Deni langu la bodi limebaki 1.5 milioni

Mm nadaiwa 12.5 m.
Kwa mtazamo na mawazo yangu hizi pesa za ELIMU ya juu ilitakiwa iwe kama hisani wenye vigezo wapewe bure Tena bila kudaiwa.....hii nchi ni tajiri Sana si ndicho tumeaminishwa.
 
Wakati mwingine serikali inajiharibia yenyewe
 
Sasa hoja yako ni ipi hapa?
 
Mimi deni la kwenye salary slip liliisha kabisa likasoma 0 na wakaacha kunikata. Imepita miaka mitatu nikaletewa barua nadaiwa 3.9m.
Mbwa hao ko ulikaa kimya bila kufanya consultation nao na mwanasheria?
 
Kwani CAG anasemaje kuhusu loan board, maana sioni cha maana wanachofanya kusaidia elimu ya kijana mnyonge wa kitanzania zaidi ya kumfanya fursa.....CAG kagua loan board tafadhaaaaaaaaaaaali!!!!!!!!!
Alisema linakiuka sheria sasa sijui watekwlezaji wizara ya Elimu na Serikali wanalichukuliaje hili swala
 
Wakati huo mlifurahi sana kupata boom
sasa wakati wa kulipa mnakiona cha moto.. mzazi kama ana uwezo asomeshe kwa pesa yake mikopo ni jela

Heri mimi nimeishia la tatu c kutwa nazunguka na kapu langu la samaki mimi mwana wa mwendazake
Ndio ila sisi wengine mkataba wetu hauna riba na hiyo sheria dhulma ya bunge imekuja baada yetu nashangaa kuingizwa, nikama vile sheria ya wizi wa kuku inasema afungwe miazi miwili na bunge kubadili kuwa miaka kumi wale waliohukumiwa awali wote wanafungwa miaka kumi.
Wazo langu sisi tuliokopa 2005 hadi 2016 tunaonaje tukaenda mahakamani kusema hatuhusiki na riba wala maretantion fee.
Angalizo.
Bunge lilipotunga sheria ya madini, sheria mpya haikuhusisha mikataba ya zamani ikasema wazi itahusu vitalu vipya, hii ndo njia yakutokea.
 
Hongera sana kiongozi...
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…