Deni La Taifa: Wabunge, Wanasiasa Wachumi Na Wachumi Wanasiasa

Deni La Taifa: Wabunge, Wanasiasa Wachumi Na Wachumi Wanasiasa

Asante sana mkuu Mchambuzi kwa mada hii inayotugusa wote...

Kinachoniogopesha mimi katika suala hili ni hiki: Inawezekana kabisa wanaotukopesha wanajua kuwa hatuna uwezo wa kulipa madeni haya ila wanafahamu namna nyingine ambayo tutalipa madeni haya...ndio maana wanaendelea kutukopesha kwa kasi huku wakitufariji kuwa bado tunakopesheka!

Kitu kingine kinachonitia hofu ni malengo yetu na sababu za kukopa...Ni sawasawa na mlevi anayekopa hela ili akanywee bia. Asikwambie mtu bwana kama kuna hela unayotakiwa kuionea uchungu zaidi basi ni hela ya mkopo! Sisi hatuna discipline kabisa kwenye masuala ya pesa na inapofikia kwenye mikopo tunaichukulia kama ni zawadi na sio kitu ambacho sisi au wanetu/wajukuu watakuja kulipa huko mbele!
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mchambuzi,
Kuna swali lako umeniuliza huko nyuma nitaliangalia nikipata muda wa kutosha.
Umeongelea jambo moja muhimu sana katika #40 kwamba sisi tume violate principle zote za fiscal discipline.
Kwamba hatuwezi kukusanya na tunatumia hovyo. Kwamba mapato na matumizi hayawiani kabisa.

Wakati huo huo ni wazuri wa kukopa. Suala la kukopa ni siri ya elite ambao ndio wanafaidika nayo( report ya CAG) kwamba bilioni 600 are unaccounted for! na wala hakuna anayekuwa na wasi wasi.

Huu ukopaji ni sehemu ya violation ya principle za fiscal discipline. Kwamba tunakopa ili kununua vitu ambavyo huwezi kuvielezea baadaye. Hatuna sababu ya kukopa kwa ajili ya chakula! tunatakiwa tuwekeze katika uzalishaji wa chakula kwanza. Ni aibu kukopa chakula! wenzetu wanakopa kwa maendeleo siyo kununua mahindi. Hatuna sababu.
Bila kuwa na fiscal disc huwezi ku-manage revenue collection,debt na budget. Ni vurugu tu!

Bandiko hilo umeelezea kukopa kwa faida ya wachache, nadhani unanikumbusha jinsi ambavyo tunakopa mafuta ya kuendesha mitambo ya umeme kutokana na mgao unaosababishwa kwa makusudi na wakopeshaji.
Deni la ndani linazidi kutuna. Nadhani hivyo ndivyo inavyookea kwa chakula vinginevyo tusingekuwa na tatizo la chakula hata siku moja.

Nakumbuka kule Somalia, watu wakitafuta pesa basi wataanzisha mapigano ili mashirika ya kimataifa yatoe misaada ambayo inasimamiwa na wale wale walioanzisha vita. Ndivyo ilivyokuwa Burundi, kwamba wapiganaji hawakubaliani ili vikao viendelee Arusha na familia zao zikiishi uhamishoni kwa gharama za misaada ya usuluhishi.

Mkuu Kimbunga, hoja yako ina mantiki sana, tatizo ni kuwa katika nchi corrupt kama yetu ambayo inakosa kila aina ya management na political will, mimi sikubaliani na shughuliza ukandarasi kupewa wazawa.
Heri apewe mjapan mwenye aibu anayeweza kusema hiki si sahihi kuliko wazawa.

Mkuu Kimbunga, si wakandarasi wazawa ndio hao wanakusanya kifusi na kuita ghorofa halafu watu wanafunikwa?
Miradi yote waliyopewa wazawa kilichofanyika ni 10% tu na siku hizi ni pasu pasu. Unabaki na nusu nusu wanagawana wenye mradi. Kwa kweli nasimama kusema ni afadhali iende huko nje tubaki japo na daraja kuliko kubaki nchini bila daraja.
 
Unajua viongozi wetu wanapenda kucheza na takwimu na kupuuza facts, kwa ajili ya kuonesha kuwa wanafanya kazi lakini inafact hawafanyi kazi. Kimisngi naona suala la bajeti bado sio bomu la kisiasa kwa waliomadarakani, kwa hiyo wanajua tu bajeti itajadiliwa kwa siku mbili au tatu na itapitishwa bila kupingwa, lakini suala la bajeti na jinsi tunavyomanage finances inatakiwa lingaliwe kwa makini zaidi.


Mkuu, huu ndio uzi unaoshikiliwa sio tu na wanasiasa wetu bali hata pia wataalam ambao tunapaswa tutarajie bora toka kwao. Suala la uwezo wa kiuchumi wa nchi kuwa la kitakwimu zaidi badala la uhalisia ni jambo ambalo limekuwa linazungumzwa kwa muda na wadu wengi wa maendeleo na pengine kutoka na kuzungumzwa huku ni vyema baadhi yetu tukajibebesha jukumu la kuuelimisha umma kuhusiana, mosi na takwimu hizi, pili viashiria vya upimaji uwezo na tatu maana itokanayo na viashiria hivyi. Nimeona leo kwenye gazeti la The Citizen makala ya mhariri kuhusiana na ulazima wa ukweli kufahamika kuhusiana na deni la taifa. Ukichanganya maudhui ya tahariri hii na yale toka kwa ripoti za CAG kuna picha ya mbali inayoonekana kuhusiana na umiliki wa deni la taifa hususani ule unaohusiana na mafao ya watumishi. Suala hili la ukopaji unaohusisha vizazi mbalimbali ni jambo muhimu linalopaswa kuzingatiwa katika midahalo kama hii kutokana na hali ya sintofahamu itokanayo na kesho (future uncertainties). Je ni sahihi kumnyonya mfanyakazi wa leo kwa kumpoka stahili zake kwa ajili ya matumizi ya anasa? Je matumizi haya ya michango ya watumishi wa sasa yanalipa/yanawekezwaje maana hili nalo ni muhimu ili kujua endapo watumishi wa leo watawezwa kuja kupokea mafao yao pindi wakistaafu (ikiwa hii mifuko itakuwa na fedha za kulipa).

Jambo lingine la mzingi kuhusiana na matumizi ya takwimu ni kwamba takwimu ni tarakimu zingine tu na unless wananchi tuna uelewa mzuri wa viashiria mbalimbali ya kijamii, uchumi, biashara n.k, ni rahisi sana kwa mzalishaji wa takwimu kuweza kutueleza yale ayatakayo ambayo huweza pia kutokuwa sahihi. Basic economic literacy is needed to discern what really growth stats mean, je ni sahihi kwa wanasiasa na wataalmu kutuimbia habari za nominal growth badala ya real growth yenye kuzingatia athari za mfumuko wa bei? Hapa ndipo tunapopigwa bao. Inashangaza kusikia mtu akizungumzia per capita nominal growth rates za 6% na kusifu kwamba uchumi unakuwa ilihali mfumuko wa bei katika kipindi cha tathmini ulikuwa 6% au zaidi. Je mwananchi wa kawaida anakuwa ameneemeka katika hali kama hii?

Kwa kuhitimisha, kutokana na mtambuka uliowazi wa mapato na matumizi ya serikali na utaratibu iliyojiwekea wa kuwa na dira, mipango ya miaka 5, miaka 3 pamoja na bajeti za mwaka, naona wakati umefika sasa kwa urari huu wa mapato na matumizi kuangaliwa kwa kipindi kirefu zaidi ili kuweza kubuni njia za kuhakikisha ya kwamba madeni ya kizazi kimoja hayamishwi kwenda kizazi kingine bila ya kuwa na vyanzo vya kuamimika vya riba ya kuwezesha vizazi vijavyo kuweza kulipa nakisi hizi. Public finances are indeed an array of inter-generational transactions that must be accorded a deserving treatment without excessive discounting of the future.
 
Vile vile umezungumzia suala la informal sector and taxation; kwa mujibu wa takwimu zilizopo, informal sector in Tanzania accounts for about 50% of GDP and about 70% of total workforce, yet it largely remains untaxed; Hili ni tatizo, na sina maana kwamba poor farmers and petty traders mijini waanze kutozwa kodi; Maana yangu hapa ni kwamba serikali makini inaweza kuwajengea uwezo wote hawa kwa kuwapatia incentives mbalimbali for growth and eventually formalize them hasa on condition kwamba they register na Brela na TRA kabla ya kusaidiwa katika hatua za mbele zaidi; Umakini ukifanyika, mimi sidhani kama watanzania hawa watashindwa to comply na sheria za kodi; Mkuu bongolander, katika hoja yangu ya awali kuhusiana na leakages in the circular flow of income nchini, hoja yangu ilikuwa katika muktadha huu;

Mkuu just a word of caution, the informal sector thrives on remaining pseudo anonymous and relatively from regulation. The fact that it accounts for 7 in 10 of the workforce (I am sure this stat is a bit misleading for it definitely includes those in agriculture) stems from the ease of entry and exit and the relative degree of competition the sector affords its participants. In textbook economics, this is akin to a market resembling perfect competition. Regulation and taxation irrespective of their intent, adds to the cost of doing business and so long as this marginal returns from partaking in the informal sector do not exceed this cost, chances are plenty will fail to make a decent living from the sector leading to either a formalization of activities or cessation of activities (packing up). In a country where entrepreneurial acumen is largely lacking, abrupt regulation of the informal sector could be end up driving a nail through a half buried coffin. We do not want that!. What we need is to support the sectors, help them increase their scale, efficiency and returns before we begin to tax them. Mfano mzuri ni namna ambayo mobile money transfers have revolutionized financial services in the country in the absence of regulation irrespective of the profiteering by the big telecomms. The debate should be on how best can the state support benign infrastructure and struggling businesses. MKURABITA has some useful ideas but sadly they all seem to have been forgotten save for the construction of import/export zones and whatever attractive monikers they have assumed of late.

Pia, I think it is wrong to label our employment hotbeds as informal, the question we ought to asking ourselves is whether we want to perpetuate negative connotations about entrepreneurial spirit or to harness it. Statistics on the informal sector are largely misleading as a result of the failure of the ministry of trade to hold a countrywide census of industries and trades (not had one conducted since the late 1980s). In return this is probably what underestimates the contribution of industries and trades in the national accounts and consequently, assessments of the sector's revenue potential.
 
Wadau,

Mjadala mzuri sana, naombeni ruksa nihamishie mjadala katika muktadha wa kufanya examination iwapo kuna uhusiano wowote baina ya amount of foreignaid/debt nchini, our debt servicing na poverty reduction,hasa kupitia argument iliyopo kwamba Tanzania tunasifika duniani kwa uchumi mzuri (impressive economic growth), hivyo watanzania wapo ngazi za kuelekea mbinguni in terms of maisha bora(see world bank report:Tanzania on staircases to heaven);;Mtazamo huu wa uchumi unaosifika duniani ulikuwa echoed pia na waziri mkuu pinda wiki jana bungeni dodoma;

Kwanza na awali ya yote, ni muhimu tukafahamu kwamba kwa mujibu wa hao hao WorldBank, kuna three levels zinazotumika kupima indebtness of a country:

1)Less indebted countries
2)Moderately indebted countries
3)Severely indebted countries;

Nikianza na severe category - hii hutokoea iwapo present value ya debt service to GDP katika uchumi/nchi husika is greater than 80%, au present value of debt service to exports exceeds 220%;

Category ya moderate - ni iwapo either of these two ratios above zinavuka 60% lakini hazifikii extreme levels;

Category ya tatu yani less indebted maana yake ratio hizi zipo chini ya 60%;

Nadhani debt servicing ni dhana ambayo tunaielewa na niliijadili japo kidogo kwenye bandiko namba moja lakini definition yake hata kwenye google ipo straight forward;

Nikingia kwenye hoja yangu ya msingi, foreign aid (debt) malengo yake ni kusaidia nchi maskini kukuza uchumi hivyo kuwa katika nafasi nzuri ya kupunguza umaskini miongoni mwa wananchi; Ni katika muktadha huu, serikali yetu ikaja na vision 2025 kama definitive target ya kutokomeza umaskini within the AID framework;

Kuna pande mbili za hoja juu ya uhusiano baina ya Aid/debt, economic growth and poverty alleviation:

Upande wa kwanza wa hoja unasema kwamba (waumini wakuu ikiwa ni WorldBank,IMF na serikali yetu), kwa hoja kwamba:

