Desemba 25: Je, ni siku aliyozaliwa Yesu au twaadhimisha tu kumbukumbu?

Desemba 25: Je, ni siku aliyozaliwa Yesu au twaadhimisha tu kumbukumbu?

Sijui kwa nini kuna watu hii sikukuu inawauma,wanakuja kutuandikia vimaneno vyao vyepesi vyepesi wakihisi watu hawatosheherekea...POLENI SANA Christmas itabaki kuwa Christmas......uhuru wa kuabudu na kuamini...mafundisho yenu FEKI pelekeni kwenye makanisa yenu au misikitini.
Kinachowauma watu ni kufungamanisha upagani na mambo ya kimungu, hili ndio tatizo
 
Kwanj petro alikua anaongea kiswahili
Petro akuongea kiswahili, aya na mimi nijibu swali langu Petro aliwai angalau mara moja kuadhimisha hii official day 25/December kuwa kumbukumbu ya mazazi ya Yesu?
 
Bora zetu za kuzaliwa enzi za nzige maana utajua ilikuwa ni masika na sio mwaka
Sijui kuna mtu kanielewa
 
kuhusu hayo maneno ya muandishi nimeyafupisha wa, 2 peter 2:3 Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii.
nimejifunza kutokujibu utunzi ambao hauna mashiko. huo utunzi umejaa mapokeo.
petro alikutuma ukabadili verse za vitabu vyake kama iyo 2 petro 2:3 toka KIGIRIKI kwenda KIINGEREZA/KISWAHILI au huo utaratibu ulijitungia mwenyewe ??

petro alikutuma ukacompile vitabu na maandiko yake kisha uyaweke kwenye kitabu kinaitwa BIBLIA au huo utaratibu ulitungia mwenyewe ??

mlolongo wa mambo uliojitungia mwenyewe ni mrefu sana. mengine unaweza ongeza mwenyewe.
 
petro alikutuma ukabadili verse za vitabu vyake kama iyo 2 petro 2:3 toka KIGIRIKI kwenda KIINGEREZA/KISWAHILI au huo utaratibu ulijitungia mwenyewe ??

petro alikutuma ukacompile vitabu na maandiko yake kisha uyaweke kwenye kitabu kinaitwa BIBLIA au huo utaratibu ulitungia mwenyewe ??

mlolongo wa mambo uliojitungia mwenyewe ni mrefu sana. mengine unaweza ongeza mwenyewe.
naona umeibuka na nadharia za kikatoliki.
"There is in them no evidence whatever to suggest that it was the expectation of the writers that what they had written would one day be gathered together to become a part of the New Testament." (Campaigners for Christ Handbook, p. 162).

2 Timotheo 3:16 Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki;

Hata kama yangekuwa vipandevipande tungeyasoma. Hata kama Yasingekusanywa pamoja ningeyakusanya mimi leo na kutengeneza app kulingana na current technology wala sio jambo la kujivunia au swali la kuuliza.

maoni ya wananzuoni wa imani yako naona yamekukaa kuliko hata Maandishi wazi ya maandiko.
 
Kinachowauma watu ni kufungamanisha upagani na mambo ya kimungu, hili ndio tatizo
nyie msiofungamanisha endeleeni,acheni watu wafanye mambo yao na nyie fanyeni yenu mbinguni kila mtu anakwenda mwenyewe,tangu mmeanza hili zoezi mshapata wangapi????😀😀😀😀 mnachekesha kweli
 
maoni ya wananzuoni wa imani yako naona yamekukaa kuliko hata Maandishi wazi ya maandiko.
mwanazuoni wangu mkuu ni Yesu kristo mwenyewe na baadae ni mitume 12 aliopenda waendeleze kazi yake hapa duniani kisha wakifuatiwa (succesors) na wazee(maaskofu) kuanzia holy father (pope) st peter mpaka pope francis kisha wafuasi wengine wengi wa kristo kuanzia karne ya kwanza kabisa mpaka sekunde hii unaposoma hii post. HAO NDIO WANAZUONI WANGU MIMI ONESHA WA KWAKO SASA.
naona umeibuka na nadharia za kikatoliki
nawe ibuka na panguzi kwa kutumia nadharia za kisabato. na ukimaliza ulete ushahidi wa kimaandiko wa mambo lukuki ambayo umejitungia (kinyume kabisa na 2 peter 2:3) ukianza na niliokuonesha hapo juu

imeandikwa
Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii.
 
mwanazuoni wangu mkuu ni Yesu kristo mwenyewe na baadae ni mitume 12 aliopenda waendeleze kazi yake hapa duniani kisha wakifuatiwa (succesors) na wazee(maaskofu) kuanzia holy father (pope) st peter mpaka pope francis kisha wafuasi wengine wengi wa kristo kuanzia karne ya kwanza kabisa mpaka sekunde hii unaposoma hii post. HAO NDIO WANAZUONI WANGU MIMI ONESHA WA KWAKO SASA.

nawe ibuka na panguzi kwa kutumia nadharia za kisabato. na ukimaliza ulete ushahidi wa kimaandiko wa mambo lukuki ambayo umejitungia (kinyume kabisa na 2 peter 2:3) ukianza na niliokuonesha hapo juu

imeandikwa
Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa; ambao hukumu yao tangu zamani haikawii, wala uvunjifu wao hausinzii.
Asante kwa maoni yako kuhusu Yesu. Hata wafuasi wa Kibwetere walikuwa na kauli hizohizo hadi siku wanajikuta majivu.

Msaada tu kidogo.
Petro hajawahi kuwa papa. Ukatae ukubali haibadilishi huu ukweli. Hayo ni mapokeo na makaririsho ya imani tu.
Kumuita huyo Papa Holy father ni Kufuru kwa Mungu Muumba wa Mbingu na Nchi na Kumdharau Yesu na Mafundisho yake.
Mimi Yesu sio Mwananzuoni wangu Bali ni Mungu wangu, Bwana na Mwokozi wangu aliye Hai.
Maneno Yake, Kupitia Maandiko matakatifu Mwanzo hadi Ufunuo, Vitabu 66 aliyoyanena kupitia mawakala wa kibinadamu ndio Mwanzo na Mwisho wa wananzuoni wangu.
Nadhani unajenga hofu na wasiwasi na EGW, Hata Yeye sio mwananzuoni wangu ila ni mtumwa mwenza wa Yesu na anasema

