Mchambuzi
JF-Expert Member
- Aug 24, 2007
- 4,850
- 9,434
Deni la Taifa letu linazidi kupaa. Kwa mujibu wa takwimu za hizi karibuni, Deni hili tayari limeshavuka dollar za kimarekani Billion kumi na tano, sawa na takribani shillingi trilioni ishirini na tatu za Kitanzania.
Moja ya Vigezo muhimu vya kupima utendaji wa serikali yoyote ile duniani ni suala zima la nidhamu ya katika mfumo wake wa mapato na matumizi ya fedha za umma (Fiscal Discipline). Ukiachilia mbali fiscal discipline, vigezo vingine muhimu ni Ajira kwa raia wake, mfumo wake wa Elimu, mfumo wa Afya, Ufanisi Katika Mhimili wa Mahakama (Judicial Efficiency) n.k. Lakini mafanikio katika maeneo yote haya hutegemea sana kigezo muhimu kuliko vyote ambacho ni Fiscal Discipline ya Serikali husika. Kwahiyo kwa leo Mada yangu italenga zaidi kwenye suala zima la Fiscal Discipline. Kinachonisukuma kuja na mada hii ni masuala makuu mawili:
Kwanza ni upotoshaji wa baadhi ya wanasiasa hasa ndani ya bunge letu kuhusiana na deni la taifa, hasa katika hoja zao mbili kwamba: Moja, hoja kwamba ni jambo la kawaida kwa nchi kuwa na madeni, na Mbili, ni hoja ya baadhi ya wanasiasa kwamba Deni letu la taifa ni dogo sana ikilinganishwa na nchi nyingine nyingi, hivyo wananchi hawana haja ya kuwa na wasiwasi wowote. Dhamira yangu ya pili kuja na mada hii imesukumwa na ukweli kwamba wabunge wetu wengi, licha ya kuwa na hoja za kizalendo zinazolenga kujadili juu hatari inayotukabili kama taifa kuhusiana na kuendekea kukua kwa deni la taifa kwa kasi, wabunge wengi hawapo well informed to challenge vya kutosha serikali juu ya suala hili kwani mara nyingi hoja zao hupwaya na kuishia kuwa hoja za kisiasa, hivyo kushindwa nguvu kwa hoja za wanasiasa wasiojali nidhamu ya matumizi na mapato ya fedha za umma;
Nikiingia moja kwa moja katika hoja hizi za wanasiasa, kuna ukweli kwamba kwa taifa lolote, Deni la taifa/umma ni jambo la kawaida na la Lazima. Kwa kuangalia conventional methods za kupima iwapo deni la taifa ni mzigo au hapana ambapo vigezo kama vile uwiano wa deni la taifa na pato la taifa (Debt to GDP Ratio) hutumika, kuna uwezekano wa umma kuaminishwa kwamba Tanzania ipo katika nafasi nafuu kuliko mataifa mengi in terms of national debt. Kwa mfano, kwa sasa, Debt to GDP ratio ya Tanzania ni around 47% huku kwa taifa kama marekani uwiano huu ni around 110% huku Japan Debt to GDP ratio ikiwa ni zaidi ya 200%. Katika hili, imekuwa jadi kwa wanasiasa (CCM) kujadili kujenga hoja zao nilizojadili awali, aidha kwa kujua au kutojua kwamba hoja zao zipo crafted zaidi kisiasa kuliko kiuchumi. Lakini katika mazingira yetu ambapo we glorify politics and defy economics, utamaduni huu sio jambo la ajabu.
Pengine at this juncture, ni muhimu kujadili, japo kidogo, dhana mbili muhimu ambazo ni kama chanda na pete katika mlinganyo mzima wa mfumo wa mapato na matumizi ya fedha za umma (fiscal system). Dhana hizi ni National Debt (Deni la Taifa/Umma) na Fiscal/Budget Deficit. Wengi mnaelewa maana yake dhana hizi hivyo nitajadili kwa ufupi sana kama njia ya kujenga muktadha wa mjadala.
1. Budget au Fiscal Deficit: Kwa lugha nyepesi,budget/fiscal deficit hujitokeza pale ambapo mapato ya serikali yanakuwa madogo kuliko matumizi ya serikali katika economic cycle husika. Hali hii ya mapato kuwa madogo kuliko matumizi ya serikali kwa ajili ya huduma mbalimbali za kijamii, na gharama za kuendesha shughuli za serikali kwa ujumla, hupelekea serikali huska kuchukua uamuzi wa kukopa kutoka vyanzo vikuu viwili aidha vyanzo vya ndani, vyanzo vya nje au vyote kwa pamoja. Kila chanzo kina mchakato wake, faida zake lakini pia na changamoto zake, yote ambayo tutayadili huko mbeleni, lakini kwa sasa niseme tu kwamba tangia uhuru, kwa wastani, serikali imekuwa inategemea zaidi mikopo kutoka kwenye vyanzo vya nje (kwa zaidi ya 70%), huku vyanzo vya ndani vikitumika kwa kiwango kisichozidi 30%.
