Deborah Fernandez ni mchezaji wa kawaida Sanaa, Simba Bado timu haijakaa vizuri tunajipa moyo tu

Deborah Fernandez ni mchezaji wa kawaida Sanaa, Simba Bado timu haijakaa vizuri tunajipa moyo tu

Kwanza kabla ya yote namshukuru Mungu Huwa nikileta mada hapa jamii sports, kwa mara ya kwanza watu Huwa wanaichukulia tofauti ila baada ya mda ukweli unadhibitika!!. fuatilia mada zangu za humu jamii sports utanielewa.

Sasa twendeni sambamba kwenye mada husika kama kichwa Cha habari hapo juu kinavyoeleza

Deborah Fernandez ni mchezaji ambaye Simba imemsajili miongoni mwa maingizo mpya misimu huu ila ulishawahi jiuliza kwanini ghafla sikuizi hapati nafasi?? na mara nyingi anaanzia benchi?

Huyu mwamba naweza kusema kwa pale Simba kwenye nafasi yake ambaye pia wapo watu kama okejepha, Ngoma, mzamiru na kagoma....yeye ndio mchezaji mwenye mchango mdogo kuliko hao wenzake kwanini??

Huyu jamaa sifa yake kubwa ni kufanya interception ya mipira TU, sio mzuri kwenye kupanda as box to box....Wala sio mzuri kwenye kupiga pasi sahihi ( mara nyingi pasi zake zinapotea kirahisi, usibishe fuatilia ), hivyo Hana sifa ya kuwa central midfielder.....kidogo kwenye DM (Defensive midfielder) anajitahidi kwa sababu ya uwezo wake mkubwa wa kufanya interception ila ni kwa asilimia kama 45% TU.

Kocha fadlu kumuanzisha Fernandez benchi sio kwa bahati mbaya ila Kuna vitu jamaa hampi ndio maana mara nyingi ana opt kuanza na okejepha na Ngoma.....Ngoma mzuri kwenye kupiga pass za hatari, okejepha mzuri kwenye interception na kufanya maamuzi ya haraka....hivi vitu kwa hawa wachezaji wawili Fernandez

Hana kabisa na ndio inanifanya kuanzisha hii thread, sio kwa chuki Wala kushurutishwa Bali ni kuona na kuutazama mpira kwa jicho la tatu

Mwisho, kama umeelewa hayo maelezo hapo juu, utakubaliana nami kuwa, Simba Bado shida kubwa IPO kwenye kiungo wa chini.....ahoua mnambebesha mzigo Bure TU!!!!

Wale viungo wawili wa chini Bado hamna mutual combination kabisa....kocha anachofanya nikujaribu TU nani akicheza na nani angalau ila tiba Bado haijapatikana

Mpaka Leo ni zaidi ya misimu mitatu tumekosa kabisa kiungo mkabaji asilia, tuliaminishwa okejepha, ila ni kiungo mkabaji asilia??? ( Ni uongo si ndio??? na mpira haudanganyi ).....angalau yufuph kagoma ila naye pancha nyingi sio wa kumtegemea Toka tupo Singida..

Mambo ni mengi mda mchache, ila kiufupi na kumalizia Simba Bado haijakaa vizuri kama wengi tunavyoaminishana, Tuombeane uzima TU na haya maoni viongozi wa Simba popote walipo wayachukue na kuyafanyia kazi.......NIMEMALIZA

remember the post 29/11/24
Atupokei ushauri wa motivation speaker things are change, Debora kuanzia benchi ni mbinu ya mwalimu kuisoma mechi dhidi ya mpinzani kwisha
 
Deborah anapenda kucheza na jukwaa akipata mpira lazima afanye uturn, pasi zake nyingi hazifiki inabidi afanye marekebisho Kama sio uharaka wa Camara alishatuchomesha.
 
Mashabiki sijui tunatatizo gani,ujuaji mwingi ,hata ungeambiwa umlete mchezaji unayemtaka na unapewa uwezo wa kifedha wa kumleta baada ya mda unaweza kumfukuza mwenyewe. Hakuna mchezaji aliyekamilika kama Fernandes ana mapungufu kiasi hicho ni mchezaji gani sasa pale Simba anafaa? Hebu tupunguze ujuaji wa kila kitu.
Mchezaji akifanya vzr atapewa sifa zake, na pia akikosea akubali kukosolewa ili kuongeza juhudi....unataka tuongee kinafki kumsifia mchezaji wakati hafanyi vzr??, makosa mengi???, siishi kwenye ulimwengu huo mkuu
 
Simba inahusika vipi yanga kukandwa? Sisi tunafanya yetu mkuu na nyie fanyeni yenu😂
Kwani nyie saivi wimbo si ubaya ubwela kwamba mko vizuri kauli ambazo zimeibuka gafla baada ya yanga kupoteza match 2 wakati mwanzo mlikua mnasema kwamba mnajenga team.
 
Back
Top Bottom