“He [Christ] pointed to the Scriptures as of unquestionable authority, and we should do the same. The Bible is to be presented as the word of the infinite God, as the end of all controversy and the foundation of all faith” (COL 39, 40).
'' Yeye Yesu alielekeza katika Maandiko kama mamlaka isiyokosolewa, na sisi tunapaswa kufanya hivyohivyo. Bibilia inapaswa kuchukuliwa kama neno la Mungu asiye na ukomo, na Mwisho wa migogoro yote na misingi ya imani yote''.
Mwananzuoni yoyote anapaswa kupigia magoti Neno la Mungu maoni yake yote lazima yafungwe katika Bibilia.
Siamini kama wewe kuwa hata kauli ya Papa inauzito sawa na Bibilia, Tamko la kikanisa linauzito sawa na Bibilia. Kwaku Kuamini hayo ni ukafiri. Siku Papa akiingiwa na Shetani kama Petro dakika chache Baada ya Kusifiwa na Yesu kwa Kumtambua na kutoa tamko la kishetani na Yesu akamwambia '' Rudi nyuma wewe Shetani''. kwa Imani yako wewe na kanisa zima la katoliki hamtakuwa na Jinsi itabidi mpigia magoti hiyo kauli na kuifuata. Yesu hawezi kuhatarisha maneno yake kizembe hivyo. Msingi Ni Bibilia, Sio hao watu mashuhuri wa imani na matamko yao.

Angalia Ndugu yangu Sala na Kazi, pamoja na Yeyete atakayependa. Umejiweka kwenye hatari Kubwa ya Kupotezwa na Mwovu shetani kwa Kitoboa Ufunuo wa Yohana na kukubwisha matamko na kauli za mitume wako wa .com kuwa na uzito sawa na Maandiko Matakatifu.

Mambo haya nitaendelea kusema, kuonya na kufundisha hadi utimilifu wa dahali. Maana ni Kweli na hakika.

Mfano Mdogo tu.
Unaposema Petro ni Papa wa Kwanza, Kwa Nini Yohana asiwe papa wa pili maana ndiye mtume wa Mwisho kufa kwa mujibu wa masimulizi. Badala Yake mmempa Upapa wa Pili Baada ya Petro St Linus. Na Andiko lwa wananzuoni wako hao Catholic Encyclopedia (1913) Vol 9 inasema haina uhakika kama Linus huyo ndio wa kwenye bibilia (Kitabu cha timotheo) au ni mtu mwingine?
 
Asante kwa maoni yako kuhusu Yesu. Hata wafuasi wa Kibwetere walikuwa na kauli hizohizo hadi siku wanajikuta majivu.

Msaada tu kidogo.
Petro hajawahi kuwa papa. Ukatae ukubali haibadilishi huu ukweli. Hayo ni mapokeo na makaririsho ya imani tu.
Kumuita huyo Papa Holy father ni Kufuru kwa Mungu Muumba wa Mbingu na Nchi na Kumdharau Yesu na Mafundisho yake.
Mimi Yesu sio Mwananzuoni wangu Bali ni Mungu wangu, Bwana na Mwokozi wangu aliye Hai.
Maneno Yake, Kupitia Maandiko matakatifu Mwanzo hadi Ufunuo, Vitabu 66 aliyoyanena kupitia mawakala wa kibinadamu ndio Mwanzo na Mwisho wa wananzuoni wangu.
Nadhani unajenga hofu na wasiwasi na EGW, Hata Yeye sio mwananzuoni wangu ila ni mtumwa mwenza wa Yesu na anasema

“He [Christ] pointed to the Scriptures as of unquestionable authority, and we should do the same. The Bible is to be presented as the word of the infinite God, as the end of all controversy and the foundation of all faith” (COL 39, 40).
'' Yeye Yesu alielekeza katika Maandiko kama mamlaka isiyokosolewa, na sisi tunapaswa kufanya hivyohivyo. Bibilia inapaswa kuchukuliwa kama neno la Mungu asiye na ukomo, na Mwisho wa migogoro yote na misingi ya imani yote''.
Mwananzuoni yoyote anapaswa kupigia magoti Neno la Mungu maoni yake yote lazima yafungwe katika Bibilia.
Siamini kama wewe kuwa hata kauli ya Papa inauzito sawa na Bibilia, Tamko la kikanisa linauzito sawa na Bibilia. Kwaku Kuamini hayo ni ukafiri. Siku Papa akiingiwa na Shetani kama Petro dakika chache Baada ya Kusifiwa na Yesu kwa Kumtambua na kutoa tamko la kishetani na Yesu akamwambia '' Rudi nyuma wewe Shetani''. kwa Imani yako wewe na kanisa zima la katoliki hamtakuwa na Jinsi itabidi mpigia magoti hiyo kauli na kuifuata. Yesu hawezi kuhatarisha maneno yake kizembe hivyo. Msingi Ni Bibilia, Sio hao watu mashuhuri wa imani na matamko yao.

Angalia Ndugu yangu Sala na Kazi, pamoja na Yeyete atakayependa. Umejiweka kwenye hatari Kubwa ya Kupotezwa na Mwovu shetani kwa Kitoboa Ufunuo wa Yohana na kukubwisha matamko na kauli za mitume wako wa .com kuwa na uzito sawa na Maandiko Matakatifu.

Mambo haya nitaendelea kusema, kuonya na kufundisha hadi utimilifu wa dahali. Maana ni Kweli na hakika.

Mfano Mdogo tu.
Unaposema Petro ni Papa wa Kwanza, Kwa Nini Yohana asiwe papa wa pili maana ndiye mtume wa Mwisho kufa kwa mujibu wa masimulizi. Badala Yake mmempa Upapa wa Pili Baada ya Petro St Linus. Na Andiko lwa wananzuoni wako hao Catholic Encyclopedia (1913) Vol 9 inasema haina uhakika kama Linus huyo ndio wa kwenye bibilia (Kitabu cha timotheo) au ni mtu mwingine?
hao wafuasi Wa kibwetele hawana tofauti yeyote kabisa na wale wafuasi Wa bwana mmoja kule marekani aliyewaambia wafuasi wake kuwa kristo angerudi tarehe Fulani, mwezi Fulani then wafuasi wake wakafanya mambo fulanifulani yasio na tofauti yeyote na wafuasi Wa kibwetele. tofauti ni moja tu kibwetele aliwapiga moto wafuasi wake ila huyo bwana Wa huko maeekani yeye aliwatungia wimbo kwamba BWANA ATARUDI UPESI wimbo ambao unaimbwa mpaka leo na wafuasi wake wasiojua kuwa yesu alitahadharisha HAKUNA AIJUAYE SIKU WALA SAA.

