Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Mungu hahitaji tulipe chochote au tupitie kwa yeyote ili atusamehe dhambi. Ni neema na rehema zake hutuondolea hatia na kutuweka huru mbali na dhambi katika Jina la Yesu.
Ni kweli kabisa, ila Kuna wakati Mungu hutumia watumishi wake kutupa muongozo au kutuhudumia.

Mfano kwa muumini mpya lazima aongozwe sala ya toba na mtu mwingine ili kumpokea Kristo, yeye binafsi bila muongozo huenda asiweze.

Kwa mchawi anayetaka kusalimisha uchawi na kumpokea Kristo, lazima afanyiwa hiyo huduma na Kristo kupitia mtumishi wake itakayomtenga na maagano aliyoingia na Ulimwengu wa giza, yeye binafsi sio rahisi kufanya hayo.

Hata Sauli (mtume Paulo) licha ya kutokewa na Yesu njiani, bado Yesu alimtuma Anania akamwekee Paulo mikono ndipo macho yake yakafunguliwa na rasmi kuanza maisha mapya.
 
Imeandikwa afichaye dhambi hatafanikiwa.

Dhambi tajwa hapo juu, kwamwe huwezi tubu pekeako sirini ukatoboa.

Ni kheri kutii kuliko kuwa mbishi.

Amen
Dhambi haifichwi lakini imani yangu inaniambia Mungu anajua kilichopo ndani ya moyo wako na anaona mwisho kabla ya mwanzo

Hivyo suala la kutubu ni wewe na Mungu kupitia upatanisho wa Kristo Yesu ambaye ndie mpatanishi mkuu

Hupaswi kwenda kwenye kitubio na kumueleza mchungaji au padri dhambi zako nae akwambie tu umesamehewa
 
Si kweli, dhambi yeyote mtu unaweza kutubu ukiwa peke yako.....watumishi wa Mungu ni malaika tu.
 
Roho mtakatifu ndiye aliyetoa ujumbe huo kupitia mtumishi wake.

Kabla ya kupinga, ikiwa umejazwa Roho mtakatifu, omba akuthibitishie ikiwa ujumbe huo umetoka kwake au la.
Nyinyi ndo mnafanya wakristo tuonekane hatuna akili.
 
Siku hizi bangi inavutwa na walokole sana
Hawa vijana wa makanisani wengi ni wapuuzi. Kazi yao ni kupiga vinanda, kuimba na kupiga drums hawana muda wa kusoma biblia wakidanganywa na mtume wao moja kwa ktk social media
 
Acheni kutengeneza mazingira ya kupiga ela. Achani kutaabisha watu. Maandiko Yako wazi kwa kila kitu. Hio ya kutoa sadaka ni uwongo mtipu. Pili kwenda kwa wachungaji ni part tu ya process ya kutubu. Wale kazi Yao ni moja tu iukusaidia usirudie kosa basi. Mwisho hayo madhambi kibao ulioorodhesha toa na maandiko
 
Leta andiko

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Mbona huwa mnapinga kuungama kwa Padre?.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Siyo.

Tendo la NDOA ni Tendo TAKATIFU, kitanda Cha NDOA ni kitakatifu.

Amen
Ndiyo nakwambia tuwe tunafika tu na kuchomeka bila manjonjo yeyote ?

Maana kwa mujibu wako wewe hata kunyonyana ulimi itakuwa ni dhambi.

Alafu unaruka ruka tu huleti maandiko ili tukkunge mkono.