2. National Debt/Deni la Umma/Taifa - maana yake pia ni straight forward kwa walio wengi lakini pengine nisisitize tu kwamba deni la taifa ni mrundikano wa Fiscal Deficits za economic cycles mbalimbali/ miaka nenda miaka rudi. Ni kutokana na hali hii, Deni la taifa na fiscal/budget deficit vina uhusiano wa karibu sana kwani kukopa/mikopo represents a predominant source to finance deficit ya economic cycle husika. Kwahiyo deni la Umma/taifa pia hutazamwa kama asilimia ya pato la nchi ili kuakisi overall fiscal health ya uchumi husika;
Nikirudi katika hoja yangu ya msingi juu ya upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya wanasiasa, ni jambo la kawaida kwa wanasiasa wetu to glorify politics and defy economics kwani to them, Politics is supreme to every kind of common sense and rationality. Porojo zao bungeni na maeneo mengine kutetea ukubwa wa fiscal deficit ni moja ya vituko vyao to defy economics and glorify politics. Nitafafanua. Katika nchi za wenzetu walioendelea kiuchumi, hasa nchi ambazo wanasiasa wetu huzifananisha na Tanzania in terms of Debt to GDP ratio kisha kujenga hoja kwamba ratio zao zipo juu yetu (e.g. USA over 100%, & Japan over 200%) kuliko Tanzania (i.e. around 47%) na kusisitizia umma wetu kwamba tupo salama, wanasiasa hawa aidha kwa makusudi au mere ignorance, wanakosa ufahamu kwamba, suala zima la usimamizi wa mapato na matumizi katika mfumo wa fedha za umma kwa wenzetu huzingatia Sheria au Kanuni kuu mbili namely:
1. The Golden Fiscal Rule; na
2. The Sustainable Investment Rule.
Pengine ufafanuzi wangu juu ya kanuni hizi mbili utasaidia to shade more light kuhusu jinsi gani wanasiasa wetu wanavyokuwa wapotoshaji. Tukianza na Golden Fiscal Rule, kanuni hii inasema kwamba katika mzunguko wa uchumi husika (in any given economic cycle), serikali inatakiwa kukopesha fedha na kuzitumia fedha hizo katika uwekezaji (investment) kuliko katika matumizi ya kawaida. Swali la kwanza la kujadili ni je:
· Kwa kiasi gani Wanasiasa wetu wanazingatia Golden Fiscal Rule katika ujenzi wa hoja zao?
Kama tutakavyojadili baadae, ni dhahiri kwamba tangia uhuru kanuni hii imekuwa inakiukwa. Kwa mfano zingatia jinsi gani serikali katika bajeti zake zote imekuwa iki allocate sehemu kubwa ya fedha za umma katika matumizi ya kawaida (posho, mishahara, manunuzi ya umma n.k) kuliko kuwekeza katika maeneo yenye manufaa kwa umma. Bungeni wapo wanaojengahoja ju ya jinsi gani fungu la matumizi ya kawaida huwa kubwa zaidi ya lile la maendeleo, lakini kwa vile hoja zao hujengwa bila ya utashi wa kiuchumi, hasa unao challenge Serikali kwa misingi ya kanuni za kiuchumi, hoja nyingi za namna hii pamoja na umuhimu wake zinaishia kuwa defeated na hoja za wanasiasa waliokosa nidhamu ya usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma.
Tukiingia kwenye kanuni ya pili The Sustainable Investment Rule, kanuni hii inasema kwamba katika mzunguko wa uchumi husika (in any given economic cycle), uwiano baina ya sekta ya umma na pato la taifa (net public sector to GDP) has to be set within a stable and judicious/responsible level. Kwa mfano Waingereza wao kuna wakati kiwango chao walilenga kiwango chao kiwe chini ya 40% ya GDP.
Swali la pili la kujadili ni je:
· Kwa kiasi gani Wanasiasa wetu wanazingatia the Sustainable Investment Rule katika ujenzi wa hoja zao?
Katika hili pia, kama tutakavyojadili, serikali katika miaka yake yote ya bajeti za mwaka imekuwa ikienda kinyume na kanuni/sheria hii yenye nia ya kuhakikisha kwamba kunakuwepo na fiscal discipline.
Ili kuufanya mjadala unoge na ueleweka zaidi, pengine tuzidi kutafuta majibu kwa maswali mengine mawili muhimu yafuatayo:
· Kwanini nchi za wenzetu walikuja na sheria/kanuni hizi?
