Deni langu la bodi limebaki 1.5 milioni

Wazo zuri tuangalie namna ya kujiorganise kutumia wanasheria wa vyama vya wafanyakazi tukafungue shauri mahakamani kwa ajili ya retention fee
 
Mimi hawajaanza kukata na nakaribia kustaafu sijui kitatokea nn huko mbele
 
Kwani CAG anasemaje kuhusu loan board, maana sioni cha maana wanachofanya kusaidia elimu ya kijana mnyonge wa kitanzania zaidi ya kumfanya fursa.....CAG kagua loan board tafadhaaaaaaaaaaaali!!!!!!!!!
 
Likiisha kaushia usiende kuulizia
 
Angekuwepo bwana yule angefurahi sana akisikia neno mnyonge au wanyonge.
Wanyonge ni watu wazuri sana, unawatengenezea tatizo halafu unalitatua baadae. Hawa ni wazuri sana kwa kujipatia kura.
Hata hili tatizo la Retention fee watalitatua wenyewe waliolitengeneza
 
Nenda bodi HESLB, nakuhakikishia utakuta deni la mil11.5., milioni kumi na moja na laki tano.

Everyday is Saturday................................😎
Haya ndio mambo ninayoogopa. Kila nikitaka kuulizia deni naghairisha sababu ya huu ujinga
 
Hiyo ya kwenye salary slip na kwao ni tofauti, deni halisi wanalo wao, usisahau july mwaka mpya wa fedha linaongezeka.... haitakua 1.5 tena
Watu tunaidai serikali madeni ya 2016 hadi leo hatujalipwa na sisi tudai riba?
 
Ndio maana kaka yangu alimwambia mwanae ww nitakusomesha kibabe hivi hivi maana utakuja upate shida kulipa deni wakati unaweza kua na majukumu mengi sasa.Sasa nimeelewa kwa nn alikomaa kulipa ada.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…