*Kuna uhusiano wa moja kwa moja baina ya Aid/debt na poverty alleviation; foreign aid/mikopo ya riba nafuu being viewed kama transfer of resources kutoka nchi tajiri kwenda nchi maskini kama yetu, hoja inaendelea kwamba - resources hizi zikitumika vyema,basi zitasaidia to maximize economic growth na kupunguza kasi ya umaskini nchini; kuna sababu ya hoja hii kujengwa kwa mtindo huo kwani-kukua kwa uchumi wa nchi maana yake kuna ongezeko la uzalishaji wa bidhaa na huduma ndani ya uchumi husika katika sekta mbalimbali, na matokeo yake ni kwamba new jobs are created, existing jobs zinalipa wafanyakazi more salaries, wananchi wanapata choice ya bidhaa na huduma mbalimbali na za bei nafuu na ubora zaidi kutokana na ushindani katika uzalishaji, serikali inapata vyanzo zaidi vya kodi etc; katika mazingira haya, serikali inakuwa katika nafasi nzuri zaidi kuboresha huduma za kijamii kwa wananchi(hasa elimu na afya),serikali inakuwa na mapato ya kuiwezesha kuja na miradi mbalimbali ambayo ni labour intensive hivyo kutoa ajira, kwa mfano infrastructure development,serikali inakuwa katika nafasi nzuri ya kusaidia wakulima kupitia research, extension na irrigation schemes, lakini muhimu zaidi, serikali yenye political will kuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuleta mabadiliko (reforms) ya kimfumo na kitaasisia, hasa katika maeneo yenye kuleta hurdles katika livelihoods za wananchi walio wengi;

Huo ni upande wa kwanza wa hoja juu ya link kati ya aid/debt,poverty alleviation na economic growth kwenye uchumi maskini kama Tanzania; Kuna upande wa pili wa hoja ambao in a way ni vice versa unaosema hivi:

As long as madeni ya nje katika taifa husika yanaliweka taifa hilo on a future obligation to pay, growth potential ya nchi itakuwa affected negatively; kwa maana hii, growth yetu kwa miaka kumi ya wastani wa 7% kwa mwaka explanation yake ni nje ya Aid/debt framework na tutajadili hili uzi ujao; vinginevyo point ya msingi ya upande huu wa pili wa hoja ni kwamba - debt servicing ina negative impact on "growth and investment" na ndio maana ukiondoa chota chota ya madini na oil na gesi activities katika mlinganyo wa GDP ya nchi, uchumi wetu hauna tofauti kubwa sana in terms of growth na ule wakati wa ujamaa especially 1968-1978 ambapo wastani wake ulikuwa almost 6% katika kipindi chote; na tofauti na sasa, uchumi ule ulikuwa ni pro-poor growth kwani ulitokana na uzalishaji wa wananchi kwenye kilimo, viwanda, miradi mikubwa ya umeme n.k hivyo kutoa ajira kwa umma, na kuwaongezea vipato; pia enzi za ujamaa, sehemu kubwa ya pato la nchi kutoka kwenye exports ilirudi kwa wananchi; leo hakuna kitu kama hicho na the impressive GDP growth haina uhusiano wa maana na output,employment and incomes za walio wengi; kwa nchi kubwa kama marekani, hata growth rate ya 2% makes a huge difference kutokana na GDP kuwa inward looking kuliko sisi ambayo zaidi ni Outward looking or oriented;

Kwahiyo upande huu wa hoja una ujasiri wa kuhitimisha kwamba uhusiano baina ya aid/debt na GDP growth rates hata tukiachilia mbali impact on poverty reduction, ni uhusiano mdogo sana; this line of argument strengthens mtazamo wa wadau wote humu nguruvi3, kimbunga,bongolander,patlending,majany et al kwamba hatuendelei kutokana na misuse of funds;

Kama tupo pamoja, nihitimishe uzi huu kwa kusema kwamba - position ya worldbank, mizengo pinda na wanasiasa wengi wa ccm kwamba tunaelekea kuzuri ni position FLAWED;Hakuna link baina ya wingo wa mikopo yetu/ukubwa wa deni la taifa na kasi ya kukua kwa uchumi na kupungua kwa umaskini;hii inatokana na sababu nyingi lakini ikiwa ni pamoja na hoja yangu huko nyuma uzi kwamba faida ya mikopo hutokea pale tu rate of return on investments exceeds the cost of capital; kwetu hili ni vice versa i.e, returns za mikopo yetu licha ya kwamba taarifa zake hazipo transparent, lakini ni dhahiri kwamba returns zake zipo less that the cost of capital (principal na interests) kwani most of the funds from debt haziendi kuwekezwa kwenye sekta ambazo zinasaidia to generate GDP growth kwa faida ya wengi, na pia haziwekezwi vya kutosha kwenye sekta zenye mchango mkubwa kwa productivity ya taifa kama afya na elimu; most of these funds zinaishia kwenye posho, mishahara, procurement, magari ya kifaharu ya ccm na serikali yake, ma bungalow ya mafisadi sehemu mbalimbali ndani na nje ya nchi n.k;

Nitarejea for more, hasa kujadili zaidi uhusiano baina ya deni la taifa, kasi ya kukua kwa uchumi na kupungua kwa umaskini, hasa kufanya an examination katika uchumi wetu;

Cc nguruvi3,bongolander,zakumi,kimbunga,majany,pasco,patlending,mwalimu et al

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Patlending,

bandiko lako namba 44 presents us with a 'double edged sword' scenario whereby on the one hand, tukianza kutoza kodi informal sector without first kuwajengea capacity ya kuwawezesha kushiriki na kuwa na mchango in the main stream economy (formal economy), you are setting yourself/government for a major disaster;

On the other hand, by nature (almost), being informal implies kwamba - your activities (in most part) escape most taxes (not all taxes); And this can happen against the following background:

1. One Key link baina ya serikali na raia wake ni suala la kodi na matumizi yake katika utoaji wa huduma za jamii pamoja na public goods kama vile barabara, security n.k, zote ambazo chanzo chake ni mapato ya kodi;
2. Informal sector is where most economic activities plus livelihood strategies za wananchi walio wengi take place bila ya kujalisha size ya sekta hii ni underrated or overrated;
3. Wengi wa wananchi wenye shughuli katika sekta hii ni wananchi maskini ambao wanahitaji sana huduma za kijamii (hasa elimu na afya) ili kuwaondoa katika lindi la umaskini;
4. Legitimacy ya serikali yoyote inachangiwa sana na effectiveness na efficiency yake katika kukusanya kodi na matumizi ya mapato ya fedha za walipa kodi;

Swali linalofuatia ni je:

* Whats your Cost - Benefit analysis socially, politically and economically, kuhusiana na kuwaacha wananchi waliopo kwenye informal sector waendelee kuwa 'free riders' of various social services offered by the government pamoja na public goods mbalimbali kama vile street lighting, flood control systems, national defense, public security..., at the expense of tax payers (formal sector)? Is there any sustainability hasa on the benefits? And whats the optimal level in your view na such a level ina variables gani to consider, e.g. population growth, informal sector growth, health problems, illiterary, unemployment levels...? Pia hapa you should take into account juu ya political dimension of poverty ambapo nchi inaweza kuingia kwenye vurugu kutokana na madai ya wananchi maskini kwamba serikali haiwajali, serikali hiyo hiyo ambayo pia inaogopa to formalize them ili iweze kuwasaidia vizuri, hasa kwa kutegemea michango yao kupitia kodi...

Nilimuuliza nguruvi3 swali linalofanana na hili i.e. tufanye nini ili kuongeza our tax base huku mchakato ukileta faida kuliko hasara kwa taifa kisiasa, kijamii na kiuchumi; Ni swali gumu, mimi pia najaribu kutafakari mengi kwa kina;

Two more things to note:
1. Tunaambiwa kwamba our tax base has already been exhausted;
2. Tunaambiwa kwamba potential revenue to GDP ration ya taifa letu ni 21%; Mwaka wa fedha uliopita ilikuwa around 16%, huku serikali ikiahidi kwamba mwaka huu wa fedha (2013/14) kiwango hiki kitafikia 18%, na 2015 kufikia 20%; Kwa maana hii, we are 3% away from reaching our potential Revenue to GDP ratio, kwani mwaka huu serikali ilisema tunafikia 18%, huku potential ikiwa ni 21%; It would be interesting kujua uhusiano uliopo baina ya 21% ratio ya revenues to GDP na contribution ya informal sector to GDP which is said to be at 50%; pia hawa waliopo informal sector ni 70% of the labour force of which hatujui mchango wao katika kodi iwapo unaenda sambamba na na lengo la 21% revenue to GDP ratio, utatokana na income taxes au taxes za namna gani...
 
Patlending,

bandiko lako namba 44 presents us with a 'double edged sword' scenario whereby on the one hand, tukianza kutoza kodi informal sector without first kuwajengea capacity ya kuwawezesha kushiriki na kuwa na mchango in the main stream economy (formal economy), you are setting yourself/government for a major disaster;

On the other hand, by nature (almost), being informal implies kwamba - your activities (in most part) escape most taxes (not all taxes); And this can happen against the following background:

1. One Key link baina ya serikali na raia wake ni suala la kodi na matumizi yake katika utoaji wa huduma za jamii pamoja na public goods kama vile barabara, security n.k, zote ambazo chanzo chake ni mapato ya kodi;
2. Informal sector is where most economic activities plus livelihood strategies za wananchi walio wengi take place bila ya kujalisha size ya sekta hii ni underrated or overrated;
3. Wengi wa wananchi wenye shughuli katika sekta hii ni wananchi maskini ambao wanahitaji sana huduma za kijamii (hasa elimu na afya) ili kuwaondoa katika lindi la umaskini;
4. Legitimacy ya serikali yoyote inachangiwa sana na effectiveness na efficiency yake katika kukusanya kodi na matumizi ya mapato ya fedha za walipa kodi;

Mkuu sababu kuu ya kulipa kodi inatokana na haja ya kuwekeza katika huduma mbalimbali ili mlipaji kodi aje afaidike. Kwa mantiki hii ni muhimu kodi ikaonekana inamnufaisha mwanachi na vile vile pia zoezi zima la ulipaji kodi zikiwemo sheria, taratibu na kanuni husika zikamfanya mwananchi aone ulipaji kodi ni sehemu ya maisha yake na alifanye mwenyewe kwa hiari pasi shuruti. Kama vile ulivyoainisha kuwa sekta isiyo rasmi bado inalipa baadhi ya kodi na tozo mbalimbali kama vile VAT, kodi za mazao, tozo mbalimbali za maliasili, ushuru wa vizuizini n.k, vyote ambavyo havichukui muda mrefu kuvifanya, je unafikiri sekta hii inautayari wowote ule wa kubadili namna inavyojiendesha kwa kujirasimisha pale ambapo mzigo wa kodi halali ni kwa wastani asilimia 45.3 ya faida, tozo za kodi kwa ujumla zinaweza fika 48 kuanzia kodi husika za faida, tozo za uajiri pamoja na zingineo na pia ulipaji kodi unaoweza kuchukua mpaka masaa 172 au siku 7 (kwa mujibu wa tafiti ya mifumo kodi ya PwC, benki ya dunia pamoja na IFC ya mwaka 2013) ? Pili mwamko wa kulipa kodi kwa wanachi ni mdogo kutokana na kwamba ni nusu tu ya wananchi wanaona manufaa ya kodi yao katika huduma za jamii (Fjeldstad et.al, 2009). Ukichanganya haya masuala mawili kwa pamoja inakuwa ni rahisi kuona namna gani mwamko wa kodi ni mdogo sio tu kwa wale walio rasmi hata kwa wale wasio rasmi.