Nikianza na Golden Fiscal Rule, sababu ya msingi ya kuja na sheria hii ambayo wabunge, wanasiasa na policy makers Tanzania ni muhimu waelewe ni kwamba - nia yake ni kuhakikisha kwamba ZIGO la matumizi ya umma yanayolazimisha mikopo lazima yaangukie across generations fairly; Idea hapa ni kwamba angalau serikali iwe na political will kujaribu kuhakikisha kwamba all public consumption zinazofaidisha kizazi cha sasa lazima ilipwe na kizazi kilichoingia katika deni/mkopo husika; Chini ya sheria hii, inatamka explicitly kabisa kwamba serikali haitakopesha kwa ajili ya matumizi ya kawaida yani (current spending or expenditure) bali kwa ajili ya investments. Nia hapa ni kuhakikisha kwamba hata kama vizazi vijavyo vitakutana na deni la mababu zao, basi angalau vizazi hivyo vifaidike na madeni watakayowakuta, hasa iwapo fedha hizo zilikuwa invested kwa faida ya vizazi vya wakati huo na vile vitakavyofuata.
Nikiingia kwenye Sustainable Investment Rule, kanuni au sheria hii ina compliment ile ya golden fiscal rule kwa nia ile ile ya kujaribu to avoid creation ya excessive burden ya debt repayments kwa vizazi vijavyo. Kwa sheria hii, serikali inahakikisha kwamba deni linadhibitiwa katika kiwango ambacho hakita prove kuwa unsustainable or unfair kwa vizazi vijavyo. Swali lingine muhimu kujadili ni je:
· How much Debt is too Much Debt?
Kama nilivyojadili awali, moja ya kipimo iwapo deni la taifa ni mzigo au sio mzigo kwa walipa kodi ni kwa kuangalia uwiano wa deni la taifa kwa pato la taifa i.e. Debt to GDP ratio. Ni katika hili ndipo tunaona nchi kama Marekani uwiano huu kwa sasa upo zaidi ya 100%, Japan zaidi ya 200%, wakati kwetu Tanzania kwa sasa uwiano ukiwa takribani 47%, suala lilalopelekea baadhi ya wanasiasa, wabunge na policy makers, aidha out of ignorance or arrogance, kujenga hoja kwamba tofauti na mataifa kama Japan na Marekani, sisi tupo salama salmini. Huu ni upotoshaji kwa maelezo yafuatayo:
Ni muhimu kwa viongozi wa namna hii kuelewa kwamba nchi kuwa na uwiano mdogo (i.e. Debt to GDP ratio) haina maana kwamba nchi hiyo ipo salama ai haipo katika hatari yaku default. As a matter of fact, historia ya uchumi wa kimataifa unaonyesha kwamba nchi nyingi ambazo zimekuwa ziki default madeni yao zile zenye Debt to GDP ratios way below 60%. Kwa maana hii, tofauti na wanasiasa wetu uchwara wanavyopenda umma wa watanzania uamini, Tanzania ipo katika hatari zaidi to default kuliko mataifa kama Japan, Uingereza au Marekani.
· Je kwanini nchi yenye high Debt to GDP ratio inaweza kuwa salama zaidi kuliko nchi yenye low ratio?
Jibu ni simple sisi Tanzania tupo more likely kukopa fedha katika sarafu nyingine kubwa nje ya fedha zetu za madafu (shilling za kitanzania). Kwa mfano ukitazama historia ya uchumi wetu, vyanzo vikubwa vya mikopo yetu karibia mara zote imekuwa ni vyanzo vya nje ya nchi, hivyo kukopa in dollars kuliko kutoka vyanzo vya ndani ambavyo vingeweza kutegemea sarafu yetu (yani shillingi). Kwa wastani, uwiano baina ya deni letu la nje na la ndani miaka yote umekuwa sio chini ya 70% (nje) na sio zaidi ya 30% (ndani). Kwahiyo, tofauti na wenzetu kama Japan, UK au USA, sisi hatuwezi kutumia mfumuko wa bei (printing money) to devalue sehemu kubwa ya deni letu kwa ufanisi iwapo tunalemewa na madeni. Hivyo njia pekee inayobakia kwa ajili ya wokovu wetu ni aidha wakubwa (IMF, WorldBank na washirika zao) watufanyie debt restructuring, watusamehe with strings attached katika rasilimali zetu, vinginevyo kinachofuatia ni defaulting ;
Ni muhimu pia at this juncture tukafahamu kwamba mbali ya Debt to GDP ratiokuwa moja ya vipimo vikubwa vya severity ya deni la taifa, kipimo kingine muhimu ni kile cha debt service ratio i.e. the ratio of debt service payments (principal plus interests) of a country to the export earnings of that particular country. Uwiano huu ukiwa chini, maanayake ni kwamba uchumi wa taifa husika una afya zaidi kuliko nchi yenye uwiano ulio juu.
Ni muhimu kwa wanasiasa wetu kuelewa kwamba tofauti iliyopo baina na matumizi ya debt to gdp ratio na ile ya debt service ratio. Kwa mfano, kipimo sahihi cha kubaini severity ya deni la taifa kwa nchi inayokopa kupitia vyanzo vyake vya ndani (local currency), key ratio to determine how large the debt is, ni debt service ratio. Na kwa nchi ambayo inakopa kupitia vyanzo vya nje (sarafu ya dollar), important ratio kuitazama ni debt to GDP ratio. Baadae tutaangalia ratio hizi kwa undani zaidi katika muktadha wa Tanzania ili kuelewa zaidi changamoto zinazotukabili. Kwa mfano, tutaona kwa undani zaidi jinsi gani Tanzania tunalipa more to service the debt kuliko tunavyotumia/wekeza kwenye sekta muhimu kama vile sekta ya Afya n.k.
