Demokrasia inatupotezea sana muda na nguvu

Demokrasia inatupotezea sana muda na nguvu

Red Giant

JF-Expert Member
Joined
Mar 9, 2012
Posts
15,657
Reaction score
20,967
Demokrasia imekuwa kitu cha hovyo sana kinachorudisha nchi nyuma, hasa nchi za kiafrika. Wanasiasa hawawazi tena maendeleo bali wanawaza jinsi ya kuingia madarakani na jinsi ya kubaki madarakani. Hakuna anayejali maslahi ya nchi. Kenya walianza kuongelea uchaguzi wa 2022 miaka 3 iliyopita.

Rais Samia anaongelea uchaguzi wa 2025 leo. Nchi haina dira yoyote bali ni kusikiliza kelele huku na huko na kuzifanyia kazi, imaendeshwa kwa matukio.

Kwenye demokrasia Serikali inatapanya mali, inakopa na kufuja ikijua kesho mzigo wa deni siyo wake. Ndiyo maana kila utawala mpya ukiingia utakuta unalalamika hazina imekombwa.

Tungerudi tu kwenye chama kimoja. Au tukae chini tuumize vichwa tuje na utaratibu mwingine na si demokrasia. Demokrasia ni uongo.
 
umenikumbusha kipindi cha wimbi la kununua viongozi wa wapinzani, wabunge na madiwani aisee kilikuwa kipindi cha mavuno kweli kweli
Pesa na nguvu nyingi sana vinatumika kubaki madarakani.
 
Hapo Tatizo ni demokrasia au tatizo ni sisi waafrika?.Elekeza lawama zako sehemu sahihi maana demokrasia ni pana na iko sehemu nyingi duniani ila sehemu kubwa ya matatizo uliyoyataja yako Afrika.kwahiyo hadi hapo tatizo ni sisi wakazi wazawa wa Afrika nasio demokrasia.
 
Hapo Tatizo ni demokrasia au tatizo ni sisi waafrika?.Elekeza lawama zako sehemu sahihi maana demokrasia ni pana na iko sehemu nyingi duniani ila sehemu kubwa ya matatizo uliyoyataja yako Afrika.kwahiyo hadi hapo tatizo ni sisi wakazi wazawa wa Afrika nasio demokrasia.
Kama mfumo unaruhusu matatizo kwa karibu bara zima basi haufai kabisa. Au hautufai kabisa. Na si Africa tu, huko South Amerika na South East Asia shida tupu.
 
Pesa na nguvu nyingi sana vinatumika kubaki madarakani.
Sasa hebu jiulize je isingekuwepo kabisa hiyo demokrasia japo niya uongo uongo unadhani hali ingekuaje.Naamini kwa sehemu kubwa zingetumika nguvu kubwa zaidi hadi kuuana kwa ajili ya vyeo na madaraka.
 
Yaaan we acha tu hawa watu hawajawah ishi na mawazo ya watu wa hali ya chini
Demokrasia inatudanganya kuwa mtu wa chini anaweza kuwa na sauti katika kuendesha nchi au sera za nchi. Hiki ni kiinimacho tumepigwa.
 
Kama mfumo unaruhusu matatizo kwa karibu bara zima basi haufai kabisa. Au hautufai kabisa. Na si Africa tu, huko South Amerika na South East Asia shida tupu.
Uko kote ulikokutaja tatizo ni jamii yenyewe ya watu walivyo.Ila ni afadhali kwa hiyo demokrasia kidogo iliyopo kuliko isingekuwepo kabisa.Kwa kadri tutakavyokua tunazidi kustaarabika ndivyo ambavyo demokrasia itakavyozidi kukomaa.Sisi bado ustaharabu na kuheshimiana ni kidogo ila zama zinazidi kutubadilisha taratibu.
 
Sasa hebu jiulize je isingekuwepo kabisa hiyo demokrasia japo niya uongo uongo unadhani hali ingekuaje.Naamini kwa sehemu kubwa zingetumika nguvu kubwa zaidi hadi kuuana kwa ajili ya vyeo na madaraka.
Si lazima. Libya iliendeshwa kibabe na ilikuwa tulivu kwa miaka mingi. Huko North Korea hatusikii watu kuuuana kama walivyouawa watu Zanzibar mwaka jana, au Kenya 2008.
 
Sama nini, demokrasia inatudanganya kuwa mtu wa chini anaweza kuwa na sauti katika kuendesha nchi au sera za nchi. Hiki ni kiinimacho tumepigwa.
Mtu wa chini ni yupi?.Tatizo ni elinu na uelewa wa wananchi kua nchi.Ata hao unaowaona kua ni wakubwa lazima walianzia chini wakafanya jitihada zakufika juu.Na ni demokrasia ndio ambayo ilitoa mwanya wakafika uko.
 
