Deni la ujenzi wa reli ya SGR ni kitanzi kitakachotunyonga tusipokuwa makini

Missile of the Nation

JF-Expert Member
Joined
May 24, 2018
Posts
15,101
Reaction score
56,054
Mwaka 2017, nchi yetu ilipata mkopo wa dola za kimarekani kutoka benki ya Exim ya Uturuki ya dola za kimarekani bilion 1.2 ambazo ni sawa na takriban shilingi Trillion 2.76 za kitanzania kwa ajili ya Ujenzi wa kipande cha Dar es salaam mpaka Morogoro tu.

Kwa mujibu wa tweet ya mheshimiwa Zitto ya october mwaka 2017, Ndugu Zitto aliufahamisha umma kuwa riba ya mkopo huo ni 9%
Ndugu Zitto alikuwa anashangaa aina ya mkopo huo kutoka kwa waturuki wakati Wachina hapo mwanzoni tulishakubalina nao waijenge hiyo reli kwa riba ya 1% tu na mkopo huo kutoka kwa wachina tulikuwa na unafuu wa kuanza kuulipa baada ya miaka 20 kupita kwanza!

Sasa mimi nitajikita kwenye riba ya mkopo wa kipande kifupi tu cha reli hiyo cha kutoka Dar es salaam mpaka Morogoro halafu wewe mwenyewe msomaji utajaza mwenyewe ni pesa ngapi tutalipa kwa mikopo ya kujenga vipande vingine vya reli hiyo kama kile cha kutoka Morogoro mpaka Makutopora, na Makutoora mpaka sehemu nyingine hadi mwisho

Nimechukua pesa tuliyokopa, dola bilion 1.2 kama principle, na interest ya 9% aliyoisema mheshimiwa Zitto kisha nikatumia calculator ya online kuangalia, Je deni la kipande hicho pekee cha Dar es salam Morogoro baada ya miaka 20 itakuwa shilingi ngapi?

Nimetumia calculator inayopatikana hapa:

Compound Interest Calculator - The Calculator Site

matokeo niliyopata ni kuwa jumla ya riba tutakayopaswa kulipa ni takriban dola bilion 6 sawa na shilingi Trillion 13. 8 kwa kipande kidogo tu cha Dar hadi Morogoro baada ya miaka 20.

Sasa najiuliza, Je tumejipangaje kama taifa kuja kubeba mzigo huu wa deni?

Kama kipande kifupi tu cha hiyo reli kinaweza kutupelekea kulipa shilingi Trillion 13. 8 kama riba baada ya miaka 20, Je tutalipa shilingi ngapi kwa ajili ya kulipia mikopo yote ya reli nzima?

Tunaweza kuwa tunaimba na kufurahia SGR kumbe ikageuka kuw kitanzi cha kutunyonga kiuchumi huko mbeleni.

 
Hii haiwezi kuwa kweli maana magufuli alituhakikishia na kutuaminisha kuwa yeye Ni mzalendo sana na anaipenda nchi hii sana hivyo hataki mikopo ya riba kubwa ndo maana akawakataa wachina,hizo figure utakuwa umezisoma kinyumenyume maana nahisi umetumwa na beberu wewe
 
Wakiwa majukwaani wanasema tunajenga kwa pesa za ndani. Hawa watu wanatuona wote hamnazo.

Huyo anayeshurutisha watu kusema ni fedha za ndani badala ya mkopo, anajua wakati huo hatakuwepo. Ndio maana anabana vyombo vya habari kuandika habari hizo. Saa hii anasaka sifa za kisiasa, lakini moto wake huko mbeleni haimruhusu. Tuombe huo mradi ujiendeshe kwa faida kuepuka balaa huko mbeleni. Ila wasiwasi wangu wa huo mradi kujiendesha kwa faida ni pale ninapoangalia kinachoendelea kwenye huu mradi wa mwendo kasi hapa mjini.
 
Mbona tuliambiwa hela tunazo zakutosha na tunajenga kwa pesa zetu wenyewe, japo kwenye kulipa mkopo tutalipa kwa pesa zetu wenyewe
 

Hizo sifa anazosaka amefanikiwa kuwapata watu wenye upeo mdogo kwa muda mfupi, lakini tunaojua mambo kwa undani,tunajua kuwa anachemka. Ngoja tuendelee kunywa mtoto nyama tutazikuta chini.
 
Porojo tu Hakuna evidence yeyote ya kutushawishi, tweet ya zito ndio hitimisho lako! Ni chizi tu atakae waamini wajasiriasiasa (wapinzani uchwara) ambao wanajulikana wazi wao ni pinga pinga aka vibaraka wa mabeberu,ishu ya Corona ndio tulijua Hawa wajasiriasiasa ni mbwa mwitu waliovaa ngozi za kondoo hamuaminiki kwa chochote

Viva CCM Viva magufuli

Mungu mbariki magufuli
 
Acha tu Kashazoea kupiga kwenye barabara hadi huku ni UPIGAJI tu.
 
Unamwamini jiwe?
 
Kwanza nina uchungu niliambiwa kuwa nitapewa noa yangu mara baada ya barick kutupa mlungula wetu.kingine niliambiwa kila kijiji kitapewa milioni 50 mpaka sasa tunapumulia mashine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…