DED Magu angalia sana Idara ya Elimu Msingi

DED Magu angalia sana Idara ya Elimu Msingi

Hagwila,
Yaani hapa hata kama ni mtoto mdogo unaelewa tu kuwa huyo afisa anayesifiwa lazima yuko nyuma ya pazia katika kuandika habari hii.

Yaani wewe mmoja tu uwe msafi kuliko wote hao umekuwa Mungu?

Acheni kuchafua wenzenu kwenye mitandao ya kijamii.

Taratibu za kiutumishi ziko wazi.
 
Uongo! Uratibu milion kwa kipi? Mbn uratibu hauna mafungu yoyote? TUHUMA ZA KUPIKA.
 
Yaani hapa hata kama ni mtoto mdogo unaelewa tu kuwa huyo afisa anayesifiwa lazima yuko nyuma ya pazia katika kuandika habari hii.
Yaani wewe mmoja tu uwe msafi kuliko wote hao umekuwa Mungu?
Acheni kuchafua wenzenu kwenye mitandao ya kijamii.
Taratibu za kiutumishi ziko wazi.
Nyeusi ni nyeusi tu, ukiita nyeupe ni uongo; lakini ukiwa mnafiki unaweza kufanya hivyo ili kujifariji, lakini wenye kutambua mambo watang'amua.

Kanusha kwa hoja tuhuma zinazotolewa dhidi ya hao wanaolalamikiwa; na kama una malalamiko dhidi ya SLO aliyehamishwa yiweke bayana.

Tunajua taratibu za kiutumishi zipo lakini lazima ziwe na mahali pa kuanzia na panaweza kuwa hapa.

Tamaa ikikomaa huzaa dhambi, na dhambi ikikomaa huzaa mauti; huo ndio mtiririko. Mtaka nyingi nasaba, hupata mingi misiba.
 
Uongo! Uratibu milion kwa kipi? Mbn uratibu hauna mafungu yoyote? TUHUMA ZA KUPIKA
Wewe unauona Uratibu ni mdogo? Posho ya 250,000/= kila mwezi nje ya mshahara, pikipiki mpya na fuel allowance (sijui kiasi gani); watu wenye roho za korosho wanaumia!!
 
Yaani hapa hata kama ni mtoto mdogo unaelewa tu kuwa huyo afisa anayesifiwa lazima yuko nyuma ya pazia katika kuandika habari hii.
Yaani wewe mmoja tu uwe msafi kuliko wote hao umekuwa Mungu?
Acheni kuchafua wenzenu kwenye mitandao ya kijamii.
Taratibu za kiutumishi ziko wazi.
Hakuna mtu aliye nyuma ya pazia; malalamiko haya nimeyatoa mimi binafsi kutokana na historia ya mambo yanayoendelea kwenye ofisi ya DEO Magu tangu enzi za Salyankanga kabla hata huyu Afisa aliyehamishiwa Misungwi na Glory hawajaletwa Magu.

Afisa aliyehamishiwa Misungwi hajashushwa cheo na uhamisho wake amelipwa; ana sababu gani ya kuwa nyuma ya malalamiko yangu wakati amepata hela?

Mimi nimewasilisha malalamiko yangu kwa DED Magu kutokana na udhaifu unaoonekana kwenye ofisi ya DEO Magu wa rushwa, uonevu, unyanyasaji na majungu dhidi ya waalimu na watumishi wenye uwezo; mambo hayo hayana heri kwa mustakabali wa elimu ya watoto wetu wa wilaya ya Magu.

Siwezi kuwa DEO au afisa yeyote hapo halmashaurini; lakini mimi ni mzazi ambaye nahitaji wanangu na watoto wote wa Magu wapate elimu bora. Elimu hiyo bora itapatikanaje iwapo ofisi inayosimamia haiko sawa?
 