Sasa hapo sijui mjinga Wa kuchomwa moto mpaka majivu ni nani ?
Ni wale walioambiwa yesu atarudi TAREHE FULANI MWEZI FULANI au ni KANISA lenye kuwaambia wakristo KESHENI MKISALI NA KUFUNGA MAANA HAMJUI SIKU WALA SAA WALA TAREHE WALA MWEZI HATA MWAKA WALA KARNE WALA MILENIA HAIJULIKANI, NI KAMA MWIZI TU AJAVYO. Hivyo Ni nani Wa kuchomwa moto mpaka majivu natumaini una akili na utashi hapo utajaza mwenyewe.

Hàlafu umaanza lini kuleta habali ambazo ni masimulizi/mapokeo (nazungumzia kuhusu yohane uliemtaja hapo mwisho nataka maandiko tena matakatifu na sio masimulizi/mapokeo). Umeanza lini kunukukuu habali za mapokeo/masimulizi amabayo kwako ni upagani sababu yako nje ya biblia. Unajua ni nani aliyekuletea hayo unayoyaita masimulizi kuhusu yohane kuwa ni mtume wa mwisho kufa nikikwambia ni kabisa katoliki utakataa ??

Leta andiko linaloonesha kuwa Hugo yohane unayemtaja hapo mwisho ndiye mtume Wa mwisho kufa na sio habali za mapokeo ya wanazuoni wako au masimulizi ya kipagani.
 
nyie msiofungamanisha endeleeni,acheni watu wafanye mambo yao na nyie fanyeni yenu mbinguni kila mtu anakwenda mwenyewe,tangu mmeanza hili zoezi mshapata wangapi????😀😀😀😀 mnachekesha kweli
Mkuu sio tatizo lao ni tatizo la kihistoria na vipaumbele vya waanzilishi wao. Kipaumbele naomba moja ni kupambana na ukristo kwa mwavuli Wa kabisa katolki
 
kabla hajazaliwa ALIKUWEPO.
Kuzaliwa katika mwili, na Kufufuka ilikuwa ni lazima sio fumbo, na ilitabiriwa na yeye alisisitiza.
halikuwa suala la bahati nasibu.
Utamaduni kwa Kuadhimisha Birthday kwenye Bibilia ulifanywa na wapagani (herode na farao ) na wafalme wa israel waliomuasi Mungu na kuiga desturi za nje.
Kusherehekea birthday ni kuhafifisha Uungu wake, Yeye alikuwepo siku zote, Ni alfa na Omega.
Tusmlazimishe kuwa binadamu kama sisi eti Mungu anabirthday, labda kama tungekuwa hatujui kama alikuwepo kabla ya kuzaliwa. hii sikukuu inamuhafifisha Yesu achilia mbali makandokando yake mengine.
Samahani mm sio mtaalam sana wa mambo ya imani,,,

Ila naona kama mnatafautiana imani hapo,,mwenzio anaamini katika Mungu baba,Mungu mwana na Roho mtakatifu wewe mitale na midimu unaamini YESU ndio Mungu mwenyewe
Wakatoliki wanakitu wanakiita FUMBO LA IMANI,,huwezi kulipinga kwa namna yeyote kwa sababu halikuhusu,,ukifanikiwa kulisoma utaelewa anamaanisha nn,,yaani Fymbo hilo ndio siri ya Kanisa,, mengine yote ni blaa blaa

Please naomba utafute hilo fumbo
 
Mkuu sio tatizo lao ni tatizo la kihistoria na vipaumbele vya waanzilishi wao. Kipaumbele naomba moja ni kupambana na ukristo kwa mwavuli Wa kabisa katolki
watapata tabu sana kama ndio mapambano wanayaendesha kwa hoja nyepesi namna hiyo.......wanapaswa kuangalia na ukubwa wa hicho wanachopambana nacho.
wanatia huruma
 
Amina, haya siyo maoni ni ndiyo ukweli na lazima ujue msingi mkuu wa mafundisho unabaki kuwa biblia, theolojia ya kanisa katoliki haimfundishi binadamu imani ambayo Mungu amefugwa na maandiko (Biblia) kwetu Mungu hana mipaka anatenda mambo makuu na mapya kila uchao.

Sasa wewe Mungu wako aliyelimited na biblia, si wa kwanza ata mafarisayo na masadukayo walipatwa na hali hii..! Yesu anaishi mioyoni na anatenda leo na kesho.
Kumbe kweli nyie mna nia ovu kwa binadamu. Yaani mnaweza jitungia mambo yenu wenyewe kwa kuwa hamuwi limited kwenye Biblia na mkafanya mafundisho ya uongo kwa kisingizio hicho. Mungu anawaona. Lazima uwe na akili ya kujiuliza. Kama Yesu mwenyewe alibaki kwenye maandiko nyie ni nani hata muwe na mafundisho yasiyotokana na Biblia takatifu. Hiyo ina tofauti gani na upagani, kwani nao chanzo cha Imani yao siyo Biblia.
Kama kanisa linaweza kuamua kuwa na chanzo chake cha rejea badala ya Biblia, sasa hiyo itakuwa ni machafuko. Kumbe ndio maana tafisri ya kwamba nyie ndio Babel inawahusu

YESU aliwachochea watu waliheshimu Neno la Mungu, Biblia. Jambo hilo linaonekana wazi kutokana na majibu yake alipojaribiwa na Ibilisi. (Mathayo 4:4-11) Kwa mfano, Yesu alitenda jinsi gani Shetani alipomshawishi ageuze mawe yawe mikate? Yesu alipinga kishawishi hicho kwa kunukuu maneno ya Musa ambayo yaliongozwa na roho ya Mungu, na unaweza kuyasoma kwenye Kumbukumbu la Torati 8:3. Na wakati Ibilisi alipomtolea Yesu utawala wa falme zote za ulimwengu kwa kubadilishana na tendo moja tu la ibada, Yesu alimjibu namna gani? Alikataa na kutaja kanuni ya Kimaandiko ambayo unaweza kuipata kwenye Kumbukumbu la Torati 6:13.

Fikiria jambo hili! Ingawa Yesu alikuwa Mwana wa Mungu, alitegemea kabisa Biblia alipokuwa akifundisha. Na bila shaka hakupuuza kamwe Neno la Mungu na kufuata mapokeo ya wanadamu. (Yohana 7:16-18) Hata hivyo, viongozi wengi wa kidini wa siku za Yesu hawakuliheshimu Neno la Mungu kama Yesu alivyoheshimu. Kwa nini? Waliyaona mapokeo ya wanadamu kuwa ya maana sana kuliko Maandiko Matakatifu. Yesu aliwaambia hivi waziwazi wanaume hao wa kidini: “Mkalitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu. Enyi wanafiki, ni vema alivyotabiri Isaya kwa habari zenu, akisema, Watu hawa huniheshimu kwa midomo; ila mioyo yao iko mbali nami. Nao huniabudu bure, wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”—Mathayo 15:6-9, Union Version.

