Degree 5 Bora Zinazotakiwa Kupewa Heshima

Degree 5 Bora Zinazotakiwa Kupewa Heshima

Malalamiko mengi humu ni wasomi kuambiwa waende Veta. Sidhani kama kuna mahali amesema kuwa wasomi wenye digrii wote hawana ujuzi. Ukweli ni kuwa wasomi wetu wengi hawana ujuzi (skills) wao ni academicians zaidi. Veta itawapa skills zinazohitajika kama wameshindwa kupata kazi zinazoendana na usomi wao. Wengi wa hao unaowataja wangefaidika zaidi katika fani zao kama wakienda Veta. Nadhani amewataja digrii holders kwa sababu wao ndio mara nyingi wanalalamika kutopata ajira serikalini pamoja na wao kuwa wasomi. Anaco washauri ni kuwa inabidi waanze kuangalia maeneo mengine yatakayowawezesha kujiajiri. Maeneo hayo ni pamoja na ufundi uashi, ufundi seremala, ufundi wa mitambo, upishi, ushonaji, ufundi bomba, ufundi wa kutengeneza simu n.k. Kama msomi umeridhika na hapo ulipo, ushauri wake haukuhusu. Mpotezee tu.

Amandla...
Mkuu; hizo degrees au tuseme hatujaanza kuwa na wasomi leo. Wasomi wamekuwepo toka kitambo na waliajiriwa bila kwenda veta. au nadanganya bro?
Veta ilitumika sana kwa vijana Std 7 ambao hawakubahatika kuendelea na masomo Sekondari, vijana F4 ambao hawakufaulu kuendelea na masomo A-level au vijana waliokatiza masomo yao kwa sababu fulani.
Sasa unapowaelekeza (kwa ushauri au agizo -whatever) wale waliokwishapita A-level na kumaliza chuo wafanye U-turn waende VETA huoni ni kama unawadhalilisha? Yan mheshimiwa anataka kusema hao vijana wasomi walikuwa vipofu (walijizima data/walijitoa ufahamu) hawakuiona VETA walipokuwa wanajiunga vyuoni???
Ujuzi wa kiwango cha juu ni ule unaopatikana kutokana na uzoefu(Field Experiance) kazini. Huko VETA ni mojawapo ya maeneo ya kujifunzia na kutoa cheti kuthibitisha umejifunzia wapi Utaalam wako. Vyuo vya VETA ni kama vyuo vingine ila ni chuo kwa kada za awali.
Kumwambia deg. holder aende veta ni sawa na kumwambia daktari arudi O-level akajifunze biology. Hiyo sio poa.
 
Ushauri halali ndio agizo. Angesema wenye digrii wote wafukuzwe ili waajiriwe wenye vya Veta, yeyote ambae angemtii angeshughulikiwa na Mahakama au taasisi nyingine.
Mfano wako sio sahihi. Kamw wewe umeniajiri una haki ya kuniagiza unachotaka ili mradi kisilete madhara katika usalama wa nyumba. Ukiniagiza nitoe tiles nitazitoa kwa sababu haitahatarisha usalama wa wanaotumia nyumba. Au ukiniletea tile za kichina wakati nimekushauri zitumike za Spain siwezi kukataa kuziweka.

Lakini ukiniambia nipunguze nguzo, hapo nakuachia kazi. Ni kama wale mafundi Kariakoo ambao waliambiwa waongeze basement na wakatii ingawa walihofia kuwa itaathiri jengo? Walipaswa kukataa. Au kama wewe ni daktari halafu akaingia PM katika chumba cha operation akasema kuwa anadhani uondoe miguu yote ya mgonjwa kwa sababu anaamini yote ime oza, utaikata kwa sababu wazo la Mkubwa ni amri? Hivyo hivyo katika huu ushauri wa PM. Wale wanao ona unawafaa waufuate, na wale wanaoona hauwafai waachane nao.

Amandla...
Kungelikuwapo na wanao ona ushauri unawafaa; kusingelikuwapo na malumbano yote haya. Malumbano yote haya ni Ishara kwamba ushauri wake umeibua kero kwa walengwa. Bora angekaa kimya.
PM amesahau kwamba anatoa ushauri kwa watu ambao tayari hawana chanzo cha fedha eti waende mahali (VETA) panapohitaji fedha ili uipate huduma unayoitaka. Ushauri huo hautekelezeki na halafu Ushauri huo sio endelevu(Sustainable) kwa sababu ni wa mtu mmoja. Veta hawajakaribisha wenye deg. na Serikali haina mwelekeo wa kuwasaidia Malipo ya Chuoni.
PM amesahau kwamba VETA hawana uwezo wa kuwachukua wote wenye deg. kama wakikubali ushauri wake na Serikali ikakubali kuliwezesha jambo hilo.
PM hakuipembua jamii (Audience) iliyokuwa inamsikiliza. Ametoa a Blanket Statement (Ametupa mtama kwenye kuku wengi).
 