Nikiwa kama mzalendo, nilifurahishwa na hatua ya serikali kuamua kupunguza utegemezi toka nje kwenye matumizi yake ya mwaka. Nilitarajia kuwa uamuzi huu ungekuwa ni kimeng'enya (catalyst) kizuri cha kuisogeza serikali karibu na wananchi kupitia mlango wa uongezekaji wa uajibikaji kutokana na kuongezeka kwa matumizi ya fedha zetu wenyewe. Ila kilichotokea ni tofauti na matarajio, utegemezi umehama toka kwa mashirika ya kimataifa na nchi wahisani kwenda kwa taasisi binafsi za fedha, wakoloni mamboleo China pamoja na mifuko ya hifadhi ya jamii. Wakati huo huo, uwajibikaji umeishia katika nadharia kwa kuunda vyombo mbalimbali visivyokuwa na meno wala nia madhubuti ya kujenga uhusiano baina ya serikali na wananchi. Suala hili linaturejesha katika mdahalo mzima wa sekta isiyo rasmi na upinzani wake katika kuchangia mfuko wa serikali. Kwa kifupi ni kwamba, wasio rasmi hawaoni umuhimu wa kulipia chochote kwa sababu hawaioni serikali ikiwa upande wao katika kuwasaidia kupata mitaji ya kupanua shughuli zao, teknolojia na mafunzo stadi ya kuongeza ufanisi, miundombinu (hii ni public goods ambazo hakuna mwenye uwezo wa kuwazuia kutumia hata pale wanapokuwa hawajachangia na mara nyingi wanaona kuwa ni haki yao kutokana na kusalitiwa na watawala wao pindi wanapowahitaji), msaada wa kisheria, masoko n.k

Katika hili kabla la kuanza kufikiria kuwatoza kodi ni vyema tukarejea katika sababu hasa ya kushamiri na watu kuingia katika sekta zisizo rasmi na pia tukatambua umuhimu wa kuboresha shauku ya ujasiriamali badala ya kuiadhibu wakati ambapo taifa inahitaji fikra toka nje ya boksi.

Swali linalofuatia ni je:

* Whats your Cost - Benefit analysis socially, politically and economically, kuhusiana na kuwaacha wananchi waliopo kwenye informal sector waendelee kuwa 'free riders' of various social services offered by the government pamoja na public goods mbalimbali kama vile street lighting, flood control systems, national defense, public security..., at the expense of tax payers (formal sector)? Is there any sustainability hasa on the benefits? And whats the optimal level in your view na such a level ina variables gani to consider, e.g. population growth, informal sector growth, health problems, illiterary, unemployment levels...? Pia hapa you should take into account juu ya political dimension of poverty ambapo nchi inaweza kuingia kwenye vurugu kutokana na madai ya wananchi maskini kwamba serikali haiwajali, serikali hiyo hiyo ambayo pia inaogopa to formalize them ili iweze kuwasaidia vizuri, hasa kwa kutegemea michango yao kupitia kodi...


Mkuu swali hili sio rahisi kulitolea jawabu kwa sababu linamaudhui mengi tofauti. Mosi, ni vyema tukatambua kuwa si wote walio katika sekta zisizo rasmi ni masikini. Omari (1989),Wuyts (2001), Becker (2004) na Muller (2005) wameainisha kuhus uwepo wa wajasiriamali walio rasmi katika sekta hizi ambao huzitumia kutokana na mianya yake ya ukwepaji kodi, taratibu za uajiri, gharama ndogo za ajira n.k . Uwepo wa mabepari hawa hufanya tathmini ya sekta isiyo rasmi kuwa ngumu kidogo hususani katika suala la faida na hasara zake kwani huwa na uhusiano mkubwa baina ya matumizi ya sekta zisizo rasmi kama njia ya kusafisha fedha haramu, kuondoa nakisi kwenye vitabu vya mahesabu na kunyanyasa watumishi.

Kitu pekee kinachoweza kutuunganisha katika tathmini ya sekta hii ni suala la ajira. Katika hili jambi kuu ni uwezo wa mfumo usio rasmi kumwezesha mwajiriwa wake kuweza kupata mlo wa kila siku na pengine kuweza kujijenga kiufanisi amabo unaweza kumpatia uhuru wake kiuchumi. Ni kweli kwamba ajira nyingi katika sekta hizi huwa ni za malipo madogo, jambo ambalo huzua maswali kedekede kuhusu busara ya kuzirasimisha na kutoza kodi ajira hizi, kuingiza taratibu na sheria za ajira na usalama maeneo ya kazi, masaa ya kazi n.k. Mtazamo wangu binafsi ni kwamba serikali inapaswa ilenge zaidi kwenye kuhakikisha washiriki wa sekta hii wanajiajiri wenyewe na si waajiriwa wa mabepari wachache wenye kutaka kukwepa mkono wa serikali. Kwa kuwawezesha washiriki kuwa wakuu wao wenyewe wa kazi, serikali itaweza kuwa na sababu nyingi za kuwatoza kodi mbalimbali. Labda tu tumalizie kwa hapa, mtazamo wangu mimi ni kwamba kodi ni aina ya uwekezaji ambayo inatumia mfumo wa nipe-nikupe (quid pro quo), kwa wale walio katika sekta rasmi, kodi ni njia ya serikali kuchukua mchango wake katika kuwaelimisha na afya n.k ila kwa wengi ambao hawakubahatika pengine kutokana na mapungufu sera au sababu nyinginezo, serikali haina cha kuwadai kwenye kodi. Hivyo ni vyema kwanza ikawekeza kwenye kuwajenga kabla ya kuanza kuwadai kisicho chao. Mtazamo kama huu umekuwa unajidhihirisha siku hadi siku kwenye namna ambavyo vijana wengi katika sekta hii hususani wale wanaojihusisha na biashara ya usafiri kama vile bodaboda, vibarua masokoni na kwenye maeneo ya ujenzi, watumishi wa kwenye daladala, n.k wamekuwa wanatenda kana kwamba ya vile wapo juu ya sheria. Well swali la kujiuliza are they? Of course not ila effective governance including taxation is a quid pro quo business. Unless you give something, you shouldn't really expect anything in return.
 
Kimbunga,

Karibu sana katika mjadala; hoja zako hapo juu ni very compeling; Kuna two main arguments supporting nchi kukopa - political and economic arguments:

Nikianza na economic argument for borrowing ni kwamba borrowing is desirable as long as the rate of return on the said investments exceeds the cost of capital; investments hapa again maana yake ni zile kanuni za fiscal discipline kwamba mkopo lazima utumike zaidi on investments katika sekta zenye direct impact kwa maisha yalio wengi kama vile afya, elimu, kilimo, sio kutumia mikopo kwa ajili ya matumizio ya kawaida (mishahara na posho za watumishi wa serikali, wabunge, procurement deals za kampuni za wakubwa etc);

The second argument supporting borrowing ni political ambayo inasema kwamba - faida za mikopo will be felt with the current generation while mzigo wa kulipa madeni utabebwa na kizazi kingine; debt crisis ya Argentina ni mfano mzuri wa jinsi gani political argument ilitumika kufaidisha kikazi kimoja na kuja kuwa balaa kwa kikazi kingine;

In our case, hata hiyo economic argument haina mashiko kwani its obvious kwamba we borrow even at times when the rate of return falls below the cost of capital; kujua hili, tazama our debt service na jinsi gani ni kubwa kuliko hata our investments in Education and Health sectors;

Political argument kwetu Tanzania nayo haina mashiko licha ya ukweli kwamba hata ingekuwa na mashiko, it violates zile kanuni mbili za fiscal discipline, hasa the sustainable investment rule yenye lengo to avoid creation of an excessive burden ya debt repayments kwa vizazi vijavyo; Lakini hata kama for political reasons tuna amua kuvunja hii kanuni, bado the political argument supporting borrowing haina maana Tanzania kwa sababu gains of borrowing are not felt by the majority of the current generation bali wachache wanaofaidi mabilioni yasiyojulikana yapo wapi per CAG report;

Cc Nguruvi3, Bongolander

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums


Mchambuzi nimependa sana hizo line mbili za argument. Unajua watanzania tuliowengi kwanza hatujui ni wapi, lini na kwanini serikali yetu inakopa. Tunasikia tu tuna deni, yaani hapa tulipo tunadaiwa lakini hatujui tunadaiwa kwa nini.

Nianze kwanza kwa line ya kwanza ya hoja ya kiuchumi. Kwenye hilo mimi ni layman kabisa, labda wewe na members wengine mnaweza kunifungua macho. Hela tunazokopa tunaziwekeza wapi? je investement ya mkopo inaelekezwa kwenye maeneo ambayo yana return, yaani kwenye maeneo ambayo tunazalisha na kupata uwezo wa kujitegemea na kulipa madeni hayo? au tunakopa kwa jili ya kuwalipa mishahara watu ambao hawazalishi na kununua magari ya anasa ambayo hayasaidii kenye uzalishaji.

Kuna kitu kimoja kinakera sana kuhusu mentality ya wanasiasa wetu. Utasikia wanajidai kuwa tumewajengea barabara, tumewaletea maji, lakini ukiangalia ukweli utasikia hizo pesa ni mkopo kutoka benki kuu au IMF. Nimesikia wanasiasa wengi sana wakijidai kwa hili, lakini ukiuliza unasikia hela ni mkopo. I think this one telles all about the second line of argument on this, yaani wanasiasa kujitafutia ujiko kwa expense ya vizazi vijavyo.

Mchambuzi hivi kweli Tanzania tuna sera au plan inayoelekeza namna ya kukopa na kuinvest, na kama kuna lolote ambalo tunafanya kama nchi kutua mzigo wa madeni? kama unajua ningependa kujua pia kuwa ni asilimia ngapi ya revenues zetu inatumika kuservice deni la taifa.
 
1. Tunaambiwa kwamba our tax base has already been exhausted;
2. Tunaambiwa kwamba potential revenue to GDP ration ya taifa letu ni 21%; Mwaka wa fedha uliopita ilikuwa around 16%, huku serikali ikiahidi kwamba mwaka huu wa fedha (2013/14) kiwango hiki kitafikia 18%, na 2015 kufikia 20%; Kwa maana hii, we are 3% away from reaching our potential Revenue to GDP ratio, kwani mwaka huu serikali ilisema tunafikia 18%, huku potential ikiwa ni 21%; It would be interesting kujua uhusiano uliopo baina ya 21% ratio ya revenues to GDP na contribution ya informal sector to GDP which is said to be at 50%; pia hawa waliopo informal sector ni 70% of the labour force of which hatujui mchango wao katika kodi iwapo unaenda sambamba na na lengo la 21% revenue to GDP ratio, utatokana na income taxes au taxes za namna gani...

Mchambuzi hiyo ya pili naweza nikasita kuikanusha japokuwa ni wazi kabisa siiamini. lakini ya kwanza ni total bullshit kusema serikali imeexhaust vyanzo vya kodi. I am sure hapa JF ukiwaambia watu watoe mapendekezo kuhusu vyanzo vya kodi, in one day watu wanaweza kuja na vyanzo si chini ya vitano. Hapa naweza kuungana mkono na Ben Mkapa, kuna uvivu fulani wa kufikiri kwenye kauli hizo.
 
Patlending,

Nashukuru sana kwa mchango wako muhimu; Nitajaribu jadili hoja zako kwa kadri nitakavyoweza:

Kwanza naungana na wewe kwamba kinachoweza tuunganisha katika tathmini ya sekta isiyo rasmi ni suala la ajira; na pia umeelezea mikakati mingi ya serikali katika hilo pamoja na changamoto zake; kabla sijaingia ndani zaidi katika hili, napenda kukuuliza, je, iwapo approach sahihi ya kutathmini sekta hii ni suala la ajira, je unakubaliana na mtazamo wa serikali kwamba unemployment nchini ni 11%? Tathmini yetu ianze kwa kuangalia suala la unemployment in Tanzania from this point of view?

