DENI LA TAIFA: Benki ya dunia yaitahadharisha Tanzania

Nanukuu:

Waziri wa Fedha na Mipango wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip mpango ametangaza kuwa deni la serikali limeongezeka kwa zaidi ya Trilioni moja.

"Deni la serikali limeongezeka na kufikia Sh.Trillioni 51.03 kutoka shilingi Trilioni 49.86 ya mwaka 2018 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 2.35". Alisema leo bungeni.


Mimi kama mwananchi wa kawaida naomba sana raisi atakayechaguliwa adili na vipaombele vya miaka 5 yaani 2020-2025 tusichoshane kutengeneza vitu vya vizazi vijavyo wakati tuliokupigia kura tunateseka tu mtaani katika vitunavyoona ni UPUUZI NA HAVINA MANUFAA KWA WAKATI TULIOPO NI MIRADI YA UJENZI KUWA MINGI KULIKO SEKTA YA KILIMO UVUVI NA HOSPITALI bado sana havijafikia kiwango kizuri hivyo basi wakati ujao tujaribu kuangalia na huku ..DENI NI KUBWA SANA maisha ni magumu kwa mtu mmoja mmoja😊😎
 
Asante mleta mada. Nipo napitia nukta kwa nukta hapa nije na maswali magumu kwa hii serikali ya......
 
Naona racist wamejaa kwenye hii thread hahaha, hamtaki tuambiwe ukweli kua tupunguze kukopa?
Kukopa tunakopa sana tu, japo tuna uafadhali kuliko mataifa mengi, ila still tunakopa na kukopa lazima ulipe. Hata marekani wana madeni kibao toka China, ila wanaweza pigana, sisi tuna uwezo huo?
 
Tuna Chato International Airport hata kama haikuwahi kuwa kwenye mpango wa Taifa wa maendeleo wa miaka mitano we don’t care
haha wenyewe (wenye nchi) wanakwambia chato ipo tanzania...kwahiyo freshi tuu
 
mkuu...kati ya reli na magereza wewe unaona magereza ni bora?? hii nchi ngumu aisee..
 
Tatizo sio kukopa tu. Ni aina ya mkopo na matumizi ya mukopo yenyewe. Mikopo ya mashirika makubwa inakuwa na riba ndogo. Mikopo kutoka benki za biashara ina riba mara mbili au hata tatu ya riba kutoka mashirika makubwa yanayotoa mikopo. CAG alinukuliwa akisema tatizo halipo kwenye kiwango cha mkopo bali ni kwa sababu mikopo yetu mingi ni ya kutoka kwenye mabenki ya biashara. Hapa tulipofika, tunatumia nusu au zaidi kidogo ya makusanyo yetu yote kulipa tu deni na riba yake. Na kwa vile hii mikopo inatumika kwenye miradi ambayo haitaanza kuzaa faida mpaka baada ya miaka kadhaa, pesa ambazo zingeingia mitaani "zizunguke" zinatumika kulipa hiyo mikopo na riba. Matokeo yake mzunguko wa fedha ni mdogo, na maisha yanakuwa magumu zaidi. Tena kilimo hakitengewi bajeti kubwa kwa vile pesa zinalipa madeni. Ndio maana japo uchumi unapanda, unapata tu kwenye kipato cha makampuni machache makubwa lakini kipato cha watu vijijini kinapungua. Itatubidi tusubiri mpaka hiyo miradi inayofanyiwa uwekezaji sasa ianze kulipa ndipo ugumu wa maisha utakapopungua. Tuendelee tu kumwomba Mungu.
 
Safi. Tupunguze Sana matumizi ya kujenga mabarabara, shule, Maji, nk. Tulipane tu mishahara na kulipa madeni tuliyokupo zamani. Kama Alivyofanya Rais Mkapa 1995/2000 ndipo tuaze kujenga na kununua Trein na ndege. Mabarabara na maji Kama tunaogopa madeni ya taifa
 
Mkuu kwa ubinafsi huo ndiyo maana leo tupo hapa, sisi watu weusi tuna ubinafsi sana na tutachelewa miaka yote.

Mtu aanze kudili na vitu vya leo halafu wajukuu zako wakija watakua wanalia hivihivi kama tunavolia sisi.

Tatizo ni kwamba tunataka maisha ya wenzetu ambao mababu zao waliteseka kwaajili yao, tunatakiwa tupambane kwaajili ya vizazi vijavyo ili nao hapo baadae wasijekulia kama tunavolia sisi.

Mkuu unafikiri wale mababu zao akina David Livingstone wangekubali kuja huku kwetu kutafuta maisha ya taabu huku wakipatwa na maradhi mpaka wanakufa hukuhuku Africa kwa mawazo yako walikua wajinga?

Walikua wanapambana ili vizazi vya baadae visipate shida.
 
mkuu...kati ya reli na magereza wewe unaona magereza ni bora?? hii nchi ngumu aisee..


Mkuu watuhumiwa/mahabusu wamerundikwa huko Magereza, mi nilisuggest tu maana options zipo nyingi

Hiyo trillion 16 ingewekezwa kujenga barabaraza lami, vyuo vya beta na vyuo vikuu na sio reli

Sekta ya viwanda nchini kwetu sio kubwa sana kiasi cha kufanya tujenge reli ya gharama ambazo ni sawa na makusanyo ya Kodi ya mwaka mzima ya Central government


Kujenga barabara za lami tulikuwa tunapiga ndege wawili kwa Jiwe moja, maana wakulima na wenye viwanda barabara za lami zingewaservice vizuri tu
 
Kwa hela zetu za ndani!.....hahaha[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…