Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Wewe hujaandika kwenye bandiko lako sadaka ya ukombozi ? Tunapiga kwenye hila kwingine hakuna tabu

Yaani hapo ndio adui kakaa ili kushusha thamani ya kazi ya msalaba

Tunafuta ujinga kwanza wengi wasipotezwe


Kula hiii afu tuendelee na swala la umuhimu wakushirikisha watumishi Wa Mungu hasa kwenye dhambi ainishwa
Au dhambi zinazokuzinga Kwa wepesi.


1 Petro 1:18 Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; mpate kutoka katika mwenendo wenu usiofaa mlioupokea kwa baba zenu;
1 Petro 1:19 bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.
safi sana. hapo kwenye "si kwa fedha au dhahabu" hapo wengi wajue. hakuna pesa hata zingejaa dunia nzima zenye uwezo kusafisha dhambi. shetani huwa analeta kidogokidogo kafundisho, baadaye linakuwa fundisho kuu watu wanahama kwenye kazi ya msalabani nakuishi kwenye cults.

kuna imani moja iliibuka mwaka 2003 hivi kama sikosei, ni ya mtu mmoja aliitwa Munuo, ndugu mmoja alikuwa kanisa la lutheran akahudhuria hiyo mikutano ya mwakasegee weee, akaanzisha kanis alake. yule mtu alikuja kuanzisha kanisa la Siloam, ambalo sasaivi wamebadili jina linaitwa Kanisa la Mungu Baba. wapi ndugu zangu wa karibu nawafahamu wanasali huko, na hata kipindi Munuo yupo hai niliwahi kwenda pale mbezi, nikaona uchafu mtupu nikakimbia mazima.

wale walichofikia kwa sasa, kutokana na hayohayo wanayaita mafunuo (amefunuliwa na Mungu ila kwenye Biblia hakipo), wanasema DAMU YA YESU IMEPUNGUA NGUVU, NA JINA LA YESU LIMEPUNGUA NGUVU, WANASEMA MASHETANI WAMELIZOEA SANA SIKIU HIZI HAYAKIMBII. KWAHIYO WAO HAWAOMBI KABISA KWA JINA LA YESU WALA DAMU YA YESU KWAO SI CHOCHOTE, WANAOMBA KWA JINA LA MUNGU BABA. yupi? wanamjua wenyewe. na Munuo alijiita yeye ni elitha Mungu mkuu. walimgeuza yule Munuo aliyejibadilisha na kujiita Eliya Mungu wa pili, wakamwita Eliya Mtishbi, yule aliyetabiriwa Malaki kwamba takuja (bila kujua huyo eliya ni Yohana Mbatizaji). Munuo alikuja kuugua tetenasi, akafia pale hospitali ya lugalo, hawakuzika siku kadhaa wakiamini atafufuka, wakaona ataoza tu wakaenda kuzika ile njia ya bagamoyo kule. wakati wa maziko kuna picha walipiga ni kama jini lilikuja kama kitu kinapanda wakasema amepaa, amepaaje wakati amezikwa hadi kaburi lake lipo na hajawi kufufuka?

hawa hawana tofauti na wengine wanaitwa the Branhamites, wafuasi wa mtumishi mmoja wa Mungu aliitwa William Branham wa Marekani, alikuwa na nguvu za MUngu mno hadi moto ulishuka waziwazi, ila sasa, ilifika kipindi akapotoka, akaanza kufundisha upotofu kwamba yeye ndiye Eliya, wasaidizi wake wakamwambia wewe usifundishe kwasababu alikuwa hajasoma shule kabisa na Biblia alikuwa haijui ili anajua tu kuweka mikono na kuponya magonjwa. akagoma. MUngu alimfunulia mtumishi wake mmoja aliitwa KENETH HAGIN kwamba Mungu amepanga kumwondoa aokoe roho yake kwasababu ameanza kufundisha mapotofu, akapata ajali akafa. cha kushukuru Mungu aliamua kumuondoa ili aponye roho yake. wafuasi wake pia hawakuzika wa siku nyingi wakidhani angefufuka, wakaishia kuwa na dhehebu la jina lake hadi leo.