Pia, baadae tutajadili kwa undani juu ya jinsi gani wanasiasa na policy makers wengi wamekuwa wakipuuzia management ya domestic debt na badala yake kujikita zaidi katika management ya external debt ambapo wamekuwa wakijikita na external debt management sana sana kutokana na pressure kutoka nje ya nchi kuliko political will. Vile vile tutajadili kwa undani jinsi gani external debt can be a threat to national security and nationa sovereignty, na kuna wakati baba wa taifa wakati ule anapingana na mzee mtei na kina IMF aliwahi kuhoji Je, kwani hao ni wajomba wetu huko nje mpaka watusaidua fedha? Vile vile tutajadili kwa undani kuhusu suala zima la nani wanatukopesha, mchakato wake upo vipi, na transparency kwa walipa kodi
Nihitimishe katika maeneo mawili: Kwanza ni msisitizo kwamba budget/fiscal deficit ni matokeo ya mapato ya serikali kuwa machache kuliko matumizi ya serikali in a given economic cycle. Kwa wenzetu wenye nidhamu ya juu kwenye suala hili (Fiscal Discipline), ongezeko la revenue ni matokeo ya ongezeko la output (GDP), income za individuals and income za businesses, na pia taxing the wealthy. Lakini kwetu Tanzania kuna kila ushahidi kwamba kasi ya kukua kwa uchumi (GDP growth) na ongezeko la vipato (biashara na individuals) havina uhusiano mkubwa na ongezeko la ukusanyaji wa kodi. Kwa mujibu wa utafiti mmoja, Tanzania ina potential ya kukusanya kodi at 21% of GDP. Kwa sasa, takwimu zinasema tupo somewhere around 16% lakini in reality, kiasi kinachokusanywa ni wa below the stated figure of 16%.
Pamoja na mapungufu haya, lengo la serikali ya Tanzania ni kufikishia mapato ya kodi kufikia 20% ya GDP ifikapo mwaka 2015 huku serikali pia ikilenga kupunguza utegemezi wa wahisani katika bajeti kufikia chini ya 10%; Kwa zaidi ya miaka 40, kiwango hiki kimekuwa kikicheza kati ya 30% na 40%; Katika miaka ya hivi karibuni, tumefanikiwa kushuka zaidi na kufikia in upper 20 percent. Swali linalobakia ni je, tuna mikakati gani endelevu ya kuhakikisha kwamba tunafikisha kiwango hiki kuwa in single digits i.e. kuifanya Tanzania iweze kujitegemea katika bajeti yake kwa at least 90% ifikapo 2015? Tunarudi pale pale we defy economics and glorify politics. Huwa tuna malengo mengi lakini yanaishia hewani kutokana na Lack of POLITICAL WILL. Tumeona initiatives mbalimbali za kina Zitto Kabwe, January Makamba na wengine bungeni kuhusiana na masuala kama vile kuongeza makusanyo ya kodi on projects and investments that are natural resource based, kuja na sheria kali kudhibiti money laundering, suala la capital gains tax, property tax, regulation of the real estate sector n.k. Ni muhimu kwa wanasiasa kutambua kwamba deficits huchangiwa sana na uzembe katika maeneo muhimu kama haya., na bila kuweka political will katik maeneo kama haya, Taifa kufikia 90% katika kujitegemea kibajeti na taifa kufikia potential yake ya 21% of GDP in tax revenues itaendelea kuwa ndogo za mchana;
Pili na Mwisho, tuelewe tu kwamba mjadala hapa au hoja ya msingi hapa sio kwamba tunatarajia serikali yetu kulipa deni lake lote and make Tanzania become a debt free nation kwani katika taifa lolote lile, debts rarely gets repaid. So the issue sio serikali ilipe madeni yake yote bali kama nilivyojadili tuwe na political will kuzingatia masuala kama vile golden fiscal rule na sustainable investment rule. Pia ni muhimu kwa political will kuhakikisha kwamba debt levels do not crowd out indigenous/local businesses or reduce their confidence, kwani unlike multinationals ambazo nyingi aidha hazilipi kodi au hazina activities zenye backward and forward linkages that create values senye manufaa kwa wananchi walio wengi, local businesses ni key katika kufanikisha haya in terms expanding the tax base, creating jobs n.k; Mwisho, kuna umuhimu wa kuhakikisha kwamba serikali inakuwa na uwezi to service its debt bila ya kuathiri investments katika sekta muhimu za uchumi zenye kugusa maisha ya walio wengi kama vile Elimu, Afya na Kilimo. Serikali yetu imekuwa inalegalega sana katika kutenga fedha za kutosha per agreements mbalimbali za kimataifa kama vile bajeti ya kilimo kuwa at least 10% of the GDP, huku pia allocation of budgets as percentage of GDP kwenye sekta muhimu kama afya na nyinginezo, the government has been living below its commitments.