BrAsMaRiLiSaShElMa, Likewise nipo wilaya hii na nina malalamiko yangu ambayo majibu nipewayo ni ya hovyo sana. Hawa aliowataja ukiwa confront kwa hoja wanaona kama unawaonea kisa ni wanawake.
 
Likewise nipo wilaya hii na nina malalamiko yangu ambayo majibu nipewayo ni ya hovyo sana. Hawa wa.pumba.vu aliowataja ukiwa confront kwa hoja wanaona kama unawaonea kisa ni wanawake.
Mkuu kandukamo1; hawa watu wanakera sana; lakini ni heri kusema kuliko kunyamaza. Kama wanaendelea kukupa majibu yao ya hovyo hovyo, weka mambo hadharani kila mtu aone u.pumba.vu wao; anaweza kutokea mkombozi.

Mbona kuna wanawake ambao ni watumishi bora na mahiri sana kwa uwezo wao? Hao waliotajwa kwenye malalamiko haya hawana uwezo, ni "mizigo" tu ya watu huko mkoani wamepewa machaka. Ukiona mbwa yuko juu ya mti usidhani kapanda mwenyewe, kapandishwa huyo!!
 
Hata Geita DC imewaka moto matokeo ya Std VII 2019 kimkoa imeshika nafasi ya mwisho kutokana na DEO Said kuwavuruga walimu wakuu na kuwapoka madaraka. Rushwa ya ngono na kuwapa cheo walimu wakuu kwa M.1 kwake kawaida.

Mbaya zaidi kwenye kikao cha wenyeviti wa walimu wakuu kilichofanyika Dodoma alimuacha Mwenyekiti aliochaguliwa na walimu wakuu na kumpeleka Rafiki yake Mkuu kutoka katoro.

Kwa hiyo walimu wamekufa moyo wa ufundishaji. Jamaa anajiita yeye ni Afisa usalama. Serikali kazi kwenu.

Takukuru changamkeni.
Hao ndio tunaowatafuta hivi kwa nini watu wanapenda kuisingizia idara kuficha maovu?
 
Samahani kwa kudandia mada. Jana kuna walimu walikuja ofisini kwangu nikawasikia wakilalamika eti kwenye halmashauri yao kuna maofisa baadhi wameenda wao kusimamia mtihani wa kidato cha nne badala ya kuteua walimu ambao wako shule kila siku. Hii nayo imekaaje?
 
Samahani kwa kudandia mada. Jana kuna walimu walikuja ofisini kwangu nikawasikia wakilalamika eti kwenye halmashauri yao kuna maofisa baadhi wameenda wao kusimamia mtihani wa kidato cha nne badala ya kuteua walimu ambao wako shule kila siku. Hii nayo imekaaje?
Halmashauri gani?
 
Hagwila.
Nakupongeza kwa kuamua kuliweka wazi hili na inaonesha wazi upo well detailed, wahusika wakipita hapa au hata wakihitaji msaada wako “piyemu” bila shaka utawapa ushirikiano wa kutosha. Concern yangu ni huyo mbunge ambaye naona unamtaja kwa kurudiarudia kuonesha una imani naye.

Huyu mbunge wenu (Kiswaga) mbona ni kilaza mzuri tu zaidi ya umaarufu wa kibiashara na ku-take advantage ya raia wa “ndoho tabu”, japo hoja yako ni ya msingi sana na binafsi natamani kuona hiyo network ya kina Johari ikiwa overhauled. Pengine mwandikie ujumbe DED moja kwa moja au hata Jafo kwa njia ambayo ujumbe utawafikia.
 
Acha watu wazungumze kama ni majungu pita hivi
Mkuu namba force huyo anayesema majungu kazini hajui asemalo. Huyo Salyankanga alikuwa DEO wa hovyo sana aliyedidimiza kabisa morali ya waalimu wengi kwa sababu ya rushwa. Mawakala wake hapo ofisini walikuwa ni haohao wakina Johari, Prisca na kakijana kanaitwa Buhatwa ni kakiraka hapo vifaa na takwimu. Salyankanga hakuwa na aibu ya kuomba rushwa; alikuwa radhi kumgandamiza mwalimu mwenye elimu na uwezo, anayestahili madaraka kisa hajatoa rushwa, ama ya pesa ama ya ngono kama ni mwanamke.

