Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

huyu jamaa anachanganya sana pia kuhusu kukutana na Mungu, kukutana na Mungu sio lazima ukutanishwe kwa kuwekewa mikono ya mtu mwingine, unakutana na Mungu moyoni. kuna watu wameingia chumbani kusali, Mungu akawashukia kwa kuangalia mioyo yao, na Mungu akishuka, huhitaji tena kwenda kuondolewa sijui laana sijui nini za ukoo kama anazosema, Mungu ameingia moyoni, hayo mataputapu yataendelea kukaa kwako yanatafuta nini sasa? manake ukiona bado yapo, haujakutana na Mungu, tafuta Mungu.

wengi wa waliotegemezi wa maombezi kama huyu anayetaka kutapeli watu hapa, siku zote huwa hawakutani na Mungu. ni wapenzi wa miujiza na wamefanya ukristo kuwa kama uganga wa kienyeji, na hakuna hata mstari mmoja wa Biblia wanasimamia kuwasapoti, ni mawazo ya kibadamu na chanzo chake ni shetani. imefika wakati watu hata kusoma Neno, kufunga kutafuta uso wa Mungu, kuabudu kwa kweli au kuomba ujazo wa Roho Mtakatifu hawahitaji, wanachotaka waende pale kwa nabii awatabirie wapate wanachopata, waondoke, maisha rahisi tu hivyo. hawajui kuwa shetani pia huwa anaweza kufanay miujiza, na ukiangalia miujiza yao yote haidumu kwasababu ni mazingaombwe tu ya shetani. mshindwe kwa Jina la Yesu.
 
ukitembea na mke/mume wa m2 hautasamehewa ata ukiombewa na watumishi,,,sharti ni lazima atafutwe mume/mke wa uliyezini nae na uwaombe msamaha akikusamehe utasamehewa!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
dini safi
sadaka ya ukombozi
madhabahu
mtumishi a.k.a mchungaji? why kwanini?
hata kale za wana wa israel walitumia madhabahu, sadaka ya ukombozi na dini safi,
sasa hata mimi naomba kueleweshwa ndugu? mtumishi atacheza kama nani au kazi yake halisi katika kutubu dhambi hizo ni ipi je atakua reporter au ni kazi zipi tafadhali naomba elimu hii inifae
 
Jinsi mlivyokuwa wa mchongo WIZI haujaorodhesha badala yake umeweka dawa za nguvu ya kiume na punyeto.
Wizi mmeshindwa kuuweka kwasababu watanzania wote ni wezi.
Mmechagua vile vitu ambavyo ni popular ili mzidi kuwatisha watu muendelee kutafuna sadaka.
 
Sadaka niliyoiongelea Si sadaka ya kufanyika mbadala Ili usamehewe dhambi, HAPANA.

Mtu anayejichua Kwa Mfano, awe kwenye NDOA au nje ya NDOA,

Ukijichua, katika Ulimwengu wa Roho umefunga NDOA kabisa katika Ulimwengu wa Roho.

Na ndoa hiyo, lazima Mahari imetolewa na mapepo, hivyo ajichuaye, ni mfungwa kamili.

Kuondoa hati ya NDOA ya NDOA ya kiroho, kuondoa sadaka hiyo na Mahari hiyo, lazima ukomboe na sadaka na Damu ya Yesu.

Unahitaji kufundishwa na Roho mtakatifu.

Pia maandiko yapo, nikikuletea maandiko utaamini?
 
Sala ya toba kwa mwizi umeiona wapi wewe
LUKA 23:42-43 mwizi anamwambia ee Yesu unikumbuke katika ufalme wako na YESU anajibu leo hii tutakuwa wote peponi. Toba kwa Yesu haina formula yeye ndie mwamuzi
 
Madalali mapato yamepungua mnaanza vitisho 😂 😂 😂
Ujumbe ni Kwa waliookoka. Ikiwa umesoma na kuamini, Sharti uokoke kwanza ndo utoe sadaka,

Sadaka za mbwa hazipokelewi madhabahuni,

Amen
 
Unachekesha sana
Huo ndo UKWELI.

Elia mtishibi alilishwa na Mungu kupitia kunguru.

TOBA itangulie sadaka, kamwe usitoe au usilete sadaka madhabahuni sadaka chafu, umeiba, umetapeli,hiyo unajidanganya.

Ni LAANA unajitafutia Kutoa sadaka itokanayo na wizi. Nk nk
 
HUMU NDANI KILA MTU NI LECTURER HAKUNA KILAZA NDIO MWANZO WA UPOTOFU KILA MTU NI MJUAJI
 
Haya maneno ya Yesu Kristo:
‭Mathayo ‭11:28‬-29

[28] Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.

[29] Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu;


**Dini imekuwa sehemu sehemu ya kumweka mwanadamu na Mungu.

Inataka control juu ya maisha ya mwanadamu badala ya Mungu kuwa kiongozi wa maisha ya mwanadamu.
 
LUKA 23:42-43 mwizi anamwambia ee Yesu unikumbuke katika ufalme wako na YESU anajibu leo hii tutakuwa wote peponi. Toba kwa Yesu haina formula yeye ndie mwamuzi
Asante mtumishi Kwa majibu murua.

Muuaji alitubu hadharani mchana kweupe,na akasamehewa.

Ubarikiwe.
 
Weka andiko ya haya unayosema tofauti na hapo hizi ni porojo na upotoshaji.
 
Sadaka itokanayo na wizi haipokelewi madhabahuni.

Ukitoa sadaka ya aina hiyo unajidanganya.

Kahaba, ukilipwa malipo ya ukahaba, ukachukua sadaka ukatoa madhabahuni, haipokelewi na Mungu.

Sadaka za aina hizo zimepelekea wengi kufa kabla ya wakati wao.

Kamwe, usitoe sadaka ya mbwa madhabahuni, UTALAANIWA Badala ya kubarikiwa.

Amen
 
hayo mafundisho mnayatoa kwenye mstari gani wa Biblia? ukiona huna mstari jua ni mafundisho ya kuzimu, na mnayafurahia. sikia;
1. mfano wako wa mtu kujichua, anayezini, shoga, mwizi, au dhambi yeyote ile, unapoifanya unakuwa umefungua mlango wa mashetani kuingia kwako, na yanakufanya mfungwa; sawa. kuondoa hati ya ndoa ya kiroho au kifungo chochote hakuhitaji jitihada ya mali zetu/sadaka au chochote, ni kuomba Neema ya Yesu Kristo kwa njia ya kafara la Damu yake afute hati hizo za ndoa, avunje vifungo hivyo vyote, akuweke huru. kwani nini maana ya "njoni kwangu ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha?", mzigo wowote wa dhambi Yesu hakushindwa kulipa garama. unachohitaji ni kumwendea Mungu kwa kusikitika toka moyoni kwamba umetenda dhambi na unahitaji neema yake akusamehe na kukuondoa kwenye vifungo hivyo kwa Yesu Kristo, nawe unasamehewa.

najua shida yako, umepokea mafundisho ya manabii wa uongo ukayameza kama yalivyo, na ni ngumu sana kwako kufunguka, hadi Mungu mwenyewe akufungue. nakuomba leta maandiko uliyonayo ili tukufafanulie, manake hapa unapotosha watu na unamkosea Mungu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…