Moja ya Vigezo muhimu vya kupima utendaji wa serikali yoyote ile duniani ni suala zima la nidhamu ya katika mfumo wake wa mapato na matumizi ya fedha za umma (Fiscal Discipline). Ukiachilia mbali fiscal discipline, vigezo vingine muhimu ni Ajira kwa raia wake, mfumo wake wa Elimu, mfumo wa Afya, Ufanisi Katika Mhimili wa Mahakama (Judicial Efficiency) n.k. Lakini mafanikio katika maeneo yote haya hutegemea sana kigezo muhimu kuliko vyote ambacho ni Fiscal Discipline ya Serikali husika. Kwahiyo kwa leo Mada yangu italenga zaidi kwenye suala zima la Fiscal Discipline. Kinachonisukuma kuja na mada hii ni masuala makuu mawili:
Kwanza ni upotoshaji wa baadhi ya wanasiasa hasa ndani ya bunge letu kuhusiana na deni la taifa, hasa katika hoja zao mbili kwamba: Moja, hoja kwamba ni jambo la kawaida kwa nchi kuwa na madeni, na Mbili, ni hoja ya baadhi ya wanasiasa kwamba Deni letu la taifa ni dogo sana ikilinganishwa na nchi nyingine nyingi, hivyo wananchi hawana haja ya kuwa na wasiwasi wowote. Dhamira yangu ya pili kuja na mada hii imesukumwa na ukweli kwamba wabunge wetu wengi, licha ya kuwa na hoja za kizalendo zinazolenga kujadili juu hatari inayotukabili kama taifa kuhusiana na kuendekea kukua kwa deni la taifa kwa kasi, wabunge wengi hawapo well informed to challenge vya kutosha serikali juu ya suala hili kwani mara nyingi hoja zao hupwaya na kuishia kuwa hoja za kisiasa, hivyo kushindwa nguvu kwa hoja za wanasiasa wasiojali nidhamu ya matumizi na mapato ya fedha za umma;
Nikiingia moja kwa moja katika hoja hizi za wanasiasa, kuna ukweli kwamba kwa taifa lolote, Deni la taifa/umma ni jambo la kawaida na la Lazima. Kwa kuangalia conventional methods za kupima iwapo deni la taifa ni mzigo au hapana ambapo vigezo kama vile uwiano wa deni la taifa na pato la taifa (Debt to GDP Ratio) hutumika, kuna uwezekano wa umma kuaminishwa kwamba Tanzania ipo katika nafasi nafuu kuliko mataifa mengi in terms of national debt. Kwa mfano, kwa sasa, Debt to GDP ratio ya Tanzania ni around 47% huku kwa taifa kama marekani uwiano huu ni around 110% huku Japan Debt to GDP ratio ikiwa ni zaidi ya 200%. Katika hili, imekuwa jadi kwa wanasiasa (CCM) kujadili kujenga hoja zao nilizojadili awali, aidha kwa kujua au kutojua kwamba hoja zao zipo crafted zaidi kisiasa kuliko kiuchumi. Lakini katika mazingira yetu ambapo we glorify politics and defy economics, utamaduni huu sio jambo la ajabu.
Pengine at this juncture, ni muhimu kujadili, japo kidogo, dhana mbili muhimu ambazo ni kama chanda na pete katika mlinganyo mzima wa mfumo wa mapato na matumizi ya fedha za umma (fiscal system). Dhana hizi ni National Debt (Deni la Taifa/Umma) na Fiscal/Budget Deficit. Wengi mnaelewa maana yake dhana hizi hivyo nitajadili kwa ufupi sana kama njia ya kujenga muktadha wa mjadala.
1. Budget au Fiscal Deficit: Kwa lugha nyepesi,budget/fiscal deficit hujitokeza pale ambapo mapato ya serikali yanakuwa madogo kuliko matumizi ya serikali katika economic cycle husika. Hali hii ya mapato kuwa madogo kuliko matumizi ya serikali kwa ajili ya huduma mbalimbali za kijamii, na gharama za kuendesha shughuli za serikali kwa ujumla, hupelekea serikali huska kuchukua uamuzi wa kukopa kutoka vyanzo vikuu viwili aidha vyanzo vya ndani, vyanzo vya nje au vyote kwa pamoja. Kila chanzo kina mchakato wake, faida zake lakini pia na changamoto zake, yote ambayo tutayadili huko mbeleni, lakini kwa sasa niseme tu kwamba tangia uhuru, kwa wastani, serikali imekuwa inategemea zaidi mikopo kutoka kwenye vyanzo vya nje (kwa zaidi ya 70%), huku vyanzo vya ndani vikitumika kwa kiwango kisichozidi 30%.