Dini nyingi ulimwenguni, za Kikristo au zisizo za Kikristo, zinadai kwamba zinaiheshimu Biblia. Lakini unajua dini ngapi ambazo zinakataa mapokeo ya wanadamu wakati mapokeo hayo yanapopingana na mafundisho yaliyo wazi ya Neno la Mungu? Fikiria mifano miwili peke yake.

BIBLIA INAFUNDISHA HIVI: Yesu aliwashutumu viongozi wa kidini wa siku zake kwa sababu walipenda majina ya cheo na walitamani kuwa mashuhuri. Alisema kwamba wanaume hao walipenda “viti vya mbele katika karamu, na kuketi mbele katika masinagogi, na kusalimiwa masokoni, na kuitwa na watu, Rabi.” Kisha Yesu akawaambia hivi wanafunzi wake: “Ninyi msiitwe Rabi, maana mwalimu wenu ni mmoja, nanyi nyote ni ndugu. Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye wa mbinguni.”—Mathayo 23:1-10, UV.

SWALI: Je, viongozi wa dini Yenu wanapenda kuitwa kwa majina ya cheo na kutaka kuwa mashuhuri katika jamii, au wanatii amri ya Yesu na kuepuka kufanya hivyo?

Kutumia sanamu katika ibada.

BIBLIA INAFUNDISHA HIVI: “Usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu cho chote kilicho juu mbinguni, wala kilicho chini duniani, wala kilicho majini chini ya dunia. Usivisujudie wala kuvitumikia.”—Kutoka 20:4, 5, UV.

Mtume Yohana aliwaandikia hivi Wakristo: “Epukaneni na sanamu za miungu!”—1 Yohana 5:21, Biblia Habari Njema.

SWALI: Je, dini hiyo inatii amri ya Biblia iliyo wazi ya kuepuka kutumia mifano na sanamu katika kumwabudu Mungu?
''Other' sources of your faith allow you overlook those bible facts and behave on your own way. na mnataka kutufundisha kuwa tusifuate Biblia.
Za kuambiwa changanya na zako ndugu
 
"KUNA MSEMO WA KISWAHILI UNAOSEMA, "MWANAFUNZI HAMPITI MWALIMU WAKE" Mwisho utajua kuwa kanisa katoliki ndilo baba wa theolojia na mafundisho yote ya imani za Ukristo.


Katika hili nakaa kimya Nachukua mafundisho ya Mwl. wangu wa Maandiko Matakatifu Pd. Titus Amigu kama yalivyo na kuwapa katika maandalizi ya kusherekea Krismasi hii 2018.

TAREHE YA KUZALIWA KWA KRISTO
Nimeombwa nifafanue tarehe ya kuzaliwa Yesu Kristo kama ni kweli ni tarehe 25 Desemba au la.
Lakini kwa ajili ya kuwekana sana nimeyagundua maswali mawili yanayoweza kufuata baada ya kujibu swali hili la msingi. Ndiposa nimeambatanisha majibu kwa maswali hayo ya nyongeza. Swali moja ni kwa nini tunaadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo kila mwaka na lingine ni Yesu alitungwa mimba lini. Nifuatilie.
Nitaanza kujibu swali la kwa nini tunaadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo kila mwaka, kisha nitajibu swali la tarehe ya kuzaliwa Yesu Kriisto na kumalizia na swali la Yesu alitungwa mimba lini. Mpangilio huu unasababishwa na mantiki ya majibu yenyewe.

1. Kwa nini tunaadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo kila mwaka?
Najibu kifupi. Tunaadhimisha kuzaliwa kwa Yesu Kristo kila mwaka kwa ajili ya kujichumia faida zake ya kiroho na maadhimisho yenyewe si suala la kumzalisha Yesu tena na tena isipokuwa kuliishi upya tukio hilo kila mwaka. Hivi, tunapoadhimisha Krismasi si kwamba Yesu Kristo anazaliwa upya kila mwaka, isipokuwa tunakumbuka upya kuzaliwa kwake. Ni kumbukumbu (anamnesis).
Narudia, tunachofanya si kumzalisha upya Yesu Kristo kila mwaka isipokuwa ni kuliadhimisha tukio upya au kulikumbuka upya tukio (anamnesis). Tukio hilo lilikuwa muhimu kwa vile mtoto aliyekuwa anazaliwa alikuwa anakuja kuwa shujaa wetu.
Haiwezekani kumzalisha Yesu kimwili kila mwaka na ndivyo isivyowezekana kwa binadamu yeyote. Yesu alikuwa Mungu - Mtu lakini alikuwa mwanadamu kweli na siyo mcheza « Ze comedy » fulani. Kwa ukweli huo, bila shaka, tunajua wote kwamba Yesu, kama binadamu wa kweli, alizaliwa hapa duniani mara moja tu. Aghalabu, tunajua kwamba Yesu hatazaliwa tena na ndiyo kisa tunasubiri kurudi kwake mara ya pili kwa vindumbwendumbwe vya kiyama, ufufuko wa wafu na hukumu ya pili kwa kila mwanadamu. Kwa hilo, tumetahadharishwa wote tukae chonjo: tukeshe usiku na mchana, tujiandae kwa kuishi kwa imani isiyo na mawaa na utendaji wa kiadilifu huku tukiikimbia dhambi kama ukoma.

Kumbe, kuadhimisha tukio upya au kulikumbuka upya tukio siyo KULITUKIZA upya tukio. Acha nikupeni mifano miwili. Kuadhimisha upya tukio la uhuru wa nchi au kukumbuka upya siku ya kupata uhuru si kupata uhuru kwa mara nyingine. Kuadhimisha upya tukio la kufunga ndoa au kukumbuka upya siku ya kufunga ndoa si kufunga ndoa kwa mara nyingine.Vivyo hivyo, kuadhimisha siku ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo fulani si kumzalisha upya.
Si siri, Noeli au Krismasi ni siku ya kuzaliwa shujaa wetu. Siku ya kuzaliwa Mkombozi ni karibu nusu ya ukombozi wenyewe. Au sivyo? Ndiyo kisa basi, furaha haiwezi kuzuiliwa na mtu yeyote wala kwa sababu yoyote. Ni lazima kuifurahia sikukuu ya mtu wa maana hivyo. Mtu asiyeweza kuifurahia siku kama hiyo kuna mawili: ama ni mwendawazimu asiye na habari na mambo ya maana duniani au ni mfanyakazi wa kwenye kiwanda cha sumu. Vinginevyo, mtu mwenye akili timamu na anayefanya kazi za kawaida za kibinadamu sharti afurahi sana.