Arusha kuna kanis akubwa kabisa la hawa watu wanaitwa the Branhamites, wanaweka hadi picha zake kwenye magari, Dodoma pia yupo jamaa anajitangaza kwenye mitandao, ni dhehebu kabisa la upotofu.

hivyo shetani huwa analeta kafundisho kamoja tu, halafu anatengeneza cult fulani itakayopotosha watu wengi ili aingie nao motoni. mafundisho mengi ya mwalimu kama ya mzaliwa wa kwanza, ukombozi kwa sadaka n.k, ni ya upotofu, hadi kina Benny HInn wamekuja kutubu hivi karibuni kwenye issue za kupanda mbegu, wamekiri walikuwa wanashurutishwa na walienda visivyo, kwasababu karama za Mungu hazinunuliki, hatuna uwezo huo kununua karama za Mungu au hata msamaha. Mungu asaidie kanisa lake linapotoshwa na hawa watu.
 
Kwa upande wa muibiwa ndio sijakuelewa, hapo mtumishi anamalizaje, Kwa hapo ndio hujafafanua.
Mungu anaweza yote.

Maombi yanaweza kubadili Kila kitu, Mungu akiingilia kati, Mtumishi ataenda na kumweleza mwibiwa mke na ataelewa, utaenda na kuomba msamaha Ukiwa na mtumishi, utalipa fine iliyosawa na Mahari alotoa muoaji au itakayoridhiwa na muibiwaji, unaweza pia usitoe hata mia kulingana na moyo wa muibiwaji ulivyona na mtasameheana.

Na jambo Hilo itamalizwa, na mtaapizana wote wahusika libaki Siri Ili kuondoa vidole vya maadui.

Mungu atasamehe na kuondoa hatia hiyo moyoni.

Ndo ujue dhambi zote ni sawa mbele za Mungu,ila zipo dhambi ni mtihani,

Tuziepuke kabisa.

Amen
 
Kwa maelezo uliyoweka hapa nimejua shida ni ufahamu wako na anayeweza kukusaidia ni Roho mtakatifu pekee

Ni swala la Muda nadhani mi sina neno maana nimeshajua tabu ipo wapi?
Roho mtakatifu ndio mwalimu wangu, sauti yake ndiyo nitakayoitii.

Ubarikiwe.
 
Nimekwambia sitakujibu, usilazimishe.
wewe usiponijibu mimi nitaendelea kukupiga misumari kwasababu mapotofu unayosambaza yanaharibu kanisa la Mungu. unatumiwa na shetani wewe. na pia huna uwezo kunijibu kwasababu huna mstari wowote wa kusimamia, ni fikra tu za kichwani shetani amewawekeeni. utalaizmishwa kuelewa hata kama huelewi.
 
Mungu anaweza yote.

Maombi yanaweza kubadili Kila kitu, Mungu akiingilia kati, Mtumishi ataenda na kumweleza mwibiwa mke na ataelewa, utaenda na kuomba msamaha Ukiwa na mtumishi, utalipa fine iliyosawa na Mahari alotoa muoaji au itakayoridhiwa na muibiwaji, unaweza pia usitoe hata mia kulingana na moyo wa muibiwaji ulivyona na myasameheana.

Na jambo Hilo itamalizwa, na mtaapiza wote wahusika libaki Siri Ili kuondoa vidole vya maadui.

Mungu atasamehe na kuondoa hatua hiyo moyoni.

Ndo ujue dhambi zote ni sawa mbele za Mungu,ila zipo dhambi ni mtihani,

Tuziepuke kabisa.

Amen

Bado hujanijibu swali langu, je mtu akiwa nchi ya mbali au mlikutana kwa emergency na hamjuani ndio habari ikaishia hapo na hakuna mawasiliano, na hujui ana mume au hana! Hoja yangu ndio iko hapo na hujajibu.
 
safi sana. hapo kwenye "si kwa fedha au dhahabu" hapo wengi wajue. hakuna pesa hata zingejaa dunia nzima zenye uwezo kusafisha dhambi. shetani huwa analeta kidogokidogo kafundisho, baadaye linakuwa fundisho kuu watu wanahama kwenye kazi ya msalabani nakuishi kwenye cults.