2. National Debt/Deni la Umma/Taifa - maana yake pia ni straight forward kwa walio wengi lakini pengine nisisitize tu kwamba deni la taifa ni mrundikano wa Fiscal Deficits za economic cycles mbalimbali/ miaka nenda miaka rudi. Ni kutokana na hali hii, Deni la taifa na fiscal/budget deficit vina uhusiano wa karibu sana kwani kukopa/mikopo represents a predominant source to finance deficit ya economic cycle husika. Kwahiyo deni la Umma/taifa pia hutazamwa kama asilimia ya pato la nchi ili kuakisi overall fiscal health ya uchumi husika;
Nikirudi katika hoja yangu ya msingi juu ya upotoshwaji unaofanywa na baadhi ya wanasiasa, ni jambo la kawaida kwa wanasiasa wetu to glorify politics and defy economics kwani to them, Politics is supreme to every kind of common sense and rationality. Porojo zao bungeni na maeneo mengine kutetea ukubwa wa fiscal deficit ni moja ya vituko vyao to defy economics and glorify politics. Nitafafanua. Katika nchi za wenzetu walioendelea kiuchumi, hasa nchi ambazo wanasiasa wetu huzifananisha na Tanzania in terms of Debt to GDP ratio kisha kujenga hoja kwamba ratio zao zipo juu yetu (e.g. USA over 100%, & Japan over 200%) kuliko Tanzania (i.e. around 47%) na kusisitizia umma wetu kwamba tupo salama, wanasiasa hawa aidha kwa makusudi au mere ignorance, wanakosa ufahamu kwamba, suala zima la usimamizi wa mapato na matumizi katika mfumo wa fedha za umma kwa wenzetu huzingatia Sheria au Kanuni kuu mbili namely:
1. The Golden Fiscal Rule; na
2. The Sustainable Investment Rule.
Pengine ufafanuzi wangu juu ya kanuni hizi mbili utasaidia to shade more light kuhusu jinsi gani wanasiasa wetu wanavyokuwa wapotoshaji. Tukianza na Golden Fiscal Rule, kanuni hii inasema kwamba katika mzunguko wa uchumi husika (in any given economic cycle), serikali inatakiwa kukopesha fedha na kuzitumia fedha hizo katika uwekezaji (investment) kuliko katika matumizi ya kawaida. Swali la kwanza la kujadili ni je:
· Kwa kiasi gani Wanasiasa wetu wanazingatia Golden Fiscal Rule katika ujenzi wa hoja zao?
Kama tutakavyojadili baadae, ni dhahiri kwamba tangia uhuru kanuni hii imekuwa inakiukwa. Kwa mfano zingatia jinsi gani serikali katika bajeti zake zote imekuwa iki allocate sehemu kubwa ya fedha za umma katika matumizi ya kawaida (posho, mishahara, manunuzi ya umma n.k) kuliko kuwekeza katika maeneo yenye manufaa kwa umma. Bungeni wapo wanaojengahoja ju ya jinsi gani fungu la matumizi ya kawaida huwa kubwa zaidi ya lile la maendeleo, lakini kwa vile hoja zao hujengwa bila ya utashi wa kiuchumi, hasa unao challenge Serikali kwa misingi ya kanuni za kiuchumi, hoja nyingi za namna hii pamoja na umuhimu wake zinaishia kuwa defeated na hoja za wanasiasa waliokosa nidhamu ya usimamizi wa mapato na matumizi ya fedha za umma.
Tukiingia kwenye kanuni ya pili The Sustainable Investment Rule, kanuni hii inasema kwamba katika mzunguko wa uchumi husika (in any given economic cycle), uwiano baina ya sekta ya umma na pato la taifa (net public sector to GDP) has to be set within a stable and judicious/responsible level. Kwa mfano Waingereza wao kuna wakati kiwango chao walilenga kiwango chao kiwe chini ya 40% ya GDP.
Swali la pili la kujadili ni je:
· Kwa kiasi gani Wanasiasa wetu wanazingatia the Sustainable Investment Rule katika ujenzi wa hoja zao?
Katika hili pia, kama tutakavyojadili, serikali katika miaka yake yote ya bajeti za mwaka imekuwa ikienda kinyume na kanuni/sheria hii yenye nia ya kuhakikisha kwamba kunakuwepo na fiscal discipline.
Ili kuufanya mjadala unoge na ueleweka zaidi, pengine tuzidi kutafuta majibu kwa maswali mengine mawili muhimu yafuatayo:
· Kwanini nchi za wenzetu walikuja na sheria/kanuni hizi?
Nikianza na Golden Fiscal Rule, sababu ya msingi ya kuja na sheria hii ambayo wabunge, wanasiasa na policy makers Tanzania ni muhimu waelewe ni kwamba - nia yake ni kuhakikisha kwamba ZIGO la matumizi ya umma yanayolazimisha mikopo lazima yaangukie across generations fairly; Idea hapa ni kwamba angalau serikali iwe na political will kujaribu kuhakikisha kwamba all public consumption zinazofaidisha kizazi cha sasa lazima ilipwe na kizazi kilichoingia katika deni/mkopo husika; Chini ya sheria hii, inatamka explicitly kabisa kwamba serikali haitakopesha kwa ajili ya matumizi ya kawaida yani (current spending or expenditure) bali kwa ajili ya investments. Nia hapa ni kuhakikisha kwamba hata kama vizazi vijavyo vitakutana na deni la mababu zao, basi angalau vizazi hivyo vifaidike na madeni watakayowakuta, hasa iwapo fedha hizo zilikuwa invested kwa faida ya vizazi vya wakati huo na vile vitakavyofuata.