2. Tarehe ya Kuzaliwa Yesu

i. Tarehe ya Kiblia Ipo
Ili kukata maswali yafaa tuanzie masafa haya. Watu wengine huhaha huko na huko kutafuta tarehe aliyozaliwa Yesu wakati imeandikwa waziwazi kwenye Maandiko Matakatifu. Imeandikwa, usinibishe. Luka anataja tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu waziwazi, ilikuwa ni mwaka ule Kaisari Augustino alipotangaza sensa, yaani ile sensa ya kwanza katika enzi za ugavana wa Kwirinus huko Siria.
Imeandikwa: “Siku zile, tangazo rasmi lilitolewa na Kaisari Augusto kuwataka watu wote nchini kote wahesabiwe. Sensa hiyo ilikuwa mara ya kwanza, wakati wa Kwirinus alipokuwa gavana wa Siria. Basi, wote waliohusika walikwenda kuhesabiwa kila mtu katika mji wake. Yosefu pia alifanya safari kutoka mjini Nazareti mkoani Galilaya, na kwa vile alikuwa wa jamaa na ukoo wa Daudi, alikwenda mjini Bethlehemu mkoani Yudea, alikozaliwa mfalme Daudi. Alikwenda kuhesabiwa pamoja na mchumba wake Maria ambaye alikuwa mjamzito. Walipokuwa huko, siku yake ya kujifungua ikawadia, akajifungua mtoto wake wa kwanza wa kiume, akamvika nguo za kitoto, akamlaza horini kwa sababu hawakupata nafasi katika nyumba ya wageni” (Lk 2:1-7). Umeilewa tarehe hiyo?
Sisi tunaweza kubabaika sana juu ya tarehe hii, kumbe kwa watu wa wakati ule, tarehe hii ilikuwa wazi kama mchana. Ilikuwa ni sawa na kusema huku kwetu, mtoto huyu alizaliwa mwaka ule lilipofunguliwa daraja la Kigamboni, Mheshimiwa Paulo Makonda alipokuwa mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, katika mwaka wa kwanza wa utawala wa Rais John Pombe Mgufuli. Kwetu tarehe hii ni wazi kabisa, yaani mwaka 2016, lakini baada ya karne nyingi kupita tarehe hii iliyo wazi inaweza kuwa jambo la kubishaniwa sana.

Jambo hili si geni kwetu sisi Waafrika. Anayestaajabu anatustaajabisha wenzake. Waafrika hatukujua kusoma wala kuandika. Hatukuwa na kalenda yenye kueleweka. Hivi si haba Waafrika ambao wakiwauliza wazazi wao tarehe walipozaliwa wanaambiwa mathalani, “Ulizaliwa mwaka wa neema kubwa ya maboga alipotutembelea mjomba wako”. Au “Ulizaliwa mwaka wa nzige wengi nasi tufikwa na njaa kali sana” na kadhalika. Ajabu iko wapi?
Kumbe, sisi sote tukipekua na kutaka kujua tarehe kamili ya kuzaliwa Yesu, kama aliyotuandikia Mwinjili Luka, tunaishia kupata kizunguzungu na kubishana tu. Hata hivyo, duniani si wote tunaoshindwa hesabu. Kumbe, zamani zile, kwa misingi ya tarehe ya kuzaliwa Yesu, Wakristo walishatengeneza kalenda.

ii. Tatizo la Kalenda ya Dunia
Lakini katika kuitumia kulitokea haja ya kuirekebisha. Watu wa kale waliikalia chini kalenda yao. Katika kuirejea wakagundua mushkeli fulani. Waliona kulishafanyika makosa ya miaka minne au sita hivi, yaani kwamba kalenda yao ilitindikiwa miaka minne au sita hivi.

Kasoro hiyo waliigundua pale walipopambanisha miaka ya utawala wa Mfalme Herode Mkubwa na Yesu.
Waliona wameanzia kuhesabu kwenye mwaka wa mbele zaidi wakati walitakiwa kuanzia nyuma miaka minne au sita hivi. Waligundua kwamba walipaswa kurudisha nyuma miaka ya kuzaliwa Yesu hadi ikutane na utawala wa Mfalme Herode Mkubwa. Maana yake kwa kadiri ya kalenda yao, Kristo alizaliwa mapema kuliko mwaka ule iliposemekana kwa ujumla kwamba alizaliwa.

Udadisi wao ulianzia kwenye matumizi ya jina “augustus” linalotajwa na Luka katika 2:1-7. Kumbe, jina hilo ‘augustus’ lenye maana ya “mheshimiwa” kwa Kilatini, ni jina ambalo Gaius Octavius alijipa mnamo 27 K.K. Huyu alikuwa mtawala wa Dola ya Rumi, yaani Kaisari (Mfalme) tangu 31 K.K. mpaka 14 B. K. Na tena, Herodi Mkubwa anayetajwa kutaka kumuua Kristo, alikufa mnamo mwaka 4 K.K. Hivi kuipanga kalenda yao kwa kusema, Yesu alizaliwa mwaka 1, kwa pale walipoanzia hesabu zao, yaani mwaka wa kuanza mji wa Roma, ilimaanisha kuzisahau tarehe hizi muhimu. Wakawa wameisahau miaka minne au sita nyuma.
Walijilaumu kwa kosa hilo kwani iliwapasa wakati ule ule kurudi nyuma kwa miaka michache, ili Yesu azaliwe kabla Herode Mkubwa hajafa. La sivyo, uadui wao usingelikuwapo.

Kwa maelezo haya ya kosa walilofanya wapanga kalenda wa awali zile, mwaka huu 2016 ulipaswa uwe mwaka 2020 au 2021 au 2022. Kwa vyovyote, licha ya kuligundua kosa hilo la miaka minne au sita waliiacha kalenda yao iendelee. Na ndiyo kalenda inayoendelee hadi leo hii. Hii ndiyo kalenda iliyotupatia mwaka huu kama mwaka 2016 na hivi karibuni tutaingia mwaka 2017 badala ya mwaka 2021, 2022 au 2023. Si kitu, twende tu.
Mwenye ubavu wa kiakili, atusaidie kujenga kalenda mpya. Kama unaweza wewe kuitafsiri tarehe aliyozaliwa Yesu na kuipangia kalenda kamilifu jaribu! Lakini nadhani itakuwa kazi isiyo na tija yoyote. Zaidi ya hayo, tusahihishe kalenda leo kwa faida gani au kwa faida ya nani? Acha tuendelee tu!

