Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Tumeshakubaliana kwamba damu ya Yesu pekee ndio itakayokuondolea dhambi na sio sadaka yako.
 
Mbona sasa hajanukuu mistari ya biblia walau kwa kila dhambi ili kuback up mafundisho yake?

2 Mambo ya Nyakati 7
14 ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.
 
Sadaka ni AMRI.
 
Yaani uzini na mke wa Jirani Yako sirini halafu utubu sirini?

Mwombee Mungu Roho mtakatifu akufunulie aloyasema mwenyewe kabla ya kupinga.
Hakuna kitu kama hicho mzee acha kukaririshwa ujinga na wasaka tonge, huyo sijui mchungaji sijui nabii mwenyewe unaye amini atakutubisha anakula mkeo sirini,

mambo ya imani ni magumu sana ila jua tuu kwamba mungu anafanya kazi na kila nafsi individually hakuna nafsi inayo weza iombea msamaha nafsi nyingine na ndio maana kila mtu atahukumiwa kwa makosa nandhambi zake mwenyewe.
 
Yaani fedha unampa mchugaji harafu unasema humfaidishi
 
Tumeshakubaliana kwamba damu ya Yesu pekee ndio itakayokuondolea dhambi na sio sadaka yako.
hicho ndio msimamo wangu tangu awali. ila wenzako wanasema uende na sadaka unapoenda kutubu. angalia alichoandika huyu mwenzio, nimekata baadhi ya maneno; ni sadaka ya ukombozi ipi na upi anaongelea huyu jamaa hapa? sadaka ya ukombozi ilishatolewa na Yesu, tunasamehewa bure.

DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.
 
(1 Wakorintho 6:9-10)
Au hamjui ya kuwa, wadhalimu, hawataurithi ufalme wa Mungu? Msidanganyike, waasherati, hawataurithi ufalme wa Mungu,

Wala WAABUDU SANAMU, Wala wazinzi, Wala wafirahi, Wala WALAWITI,Wala wevi, Wala watamanio, Wala WALEVI, Wala watukanaji, Wala wanyanganyi.


(Ufunuo 21:8)

Bali waoga, na wasioamini,na wachukizao, na wauwaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote,sehemu Yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo MAUTI ya pili.
 
hahahaha, nadhani unahitaji kwa kila dhambi uweke mstari kwamba utatubu na kusamehewa kama utatubu kwa mtumishi tena ukiwa na sadaka.

hiyo mistari kama ilivyo ni ya jumla, kwamba usipotubia dhambi hizo ulizoorodhesha (bila kuweka condition kwamba ukatubu wapi) hautaurithi ufalme wa Mungu. Mungu akusaidie, najua kuna siku utaelewa, na kama utajifanay shingo ngumu utalazimishwa kuelewa. hata sisi tulikuwa kama wewe.
 
Hayo ni maelekezo ya Mungu.

Sitaongeza Wala kupunguza. Ikiwa huamini, Ingia maombini uliza.

Hakuna popote nimesema lazima ubebe sadaka ikiwa huna.

Sadaka ni amri, Si Kwa ajili ya kununua msamaha.

Sadaka ni hiari na ni shukurani .

Ukombozi unahusika Kwa kutumia Damu ya Yesu, na kuvunja NDOA za kipepo na mikataba ya kipepo Kwa dhambi husika hapo juu.

Sadaka inatumika kureplace Mahari mapepo yalitoka Kwa mfungwa Ili kuzini naye Rohoni.

Amen
 
Aliyefundisha ni somo Hilo ni ROHO MTAKATIFU,

Sihitaji kufundishwa na wewe, nimeweka alichosemea Yeye na sijaongeza uongo mimi.

Wewe unaongea Kweli ya BIBLIA Kwa kupindua nilichoeleza katika thread.
 
acha kujifurahisha dogo, maelekezo ya Mungu toka mstari gani kwenye Biblia? utaje mstari unaotoa maelekezo kwamba " DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa
". au ni maelekezo ya Mungu kwenye ndoto au maono, maelekezo yako yameegemea wapi, hebu tueleze. ni kipi hicho alichosema Mungu ambacho huwezi kuongeza wala kupunguza,hahahahaha, unachekesha kweli kweli.
 
Kuhusu sadaka ya ukombozi
Mafundisho ya kipepo pekee ndiyo yatataja sadaka ya ukombozi.
Hakuna kinachoweza kumkomboa mwanadamu kutoka katika hatari ya jehanamu au mateso yoyote ya kiroho zaidi ya DAMU na JINA LA YESU.
Kama mwanadamu angekuwa na namna yoyote ya kujikomboa zaidi ya jina na damu ya Yesu basi Kristo asingekuja duniani.
Ni heri hilo jambo la kuwashirikisha watumishi wakuombee toba na kukufungua kutoka katika dhambi ila hilo la sadaka ya ukombozi ni mafunzo ya kipepo
 
(Acts 9:3-6)
MATENDO 9:3 - 6 INASEMA:

Wakati alipokuwa akisafiri, ikawa anakaribia Dameski; ghafla nuru kutoka mbinguni ikamwangaza kotekote. 4Akaanguka chini, akasikia sauti ikimwambia, Sauli, Sauli, mbona wanitesa? 5 Akasema, U nani wewe, Bwana? Naye akasema, Mimi ndimi Yesu unayemtesa. 6Lakini simama, uingie mjini, nawe utaambiwa yakupasayo kutenda. 7Na wale watu waliosafiri pamoja naye wakasimama kimya, waliisikia sauti, lakini hawakuona mtu. 8Sauli akainuka katika nchi, na macho yake yalipofumbuka, hakuona kitu; wakamshika mkono wakamleta mpaka Dameski. 9Akawa siku tatu haoni; hali, wala hanywi.

HAYA WEWE SASA TUAMBIE WAPI HAPO SAULI/PAULO ALITUBU KWA KUPELEKA SADAKA KWA MCHUNGAJI, manake tunachopishana na wewe hapa ni kwanini ubebe sadaka wakati unaenda kutubu, huoni kama umepigwa sana na hao manabii?

wewe ndio wale wanaokotaka kimstari kimoja afu wanaenda kufungua hadi kanisa, wanajiita wachungaji kufundisha watu mapotofu kama hayo.
 
Ni hayo tu Kwa Leo.

Ubarikiwe.
 
Ni hayo tu Kwa Leo.

Ubarikiwe.
wewe umechanganyikiwa au umepagawa na pepo la upotoshaji, shetani hutumia wanadamu kupotosha yaliyo ya Mungu, hata dini za ajabuajabu zilianza na watu wasiojua Neno la Mungu kama wewe na shetani anawapenda sana watu kama wewe. Mungu akusaidie, upo too vulnerable na umepotea mbali mno.
 
Message sent!!

Ubarikiwe, Mungu akipenda atakuokoa Kwa muda wake,

Muhimu umesoma message, KAZI ya muhubiri ni kuhubiri basi.

Amen
wewe hujaokoka, kaokoke upya kabisa na unatakiwa ukae mikononi mwa mtumishi anayejua Neno la Mungu akufundishe manake unaeneza mapotofu matupu na hapo ulipo wala hufanyi kazi yeyote ya Mungu, uhaiharibu.
 
Chukua sadaka kamuone mtumish akuombee.
Kwamba ww huna mdomo w kuomba
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…