kuna imani moja iliibuka mwaka 2003 hivi kama sikosei, ni ya mtu mmoja aliitwa Munuo, ndugu mmoja alikuwa kanisa la lutheran akahudhuria hiyo mikutano ya mwakasegee weee, akaanzisha kanis alake. yule mtu alikuja kuanzisha kanisa la Siloam, ambalo sasaivi wamebadili jina linaitwa Kanisa la Mungu Baba. wapi ndugu zangu wa karibu nawafahamu wanasali huko, na hata kipindi Munuo yupo hai niliwahi kwenda pale mbezi, nikaona uchafu mtupu nikakimbia mazima.

wale walichofikia kwa sasa, kutokana na hayohayo wanayaita mafunuo (amefunuliwa na Mungu ila kwenye Biblia hakipo), wanasema DAMU YA YESU IMEPUNGUA NGUVU, NA JINA LA YESU LIMEPUNGUA NGUVU, WANASEMA MASHETANI WAMELIZOEA SANA SIKIU HIZI HAYAKIMBII. KWAHIYO WAO HAWAOMBI KABISA KWA JINA LA YESU WALA DAMU YA YESU KWAO SI CHOCHOTE, WANAOMBA KWA JINA LA MUNGU BABA. yupi? wanamjua wenyewe. na Munuo alijiita yeye ni elitha Mungu mkuu. walimgeuza yule Munuo aliyejibadilisha na kujiita Eliya Mungu wa pili, wakamwita Eliya Mtishbi, yule aliyetabiriwa Malaki kwamba takuja (bila kujua huyo eliya ni Yohana Mbatizaji). Munuo alikuja kuugua tetenasi, akafia pale hospitali ya lugalo, hawakuzika siku kadhaa wakiamini atafufuka, wakaona ataoza tu wakaenda kuzika ile njia ya bagamoyo kule. wakati wa maziko kuna picha walipiga ni kama jini lilikuja kama kitu kinapanda wakasema amepaa, amepaaje wakati amezikwa hadi kaburi lake lipo na hajawi kufufuka?

hawa hawana tofauti na wengine wanaitwa the Branhamites, wafuasi wa mtumishi mmoja wa Mungu aliitwa William Branham wa Marekani, alikuwa na nguvu za MUngu mno hadi moto ulishuka waziwazi, ila sasa, ilifika kipindi akapotoka, akaanza kufundisha upotofu kwamba yeye ndiye Eliya, wasaidizi wake wakamwambia wewe usifundishe kwasababu alikuwa hajasoma shule kabisa na Biblia alikuwa haijui ili anajua tu kuweka mikono na kuponya magonjwa. akagoma. MUngu alimfunulia mtumishi wake mmoja aliitwa KENETH HAGIN kwamba Mungu amepanga kumwondoa aokoe roho yake kwasababu ameanza kufundisha mapotofu, akapata ajali akafa. cha kushukuru Mungu aliamua kumuondoa ili aponye roho yake. wafuasi wake pia hawakuzika wa siku nyingi wakidhani angefufuka, wakaishia kuwa na dhehebu la jina lake hadi leo.

Arusha kuna kanis akubwa kabisa la hawa watu wanaitwa the Branhamites, wanaweka hadi picha zake kwenye magari, Dodoma pia yupo jamaa anajitangaza kwenye mitandao, ni dhehebu kabisa la upotofu.

hivyo shetani huwa analeta kafundisho kamoja tu, halafu anatengeneza cult fulani itakayopotosha watu wengi ili aingie nao motoni. mafundisho mengi ya mwalimu kama ya mzaliwa wa kwanza, ukombozi kwa sadaka n.k, ni ya upotofu, hadi kina Benny HInn wamekuja kutubu hivi karibuni kwenye issue za kupanda mbegu, wamekiri walikuwa wanashurutishwa na walienda visivyo, kwasababu karama za Mungu hazinunuliki, hatuna uwezo huo kununua karama za Mungu au hata msamaha. Mungu asaidie kanisa lake linapotoshwa na hawa watu.
Jikite kwenye mada.