Je, mnastaajabu? Msistaajabu. Basi, tangu zamani kulikuwa na ugumu wa kupata mwaka aliozaliwa Yesu, sembuse siku na saa. Lakini, pamoja na ugumu huo wa kupata mwaka, mwezi, tarehe na saa kamili alipozaliwa Yesu, ni ukweli usiopingika kwamba, Yesu alizaliwa kama mtu. Ukweli huu hautegemei kujua kwetu mwaka, mwezi, siku na saa. Ni ukweli wa milele,

iii. Hitaji la Kusherehekea Kuzaliwa kwa Mkombozi
Tunaambiwa kwenye Biblia kwamba siku yoyote aliyoifanya Bwana lazima tuisherehekee na kuifurahia. Siyo siku kama siku isipokuwa kile kilichofanywa na Bwana. Unabisha? Bila shaka utanibisha mimi kwa vile hujishughulishi na usomaji na upembuzi wa Maandiko Matakatifu. Basi, kama huna habari imendikwa kwa wino mweusi hivi: “Hii ndiyo siku aliyoifanya Mwenyezi Mungu, tuishangilie na kufurahi” (Zab 118:24). Ndipo likaja swali tusherehekee lini kuzaliwa kwa Mwokozi wetu au kufufuka kwake? Tukio la kuzaliwa kwake ni la thamani kubwa!

iv. Uamuzi wa Utamadunisho
Lakini hapa tuongelee tarehe ya tukio la kuzaliwa tu. Hilo la kufufuka tuliweke pembeni. Kama unakubaliana nami kwa ushuhuda huo, lilibaki deni la kuzipata siku za Mungu, na hapa hiyo siku aliyozaliwa Bwana wetu ili tuishangilie na tuifurahie. Jiulize, haki na wajibu huo tungalitimizaje bila kuitafuta siku aliyozaliwa Yesu Kristo?
Basi, kwa haki waamini walitafiti tafiti mazingira yao, kwa akili waliyokirimiwa na Mungu, ili kupata siku moja waamini wapate kusherehekea kuzaliwa Yesu Kristo. Mwishoni mwa tafiti yao, wakaigundua siku ya kufaa, ndiyo tarehe 25 Desemba. Hivi, kifupi, hii haina maana kuwa 25 Desemba ndio siku kamili alipozaliwa Kristo, ila imewekwa hapo kwa sababu za kihistoria na utamadunisho uliohalalishwa. Tena ingeweza kuwa tarehe nyingine yoyote kwa sababu HATUADHIMISHI SIKU bali TUKIO LA KUZALIWA YESU. Tuelewane hapa. Hatuadhimishi tarehe 25 Desemba isipokuwa kuzaliwa kwa Yesu Kristo.

Kwa kuwa tunababaishana sana hapa duniani, yafaa leo tupitie historia hiyo japo kifupi. Hata hivyo, kwa kuwa ninayotaka kukueleza hapa yatahusisha namba na hesabu hesabu, jiandae kwa kukishikilia kichwa chako vyema kisije kikaanza kushika moto na kuwaka kwa maumivu yasiyotibika kwa dawa ya maumivu ya dawatatu. Naomba tufuatane kwa karibu sana.
Ni hivi, katika siku za mwisho za dola ya kipagani ya kirumi, ibada za kuabudu jua zilikuwa zikifanyika sana. Mjini Roma dini ya Mithras, mungu - jua wa kiajemi, ilistawi sana. Kaisari Aureliani akajengesha hekalu la jua lisiloshindika, mnamo mwaka 274. Sikukuu kubwa ya mungu - jua, ilifanyika kila tarehe 25 Desemba, siku ambayo tabia ya kupungua pungua kwa mwanga wa jua ilikoma, na hivyo kuanza kuongezeka tena. Yaani, ilikuwa kama siku ya kuzaliwa upya jua. Na tangu tarehe hiyo, siku zilianza kuwa ndefu tena.

Mambo haya ya kupungua na kuongezeka kwa mwanga wa jua, ndiyo yanayotokea huko Ulaya kila mwaka hadi leo hii. Basi, sikukuu hiyo ya jua iliitwa siku ya kuzaliwa jua lisiloshindika, maana ijapo mwanga ulikuwa ukipungua, jua lilikuwa halifi kabisa.
Tangu siku za Kaisari wa kwanza mkristo, Kostantino, tarehe ya sikukuu ya mungu - jua ikafanywa sikukuu ya kuzaliwa Bwana Yesu Kristo, Mungu asiyeshindika kweli badala ya jua, kiumbe chake mwenyewe. Wayahudi walishindwa kummaliza Yesu, alifufuka mzima. Tunajua kwamba hata jua halikupata kuwako bila NENO (Yn 1: 1- 3).
Tukisoma Kalenda ya Mashahidi iliyotengenezwa na Philocalus mnamo mwaka 354, tunaweza kuona kwamba, sikukuu ya kwanza ya Krismasi ilisherehekewa mwaka 336 huko mjini Roma. Katika kalenda hii, Krismasi iliwekwa mwanzoni mwa mwaka wa liturujia.

v. Sababu Tatu za Tarehe 25 Desemba
Yaonekana kulikuwa na sababu tatu zilizosababisha kuwekwa kwa sikukuu ya kuzaliwa Bwana hapo 25 Desemba.

Mosi, mkazo wa kiteolojia kwenye kitendo cha Yesu kujifanya mtu, kujimwilisha, yaani kuadhimisha kanuni ya imani ya Nicea (mwaka 325) kimatendo na kikamilifu zaidi. Ni kanuni hii ya imani na si ile fupi ya mitume, iliyokazia fumbo la Yesu kujifanya mtu kama sisi.

Pili, kumtambua Kristo kama mwanga wa kweli, jambo linalosemwa na Mal 4:2. Basi, Kaisari Kostantino hakuona ni vibaya sikukuu ya Yesu aliye mwanga, ikichukua nafasi ya sikukuu ya mungu - jua, kwa vile mwenyewe alikuwa mwabudu jua hapo mwanzo kabla hajabatizwa.