Pili, nakubaliana na wewe pamoja na watafiti uliowataja kwamba informal sekta haina watu maskini peke yake bali pia the well off; however, nadhani unaelewa kwamba interest yetu sisi humu ni the poor kwani they still remain to be the majority in that sector na ndio maana takwimu zinasema kwamba over 85% ya watanzania earn less than a dollar a day; how do we uplift these people from poverty by means of job creation inayochangia sio tu pato la taifa(GDP ) bali mapato ya serikali kupitia kodi bila ya kuathiri the social, political and economic stability, this needs to be our key area of analysis and discussion;na kimsingi nakubaliana na hoja zako nyingi kuhusu the way forward, nitachangia zaidi katika hilo baadae kidogo, hasa after kusikia mtazamo wako juu ya swali langu hapo juu;

Tatu ni kuhusiana na hoja yako kwamba maskini tayari wanakuwa captured na tax system kwa njia mbalimbali kama vile kupitia kodi za mazao, vizuizi n.k; kimsingi nakubaliana na wewe lakini haya yanatokea against a background ambapo sekta ya kilimo in terms of mchango wake kwa GDP is shrinking fast. It used to be at around 40 to 45% of GDP kwa muda, leo ipo in upper 20 percent; Pili, nguvu kazi sekta ya kilimo used to be at around 80% kwa muda mrefu sana, lakini leo, it is estimated to be between 65 and 70%; hii ni hatari kwa sababu, conventional wisdom says kwamba kupungua kwa labour force ya kilimo ni ishara ya agricultural transformation whereby labour inaenda into other productive sectors, hasa viwanda vilivyotokana na capital accumulation/savings za kilimo kwa ajili ya kupanua sekta nyingine, hasa viwanda; nadhani unakubaliana nami kwamba kupungua kwa labour force kilimo Tanzania hakuna uhusiano wowote na conventional wisdom ya uchumi niliyojadili;badala yake, kinachoendelea ni labour nyingi kuzidi kukimbia kilimo kwa vile hakilipi, na kuingia kwenye eneo lingine la infornal sector ambalo lipo very elusive - biashara ndogondogo za bidhaa na huduma ambazo nyingi ni, sio tu kwamba ni ngumu sana kuzi capture na mfumo wa kodi ukiachilia mbali boda boda na mambo kama hayo, bali ni very sensitive kuanza kuzitoza kodi bila maandalizi ya kutosha; kwa maana hii, ingawa upo sahihi kwamba wakulima ambao wengo ni informal, wanalipa kodi in one way or another, labour force erosion kilimo becomes counterproductive on that front;

Nne umezungumzia jinsi gani serikali inajitahidi kupunguza utegemezi wa wahisani wa nje katika bajeti yetu;swali langu kwako ni je, how sustainable is that? Kwa sasa, dependence ya donors kwenye bajeti ni less than 30% huku lengo kwa mujibu wa Mkullo (2011) ikiwa kuhakikisha utegemezi wetu unakuwa at 10% or less by 2015; bear in mind hoja yangu ya awali kwamba it has been argued kwamba our tax base has been exhausted, mwaka huu wa fedha matarajio ya mapato as pct of GDP nadhani ni 18%, huku lengo likiwa ni 21% by 2015, kiwango hiki kikiwa ndio potential ya uchumi wetu;Je, mapato ya kutufanya tuwe self reliant yatatokea wapi, wananchi?sekta ya madini na gesi? Kuna dalili gani kutuaminisha hili? Pia hapa usisahau kwamba punguzo la utegemezi wetu kwa external sources - wahisani kwenye bajeti linaenda sambamba na ongezeko la serikali yetu kuanza kutegemea vyanzo vya ndani vya mikopo tena in foreign currency, madhara yake ikiwa ni pamoja na crowding out private sector katika suala la mikopo ya biashara, lakini hasa SMEs ambazo ndio kimbilio kubwa la wananchi maskini waliokata tamaa na kilimo per my discussion earlier on;Katika hili, pia tukumbuke ripoti ya mwaka jana juu ya tathmini ya public finances conducted jointly na IMF/WB imeweka angalizo kwamba deni la taifa Tanzania is getting out of hand na bila umakini, ifikapo 2016, nchi itatumbukia katika crisis kama ya 1990s iliyopelekea uchumi wetu kuingizwa katika HIPC initiative i.e Highlt Indebted Poor Countries Initiative iliyolenga kuokoa nchi isi default debts!

Mwisho ni kuhusu mwamko wa wananchi kulipa kodi; kwa kiasi fulani upo lakini in the long run ni tatizo hasa iwapo rushwa TRA na kwingineko kunakotoza kodi wananchi itaendelea kupanda; moja ya sababu za msingi za Worldbank na IMF kusaidia to reform our tax sysyem miaka ya 1990s ilikuwa ni kupunguza rushwa kwenye ukusanyaji kodi,kuongeza ufanisi kwa kuwapa motisha watumishi wa TRA; as a result, mishahara na posho zao zikaboreshwa n.k; matokeo yake ni kwamba ingawa kuna makusanyo mengi zaidi kuliko huko nyuma, bado real targets haziwezi kufikiwa kutokana na ukweli kwamba TRA inanuka rushwa na ufisadi, na wananchi wanazidi kuona hilo katika nyanja mbalimbali za maisha yao, yet you expect wananchi hao to comply with tax rules and regulations...

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Pili na Mwisho, tuelewe tu kwamba mjadala hapa au hoja ya msingi hapa sio kwamba tunatarajia serikali yetu kulipa deni lake lote and make Tanzania become a debt free nation kwani katika taifa lolote lile, debts rarely gets repaid.

Got that. Lakini wakati tunaendelea kukopa, angalao tuwe na plan ya jinsi tutakavyolipa hili deni ninaloendelea kuongezeka kila siku.

Maana tukiendelea kulimbikiza deni bila kulipa, ipo siku hao tunaowakopa watagopa kutukopesha.
 
Nguruvi3,Vile vile umezungumzia suala la informal sector and taxation; kwa mujibu wa takwimu zilizopo, informal sector in Tanzania accounts for about 50% of GDP and about 70% of total workforce, yet it largely remains untaxed; Hili ni tatizo, na sina maana kwamba poor farmers and petty traders mijini waanze kutozwa kodi; Maana yangu hapa ni kwamba serikali makini inaweza kuwajengea uwezo wote hawa kwa kuwapatia incentives mbalimbali for growth and eventually formalize them hasa on condition kwamba they register na Brela na TRA kabla ya kusaidiwa katika hatua za mbele zaidi; Umakini ukifanyika, mimi sidhani kama watanzania hawa watashindwa to comply na sheria za kodi; Mkuu bongolander, katika hoja yangu ya awali kuhusiana na leakages in the circular flow of income nchini, hoja yangu ilikuwa katika muktadha huu;

Mkuu nguruvi3, kwahiyo upo sahihi ( at least kwa mtazamo wangu) kwamba idadi ya walipa kodi Tanzania ni ndogo kuliko our potential kwani kwa mujibu wa TRA, potential number ya walipa kodi Tanzania ni watanzania milioni 15 (kumi na tano), lakini actual tax payers to-date haizidi watanzania milioni mbili. Kwa maana hii, watanzania wenye uwezo wa kulipa kodi na ambao hawalipi kodi ni zaidi ya 85%; Nguruvi3, kwa mtazamo wako, tunageuzaje takwimu hizi ili walipa kodi Tanzania wawe angalau hata 50% ya watanzania wote wenye uwezo wa kulipa kodi na tuweke targets zipi na kwa vigezo gani?
Kabla sijachangia changamoto yako ningeseama kuwa mengi mumeyajadili katika mabandiko yako Mchambuzi, Petlanding na Bongolander ambayo nakubaliana nayo kabisa.

Bandiko#50 umesema kuwa WB ilifanya reform kwasababu ukusanyaji wetu wa kodi ulikuwa mdogo.
Pamoja na mambo mengine masilahi ya TRA yaliangaliwa kwa undani. Mimi sidhani kama tatizo lipo kwa watendaji wote wa TRA. Nadhani tatizo ni interference kutoka kwa viongozi wa serikali ambao vimemo n.k. ndivyo vinachagiza ukwepaji mkubwa sana wa kodi. Mathalani, wawekezaji hawawezi kugeuza majina ya business zao kukwepa kodi bila kuwa na baraka za viongozi.

Hatua muhimu ni kuifanya TRA iwe independent. Ndivyo nchi nyingine zinavyofanya.
Kwamba, taarifa za TRA zinaweza kufanyiwa kazi na taasisi nyingine kama bunge kwa kishindo.
Na ukweli kuwa hii ni sehemu muhimu ya uchumi, uteuzi wa viongozi wake lazima upunguze uwajibikaji kwa mtu mmoja.

Kurejea katika nukuu yako hapo juu, kuna kitu umegusia kuhusu BRELA na TRA. Nilikuwa nakwenda huko.
1. Ni lazima walipa kodi wajulikane. Kama tuna estimate ya million na wanaolipa ni 2 millions tuna tatizo kubwa.
Basically ni wale wanaolipa kwa kupitia mishahara, na biashara ndogo ndogo.

2. Kuhakikisha kuwa kila shughuli inasajiliwa na BRELA kwa kushirikiana na TRA. Na umeongelea informa sector
Hapa natofautiana nawe Mchambuzi kwasababu informal sector inapaswa kujulikana na kulipa kodi hata kama ni mkulima.

Nina maana kila mtu alipe fair share kwasababu sote tunatumia huduma zile zile za umma bila kujali vyanzo vyetu vya mapato.Hili litaongeza uchungu kwa mkulima anaposikia kuna bilion 600 unaccounted for, kuna mgao wa umeme wa kutengneza n.k. kwamba ukilipa kodi you feel it na hapo ndipo uwajibikaji wa kila mtu utakapokuwa na impact katika mabadiliko ya nchi. We need to feel pain, later evening sitting watching tv we will have the courage to pity Nchemba and Lusinde for abysmal performance at our expense. Lazima kila mtu ajaisikie maumivu ya kodi kwanza.

Informal sector ina watu wenye uwezo wa kulipa kodi. Nitakupa mfano, endapo mfanyakazi wa serikali kama mesenja anakatwa kodi kila mwezi kwa mshahara wa 200,000 ni kwanini mtu mwenye gereji anayetengeneza 600,000 asamehewe.
Kama tarishi anayelipwa 200,000 anakatwa kodi kwanani mwenye genge la nyanya anayetengeneza 200,000 asilipe.
Hii ni minimum kabisa kwa ajili ya majadiliano, tukienda kwa undani tutaona ukubwa wa sekta hii.

3. Kuwe na incentive kwa mlipa kodi, mathalani mtu mwenye rekodi za kulipa kodi hasa wale wa informal sector apewe unafuu ili naye alazimike kulipa kodi au kumlazimisha mwajiri wake kulipa kodi. Mfano mdogo tu kama mtu yupo informal sector basi akikata bima ya afya binafsi apunguziwe asilimia kadha endapo ana ushahidi wa kulipa kodi kutoka TRA.

4. Adhabu kali kwa wakwepa kodi. Kwa nchi za wenzetu mtu anapata unafuu wa adhabu ya kuiba pesa ofisini kuliko kukwepa kodi. Kukwepa kodi ni kosa linalofunga business yoyote ile. Waajiri wanaogopa sana kwasababu adhabu yake ni tatizo kubwa sana.Je, sisi tunafanya nini? Unakumbuka kesi za matycoon wa America.

5. Tuwe na ''sunshine'' list hasa ya makampuni. kwamba, mtu yoyote yule anaweza kuona kampuni gani inalipa kiasi gani.

6. Misamaha ya kodi isiwe suala la mtu mmoja au wawili. Iwekwe wazi katika taarifa za mwaka na sababu zake na jinsi gani misamaha hiyo imekuwa na manufaa au ilitarajiwa kuboresha kwa namna moja huduma za uchumi au za jamii kwa taifa. Msamaha ulitolewa na mamlaka ipi kwa kuzingatia vigezo gani.

Namna ya kuongeza mapato.
Kila mkoa upewe malengo ya ukusanyaji kodi, na hiyo iwe reflected katika mgao kutoka hazina kwa maendeleo au shughuli za uendeshaji wa mikoa husika. Nina maana pesa za kodi zisizambazwe tu bali zirudi kufanya kazi kule kuliko tarajiwa na zilikopatikana.

Kutumia mbinu za kisasa za kubaini walipa kodi, ikiwa ni pamoja na nguvu kazi ya formal na informa sectors.
BRELA na TRA ziwe huru na uongozi upatikane kwa vetting na siyo appointment.
Zipewe malengo na sio kujipangia malengo.

Mwaka juzi TRA ilisema wamekusanya 110% ya malengo, sasa inakuwaje tuna watu 13 milion wasiolipa kodi.
Malengo hayo yamefikiwa vipi na kwa hesabu gani. Huu ni udanganyifu wa kupeana bonus kwasababu wao ndio wanaopanga malengo. Haiwezekani kukawa na 110% huku 13Million hawakulipa kodi.

Kuangalia na kuziba mianya katika sehemu kuu za uchumi kama bandari, migodi n.k.
Kuziba leakage katika miradi inayotumia fedha zaidi ya ilivyokadiriwa.
Kuweka malengo ya kumalizika miradi bila kuwa na bajeti ya ziada.
Kama mradi umetengewe bilioni 120 kusiwe na bajeti ya ziada baada ya hapo.

Kuondoa ruzuku kwa miji na majiji. Hivi kwanini Jiji la Dar lipewe ruzuku na si kutoa kwa serikali.
Something is wrong! Ondoa ruzuku kila mmoja asimame kwa miguu yake. Asiyeweza akae pembeni.

Kuwaagiza TRA kutafuta vyanzo vingine vya mapato zaidi ya bia na sigara.
Kwamba kila bajeti mpya lazima kuwe na ubunifu. Hiwezekani tusubiri kodi ya vocha za simu wakati sekta ya utalii ina uwezo mkubwa sana wa kukusanya kodi pengine zaidi ya hiyo. Tunafanya nini na mito ya maji, bahari na maziwa ambayo ni resource nzuri sana za revenue.