Mada inaongelea dhambi ambazo huwezi tubu pekeako sirini Hadi USHIRIKISHE WATUMISHI.
 
hiyo ni kwa mujibu wa biblia ipi au ni experience yako binafsi
ni mafundisho ya kichwani tu ya kiongozi wake wa dini. tangu ameleta hili fundisho tumemwambia alete mstari walau mmoja anatapatapa tu. hana hata mmoja. ila anasema ni agizo kuu la Mungu. shindwa shetani kwa JIna la Yesu.
 
Roho mtakatifu ndio mwalimu wangu, sauti yake ndiyo nitakayoitii.

Ubarikiwe.
Haya Ila akusaidie kutofautisha kati ya agano la kale na agano jipya

Ujue alichokuja kufanya Kristo na kile kilichokuwa kinafanyika kabla ya Kristo msalabani inaweza ikakusadia kiasi
 
Bado hujanijibu swali langu, je mtu akiwa nchi ya mbali au mlikutana kwa emergency na hamjuani ndio habari ikaishia hapo na hakuna mawasiliano, na hujui ana mume au hana! Hoja yangu ndio iko hapo na hujajibu.
Ikiwa Yu mbali na ndo Kweli ya Mungu, unamshirikisha mtumishi pekee na utamalizana na Mungu na kusamehewa. Shahidi Yako ni mtumishi.

Nimemjibu au Bado hujaridhika?
 
Naona umekuja kwenye hoja yangu sasa na hilo ndio nataka ujibu wana Jf hapa, je mtu akiwa nchi ya mbali au mlikutana kwa emergency, wanasema one night stand na hamjuani ndio habari ikaishia hapo na hakuna mawasiliano, na humjui mke au mume wake! Hoja yangu ndio iko hapo na hujajibu, kwamba Mungu hawezi kumsamehe mtu huyo?
 
Sadaka mnazoletewa na wajinga wajinga humo ktk machumio yenu hayawatoshi naona mmevamia sana mitandao ni vitisho vya kipuuzi ili kujaribu kuongeza maokoto.
Hao matapeli na vikanisa vyao dhambi kama hizo wao wanaenda kuzitubu wapi?
Wewe unaeniondolea dhambi ni nani?
Uwezo wa kuondoa dhambi nani amekupa?
Utanipa risitibtoka kwa Mungu inayoonyesha kwamba nimesamehewa dhambi hizo?
Utajuaje kuwa Mungu ameniondolea dhambi?
Nitaamini vipi kuwa sasa nimeondolewa dhambi?
Acha utapeli.
 
Haya Ila akusaidie kutofautisha kati ya agano la kale na agano jipya

Ujue alichokuja kufanya Kristo na kile kilichokuwa kinafanyika kabla ya Kristo msalabani inaweza ikakusadia kiasi
Ndo nasema, Yesu Kristo HAKIKA kuondoa torati Bali kuitimiza.

Ndo nilasema, AGANO jipya, ZAKA Yesu ameagiza Kutoa 10/10 Si 1/10 pekee kama AGANO la kale.

All in all, Roho mtakatifu ndiye kiongozi, sauti yake ndiyo tuipasayo kutii.

Amen
 
Sadaka mnazoletewa na wajinga wajinga humo ktk machumio yenu hayawatoshi naona mmevamia sana mitandao ni vitisho vya kipuuzi ili kujaribu kuongeza maokoto.
Hao matapeli na vikanisa vyao dhambi kama hizo wao wanaenda kuzitubu wapi?
Wewe unaeniondolea dhambi ni nani?
Uwezo wa kuondoa dhambi nani amekupa?
Utanipa risitibtoka kwa Mungu inayoonyesha kwamba nimesamehewa dhambi hizo?
Utajuaje kuwa Mungu ameniondolea dhambi?
Nitaamini vipi kuwa sasa nimeondolewa dhambi?
Acha utapeli.
Acha kupotosha,

Sadaka ni Kwa ajili ya shukrani.

Damu ya Yesu inatosha kusafisha dhambi zote.

Jikite kwenye mada tafadhali.
 
Ndo nasema, Yesu Kristo HAKIKA kuondoa torati Bali kuitimiza.

Ndo nilasema, AGANO jipya, ZAKA Yesu ameagiza Kutoa 10/10 Si 1/10 pekee kama AGANO la kale.