Tatu, ujenzi wa kanisa la Mt. Petro pale Vatikani. Ujenzi wa kanisa hilo ulikuwa mgumu. Kwa nia ya kujenga juu ya kaburi la Mt. Petro, ilipasa watu wabomoe nusu mlima. Na hapo karibu na kaburi kulikuwa na altare ya mungu - jua, ambayo nafasi yake ilichukuliwa na altare ya kutolea sadaka ya kweli ya Bwana wetu Yesu Kristo.

vi.Krismasi Ilichelewa Mashariki
Kwa upande wa mashariki mwa dunia iliyojulikana wakati ule sherehe ya Krismasi ilifika baadaye kidogo:
- Siria kati ya 363 na 373 kwa ushuhuda wa nyimbo za Ephrem,
- Kostantinople mnamo 380 ambapo Gregory wa Nazienzi alihubiri kwamba Krismasi ni matukio ya Bwana kujifanya mtu na kuzaliwa kwake, taarifa ya malaika kwa wachungaji, kutolewa Bwana hekaluni alikokutana na Simeon na Anna na kutembelewa kwake na mamajusi. Gregory alihubiri kwamba, Tokeo la Bwana maana yake hasa ni Ubatizo wa Bwana, mwanga wa dunia.
- Antiokia, Krismasi ilianza mwaka 386, Misri mwaka 432, Yerusalemu kati ya 424 na 458, n.k.

vii. Tarehe Tofauti Tofauti
Kutokana na migogoro ya kihistoria, makanisa ya magharibi yameachana njia na makanisa ya mashariki. Makanisa hayo ya mwanzo hutenganisha Krismasi (25 Desemba) na Tokeo la Bwana (6 Januari), wakati yale ya mashariki, yaani makanisa ya kiorthodosi husherehekea yote bila kutenga kila tarehe 6 Januari.
Kifupi, tarehe ya kuadhimisha katika Kanisa la Magharibi na baadhi ya Makanisa ya Mashariki pamoja na walimwengu wengine ni tarehe 25 Desemba. Lakini katika baadhi ya Makanisa ya Mashariki huadhimishwa tarehe 7 Januari. Na katika makanisa ya Kiarmeni huadhimishwa tarehe 6 Januari.

Mgawanyiko huu ni wa watu. Biblia inasema kimoja tu kwamba, Kristo alizaliwa (rej. Lk 2:1-7) na akawaletea watu utukufu wa Mungu. Tarehe si jambo la kukosea usingizi. Unabisha? Unabisha nini? Hivi, ikiwa hujui siku aliyozaliwa babu wa babu yako inamaanisha hakuzaliwa na hakuwapo? Usitake nicheke ukayaona mapengo yangu mie!

viii. Je, Tarehe ni Muhimu Sana?
Tujiulize sote. Hivi, hatuwezi kumwamini Kristo mpaka tujue alizaliwa lini? Je, tunaweka kumbukumbu za tarehe za matukio yetu muhimu? Je, tunazo sikukuu zo zote za kale ambazo tunaweza kuzitamadunisha kwa kupisha sikukuu za kikristo? Je, viongozi wetu wakristo wanaweza kutusaidia nini katika kupanga liturujia yetu? Kaisari Konstantino aliwasaidia sana wakristo wenzake. Tunapowaombea viongozi wetu wajali dini zetu tunataka wafanye nini? Tunataka wasifanye chochote? Mbona Konstantino alifanya na sasa analaumiwa?

3. Tarehe ya Kutungwa Mimba Yesu Kristo
Baada ya kulijibu swali la tarehe ya kuzaliwa Yesu Kristo, nadhani sasa tunaweza kujibu swali dogo zaidi, “Bikira Maria alipata mimba lini?” Kwa maneno mengine swali dogo ni Yesu alituungwa mimba lini?
Pasipo mashaka yoyote, kwa vile Yesu alikuwa mwanadamu halisi, alichukuliwa kwenye mimba kama mwanadamu halisi yaani kwa miezi tisa vile vile. Biblia inataja tarehe ya kutungwa kwake sawia na tarehe ya kuzaliwa kwake.
Hata hivyo, tarehe ya kutungwa mimba ya Yesu Kristo kumetajwa kwa tarehe inayotupasa kuielewa vyema. Biblia inatuambia ilikuwa ni mwezi wa sita, malaika Gabrieli alipotumwa kumwendea mwanamwali Bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo lilikuwa Mariamu (rej. Lk 1:26-27).
Hata hivyo, mwezi huu wa sita si kwa hesabu za kuanzia mwanzoni mwa mwaka, isipokuwa kwa hesabu ya ujauzito wa Elizabeti, mke wa mzee Zakaria. Aya 26 inaendeleza yaliyosemwa kabla yake yaani kwamba Elizabeti alipata mimba yake uzeeni (rej. Lk 1:23-25). Hivi basi ni mwezi wa sita kwa mimba ya bi mkubwa huyo na si mwezi wa kizungu Juni.
Watu wanapoelewa mwezi wa sita kuwa mwezi wa kizungu Juni, hushikwa na homa wanapoona Wakristo wakisherehekea kuzaliwa kwa Bwana Yesu Kristo mwezi Desemba. Hao huchanganyikiwa kwa mikokotoo ya hesabu zao batili kwa kiasi kile zilivyoegemezwa kwenye mwezi walioukosea.
Wachache hawaiendi mbali ya kuajabia. Lakini wengine hudhani, kwa kituko hicho kwamba Yesu alizaliwa “njiti”. Na hapo ndipo wengine huenda kwenye kosa kubwa zaidi la kudai Yesu alikuwa mtu wa pekee kwa vile alikaa tumboni mwa mama yake kwa miezi pungufu na bado akazaliwa vyema na kukua vyema.
Huko kote ni kukosea. Yesu alitungwa mimba na kukaa tumboni kama watoto wa kawaida wa wanadamu. Kwa kuwa tarehe ya 25 Desemba ni mapato ya utekaji sikukuu ya kipagani, kwa akili, ndio utamadunisho (rej. Mt 22:37), kusudi siku ya Mungu-jua wa wapagani itumike kumtukuzia Mungu Jua wa kweli yaani Yesu Kristo (rej. Yn 1:5-9), kutungwa kwake huadhimishwa kimahesabu nyuma, tarehe 25 Machi, ndiyo sikukuu ya Kupashwa Habari Bikira Maria. Tangu tarehe 25 Machi hadi 25 Desemba ni miezi tisa kamili. Hii ndiyo mantiki ya utamadunisho wa Kikristo.