Uko kote ulikokutaja tatizo ni jamii yenyewe ya watu walivyo.Ila ni afadhali kwa hiyo demokrasia kidogo iliyopo kuliko isingekuwepo kabisa.Kwa kadri tutakavyokua tunazidi kustaarabika ndivyo ambavyo demokrasia itakavyozidi kukomaa.Sisi bado ustaharabu na kuheshimiana ni kidogo ila zama zinazidi kutubadilisha taratibu.
Mpaka lini kustaarabika? Maana yake demokrasia inachagua aina ya watu? Na ushahidi unaonekana kuwa ili ufikie demokrasia au ili uokomaze unapaswa kupitia njia zisizo za kidemokrasia. Mfano Zimbabwe, mpaka keshi liingilie kati ndipo demokrasia kidogo ikakua. Sasa watakufa wangapi, tutapata hasara ngapi hadi hiyo demokrasia ikomae.
 
Si lazima. Libya iliendeshwa kibabe na ilikuwa tulivu kwa miaka mingi. Huko North Korea hatusikii watu kuuuana kama walivyouawa watu Zanzibar mwaka jana, au Kenya 2008.
Uwezi kutoa mifano ya nchi mbili kutetea hoja yako wakati dunia ina mamia ya nchi.Ata uko usikute kilichoko ni utulivu na sio amani.sasa utulivu sio kitu chakujivunia maana ikitokea wananchi wanaishi kwa madukuduku ni rahisi zaidi kuharibu nchi kuliko kuijenga.Watavumilia kwa muda tu na viongozi wanalazimika kutumia nguvu kubwa kuhakikisha wananchi hawafurukuti kwa lolote ila ilo sio jambo lakudumu sana.Mfano ni hiyo libya yako.
 
Mtu wa chini ni yupi?.Tatizo ni elinu na uelewa wa wananchi kua nchi.Ata hao unaowaona kua ni wakubwa lazima walianzia chini wakafanya jitihada zakufika juu.Na ni demokrasia ndio ambayo ilitoa mwanya wakafika uko.
Ili usikike kwenye demokrasia lazima uwepo huko juu. Hili lipo hata kwenye udikteta na nchi za kifalme. Tatizo la demokrasia ni kutudanganya kuwa mtu wa chini anasikilizwa na ndiye anaendesha nchi.
 
Demokrasia imekuwa kitu cha hovyo sana kinachorudisha nchi nyuma, hasa nchi za kiafrika. Wanasiasa hawawazi tena maendeleo bali wanawaza jinsi ya kuingia madarakani na jinsi ya kubaki madarakani. Hakuna anayejali maslahi ya nchi. Kenya walianza kuongelea uchaguzi wa 2022 miaka 3 iliyopita.

Rais Samia anaongelea uchaguzi wa 2025 leo. Nchi haina dira yoyote bali ni kusikiliza kelele huku na huko na kuzifanyia kazi, imaendeshwa kwa matukio.

Kwenye demokrasia Serikali inatapanya mali, inakopa na kufuja ikijua kesho mzigo wa deni siyo wake. Ndiyo maana kila utawala mpya ukiingia utakuta unalalamika hazina imekombwa.

Tungerudi tu kwenye chama kimoja. Au tukae chini tuumize vichwa tuje na utaratibu mwingine na si demokrasia. Demokrasia ni uongo.


Watu wanachekesha demokrasia gani unaiongelea wakati kura zimeibiwa na uchaguzi unapagwa!. Yaani kwa akili yako kuna demokrasia Tanzania!. Tanzania tunataka kuwa na demokrasia lakini haipo bado! wananchi kukutana na kuongelea katiba hairuhusiwi.... kuongelea katiba!!!. Ni visingizio tu kuna nchi zina maendeleo sana na zina demokrasia
 
Mpaka lini kustaarabika? Maana yake demokrasia inachagua aina ya watu? Na ushahidi unaonekana kuwa ili ufikie demokrasia au ili uokomaze unapaswa kupitia njia zisizo za kidemokrasia. Mfano Zimbabwe, mpaka keshi liingilie kati ndipo demokrasia kidogo ikakua. Sasa watakufa wangapi, tutapata hasara ngapi hadi hiyo demokrasia ikomae.
Mambo mengine inategemea na mwamko wa wananchi wenyewe ukoje.Kama uko kwenye jamii ya vilaza maana yake itachukua muda kustaarabika.lakini kwavile tuko kwenye zama za mabadiliko na ukuaji wa technolojia,inakua ni rahisi kuelimika kuliko uko tulikotoka.kwahiyo nadhan ni kizazi hichi cha kwetu ndio kizazi cha mwisho cha jamii ngumu kustaarabika ila kizazi kinachokua sasa kitakua tofauti sana na sisi.
 
Back
Top Bottom