Iweje kuwe na taifa linalotegemea uvuvi nasi tushindwe tukiwa tumezungukwa na maziwa makubwa dunia na bahari kama wenzetu. Tunafanya nini kupata mapato kutoka sekata ya uvuvi?

Kwanini nchi za wenzetu kama Kenya na Uganda remittance za diaspora ziwe sehemu muhimu ya kuongeza mapato sisi tuache tu akina western union wakusanye kwa niaba yatu. Kunafanyika nini katika ku-tap kodi zitokanazo na remittance.
Mtu anaweza kudhani ni kiasi kidogo, lakini angalia kodi za makampuni halafu linganisha na income inayoweza kupatikana.

Kupunguza matumizi ya serikali ikiwa ni pamoja na ukubwa wake.
Kupunguza miradi isiyo ya lazima kwanza na kuhakiki ile iliyopo inakamilika.

Juu ya yote ni kuwa na political will na hiyo ni kazi ya wananchi.
Kwamba serikali isipo deliver ni kuiweka pembeni haraka.

Nimeona nchi moja ya magharibi, kulikuwa na mradi ambao kwasababu zisizojulikana ulizidi kwa dollar 150,000.
Hili lilikwenda na maji na waziri mkuu aliyekuwepo madarakani ingawa hakuhusika.

Niseme kama hakuna fiscal discipline, known source of income, good tax collection, na political will, tutaendelea kukopa, interest inaongezeka na siku moja watakuja tena na kusema kama rais wenu hatapanga chumba manzese ili kumwachia mwekezaji nafasi magogoni hatuwapi. Tutafanya nini!
 
Mkuu Ngongo,
Umegusia suala la mawasiliano hasa ya reli. Huko nyuma Mchambuzi ameeleza kuwa kuna uwekezaji usiozingatia principle bali utashi wa kisiasa. Yeye alisema bara bara zinazojengwa ni dendric badala ya pipeline la economy.

Katika mataifa yanayosonga mbele usafiri wa reli ni muhimu sana, utashangaa nchi kubwa kama Marekani na Uingereza bado zinatumia huku China ikija kwa kasi sana. Reli ni lifeline ya nchi zilizobahatika kuwa nazo. Sielewi kwanini reli ya kaskazini imekufa! hakuna sababu! Hata atakayesingizia mkonge na kahawa bado anapaswa kujiuliza malori yanayosafiri kila siku yanapeleka nini, mabasi yanapeleka nini.

Katika kipindi hiki cha EAC reli zile zingekuwa ni investment kwa nchi jirani. TAZARA ipo underutilized na reli ya kati iking'olewa mataruma na wawekezaji wa kihindi kwa kushirikiana na viongozi wa serikali kwa kitu kinachoitwa 10%.
It's abdurd, outrageous and insane.

Juzi kumezinduliwa mradi wa bandari ya Bagamoyo. Hii ya Dar ni underutilized and negleted.
Ukiangalia kwa makini ili bandari ya bagamoyo iwe effective na productive lazima iwe na link na railways ambazo zinaanzia Dar.Labda wanajamvi mniambie kutoka economic point of view the sustainability and viablility of Bagamoyo port.

Kuhusu ukubwa serikali, hili nalo tumeliongelea. Kwahakika hilo ni tatizo kubwa sana.
Unapokuwa na baraza la mawaziri kubwa kuliko nchi ya Ufaransa au Uingereza kuna tatizo.
Matokeo yake ni watu kutokuwa na kazi za kufanya na kujiingiza katika kupitisha miradi yao kama tulivyoona bandari.

Mkuu Majany, kelele za Nyerere zilikuwa kuhusu mataifa makubwa kutoa mikopo halafu kuchukua pesa nyingi kutoka mikopo hiyo. Mchambuzi ameeleza kuhusu south south commission na agenda zake.

Kwa ufupi alichokuwa anasema Nyerere ni kuwa badala ya kujaza mikopo kwa nchi masikini halafu kuchukua kwa mkono mwingine kikubwa zaidi ya walichotoa, nchi hizi zingetoa unafuu wa mikopo na riba au kufuta baadhi ya madeni.
Hili lingesaidia vinchi masikini vijenge uwezo wa kuweza kukopa baadaye na kulipa.

Sasa kwa upande wa Mkapa, yeye alikuwa analipa madeni kupunguza deni la taifa na riba zitokanazo.
Wakati hayo yakifanyika huduma za jamii na zile za kuwakwamua masikini zinakuwa zinazorota. Kwa maneno mengi baada ya kulipa deni tutarudi kukopa tena kwasababu hakuna uwezo uliojengwa ili kutuwezesha kuwa wakopaji na walipaji.

Ni kelele za akina Nyerere ndizo zilishtua wakubwa kwa kiasi fulani na kuja na HIPC ambayo ilitokana na mazungumzo ya Paris Club.

Tunaweza kutokubaliana kwa mambo mengi kuhusu Mwalim, lakini lazima tujiulize katika miaka zaidi ya 30 tangu ameondoka madarakani kuna mikopo gani ambayo imewekezwa kama yeye alivyofanya?

Hapa naomba kutoka nje kidogo ya mada na kuwa 'biased' bila kuudhi au kukirihisha mtu.
Nyerere alikuwa na Political will ndiyo maana project zake zililenga zaidi katika kuhakikisha tunajitosheleza kwa uchache na tunajiendeleza kutokana na nyakati.

1. Aliwekeza katika miundo mbinu. Hakuna miundo mbinu iliyojengwa au inayojengwa sasa ambayo haina blue print ya utawala wa Nyerere. Akawekeza katika vitu kama TAZARA, Reli ya Kaskazini n.k. ambazo leo zinabaki kuwa sehemu muhimu sana ya uchumi.

2. Akawekeza katika viwanda ili kuhakikisha kuwa kama hatuwezi kuuza ''AGOA'' basi tuuze kwa jirani. Ndivyo ilivyokuwa katika baadhi ya bidhaa za viwanda kama nguo, matairi, betri, maziwa kwa uchache.

Akawekeza katika kuhakikisha kuwa spea zinapatikana hapa zile za uwezo wetu, food proceesing industries n.k.
Yote yalihakikisha kuwa si tu yanakuwa na faida kiuchumi lakini yanakuwa na social impact katika vitu kama ajira.

Mazingira yanabadilika na hatutegemei hali ingebaki hivyo, lakini basi tulipaswa kuanzia alipoachia.
Sasa tumeua viwanda, miundo mbinu halafu tunakopa kuwekeza katika miundo mbinu ile ile n.k.

Nimalizie kwa kusema ili kuweza ku-tackle tatizo lazima kwanza tuanze na fiscal discipline, tupunguze leakage, tuongeze revenue kwa njia za kisasa na kitaalamu(tuache kutegemea kodi za bia na vocha za simu), tuwe na management ya kukopa na tuwe na uwezo wa ku-invest kwa kuona return iwe direct or indirect.

Tunaweza kabisa kwa muda mfupi,if and only if the ''political will'' will prevail.


Nguruvi3;

Nyerere hakuwa mtaalamu wa mambo ya pesa au uchumi wa fedha. Na kwa bahati mbaya katika kipindi chake cha utawala nchi pia ilikuwa haina utaalamu wa mambo ya pesa na hilo tatizo bado lipo mpaka sana.

Lawama halizotoa kwa nchi za magharibi na vyombo vyao vya kifedha zilikuwa hazina maana yoyote kwa sababu hata vyombo vyetu vya ndani vya kifedha vilikuwa vinaendeshwa kienyeji-enyeji tu.

Umefika watanzania tuwe serious na hili jambo. Mkopeshaji anapokupa pesa anaangalia uwezo wako wa kulipa deni

Nchi, taasisi au mtu binafsi mwenye vyanzo vizuri vya kulipa deni, siku zote atapata mikopo yenye masharti mazuri. Kwa upande mwingine, nchi yenye vyanzo vibaya itapata mikopo yenye masharti mabaya.
 
Nguruvi3;

Nyerere hakuwa mtaalamu wa mambo ya pesa au uchumi wa fedha. Na kwa bahati mbaya katika kipindi chake cha utawala nchi pia ilikuwa haina utaalamu wa mambo ya pesa na hilo tatizo bado lipo mpaka sana.

Lawama halizotoa kwa nchi za magharibi na vyombo vyao vya kifedha zilikuwa hazina maana yoyote kwa sababu hata vyombo vyetu vya ndani vya kifedha vilikuwa vinaendeshwa kienyeji-enyeji tu.

Umefika watanzania tuwe serious na hili jambo. Mkopeshaji anapokupa pesa anaangalia uwezo wako wa kulipa deni

Nchi, taasisi au mtu binafsi mwenye vyanzo vizuri vya kulipa deni, siku zote atapata mikopo yenye masharti mazuri. Kwa upande mwingine, nchi yenye vyanzo vibaya itapata mikopo yenye masharti mabaya.
Zakumi, nilipoongelea suala unalonukuu nilisema wazi kuwa natoka nje ya mada ili kuweka hoja yangu sawa. Sikuwa na maana ya ku-politicize mada hii. Nadhani turudi kwenye mada halisi. Ahsante
 
Patlending, bongolander nguruvi3, zakumi na wengine,

Samahani kwa kupotea kidogo, nitarudia hoja zenu nyingi muda sio mrefu, nimeshazipitia, na kwa vile nipo kijijini na sina computer, matumizi ya simu yananipunguza spidi kidogo lakini tupo pamoja; nitajadili hoja zenu nyingi muhimu sana ambazo zime raise very useful questions, na ningependa nizijadili katika muktadha wa bajeti inayoishia juni mwaka huu ili tupate picha halisi juu ya nidhamu yetu katika fedha za umma; wanasiasa wachumi wetu na wachumi wanasiasa huwa tunawaacha wa get away na mambo mengi kwani baada ya bajeti ywa mwaka X kutoka, huwa tuna tabia ya kuijadili na kuachana nayo; kwa mfano ikija bajeti mwaka mwingine wa fedha, mijadala yetu huwa haichambui targets na objectives za bajeti ya awali iwapo zina compliment au contradict targets na objectives za mwaka mpya wa fedha, badala yake wengi huwa tunakimbilia tu kujadili kodi na jinsi gani zinamsaidia au zinampa mwananchi nafuu huku conclusion zetu zikibaki superficial; haya nayosema tutayashuhudia mara bajeti mpya itakapotoka kwani tutaona misururu ya nyuzi ambazo hazitakuwa na uhusiano wowote kuhusiana na tumetoka wapi na bajeti iliyopita, badala yake tunaenda wapi; nina matumani kwamba angalau nyinyi mtakuwa mnarudi rudi humu kujadili bajeti mpya in the framework of analysis tuliyojitengenezea humu;

Ukitazama kwa mfano, bajeti ya kilimo tayari imeshatoka na inajadiliwa bungeni na hii ndio soul ya uchumi wa two thirds of Tanzanians lakini no one is discussing it, na wengi watakuja kuijadili pale itapotajwa ndani ya hotuba ya waziri wa fedha wakati as of today tayari its public knowledge kiasi gani kimetengwa, kwa ajili gani, lakini muhimu, jinsi gani wanavijiji wanavyoendelea kupuuzwa na ccm kwa style ile ile mwalimu aliyoonya miaka zaidi ya arobaini kwamba:

["Foreign aid is not an answer to Tanzania's problems; There are many needy countries in the world; and even if all the prosperous nations were willing to help the needy countries, the assistance would not suffice;Nor would borrowing help..Whether is is used to build schools, hospitals, houses or factories, it still has to be repaid;where then shall we get it from? We shall get it from the villages and from agriculture. If we are not careful, we might get to a position where the real exploitationin Tanzania is that of the town dwellers exploiting the peasants"]

Forty something years later, we can still resonate with a lot of this view, if not in its entirely kwani deni limezidi kupaa huku worldbank wakionya kwamba kwa mwendo wa sasa, ifikapo 2016 deni la taifa litakuwa unsustainable; yet, ukuaji wa deni hili hauendi sambamba na ukuaji wa kipato cha mkulima over time, yani kuna an inverse relationship between the two;

Pia bajeti yetu kilimo inaendelea kuwa against makubaliano ya SADC kwamba iwe at least 10% of the total budget; ni miaka si chini ya sita sasa since makubaliano haya lakini hatujawahi kufikia 10% level; yet serikali ya ccm inajisifia kwamba uchumi unakua na uzalishaji sekta ya kilimo unakuwa, swali ni je unakuwa in real terms or nominal terms? In real terms, sekta hii haijawahi kukua kuliko kipindi cha mwalimu ingawa mimibaba haupendi hoja hizi;vile vile ukiangalia nyakati hizi real growth ya sekta hii after taking care of inflation (yani kuachana na nominal growth), kiwango chake ni kidogo sana kwani inflation rate has ALWAYS been higher than growth rate ya kilimo at least since late 1980s;

