Habari zenu wadau, leo asubuhi nimepata ujumbe kutoka kwa mdau
Dena Amsi akinipa taarifa kuwa ameamua kuachana na
Mr Rocky kutokana na tabia za
Mr Rocky za kubeba beba wanawake kumchosha. Sehemu ya ujumbe huo ilisema hivi, Nanukuu "Mwenyekiti nimefikia hatua ya kuachana na mume wangu
Mr Rocky baada ya kumvumilia kwa muda mrefu nikidhani kuwa angebadilika lakini nimegundua kuwa tabia ni kama ngozi huwezi kuibadili, hivyo nimeamua kujiweka pembeni aendelee na mambo yake kwa uhuru". Mwisho wa kunukuu, Kwa mujibu wa ujumbe huo ni kuwa hadi sasa
Dena Amsi amekata kamba kwa
Mr Rocky. Juhudi zangu kumtafuta
Mr Rocky ili aelezee jambo hili zimegonga mwamba baada ya simu yake kuita muda wote bila majibu na baadae ikapokelewa na
Mamndenyi ambaye baada ya kumwambia kuwa nilitaka kuongea na
Mr Rocky kuhusu habari yake na
Dena Amsi alinijibu kuwa
Mr Rocky yuko nje ya nchi kwa mapumziko afu akasonya na kukata simu. Nimeamua kuileta hapa ili
Mr Rocky aje alizungumzie hili.
Copy:
Arushaone Nicas Mtei,
Sefeti
Erickb52,
Mungi,
Filipo et al.
Wasalaam
Baba V.