Leta reference ikiyoko kwenye biblia au Qur'an hapa tuache kubishana kwa maneno
 
Upuuzi mwingine, mbinu za kupiga pesa,
Wale wanaoenda kwa mwamposa au kuhani Musa kuombewa, watabaki mafukara, wakati viongozi wao wanazidi kuneemeka, majasiriamali ya dini.
Huhitaji mbwembwe za mtu mwingine kumfikia Mungu, nyie majitu mnawinda sadaka tu, nimeona wengi hawaoni haya kumwambia mtu atoe nusu ya mshahara wake kama sadaka! Harafu Kodi, chakula,na mahitaji mengine apate wapi!
Ategemee Mana kutoka juu?! Ila wachungaji wao wapo bize kuanzisha guest house, baa, hotel, kenge kabisa.
Viongozi wa dini wamekua waongo Sana, na wanatumia ujinga wa wananchi kuwapiga haswa,
Juzi nikamsikia Padre mmoja, anahubiri watu wa toe Sana, a kasema Israel imebsrikiwa Sana kwa sababu ya "kutoa" Sana sadaka!
Nikajiuliza, huyu mtu anaakili kweli, au anaona kila mtu ni mjinga?
China ni super power, inatoa wapi sadaka? Kule hakuna ukristo, imefika pale sio kwa sababu ya kwenda kanisani kutoa sadaka, walioandika vision ya china, hawa kuwa wakaristo, wala hawamjuhi jesus, walitumia bongo zao, wakafanya kazi, wanatumia sayansi, na tekinolojia, ndio wamefika pale,
Qatar, saudia,Malaysia, Korea, huko ni kazi tu sio kuimba mapambio,
Kasome kitabu cha Mzee Mengi, uone kazi aliyofanya kuijenga IPP media, hakuchukua ka mshahara kake aka wa anatoa fungu la kumi kila jumapili, Mara paaaap, ukwasi, huooooo! Acheni utaperi.
 
Kuna mstari wowote unazungumzia punyeto?
 
Ufunuo 21:8.
kitu ambacho huyo mkuu amecomment nawewe ulichojibu ni vitu viwili tofauti kabisa.

Huyo mkuu amesema andiko linasema tukimuomba Mungu Jambo lolote atafanya

Akimaanisha Mungu ametupa uhuru wa kumuomba kitu chochote hata msamaha na akatenda.

Wewe unasema andiko linalosema wachawi, wazinzi, wapya ,wasioamini watatupwa kwenye ziwa la moto

Mbona hizo comment mbili hazilingani...

Nilitarajia utakuja na andiko ambalo linasema wasioemda kutubu kwa watumishi watatupwa moyoni....

Sisi binadamu wote tuna uungu ndani yetu (roho mtakatifu)
Huyo hutusaidis kufikisha hoja zetu kwa Mungu kwaurahisi na sio kupitia kwa watumishi.

Jambo usilojua watumishi sio Mungu na wao hawajakamilika kabisa...wanatenda dhambi pengine kuliko wewe sasa iwaje ukamfuate yeye akuombee wakati hata yeye hana kibali mbele za Mungu kutokana na dhambi zake.
 
Si DHAMBI zote Hadi uende Kwa mtumishi, ni baadhi.

Mfano, huwezi kufirana, kuua au kuzini na mke wa Jirani Yako halafu ukatubu sirini, dhambi hizo hapo juu Zina mikataba na vifungo vya kipepo ambavyo lazima uhusishe Mtumishi.
hapa nilivyokuelewa unamaanisha Watumishi/ wachungaji wametuzidi nguvu za kiroho ndio maana inapaswa tuwafuate ili wakazishinde dhambi zilizo ndani yetu

Lakini kitu ambacho hufahamu nafasi zetu na utashi wetu ndio unaoweza kuzishinda dhambi zetu hata zikiwa kubwa kiasi gani

1 Yohana 5:4 "Kwa maana kila aliyezaliwa na Mungu ameushinda ulimwengu. Nasi tumeushinda ulimwengu kwa imani yetu."

Hapo ametuzungumzia Kwa ujumla na neno ulimwengu akimaanisha dhambi/falme ya giza (ulimwengu huu ni ufalme wa giza kwamaana ni Mali ya shetani)

pia hata biblia inagusia kuhusu usiri wetu kwenye baadhi ya mambo sio kilajambo ni la kusema....si kila dhambi ni ya kusimulia kwamaana hata ukimshirikisha mchungaj kama moyoni haujaikili ni kazi bure.
 
Acheni ubishi, kubishana na Maagizo ya Mungu si sawa.

Tangu enzi, watumishi, Waamuzi, walawi walitumika kusaidia watu wa Mungu maelekezo na maandiko yapo.

Dhambi ya zinaa na dhambi tajwa, huwezi tubu pekeako, ni maelekezo hayo,

Utii na Imani ndo vinatakiwa.
 
Si Kila dhambi.

Dhambi tajwa Zina maagano, masharti na NDOA za kipepo, dhambi hizo zinamweka mtenda kuwa mfungwa aliyenunuliwa, hivyo mtumishi ni muhimu ahusike.
 
Mkuu maandiko ni kitu kilichowazi sana..

Tunahitaji kuelekezwa ndio maana wakuu wote tunaomba utuwekee vipengele vya biblia ya hizo sehemu ili tufunguke macho na kuelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…