Je, Kutamadunisha Kitu ni Halali?
Ni halali kabisa. Wapo wanaokasirika na kufoka kwa nini Wakristo walichukua tarehe ya wapagani, 25 Desemba kusherekea jambo la Kikristo. Watu kama hao ni wasahaulifu tu, usiwajali. Utamadunisho ni uchukuaji wa kitu fulani, kukipa maana mpya au nzuri zaidi na kukitumia. Wakristo hawawezi kukataa mambo ya wapagani wala wapagani hawawezi kukataa mambo ya Wakristo. Dunia ni moja, tunashirikishana. Wakristo hawana uwezo wa kuvumbua kila kitu chao. Tena hawapo Wakristo wa kanisa lolote waliovumbua vyote wanavyovitumia wenyewe. Asikudanganye mtu.
Kumbe, wanachogundua upande mmoja wa dunia, wewe wa upande mwingine unaweza kukichukua na kukitumia kwa manufaa yako. Cha wapagani kinaweza kutamadunishwa na Wakristo wakakitumia, na cha Wakristo kinaweza kuchukuliwa na Wapagani wakakitumia. Usinibishe.
Yafuatayo ni mambo ya uvumbuzi wa wapagani nasi tunatumia tena kwa furaha kabisa. Labda hatujui. Suruali, viatu, miwani, kioo, herufi, hesabu, kusoma na kuandika, matibabu ya hospitali n.k. Kama wewe ni mmoja wa wale wasiotaka kabisa mambo ya wapagani, usivitumie vitu hivi kuanzia kesho.

Huenda majibu haya yamekuzidi urefu. Lakini yasome moja moja kwa umakini mkubwa kama unataka kuujua ukweli. Kuyasoma majibu haya kwa umakini ndiyo gharama ya kujua tarehe ya kuzaliwa Bwana Yesu.
NAWATAKIENI NYOTE MAANDALIZI MEMA YA SIKUKUU YA KRISMASI. KILA LA HERI NYOTE!

(Kwa hisani ya Pd. Titus Amigu aliyetoa mafundisho haya)
umeeleweka vyema
 
View attachment 957929

nadhani ameeleza vizuri sikukuu hiyo ni makubaliano ya kanisa lake ila sio agizo la Yesu.
Haikukumbukwa na Mitume.
Haikukumbukwa hata na hao wafuasi wa mitume wa awali.
Watu ni vizuri wakaelewa hilo pia.
Maoni ya kikundi binafsi yasibebeshwe hadhi ya kuwa universal obligation kwa kila mcha Mungu.

Kuiga mambo ya wapagani ni sawa na Kutoka Nuruni kwenda kutafuta mwanga gizani.
Watu wa Bibilia hawakuhangaika na haya masherehe maana walijua Kuzaliwa na Kufa kwa Yesu mioyoni mwao ni Jukumu la Kiroho la mkristo kila siku sio sikukuu ya kula ubwabwa na kununua mimea kuijaza sebuleni.
Maoni ya wanadamu, yanapaswa kutenganishwa na maandiko katika matamshi na maandishi.
maelezo mengi mazuri yalioandikwa kwa lugha shawishi ila hayana uzito wowote kwenye maandiko matakatifu mzani umeelemea kwenye utamadunishwaji na masimulizi ya kale.
Yeye mwenyewe vip hanaga birthday?
 
hao wafuasi Wa kibwetele hawana tofauti yeyote kabisa na wale wafuasi Wa bwana mmoja kule marekani aliyewaambia wafuasi wake kuwa kristo angerudi tarehe Fulani, mwezi Fulani then wafuasi wake wakafanya mambo fulanifulani yasio na tofauti yeyote na wafuasi Wa kibwetele. tofauti ni moja tu kibwetele aliwapiga moto wafuasi wake ila huyo bwana Wa huko maeekani yeye aliwatungia wimbo kwamba BWANA ATARUDI UPESI wimbo ambao unaimbwa mpaka leo na wafuasi wake wasiojua kuwa yesu alitahadharisha HAKUNA AIJUAYE SIKU WALA SAA.

Sasa hapo sijui mjinga Wa kuchomwa moto mpaka majivu ni nani ?
Ni wale walioambiwa yesu atarudi TAREHE FULANI MWEZI FULANI au ni KANISA lenye kuwaambia wakristo KESHENI MKISALI NA KUFUNGA MAANA HAMJUI SIKU WALA SAA WALA TAREHE WALA MWEZI HATA MWAKA WALA KARNE WALA MILENIA HAIJULIKANI, NI KAMA MWIZI TU AJAVYO. Hivyo Ni nani Wa kuchomwa moto mpaka majivu natumaini una akili na utashi hapo utajaza mwenyewe.

Hàlafu umaanza lini kuleta habali ambazo ni masimulizi/mapokeo (nazungumzia kuhusu yohane uliemtaja hapo mwisho nataka maandiko tena matakatifu na sio masimulizi/mapokeo). Umeanza lini kunukukuu habali za mapokeo/masimulizi amabayo kwako ni upagani sababu yako nje ya biblia. Unajua ni nani aliyekuletea hayo unayoyaita masimulizi kuhusu yohane kuwa ni mtume wa mwisho kufa nikikwambia ni kabisa katoliki utakataa ??

Leta andiko linaloonesha kuwa Hugo yohane unayemtaja hapo mwisho ndiye mtume Wa mwisho kufa na sio habali za mapokeo ya wanazuoni wako au masimulizi ya kipagani.
Hao jamaa wafuate uwahoji mwenyewe ila mimi naamini haya.
Yesu anakuja Upesi licha ya kutojulika siku au saa.
Hakutaja siku lkn alitaja dalili, Nawaambia wakazi wa ulimwengu kuwa Yeye aliyesema anakuja mambo aloyotabiri yanatokea kwa spidi kubwa.
Nawaambia wajiandae muda wote sekunde zote maana hawajui saa wala siku.
Sio Mimi tu na wote wanaoamini Bibilia kama kitabu chao kukuu cha imani bila matamko ya wakuu wa kidini au masimulizi ya kimapokeo.

Hayo nimekupa maana unayaamini wewe. Nilitegemea uonyeshe msimamo imara kutetea na kuyafafanua.
Kama unakana na unavyoamini na unaogopa kuvijengea hoja, mkuu unakuwa unautoa mjadal kwenye uhalisia na kuusimika kwenye unafiki na usanii.

Ubarikiwe. naomba maoni yako kwenye mambo yako unayoyaamini, na umekiri kwa maandishi kuwa unayaamini, na umeayatumia kujenga hoja.
 
Back
Top Bottom