Kwa taarifa yako hakuna nchi ambayo serikali ina wajibu wa kutoa ajira kwa wananchi wake. Serikali inaweka mazingira ya ajira kupatikana. Serikali haikuambii usomee nini. Ni wajibu wako kuangalia soko (ikiwa pamoja na serikali) linahitaji fani gani. Hauwezi kuilaumu serikali kama wewe leo utaamua kusomea typing halafu ukakosa kazi kwa sababu serikali haina typewriter. Jukumu la kuhakikisha kuwa una elimu itakayokuwezesha kuajiriwa au kujiajiri ni lako. Sio la serikali.

Kwa taarifa yako hata wahitimu wa Veta wameenda shule. Sio nyinyi peke yenu mlioenda vyuoni ndio mmeenda shule.

Amandla...
Hii 👆👆 umeijibu kitaalam zaidi bro.:OkayChamping:
 
Kungelikuwapo na wanao ona ushauri unawafaa; kusingelikuwapo na malumbano yote haya. Malumbano yote haya ni Ishara kwamba ushauri wake umeibua kero kwa walengwa. Bora angekaa kimya.
PM amesahau kwamba anatoa ushauri kwa watu ambao tayari hawana chanzo cha fedha eti waende mahali (VETA) panapohitaji fedha ili uipate huduma unayoitaka. Ushauri huo hautekelezeki na halafu Ushauri huo sio endelevu(Sustainable) kwa sababu ni wa mtu mmoja. Veta hawajakaribisha wenye deg. na Serikali haina mwelekeo wa kuwasaidia Malipo ya Chuoni.
PM amesahau kwamba VETA hawana uwezo wa kuwachukua wote wenye deg. kama wakikubali ushauri wake na Serikali ikakubali kuliwezesha jambo hilo.
PM hakuipembua jamii (Audience) iliyokuwa inamsikiliza. Ametoa a Blanket Statement (Ametupa mtama kwenye kuku wengi).
Hapana. Watu wako sensitive bila sababu. Hawana chanzo cha fedha lakini wana elimu. Hapo tayari wana advantage kubwa sana ukilinganisha na majority ya watanzania ambao hawana chanzo cha fedha na hawana elimu.
Sidhani kama Veta ina mfukuza mwenye digrii.
Mimi naona tatizo kubwa la wasomi wetu ni sense of entitlement. Wanaamini kuwa serikali na jamii ina wajibu wa kuwapa ajira. Hilo sio kweli.

Amandla...
 
Before hatujasema yule ni bora yule sio bora yule ni bora zaidi yule sio bora wala mhimu sana tujiulize

Je, hizo shahada zimetusaidia vipi kama taifa kuwa innovative na creative kufikia mapinduzi makubwa ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiutamaduni, kiteknolojia kama inchi za wenzetu Japan, China na kwingineko inchi ambazo historia inaonyesha miaka 60 nyuma Tanzania tulikuana uchumi na maendeleo yanayoelekeana na inchi tajwa hapo juu!!??

kimsingi, hapa kila mtu anaweza kuwa na shahada moja, mbili ama tatu lakini tujiulize hizo shahada zetu zimeleta tija gani kwenye familia, jamii au taifa letu. Unaweza kusema hapa una shahada ya Medicine lakini ukawa hauna tija yoyote lakini mtu alie na elimu ya cheti VETA akawa na tija kubwa sana kwenye jamii na taifa kwa ujumla.

My take, shahada zote ni bora kwa sababu kila moja ina eneo lake lankiutendaji na nimhimu kwa eneo husika.

Sad story ni kwamba wasomi wengi ngazi ya shahada plus, wamekua watu wa ovyo kuliko kundi la watu ambao hawakupata elimu ya chuo kikuu.

#Hii inchi inafelishwa na wasomi.
 
Kuna hizi mbili zinazotolewa na Veta nazo ni bora sana
Bachelor of Accounts with Welding.
Bachelor of Human resources and Tailoring
 
Hapana ni mafundi
Mafundi wanawezaje kujenga pasipo usanifu wa Wahandisi?