Na alikuwa radhi kumpa madaraka mwalimu yeyote hata asiye na uwezo wa uongozi, ilimradi mwalimu huyo ametoa rushwa; kama alivyomtoa mwalimu Mary Maganga kutoka Nyambitilwa aliposhindwa kumudu shule, kukosana na jamii mpaka wananchi wakataka kumchomea ofisi ya shule!!

Salyankanga alikula rushwa kutoka kwa huyo mama akamhamishia Magu S/Msingi ambako yuko hapo mpaka sasa hivi; anavurugana na waalimu, kamati ya shule na wazazi kwa ubabe na ubadhirifu.

Kabla ya mwalimu huyo kuhamishiwa Nyambitilwa S/Msingi, alikuwaa Nyanguge S/ Msingi ambako nako alivurunda!
Kwa nini mwalimu kama huyo asivuliwe madaraka? Mbona wengine wengi tu wamevuliwa madaraka baada ya kuvurunda kwenye ualimu mkuu? Rushwa...rushwa...rushwa; safari bado ni ndefu sana!
 
Asante sa
Hagwila.
Nakupongeza kwa kuamua kuliweka wazi hili na inaonesha wazi upo well detailed, wahusika wakipita hapa au hata wakihitaji msaada wako “piyemu” bila shaka utawapa ushirikiano wa kutosha.... concern yangu ni huyo mbunge ambaye naona unamtaja kwa kurudiarudia kuonesha una imani naye.

Huyu mbunge wenu (Kiswaga) mbona ni kilaza mzuri tu zaidi ya umaarufu wa kibiashara na ku-take advantage ya raia wa “ndoho tabu”, japo hoja yako ni ya msingi sana na binafsi natamani kuona hiyo network ya kina Johari ikiwa overhauled.... pengine mwandikie ujumbe DED moja kwa moja au hata Jafo kwa njia ambayo ujumbe utawafikia.
Asante sana mkuu andaskoo

JF ni mtandao mkubwa na wenye kuheshimika; naamini haya niliyomwandikia DED Magu na yaliyoandikwa na wachangiaji, wahusika watakuwa wameyaona; kuanzia DED wa Magu mwenyewe, Mhe. Jaffo (TAMISEMI), Mhe. Ndalichako (ELIMU) na Mhe. Mkuchika (UTAWALA BORA) na wengine wengi.

Kama siyo wao binafsi, naamini wasaidizi wao au colleges wao watawaambia; naamini wako serious na kazi zao kama aliyewateua alivyo.
 
Ka uzi kazuri sana haka. Sijui chochote kuhusu walimu lakini nimependa nondo zinavyotolewa. Natumaini wahusika watafanyia kazi.
 
Hakuna lolote ni fitina tu na roho mbaya inakusumbua. Unaemtetea mwenyewe hana lolote analolijua zaidi ya kuendeleza tabia za mzee saryankanga.
 
Hayajakukuta ndugu yangu; siku utakayonyanyasika kisawasawa utaelewa, japo sikuombei. Fikiria, una vigezo vyote vya kukustahilisha kupata nafasi au huduma fulani; badala ya kupewa hiyo nafasi au huduma, unaambiwa toa laki 3 hadi 5 ndipo upate hiyo nafasi au rushwa ya ngono (kwa wanawake). Kitanda usichokilalia hujui kunguni wake.
Op
Hakuna lolote ni fitina tu na roho mbaya inakusumbua. Unaemtetea mwenyewe hana lolote analolijua zaidi ya kuendeleza tabia za mzee saryankanga
Nimemtetea nani?
 
Back
Top Bottom