All in all, Roho mtakatifu ndiye kiongozi, sauti yake ndiyo tuipasayo kutii.

Amen
Roho Mtakatifu ni Mungu yuleyule aliyeandika Biblia, atakachokuambia hakitakiwi kwenda kinyume na Biblia, Mungu hawezi kujipinga, na hata akitoa lolote, lazima liendane na Neno la Mungu. sasa uletayo wewe hata misingi tu ya Neno la Mungu haviendani, ndio maana tunasema umepotoshwa na wewe unazidi kueneza mapotofu. ingekusaidia sana kama ungekubali kufundishwa ili usiendelee kukaa kwenye upotofu na kupoteza wengine. msidharau kazi ya Msalaba, hakuna dawa nyingine ya makosa yetu ila Damu ya Yesu. na imethibitika kuwa hivyo kwa Neno la Mungu na kwa maisha ya halisi kabisa.
 
Acha kupotosha,

Sadaka ni Kwa ajili ya shukrani.

Damu ya Yesu inatosha kusafisha dhambi zote.

Jikite kwenye mada tafadhali.
mada yako ni hii:

DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.


bado una msimamo huu au umebadilika? kwanini unasema watu wachukue sadaka wakamwona mtumishi awaombee? kwanini unataka watu waambatanishe sadaka ya ukombozi? Shindwa kwa Jina la Yesu.
 
Ikiwa Yu mbali na ndo Kweli ya Mungu, unamshirikisha mtumishi pekee na utamalizana na Mungu na kusamehewa. Shahidi Yako ni mtumishi.

Nimemjibu au Bado hujaridhika?

Bado sijakuelewa, lakini nashkuru kwa ufafanuzi wako.
 
Ikiwa Yu mbali na ndo Kweli ya Mungu, unamshirikisha mtumishi pekee na utamalizana na Mungu na kusamehewa. Shahidi Yako ni mtumishi.

Nimemjibu au Bado hujaridhika?
mtumishi sio njia yako kwa Mungu, Yesu Kristo/Jina la Yesu ndio connection. mtumishi hata yeye ana dhambi zake nyingi tu, yeye uliwahi kumwona hata siku moja kasimamishwa pale mbele anatubishwa na kutoa sadaka? au yeye sio mwanadamu? unafikiri wachungaji hawazini, hawafanyi maovu? hawalogi?wengi tu huwa wanasimama na Mungu ila kuna wakati wanajichanganya shetani anawakamata wanarudi nyuma na kufanya maovu, shukrani kwa Mungu ana upendo kile alichoweka ndani yao huwa anakitunza, Mungu huwatafuta na kuwarudisha kimyakimya. acha kutegemea wanadamu kama ndio daraja kwa Mungu. acha kabisa.
 
Bado sijakuelewa, lakini nashkuru kwa ufafanuzi wako.
Muhimu ni kuwa, dhambi tajwa hapo huu, usitubu kimya kimya, HATIA ya dhambi hiyo haitaodoka.

Shirikisha mtumishi wa Mungu.

Hizi ni siku za mwisho, wengi sana wako kuzimu na wanaenda kuzimu na walikuwa wameokoka, hawakujua kuwa dhambi hizo tajwa Si za kutubu sirini.

Roho MTAKATIFU analeta maonyo haya Ili WATAKATIFU wajue, wasije tupwa Kuzimu.

Amen.
 
mtumishi sio njia yako kwa Mungu, Yesu Kristo/Jina la Yesu ndio connection. mtumishi hata yeye ana dhambi zake nyingi tu, yeye uliwahi kumwona hata siku moja kasimamishwa pale mbele anatubishwa na kutoa sadaka? au yeye sio mwanadamu? unafikiri wachungaji hawazini, hawafanyi maovu? hawalogi?wengi tu huwa wanasimama na Mungu ila kuna wakati wanajichanganya shetani anawakamata wanarudi nyuma na kufanya maovu, shukrani kwa Mungu ana upendo kile alichoweka ndani yao huwa anakitunza, Mungu huwatafuta na kuwarudisha kimyakimya. acha kutegemea wanadamu kama ndio daraja kwa Mungu. acha kabisa.
No comment.
 
Back
Top Bottom