Wanasiasa wetu wachumi na wachumi wanasiasa na wabunge wasio makini wanasahau kwamba growth of output kilimo haijawahi tokana na increase ya investments in the sector via research, extension, irrigation, bali via increase in farm size kwa methods zile zile za jembe la mkono; sasa given the high land holding per person in Tanzania (close to 2 HA per person), hii strategy ya ccm kisera kupitia ilani yake ya kuongeza output ya kilimo kwa njia ya increase in land size at the expense of low investments in the sector isn't sustainable; again, economics is defied, politics is glorified, at its best;sera ni unsustainable given the fact that an increase ya pressure on this LIMITED resource (land), tunajenga a timing bomb in the sector, pengine mapinduzi, sio ya kilimo bali ya wakulima waliochoka kwani miaka nenda miaka rudi, productivity per capita ipo chini sana kutokana na sababu nimejadili hapo juu, income zao haven't substantially improved, yet they feed the urbanites, elites included, they bring in 50% of forex that doesn't flow back to them in terms of social services, leading to a scenario narrated na mwalimu hapo juu; cha kujivunia ccm when it comes to wakulima may be ni ujenzi wa barabara kurahisisha mazao yakimbie haraka nje kwa mtindo ule ule wa serikali ya ukoloni, tofauti ikiwa hawalazimisishwi kulima kwa fimbo na bunduki, kama hawataki,wafe tu njaa au kuna informal sector waiting for them to diversify their livelihoods kwa kuuza vocha,mikanda ya video n.k huko mijini; mafanikio mengine pengine ni kumfikishia mkulima mnara wa simu;lakini mnara huo haujamsaidia kutattua the imperfection of market information kwake kwani hawajui masoko yapo wapi, hawajui bei nzuri zaidi ipo wapi, wakijaribu bahatisha kwa kwenda nchi jirani kuuza mazao yao, serikali ile ile ambayo mwalimu kaijadili japo juu inakuja mzuia na ni kwa political reasons kuliko economic kwani mazao mengi yasingekuwa yanajiozea mikononi mwa wakulima baada ya kuingiliwa na nguvu ya dola;

Suala la mbolea na pembejeo ndio balaa kabisa jinsi gani ufisadi unavyoumiza wakulima huku serikali ikijua maovu mengi huko lakini inakaa kimya;

Nitarejea na sehemu ya kwanza ya mjadala wa maeneo muhimu ya bajeti ya 2012-13 kuhusiana na targets and objectives ili bajeti mpya ya 2013-14 ikitoka, tuweze kuipima kwa KPIs (key performance indicators) zinazoeleweka;


Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Mkuu Mchambuzi,
Katika bandiko lako hapo umeongelea mengi. Nigusie machache yaliyonigusa sana.

Kwanza ni kuhusu bajeti. Kwakweli nashangaa sana kuona watu wanakaa Dodoma bila kuuliza bajeti iliyopita imefikia malengo gani, ilikuwa na mapungufu gani n.k.

Nikuchekeshe kidogo, katika vikao vya harusi huwa kuna kitu wanasema kupitia taarifa ya kikao kilichopita. Halafu wanajadili abcd zitokanazo. Huko ni mitaani tu! imagine bungeni hawawezi kufanya hilo. Is it silly, is it ignorance or is it narcissism

Pili, umegusia Kilimo. Hili ni eneo ambalo halipewi kipaumbele hata kama ndiyo 2/3 inategemea.
Sisi si taifa la viwanda na wala biashara kama za utalii na madini hazionekani kutusaidia.
Nilidhani kilimo ndicho kingetutoa japo kwa namna fulani. Hapa ndipo ambapo tungeweza kupata export!

Sasa tunaongelea kuhusu makusanyo ya kodi kwa kutumia sigara na bia. Tunasahau kuwa hiyo ni local initiative ya ku-sustain economy, ni lazima twende katika world stage kama tunahitaji kupiga hatua.
Hapo ndipo Export inapoingia.Nadhani nyuma umeelezea vema tatizo la import/export imbalance na jinsi gani linaathiri growth au ku-encourage inflation

Wenzetu duniani baada ya mdororo wa uchumi waliamua kufanya kitu kinaitwa austerity measures.
Austerity measure zimelenga katika kuhakikisha kuwa resource zilizopo zinatumika katika kujenga upya uchumi.

Kwanini basi nasi tusiwe na Austerity measures kwa kipindi cha miaka kama 10 ili kuelekeza resource zetu katika maeneo yatakayokuwa platform ya ku-take off. Na hapa nasema huduma za jamii zisiathiriwe ikiwa ni pamoja na ulinzi na usalama.
Lakini basi tuondoe baadhi ya vitu ambavyo si muhimu kwanza.

Mtu atauliza zipi ni sehemu zisizo za muhimu?
Well, nitatoa mfano. Moja ni kpunguza matumizi ya serikali. Hakuna sababu ya kuwa na wizara ya akina mama na watoto wakati huo huo kuwa na wizara ya Afya. Vipi kama akina mama na watoto wakawa idara ndani ya wizara ya Afya.

Hatuna sababu ya kuwa na mlolongo wa viongozi wasio na kazi.
Fikiria hapa Dar. Kuna Mkuu wa Mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa wilaya, maafisa tawala, mameya na utitiri wa namna hiyo. Hawa wote wanafanya kazi gani?

Kwanini matumizi yatokanayo na kuondoa ufujaji wa fedha yasielekezwe katika kukuza kilimo(modernization of agric )eneo ambalo pengine tunaweza baada ya kushindwa utalii na madini.
 
Mkuu Mchambuzi,
Katika bandiko lako hapo umeongelea mengi. Nigusie machache yaliyonigusa sana.

Kwanza ni kuhusu bajeti. Kwakweli nashangaa sana kuona watu wanakaa Dodoma bila kuuliza bajeti iliyopita imefikia malengo gani, ilikuwa na mapungufu gani n.k.

Nikuchekeshe kidogo, katika vikao vya harusi huwa kuna kitu wanasema kupitia taarifa ya kikao kilichopita. Halafu wanajadili abcd zitokanazo. Huko ni mitaani tu! imagine bungeni hawawezi kufanya hilo. Is it silly, is it ignorance or is it narcissism

Pili, umegusia Kilimo. Hili ni eneo ambalo halipewi kipaumbele hata kama ndiyo 2/3 inategemea.
Sisi si taifa la viwanda na wala biashara kama za utalii na madini hazionekani kutusaidia.
Nilidhani kilimo ndicho kingetutoa japo kwa namna fulani. Hapa ndipo ambapo tungeweza kupata export!

Sasa tunaongelea kuhusu makusanyo ya kodi kwa kutumia sigara na bia. Tunasahau kuwa hiyo ni local initiative ya ku-sustain economy, ni lazima twende katika world stage kama tunahitaji kupiga hatua.
Hapo ndipo Export inapoingia.Nadhani nyuma umeelezea vema tatizo la import/export imbalance na jinsi gani linaathiri growth au ku-encourage inflation

Wenzetu duniani baada ya mdororo wa uchumi waliamua kufanya kitu kinaitwa austerity measures.
Austerity measure zimelenga katika kuhakikisha kuwa resource zilizopo zinatumika katika kujenga upya uchumi.

Kwanini basi nasi tusiwe na Austerity measures kwa kipindi cha miaka kama 10 ili kuelekeza resource zetu katika maeneo yatakayokuwa platform ya ku-take off. Na hapa nasema huduma za jamii zisiathiriwe ikiwa ni pamoja na ulinzi na usalama.
Lakini basi tuondoe baadhi ya vitu ambavyo si muhimu kwanza.

Mtu atauliza zipi ni sehemu zisizo za muhimu?
Well, nitatoa mfano. Moja ni kpunguza matumizi ya serikali. Hakuna sababu ya kuwa na wizara ya akina mama na watoto wakati huo huo kuwa na wizara ya Afya. Vipi kama akina mama na watoto wakawa idara ndani ya wizara ya Afya.

Hatuna sababu ya kuwa na mlolongo wa viongozi wasio na kazi.
Fikiria hapa Dar. Kuna Mkuu wa Mkoa, wakuu wa wilaya, wakurugenzi wa wilaya, maafisa tawala, mameya na utitiri wa namna hiyo. Hawa wote wanafanya kazi gani?

Kwanini matumizi yatokanayo na kuondoa ufujaji wa fedha yasielekezwe katika kukuza kilimo(modernization of agric )eneo ambalo pengine tunaweza baada ya kushindwa utalii na madini.

Mkuu tukiangalia suala la deni la taifa na jinsi tunavyotumia pesa zetu, unaweza kuona kuwa hakuna juhudi za maana za kulipa deni hilo. Kuna mentallity fulani kwa viongozi wetu kuwa nchi si kama mtu, yaani hata ikikopa kiasi gani na kuwa na deni kiasi gani haiwezi kufungwa. Mentality ya ajabu sana kwani ukiangalia kwa namna fulani unaona kabisa nchi inafungwa, japo si gerezani. Kuendelea kuservice deni la taifa ni sawa na kutoa free labour.

Nakumbuka kuna siku Mraba alikuwa anaongea kuhusu kufutiwa deni, majibu yake yalikuwa ni jambo zuri, na tutalipa zile zinazobaki ili tukope zaidi. Lakini alipoulizwa hizo tunazokopa tunatumiaje? majibu yalikuwa siasa siasa siasa.

Vile vile tukijaribu kuangalia jinsi tunavyotenga fedha za bajeti za kilimo na madini, na nyingine zinazozalisha utaona kuwa pesa nyingi haziendi kwenye investment, bali zinaenda kwenye current expenditure. sababu kubwa ya hilo ni siasa, na kutokuwa na mentality ya kuwekeza na kulipa deni. Sababu hiyo hiyo ndio inafanya kuwe na mlundikano wa maofisa hata wasiotakiwa, wasio na qualification na wasio perform. Ukiangalia baadhi ya viongozi unaweza kuona kuwa wako madarakani ku-enjoy, kupokea fadhila na wengine ni kupata ulaji, na wengine kurudisha oinvestment zao walizoweka wakati wa uchaguzi na kupata profit zaidi, na sio kufanya kazi kwa ajili ya Tanzania.

Kwa nchi kama Tanzania sekta ya kilimo, utalii na madini zilitakuwa kupewa nguvu zaidi, na kimsingi ndio sekta zenye potentila kubwa zaidi ya kutuokoa watanzania. Lakini sera halisi zilizopo (yaani zinazotekelezwa kihalisi, tofauti na zilizoandikwa kwenye manifesto) zinaifanya sekta hizo ziendelee kuwa chanzo cha ulaji kwa watu fulani, na sio kusaidia maendeleo ya uchumi na kutusaidia kulipa deni.
 
nguruvi3, bongolander,

Wakuu nguruvi3, bongolander et al

Ili kubaini nidhamu ya serikali katika maeneo haya mliyojadili, nadhani itakuwa ni jambo la muhimu sana iwapo tutaichambua bajeti iliyopita (2012-2013) katika maeneo muhimu, hasa kujikita katika kubaini MALENGO ya Serikali na VIPAUMBELE, dhidi ya CHANGAMOTO zipi bila ya kusahau Serikali ilitarajia kufanikisha vipi MALENGO husika; Ni imani yangu kwamba kwa kufanya hivi, tutakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kuipima na kuichambua bajeti ya mwaka mpya wa fedha inayotarajiwa kutangazwa hivi karibuni;

Kufikia Mwisho wa mwaka wa fedha uliopita (second quarter of 2012), ongezeko la deni la taifa kufikia shillingi trillioni 20 ilikuwa ni sawa na ongezeka la deni hili kwa 15.4% kutokea mwaka 2011; Kufikia Mwezi Machi mwaka huu (2013), deni la taifa liliongezeka zaidi na kufikia shilingi trilioni 22, sawa na ongezeko la 10% from 2012; Ingawa ongezeko hili ni chini ya ongezeko la awali la 15.4%, bado ni tatizo kama tutakavyoona;

Je tuipimaje Bajeti Mpya?