Kitaalamu kama ni jengo/Highway/dam/water project n.k civil engineer ndiye anayefanya usanifu wa kina kisha ndiyo Ujenzi unaenda kufanyika site

Hao Mafundi, ni wasaidizi wa Wahandisi katika kutekeleza Mradi.
 
Mafundi wanawezaje kujenga pasipo usanifu wa Wahandisi?

Kitaalamu kama ni jengo/Highway/dam/water project n.k civil engineer ndiye anayefanya usanifu wa kina kisha ndiyo Ujenzi unaenda kufanyika site

Hao Mafundi, ni wasaidizi wa Wahandisi katika kutekeleza Mradi.
Nyumba karibu zote nchini zinajengwa bila kuhusishwa mhandisi au mtaalamu yeyote wa majengo. Karibu majengo yote yaliyopromoka au kuungua yalisanifiwa na kusimamiwa na wahandisi.

Unazungumzia taratibu za mjini na wananchi wengi hawaishi mjini. Kwenye majengo Civil Engineer ni mshauri lakini Msanifu Mkuu ni Msanifu Majengo. Jengo lisilo la ghorofa lililosanifiwa na Msanifu Majengo linaweza kupata kibali cha ujenzi bila mchango wa mhandisi. Jengo lolote lile liliosanifiwa na Mhandisi halipewi kibali bila kuwa na mhuri wa Msanifu Majengo. Kwenye majengo, mhandisi ni msaidizi wa Msanifu Majengo. Kwa hiyo nao wadharauliwe ingawa mchango wao ni muhimu sana?

Kama nilivyosema, mhandisi mzuri yeyote anawaheshimu sana mafundi wabobezi maana uzoefu wao mara nyingi unaweza kumkwepesha matatizo na makosa mengi.

Amandla...
 
Nyumba karibu zote nchini zinajengwa bila kuhusishwa mhandisi au mtaalamu yeyote wa majengo. Karibu majengo yote yaliyopromoka au kuungua yalisanifiwa na kusimamiwa na wahandisi.

Unazungumzia taratibu za mjini na wananchi wengi hawaishi mjini. Kwenye majengo Civil Engineer ni mshauri lakini Msanifu Mkuu ni Msanifu Majengo. Jengo lisilo la ghorofa lililosanifiwa na Msanifu Majengo linaweza kupata kibali cha ujenzi bila mchango wa mhandisi. Jengo lolote lile liliosanifiwa na Mhandisi halipewi kibali bila kuwa na mhuri wa Msanifu Majengo. Kwenye majengo, mhandisi ni msaidizi wa Msanifu Majengo. Kwa hiyo nao wadharauliwe ingawa mchango wao ni muhimu sana?

Kama nilivyosema, mhandisi mzuri yeyote anawaheshimu sana mafundi wabobezi maana uzoefu wao mara nyingi unaweza kumkwepesha matatizo na makosa mengi.

Amandla...
Naelewa Uhusiano uliopo kati ya Wahandisi na Mafundi Ujenzi.

Pia Uhusiano wa Architecture na Civil/Structural Engineer

Ni kweli majengo yetu mengi ambayo sio ya ghorofa tunayoishi, yamejengwa na Mafundi tu.

Ila ni ukweli kwamba Jengo la ghorofa, haliwezi kujengwa bila Civil/Structural Engineer kusanifu(Kufanya design especially za nondo/zege n.k)

Na nikiri wazi, wakati nimetoka Chuo Kikuu nilianza kazi Kwa kuanza kupata uzoefu kutoka Kwa Mafundi

Nilikutana na Mzee mmoja ambaye alikuwa ni Fundi mzoefu sana pale Ofisini

Pamoja na kwamba nilikuwa nina miliki degree lakini nilipaswa kujifunza kazi kutoka Kwa yule Mzee

Yule Mzee nina muheshimu Kwa kutenga muda wake kuweza kunipa maarifa ya kazi za Kihandisi za vitendo

Ilikuwa natumia Siku mbili tatu hadi 5 kufanya design ya jengo la ghorofa 40 pamoja na kuandaa michoro ya nondo n.k lakini sikuwa najua jinsi ya kuanza kulisimamisha ardhini bila uwepo wa hao Mafundi wazoefu.

Wahandisi tunapotoka Chuoni, tunakuwa tunajua mambo mengi ya kwenye vitabu lakini sio ya field
 
Back
Top Bottom