliyopo. Unaweza kujenga network pia kwa kujiajiri.
 
Ni vile huwajui au sbb nchi yetu ni dhaifu sana kwenye UJASIRIAKAZI, hata UJASIRIAMALI nidhaifu

Nikupe mfano mmoja tu uliza mshahara wa CEO wa Safaricom then utafute matajiri wafanyabiashara wa kitanzania wenye kipato hicho,
Inategemea na position uliyopo. Kumtolea mfano CEO mmoja aimaanishi ajira zina mapato. Cha msingi kila mtu ashinde mechi zake
 
Back
Top Bottom