Kuna njia nyingi lakini kwangu binafsi ni kwa kuangalia mambo yafuatayo:

· Kwanza - Katika mwaka wa fedha uliopita ambao unaishia mwezi huu, Uwiano wa Deni kwa Pato la taifa (debt to GDP ratio) ulikuwa karibia 45%; Katika bandiko namba moja hapo juu nilijadili kwa kina dhana ya Sustainable investment rule ambayo inalenga katika kusimamia nidhamu katika usimamizi wa fedha za umma; Kanuni hii inahimiza juu ya umuhimu wa Debt to GDP ratio kuwa chini ya 40%; Given kiwango cha sasa ambacho ni kama 48%, kuna kila sababu ya watanzania kuwa concerned kuhusiana na debt sustainability na kuna kila ishara kwamba ratio hii itazidi kupaa; Ni katika muktadha huu, hivi karibuni World Bank ilitoa onyo kwamba kuna hatari ya nchi (Tanzania) kutumbukia katika mgogoro wa deni la taifa kwa kiwango kile kile kabla ya HIPC initiative kuikoa nchi in mid 1990s kwani Deni la Taifa lilifikia kiwango cha kuwa unsustainable hivyo kupelekea nchi kuingizwa katika HIPC initiative; Kwa mujibu wa World Bank, bila umakini, deni la taifa litafikia unsustainable levels miaka mitatu tu ijayo yani (2016);

Swali linalofuatia ni Je – Waziri wa fedha atawaeleza nini wananchi kuhusiana na suala hili?

Katika bajeti iliyopita, pamoja na hatari hii kuzizi kuwa dhahiri, Waziri wa Fedha alisisitiza sana kwamba deni la taifa lipo sustainable; Alichotakiwa kufanya waziri na serikali kwa ujumla iwapo kulikuwa na nia ya kweli ya kuokoa taifa katika janga linalotunyemelea, ilitakiwa serikali kuwekeza kwa nguvu zote kuhakikisha kwamba FISCAL DEFICIT is contained; Kama mlivyojadili (Bongolander, nguruvi3 na wengine), tatizo letu kubwa ni Ukosefu wa Nidhamu katika suala zima la usimamizi wa deni la taifa, hasa katika upande wa matumizi; Ni jambo lisilo na ubishi kwamba kwa miaka kadhaa sasa, Taifa limekuwa linakopa kwa ajili ya matumizi ya kawaida (SALARIES, ALLOWANCES, PROCUREMENT…) kuliko MATUMIZI YA MAENDELEO (elimu, afya, kilimo) and this is BAD ECONOMICS, lakini sio kitu cha ajabu kwa serikali ya CCM ambayo miaka nenda, miaka rudi imekuwa ni bingwa of defying economics and glorifying politics;

Suala la Pili - Katika mwaka wa fedha 2012 – 2013, jumla ya bajeti ilikuwa ni shillingi trillioni 15, ikiwa ni ongezeko la 12%% kutoka bajeti ya awali (2011-2012) ambayo ilikuwa ni shillingi trillion 13; Ongezeko hili la 12% linaweza kuonekana ni la maana lakini only if linaangaliwa in nominal terms lakini tukilitazama in real terms, ambapo kimsingi ni to take into account suala la mfumuko wa bei (inflation), 12% increase haikuwa na maana yoyote kwa mwananchi wa kawaida; Nitafafanua:

Katika kipindi husika (2012 – 2013), inflation rate ilikuwa around 19%, sasa katika mazingira haya, an increae of 12% ya bajeti ni useless kwa mlalahoi;

Swali linalofuata ni Je – Hali hiyo itakuwaje katika mwaka mpya wa fedha? Inflation rate leo hii ni around 9.8%, hivyo tunategemea ongezeko la bajeti kutokea mwaka uliopita kuwa by at least 9.8%; Pia Je – katika mwaka mpya wa fedha, Serikali itakuja na tamko au mikakati gani kumfidia mlalahoi kutokana na hali ngumu aliyoipata katika mwaka wa fedha uliopita, au itakuwa ni yale yale tu ya serikali ya CCM kwamba –Yaliyopita sio ndwele?

· Tatu - Katika bajeti iliyopitwa (2012-2013), Waziri wa fedha alielezea Objectives na Targets mbalimbali za serikali, ikiwa ni pamoja na:

1. Eneo la kwanza - Kuboresha miundo mbinu ya uchumi hasa Umeme, Bandari, Barabara na Reli – ni muhimu Waziri kwenye bajeti yake mpya akaelezea kwa kina ni mambo yepi yametekelezwa, kwa ufanisi kiasi gani, kwa fedha za vyanzo gani n.k; Kwa mfano, tumeona jinsi gani fedha za walalahoi zitatumika kujenga bandari mpya bagamoyo at the expense of existing ports; Serikali ifafanue the opportunity cost – yani why Bagamoyo is the best alternative to Tanga, Mtwara…, not only from the macroeconomic standpoint bali pia microeconomic standpoint;

2. Eneo la pili - Pia Serikali ilitanganza mikakati ya kushusha mfumuko wa bei katika mwaka wa fedha wa (2012-2013) into single digits (below 10%), kutokea the earlier level of about 19% first quarter ya 2012;

Leo hii inflation Rate is around 9.8%; kwa maana hii, lengo la kuishusha into single digits limefanikiwa ingawa if you round up the number, 9.8% bado ni double digits (i.e. 10%); Pia ukiangalia poor management of the economy and the ongoing shocks in the external environment, it’s hard to believe kwamba tutaweza maintain it under 10% kwa muda mrefu;

Vile vile kuna umuhimu wa kuliangalia suala la inflation kwa mapana zaidi: Je, katika kipindi hiki ambacho mfumuko wa bei umeshuka, purchasing power ya Mtanzania imepanda? Jibu ni hapana:

Tuangalia Purchasing Power Vis a Vis Inflation; Purchasing Power of the consumer's Tanzanian Shilling inapima the change in the value of consumer goods and services that a Tanzanian Shilling can buy at different periods. Kwa hiyo, iwapo the overall level of Consumer Price Index (CPI) goes up, Purchasing Power of a Tanzanian Shilling goes down; Takwimu zilizopo zinaonyesha wazi kwamba Tangia later 2009, Purchasing Power of 100 Tanzanian Shillings imekuwa ina decrease continuously, declining to Shillingi 70 na Senti 96 kufikia Machi 2013; Si ajabu Watanzania wengi bado wanachanganyikiwa kusikia mfumuko wa bei umeshuka lakini vile vile purchasing power nayo ikizidi kushuka na kujiuliza kulikoni? Hili ni jibu la Waziri kilijadili kwa watanzania;

Ni muhimu kwa serikali (waziri wa fedha) katika bajeti hii ajue kwamba as a general rule – whenever income za consumers zinapanda kwa kiwango sawa na mfumuko wa bei, maana yake ni kwamba consumers wataweza ku-maintain their current standards of living; Na iwapo incomes za wananchi zitaongezeka kwa kasi kuliko mfumuko wa bei, maana yake ni kwamba standard of living za wananchi zinaboreka zaidi; Lakini by the same token – iwapo inflation inaongezeka kwa kasi zaidi ya income za consumers/wananchi, hata kama income, wages na salaries za wananchi zinaongezeka, bado standard of living ya wananchi itaendelea to decline, Kwani pamoja na kwamba mishahara na mapato yao yanaongezeka, as long as ni kwa kasi ndogo kuliko mfumuko wa bei, they will always find their incomes falling way short to counter the rising prices; SERA YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA chini ya Ilani ya CCM inashindwa kubaini this simple economics!!

3. Eneo la Tatu kuhusiana na Objectives na Targets mbalimbali za serikali kwa mujibu wa waziri wa fedha katika bajeti iliyopita ilihusiana na mikakati ya serikali kuhakikisha inaongeza upatikanaji wa fedha (credit) kwa sekta binafsi ili ifikie 20% ya GDP ifikapo Mwezi Juni 2013; Hii ni namba muhimu sana ya kuifuatilia katika bajeti ijayo kwani tumeona jinsi gani Serikali ilivyokimbilia kwenye mabenki nchini to finance its deficit, na kunyima access to credit kwa private sector, hasa SMEs nchini;

4. Eneo la nne lililenga suala zima la uboreshaji wa katika usimamizi wa fedha za umma kama vile – expansion of the tax base – ambayo nguruvi3 uliyajadili kwa kina hapo awali; kuboresha ukusanyaji na usimamiaji wa non – tax revenues; Kuboresha ufanisi wa taasisi mbalimbali zinazokusanya kodi nje ya TRA kama vile TPDC, TMAA, na MEM kwa nia ya kuongeza pato la taifa kupitia natural resources za nchi; kupitia tena mechanism ya property taxes katika majiji; kuboresha uwezo wa manispaa na halmashauri katika ukusanyaji wa kodi; na Kupunguza mianya ya tax evasion and tax exemptions;

Itakuwa ni jambo la muhimu sana kusikia kutoka kwa waziri wa fedha ni kiasi gani cha malengo husika yamefanikiwa;

5. Eneo la Tano kwa mujibu wa waziri wa fedha ndani ya bajeti ya 2012- 2013 lililenga kupunguza utegemezi wa fedha za wahisani (za nje) katika bajeti kwa nia ya kuelekea kuwa taifa linalojitegemea kifedha kupitia vyanzo vya ndani vya kodi; Hii ni nia njema iwapo kutakuwa na vitendo kuliko rhetoric na ikumbukwe pia kwamba Mustafa Mkullo akiwa Waziri wa Fedha, alitanganza ndani ya bajeti ya 2010-2011 kwamba serikali inalenga kupunguza mchango wa wahisani katika bajeti kufikia less than 10% ifikapo mwaka 2015;

Kwa sasa ningependa kujadili zaidi kidogo eneo hili la TANO la objectives and targets za serikali ya CCM per 2012-2013 Budget:

Hali ifuatayo ilijitokeza katika bajeti ya 2012 - 2013:

Vyanzo vya fedha kwa ajili ya Bajeti ya nchi:

Serikali ilitarajia mapato ya ndani kuwa karibia shilingi trilioni tisa (sawa na 18% ya pato la taifa/GDP); Projections za mapato ya local government ilikuwa ni shilling kama trilioni 360 (sawa na 7% of GDP);

Fedha za wahisani:

Serikali ilitarajia kupata shilingi trillion kama 3.3 kutoka kwa wahisani , 840 billion/= (about 27%) ikiwa ni kupitia General Budget Support na trilioni 2.3/= (73%) kupitia misaada kwa ajili ya miradi ya maendeleo na vile vile fedha za Millenium Challenge Acccount;

Its such an irony kwamba wahisani huwa wanatoa fedha nyingi zaidi kwa ajili ya maendeleo, huku serikali ikitegea katika hilo kwa kutenga fedha nyingi zaidi kwa ajili ya posho, mishahara, procurement…; imekuwa ni desturi kwa Serikali ya CCM kupensa sana to ‘ peg’ fungu kubwa la maendeleo kwenye vyanzo vya fedha vya nje ambavyo literally havina uhakika sana (fedha za wahisani), badala ya kutafuta kwenye vyanzo vya uhakika zaidi hasa kutoza kodi za maana kwenye sekta muhimu kama madini n.k ambazo with political will, taifa lina uwezo wa kujitegemea ndani ya kipindi kifupi sana; Kwa kweli tabia hii ya kutegea wahisani kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo huku serikali ikitengza zaidi fedha kwa ajili ya posho, mishahara na procurement, inatia sana shaka juu ya umakini wa serikali katika kukuza uchumi unaomgusa mwananchi wa kawaida; Tatizo la kutegemea wa hisani ni pamoja na ifuatavyo:

Kwa mfano, kati ya jumla ya fedha kwa ajili ya matumizi ya maendeleo kwa mwaka wa fedha 2011-2012, ambazo jumla ilikuwa ni 4.9 trillioni shillings, kufikia Aprili 2012 (miezi miwili kabla ya bajeti mpya ya 2012-2-13 kutangazwa, only 2.6 trillion had been received (karibia 50%)!!!; Sababu za kucheleweshwa kwa fedha hizi ni delays in securing on time the external non – concessional loans, lakini ripoti ya CAG imetufungua macho kwamba kumbe yapo mabilioni ya fedha za mikopo ambayo hupotelea juu kwa juu, pengine kwenye akaunti za mabenki huko uswisi na kwingineko!!; Sasa ukichanganya na state of the economy in the Eurozone leo hii, tabia hii ya kutegemea fedha za wahisani badala ya fedha zetu za ndani kuletea wananchi maendeleo itazidi kuwagharimu wananchi;