Nikiingia kwenye Sustainable Investment Rule, kanuni au sheria hii ina compliment ile ya golden fiscal rule kwa nia ile ile ya kujaribu to avoid creation ya excessive burden ya debt repayments kwa vizazi vijavyo. Kwa sheria hii, serikali inahakikisha kwamba deni linadhibitiwa katika kiwango ambacho hakita prove kuwa unsustainable or unfair kwa vizazi vijavyo. Swali lingine muhimu kujadili ni je:
· How much Debt is too Much Debt?
Kama nilivyojadili awali, moja ya kipimo iwapo deni la taifa ni mzigo au sio mzigo kwa walipa kodi ni kwa kuangalia uwiano wa deni la taifa kwa pato la taifa i.e. Debt to GDP ratio. Ni katika hili ndipo tunaona nchi kama Marekani uwiano huu kwa sasa upo zaidi ya 100%, Japan zaidi ya 200%, wakati kwetu Tanzania kwa sasa uwiano ukiwa takribani 47%, suala lilalopelekea baadhi ya wanasiasa, wabunge na policy makers, aidha out of ignorance or arrogance, kujenga hoja kwamba tofauti na mataifa kama Japan na Marekani, sisi tupo salama salmini. Huu ni upotoshaji kwa maelezo yafuatayo:
Ni muhimu kwa viongozi wa namna hii kuelewa kwamba nchi kuwa na uwiano mdogo (i.e. Debt to GDP ratio) haina maana kwamba nchi hiyo ipo salama ai haipo katika hatari yaku default. As a matter of fact, historia ya uchumi wa kimataifa unaonyesha kwamba nchi nyingi ambazo zimekuwa ziki default madeni yao zile zenye Debt to GDP ratios way below 60%. Kwa maana hii, tofauti na wanasiasa wetu uchwara wanavyopenda umma wa watanzania uamini, Tanzania ipo katika hatari zaidi to default kuliko mataifa kama Japan, Uingereza au Marekani.
· Je kwanini nchi yenye high Debt to GDP ratio inaweza kuwa salama zaidi kuliko nchi yenye low ratio?
Jibu ni simple sisi Tanzania tupo more likely kukopa fedha katika sarafu nyingine kubwa nje ya fedha zetu za madafu (shilling za kitanzania). Kwa mfano ukitazama historia ya uchumi wetu, vyanzo vikubwa vya mikopo yetu karibia mara zote imekuwa ni vyanzo vya nje ya nchi, hivyo kukopa in dollars kuliko kutoka vyanzo vya ndani ambavyo vingeweza kutegemea sarafu yetu (yani shillingi). Kwa wastani, uwiano baina ya deni letu la nje na la ndani miaka yote umekuwa sio chini ya 70% (nje) na sio zaidi ya 30% (ndani). Kwahiyo, tofauti na wenzetu kama Japan, UK au USA, sisi hatuwezi kutumia mfumuko wa bei (printing money) to devalue sehemu kubwa ya deni letu kwa ufanisi iwapo tunalemewa na madeni. Hivyo njia pekee inayobakia kwa ajili ya wokovu wetu ni aidha wakubwa (IMF, WorldBank na washirika zao) watufanyie debt restructuring, watusamehe with strings attached katika rasilimali zetu, vinginevyo kinachofuatia ni defaulting ;
Ni muhimu pia at this juncture tukafahamu kwamba mbali ya Debt to GDP ratiokuwa moja ya vipimo vikubwa vya severity ya deni la taifa, kipimo kingine muhimu ni kile cha debt service ratio i.e. the ratio of debt service payments (principal plus interests) of a country to the export earnings of that particular country. Uwiano huu ukiwa chini, maanayake ni kwamba uchumi wa taifa husika una afya zaidi kuliko nchi yenye uwiano ulio juu.
Ni muhimu kwa wanasiasa wetu kuelewa kwamba tofauti iliyopo baina na matumizi ya debt to gdp ratio na ile ya debt service ratio. Kwa mfano, kipimo sahihi cha kubaini severity ya deni la taifa kwa nchi inayokopa kupitia vyanzo vyake vya ndani (local currency), key ratio to determine how large the debt is, ni debt service ratio. Na kwa nchi ambayo inakopa kupitia vyanzo vya nje (sarafu ya dollar), important ratio kuitazama ni debt to GDP ratio. Baadae tutaangalia ratio hizi kwa undani zaidi katika muktadha wa Tanzania ili kuelewa zaidi changamoto zinazotukabili. Kwa mfano, tutaona kwa undani zaidi jinsi gani Tanzania tunalipa more to service the debt kuliko tunavyotumia/wekeza kwenye sekta muhimu kama vile sekta ya Afya n.k.