Kutokana na kukosekana kwa fedha za kutosha, serikali ilipanga kutumia other sources to bridge the financing gap of about 2.8 trillion shillings, nusu ya hizi ikiwa ni kupitia domestic financial markets; Nadhani tunakumbuka hapo juu kwamba moja ya malengo ya serikali katika bajeti iliyopita ilikuwa ni pamoja na kuhakikisha kunakuwa na ongezeko la upatikanaji wa fedha (credit) kwa sekta binafsi nchini ili ifikie 20% ya GDP ifikapo Mwezi Juni 2013; Sasa hili la bridging the financial gap kwa kukopa kupitia mabenki nchini contravenes the objective hapo juu yani – goes against the government’s commitment to create a conducive environment for the private sector in Tanzania to flourish, hasa kupitia upatikanaji wa mikopo kwa sekta binafsi, hasa SMEs;

Sasa uvivu wa Serikali kuziba the financing gap kupitia more fiscal discipline na badala yake kukimbilia kwenye mabenki nchini matokeo yake ni kwamba – Benki zita prefer kuipa serikali mikopo kuliko SMEs kwani mikopo kwa serikali ni almost risk free; This puts so much pressure on inflation and interest rates kutokana na crowding effect; Pia ukopaji wa namna hii unaongeza fiscal deficits na pia debt to GDP ratio, ndio maana World Bank wanaonya kwamba kwa mwendo wa sasa wa serikali, deni la taifa litakuwa unsustainable ifikapo 2016;

Nitarudi kujadili mengine zaidi, hasa kuhusiana na changamoto zilizojitokeza katika bajeti iliyopita ili tujue yepi yatajiri katika bajeti mpya…
 
Mchambuzi najua ndani ya CCM na serikali kuna vichwa vingi kama wewe na wale waliokuwa walimu wa chuo akina mama Tibaijuka, Benno Ndulu, Samuel Wangwe, Rutasitara, Likwelile n.k, swali ambalo limekuwa linanitatiza ni kwamba hivi hawa wanataaluma wote hawatoi michango yao katika kuchambua haya masuala kwa kina au ni kwamba ushauri wao hupuuzwa? Napata shida sana kuelewa namna ambavyo taifa hili linatumia wataalam wake au jinsi wataalam wanavyolitumikia taifa.

Pamoja na haya, jambo ambalo linaonekana lipo wazi ni kwamba kuna kasumba ya watawala kujisahau na kudhani kuwa wanaongoza taifa la mazuzu wasiojitambua. Uzito wa matatizo ya sera za nchi ni jambo muhimu sana na mapungufu ya utekelezaji wa sera hizi (ikiwa ni pamoja na mikakati ya utekelezaji na bajeti husika) ni moja tu ya matatizo haya. Ni suala la kufedhehesha na kuhuzunisha pale ambapo weledi unawekwa pembeni katika kuchangia mustakabali wa taifa iwe ni katika mihimili ya demokrasia ya serikali, bunge au mahakama.

Tutajadiliana na kutoa hata kitabu toka katika uzi huu ila ni jambo lisilopingika kwamba deni ni deni tu na huakisi ahadi ya malipo ya siku za usoni. Mlipaji ni nani? ni mwananchi wa kawaida awe wa kizazi hiki au kijacho ila mwisho wa siku kwenye mizania ya malipo deni litatolewa kwenye dhamana za wananchi. Ila kwa kupitia tafiti mbalimbali za uchumi kuhusiana na Tanzania, pengine mtu unapata taswira ya kwamba baadhi yetu ndio ambao tuna wasiwasi na deni la taifa ilihali "wataalamu" hawaoni uwepo wa tatizo kama hili. Je ni kweli kwamba suala la deni la taifa linawagusa zaidi watanzania walio katika sekta rasmi wanaokatwa kodi na tozo zingine mbalimbali kuliko wale wasiokuwa katika sekta rasmi? Hofu kuhusu deni la taifa na mashaka kuhusiana na sera ya matumizi ya umma unawezekana upo zaidi miongoni mwa walipaji kodi. Hii ni dhahiri ya kwamba walipa kodi wa taifa hili hawaridhishwi na mfumo uliopo wa kodi ambao unaonekana onevu ukiwabana zaidi wachache.

Upande mwingine wa shilingi inawezekana ya kwamba serikali inatoa kipaumbele mkubwa kwa tathmini za wataalam wa nje kuliko wananchi wa kawaida kama mimi na wewe, na je kwanini isifanye hivyo? tafiti kama hizi za akina Daehaeng Kim na Mika Saito wa IMF za mwaka 2009 na hii ya David Bevan wa International Growth Centre ya mwaka 2010 (uk.22-28), hazionyeshi tatizo kuhusiana na deni la taifa na pengine hawa ndio waliokamata masikio ya wakuu wa nchi.

Pamoja na yote haya ni wazi kwamba kwa ujumla mwenendo wa uchumi wa taifa haujawaridhisha wengi kwa maana ya kwamba neema ya utapanyaji wa maendeleo haijawaangukia walio wengi. Pengine ni suala la sisi wananchi kutokuwa na matarajio halisia na kuwa na haraka ya maendeleo pasi kujali kule tulikotoka. Lakini pia ni vyema tukajiuliza ni kwanini matarajio haya yapo, je yanatokana na kuona baadhi yetu humu humu nchini wakipiga hatua za haraka kwa kasi ya ajabu? Je kutokana na kuona maendeleo ya baadhi hayatokani na vyanzo halali? Haya yote yana maudhui ya dhana ya udhalimu au unyonyaji wa namna fulani. Pengine pia ni kutokana na historia yetu ya kuwa nchi ya kijamaa ambayo inatufanya tushindwe kuafikiana na "matunda" ya ubepari yanayosababisha utowekaji wa usawa miongoni mwetu. Kilicho dhahiri hapa ni kwamba kuna vita baridi ya matabaka ndani ya Tanzania, vita ambayo inaweza ikaleta madhara makubwa katika ustawi wa taifa hili isipodhibitiwa.
 
kwa miaka kadhaa sasa, Taifa limekuwa linakopa kwa ajili ya matumizi ya kawaida (SALARIES, ALLOWANCES, PROCUREMENT…) kuliko MATUMIZI YA MAENDELEO (elimu, afya, kilimo) and this is BAD ECONOMICS, lakini sio kitu cha ajabu kwa serikali ya CCM ambayo miaka nenda, miaka rudi imekuwa ni bingwa of defying economics and glorifying politics;

Tatu - Katika bajeti iliyopitwa (2012-2013), Waziri wa fedha alielezea Objectives na Targets mbalimbali za serikali, ikiwa ni pamoja na:

1. Eneo la kwanza - Kuboresha miundo mbinu ya uchumi hasa Umeme, Bandari, Barabara na Reli – ni muhimu Waziri kwenye bajeti yake mpya akaelezea kwa kina ni mambo yepi yametekelezwa, kwa ufanisi kiasi gani, kwa fedha za vyanzo gani n.k; Kwa mfano, tumeona jinsi gani fedha za walalahoi zitatumika kujenga bandari mpya bagamoyo at the expense of existing ports; Serikali ifafanue the opportunity cost – yani why Bagamoyo is the best alternative to Tanga, Mtwara…, not only from the macroeconomic standpoint bali pia microeconomic standpoint;

2. Eneo la pili - Pia Serikali ilitanganza mikakati ya kushusha mfumuko wa bei katika mwaka wa fedha wa (2012-2013) into single digits (below 10%), kutokea the earlier level of about 19% first quarter ya 2012;

Leo hii inflation Rate is around 9.8%; kwa maana hii, lengo la kuishusha into single digits limefanikiwa ingawa if you round up the number, 9.8% bado ni double digits (i.e. 10%); Pia ukiangalia poor management of the economy and the ongoing shocks in the external environment, it’s hard to believe kwamba tutaweza maintain it under 10% kwa muda mrefu;

SERA YA MAISHA BORA KWA KILA MTANZANIA chini ya Ilani ya CCM inashindwa kubaini this simple economics!!

3. Eneo la Tatu kuhusiana na Objectives na Targets mbalimbali za serikali kwa mujibu wa waziri wa fedha katika bajeti iliyopita ilihusiana na mikakati ya serikali kuhakikisha inaongeza upatikanaji wa fedha (credit) kwa sekta binafsi ili ifikie 20% ya GDP ifikapo Mwezi Juni 2013; Hii ni namba muhimu sana ya kuifuatilia katika bajeti ijayo kwani tumeona jinsi gani Serikali ilivyokimbilia kwenye mabenki nchini to finance its deficit, na kunyima access to credit kwa private sector, hasa SMEs nchini;

4. Eneo la nne lililenga suala zima la uboreshaji wa katika usimamizi wa fedha za umma kama vile – expansion of the tax base – ambayo nguruvi3 uliyajadili kwa kina hapo awali; kuboresha ukusanyaji na usimamiaji wa non – tax revenues; Kuboresha ufanisi wa taasisi mbalimbali zinazokusanya kodi nje ya TRA kama vile TPDC, TMAA, na MEM kwa nia ya kuongeza pato la taifa kupitia natural resources za nchi; kupitia tena mechanism ya property taxes katika majiji; kuboresha uwezo wa manispaa na halmashauri katika ukusanyaji wa kodi; na Kupunguza mianya ya tax evasion and tax exemptions;

Itakuwa ni jambo la muhimu sana kusikia kutoka kwa waziri wa fedha ni kiasi gani cha malengo husika yamefanikiwa;

Mkuu Mchambuzi umegusa maeneo muhimu sana. Hizi naweza kusema ni simple economics of managing country's economy, and in order for the economy to be healthy, whoever is managing this has to attain them by hooks and crooks. Whether as an individual or the party, haya ni mambo yanayotakiwa kuangaliwa.

Hebu tuangalie tatizo moja kubwa linalofanya uchumi wetu uwe ovyo, na linalofanya tusiishi maisha bora. Umetaja vizuri kuwa Siasa zinapewa kipaumbele kuliko uchumi. Ukiangalia allocation of resources hapa Tanzania, ni wazi kabisa kuwa inalenga sababu za kisiasa, na sio sababu za uchumi. Kuwekeza sana kwenye matumizi ya kawaida kunalipa sana kisiasa, lakini ni maumivu makubwa sana kiuchumi. Ni sawa na utawala wa Mzee Mwinyi watu walikuwa wanadai pesa ziko nje nje lakini uchumi wa nchi ulikuwa ovyo kabisa. Naona tunatakiwa kuwa na sheria za ku-manage uchumi, atakachosema waziri kiwe kinabana kisheria ili mwaka unapokwisha kusiwe na visingizio vya kusema tulishindwa kutokana na sababu fulani ambazo mara nyingi zinazokuwa si za maana.

Tatizo lililopo ni kuwa watanzania hatuna mwamko wa kufuatilia jinsi uchumi wetu unavyoendeshwa, serikali inaweza kutoa ahadi na isitekelezwe na watu hawalalamiki, wabunge etu wakirubuniwa tu nao wanasahau kabisa. Kwa mfano ningependa sana kuona progress report ya kutatua tatizo la umeme, maji, barabara na infrastructure nyingine. Is it better than last year? will current budget make it even better? au ndio allocation kwa mujibu wa matakwa ya kisiasa.

La kujenga bandari Bagamoyo sijui kama kweli lina maana yoyote, linaweza kusema kisiasa na kulisema kwa namna nyingi tu, lakini kimsingi si busara hata kidogo. Mchambuzi na Nguruvi mtakuwa mnafahamu vizuri sana kuwa tatizo la bandari ya Dar es salaam ni mismanagement inayotokana na uswahili, ingeboreshwa kimiundo mbinu na management kusingekuwa na haja ya kujenga nyingine na kuwatwisha wananchi mzigo mkubwa wa deni, na bandari yenye itaanza kuchakaa hata kabla ya miaka 50 wachina kuiacha. Hakuna mahali duniani wachina walijenga banadri nzuri hata za kwao kwenyewe China ukiziona hazilingani hata na bandari ya port Elizabeth....still it is defying principles of economics. Hakukuwa na sababu ya maana ya kiuchumi yaani uchumi endelevu kujenga bandari Bagamoyo.

Lakini kuna moja la muhimu ambalo tunatakiwa kukumbuka, hata kama tukisema tukusanye fedha zaidi kutoka vyanzo vya ndani, iwe ni kodi au sio kodi, kama matumizi yake ni mabaya, kama hayaendei kwenye ivestements ambazo baadaye hazitakuwa na returns nzuri, yaani kama nyingi zinapelekwa kwenye matumizi ya kila siku, hata tukusanye maazillion ya shilingi, haina maana yoyote.
 
Back
Top Bottom