Pia, baadae tutajadili kwa undani juu ya jinsi gani wanasiasa na policy makers wengi wamekuwa wakipuuzia management ya domestic debt na badala yake kujikita zaidi katika management ya external debt ambapo wamekuwa wakijikita na external debt management sana sana kutokana na pressure kutoka nje ya nchi kuliko political will. Vile vile tutajadili kwa undani jinsi gani external debt can be a threat to national security and nationa sovereignty, na kuna wakati baba wa taifa wakati ule anapingana na mzee mtei na kina IMF aliwahi kuhoji Je, kwani hao ni wajomba wetu huko nje mpaka watusaidua fedha? Vile vile tutajadili kwa undani kuhusu suala zima la nani wanatukopesha, mchakato wake upo vipi, na transparency kwa walipa kodi
Nihitimishe katika maeneo mawili: Kwanza ni msisitizo kwamba budget/fiscal deficit ni matokeo ya mapato ya serikali kuwa machache kuliko matumizi ya serikali in a given economic cycle. Kwa wenzetu wenye nidhamu ya juu kwenye suala hili (Fiscal Discipline), ongezeko la revenue ni matokeo ya ongezeko la output (GDP), income za individuals and income za businesses, na pia taxing the wealthy. Lakini kwetu Tanzania kuna kila ushahidi kwamba kasi ya kukua kwa uchumi (GDP growth) na ongezeko la vipato (biashara na individuals) havina uhusiano mkubwa na ongezeko la ukusanyaji wa kodi. Kwa mujibu wa utafiti mmoja, Tanzania ina potential ya kukusanya kodi at 21% of GDP. Kwa sasa, takwimu zinasema tupo somewhere around 16% lakini in reality, kiasi kinachokusanywa ni wa below the stated figure of 16%.
Pamoja na mapungufu haya, lengo la serikali ya Tanzania ni kufikishia mapato ya kodi kufikia 20% ya GDP ifikapo mwaka 2015 huku serikali pia ikilenga kupunguza utegemezi wa wahisani katika bajeti kufikia chini ya 10%; Kwa zaidi ya miaka 40, kiwango hiki kimekuwa kikicheza kati ya 30% na 40%; Katika miaka ya hivi karibuni, tumefanikiwa kushuka zaidi na kufikia in upper 20 percent. Swali linalobakia ni je, tuna mikakati gani endelevu ya kuhakikisha kwamba tunafikisha kiwango hiki kuwa in single digits i.e. kuifanya Tanzania iweze kujitegemea katika bajeti yake kwa at least 90% ifikapo 2015? Tunarudi pale pale we defy economics and glorify politics. Huwa tuna malengo mengi lakini yanaishia hewani kutokana na Lack of POLITICAL WILL. Tumeona initiatives mbalimbali za kina Zitto Kabwe, January Makamba na wengine bungeni kuhusiana na masuala kama vile kuongeza makusanyo ya kodi on projects and investments that are natural resource based, kuja na sheria kali kudhibiti money laundering, suala la capital gains tax, property tax, regulation of the real estate sector n.k. Ni muhimu kwa wanasiasa kutambua kwamba deficits huchangiwa sana na uzembe katika maeneo muhimu kama haya., na bila kuweka political will katik maeneo kama haya, Taifa kufikia 90% katika kujitegemea kibajeti na taifa kufikia potential yake ya 21% of GDP in tax revenues itaendelea kuwa ndogo za mchana;
Pili na Mwisho, tuelewe tu kwamba mjadala hapa au hoja ya msingi hapa sio kwamba tunatarajia serikali yetu kulipa deni lake lote and make Tanzania become a debt free nation kwani katika taifa lolote lile, debts rarely gets repaid. So the issue sio serikali ilipe madeni yake yote bali kama nilivyojadili tuwe na political will kuzingatia masuala kama vile golden fiscal rule na sustainable investment rule. Pia ni muhimu kwa political will kuhakikisha kwamba debt levels do not crowd out indigenous/local businesses or reduce their confidence, kwani unlike multinationals ambazo nyingi aidha hazilipi kodi au hazina activities zenye backward and forward linkages that create values senye manufaa kwa wananchi walio wengi, local businesses ni key katika kufanikisha haya in terms expanding the tax base, creating jobs n.k; Mwisho, kuna umuhimu wa kuhakikisha kwamba serikali inakuwa na uwezi to service its debt bila ya kuathiri investments katika sekta muhimu za uchumi zenye kugusa maisha ya walio wengi kama vile Elimu, Afya na Kilimo. Serikali yetu imekuwa inalegalega sana katika kutenga fedha za kutosha per agreements mbalimbali za kimataifa kama vile bajeti ya kilimo kuwa at least 10% of the GDP, huku pia allocation of budgets as percentage of GDP kwenye sekta muhimu kama afya na nyinginezo, the government has been living below its commitments.