- Thread starter
- #341
KAZI yetu kuhubiri,Haya ni mambo ya imani no one can prove this.
Ndiyo maana hata mjadala wake hauwezi kuwa na mwisho.
Kuamini na kuacha DHAMBI ni uamuzi binafsi.
Amen, ubarikiwe!!
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
KAZI yetu kuhubiri,Haya ni mambo ya imani no one can prove this.
Ndiyo maana hata mjadala wake hauwezi kuwa na mwisho.
Yesu ni Mungu.Kwani Yesu SI mtumishi wa Mungu?
Petro na Musa, walifanya moja ya dhambi hapo juu?Baada ya kumsaliti Yesu, petro alienda kutubu kwa mchungaji au kuhani yupi?
Baada ya kukaid maagizo ya Mungu nabii Musa pale mlimani alienda kutubu kwa nani?
Kuwapa masikini na vilema ni sawaHujui SHERIA ya kiroho inavyofanya KAZI.
Usilolijua ni kuwa, kipato upewacho Huwa ni njia ya kufikia wengine,
Ndani ya kipato chako Kuna pesa Kwa ajili Yako, pesa ingine imepitishwa kwako Kwa ajili ya wahitaji,
Kwenye kipato hicho hicho Kuna mbegu nk nk,
Atoaye ndiye apokeaye katika Roho, na apokeaye KIMWILI ndiye Atoaye katika Roho.
Hujui matajiri ambao huwaita maskini na kuwapa sadaka Huwa wanachukua baraka za maskini hao na kujiongezea utajiri.?
Imeandikwa heri Kutoa kuliko kupokea.
Soma thread: DAWA ya Umaskini, madeni, ukata, mifuko kutoboka, uhitaji, kufilisika hii hapa - Rabbon
Itakusaidia Amen
Sasa sadaka ya nini?sasa huo mstari umeuleta wa nini hapo we nabii wa uongo?
Dhambi tajwa hapo juu, maelekezo ni kumshirikisha Mtumishi wa Mungu wa Kweli.Kuwapa masikini na vilema ni sawa
NdiyoKwahiyo kesho tena unarud..na kesho kutwa unarud na siku nyingine hivyo hivyo??
mitume wepi, na umeitoa wapi hiyo kwenye Biblia? mbona mnatumiwa na shetani aisee?
Tupe reference ya maandikoSalaam shalom.
INTRODUCTON.
Imeandikwa, Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.( 1 Yoh 1:9).
Dhambi ni kutotii, kwenda kinyume na maelekezo ya Mungu. Na Roho mtakatifu yupo kutukumbusha dhambi zetu Ili tuzitibie Ili tuendelee kuwa WATAKATIFU.
DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:
1. ZINAA NA UASHERATI.
UASHERATI ni kufanya Tendo la zinaa na mtu nje ya NDOA asiye mkeo au mumeo.
UZINZI ni kufanya tendo la uchafu, zinaa kabla ya Kuoa au Kuolewa.
Ukizini na mke wa mtu au mume wa Mtu, usijidanganye kuwa ukitubu sirini utasamehewa, HATIA itaendelea kuwepo Hadi uwatafute watumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. Watumishi Wana BUSARA ya kusuluhisha dhambi hiyo pande zote mbili Ili ufunguliwe.
2. USHOGA.
Ikiwa uliwahi kuwa shoga, ukaamua kuacha, kamwe usitubu sirini na kuishiwa hapo, USHOGA huambatana na mapepo na kufungwa NAFSI, mfungwa kamwe hawezi jifunguanpingu mwenyewe, unawahutaji watumishi wa Kweli Ili UOMBEWE na kuwekwa huru, sadaka ni LAZIMA Ili itolewe huko.
3. USAGAJI.
Mwanamke pia aliyewa kufanya dhambi hiyo, huwezi kufunguliwa na Utumwa na HATIA hiyo pekeako Kwa kutubu sirini, nenda Kwa watumishi wa Kweli, Ukiwa na sadaka ya Ukombozi.
4. PUNYETO/ KUJICHUA.
Ikiwa uliwahi kujichua, ukaamua kuacha, unahitaji kwenda Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi Ili ufunguliwe, Mpiga PUNYETO ni mfungwa, ni mke au mume wa Roho chafu katika Ulimwengu wa Roho, hivyo kufunguliwa ni LAZIMA utoe sadaka, uvunje NDOA chafu hiyo ya kiroho na hati ya NDOA chafu ya kiroho iondolewe, usipofanya hivyo, unajidanganya. Mbinguni huingii ng'o!!
Neno Hilo hapo juu ni ROHO. Amen.
5.MWANAMKE KUOA MWANAMKE/MWANAUME KUOA MWANAUME MWENZIE.
Kutubu dhambi hii sirini bila watumishi wa Mungu ni kujidanganya. Chukua sadaka, nenda Kwa mtumishi, Sema Kweli Ili UOMBEWE na kufunguliwa, NDOA haramu ivunjwe na ufungwa wako kiroho uondolewe. Amen.
6. ORAL SEX.
Ikiwa uliwahi kushiriki oral sex, kunyonya au kuramba Kwa mdomo sehemu za Siri za mwanamke au Mwanaume na ukatambua ni DHAMBI, ukaacha, Bado u kifungoni.
Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli wa Mungu ufunguliwe na Mungu.
7. ABORTION./ UTOAJI MIMBA/ KUFUNGA UZAZI/ KUTUMIA VIDONGE VYA KUPANGA UZAZI.
Kimbia haraka Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli ,beba sadaka kulingana na uwezo wako, UOMBEWE ufunguliwe.
Ukipuuza Utakataliwa GETI la Mbinguni.
9. IKIWA ULIWAHI TUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME/ KIKE.
Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.
10. MAUAJI.
Ikiwa uliwahi kuua bila kukusudia ,ukahukumiwa JELA ukatoka, ikiwa uliua Kwa Siri na hukubainika, ikiwa ulishiriki kuua, usijidanganye kuwa unaweza kutubu sirini, HATIA Ili ikuondoke uwe na Amani, Tafuta kiongozi wa Mungu wa Kweli mwenye BUSARA za Mungu, akuongoze Cha kufanya, utoe pia sadaka ya Ukombozi.
11. IBADA ZA SANAMU, KUSHIRIKI IBADA ZA WAFU NA KUTOA SADAKA KWA MIZIMU KIMILA NK NK.
Kushiriki Ibada za KIMILA na Kutoa sadaka Kwa Roho za kishetani za Mababu, ni DHAMBI pia, ni kufungwa ni Utumwa ambao huwezi kujifungua pekeako.
Ukiamua kuacha na kuokoka, hatua inayofuata ni kushirikisha watumishi kukusaidia kukutenga na madhabahu hizo.
Sadaka ni LAZIMA, sababu, Ulimwengu wa Nuru na Giza sadaka ni inevitable. Amen
HITIMISHO.
Dhambi nilizotaja hapo juu, ni baadhi tu ya dhambi ambazo huwezi tubu pekeako, zimetajwa sawasawa na Ruhusa ya Roho mtakatifu Kwa mtumishi wake sawasawa na ufunuo wake apendavyo.
NB: Si DHAMBI zote zinahitaji kuona mtumishi wa Kweli kukusaidia kufunguliwa pingu za dhambi, ni baadhi ya dhambi ambazo Zina vifungo na attachment na maagano ya kipepo na kishetani.
Mungu awabariki. Source: Nabii Justine Ibrahim, U-Tube., Promover Tv channel U-Tube.
Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wako, fuatisha Sala hii,
EE YESU, NINAKIRI KWAKO KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU,ULIANDIKE KATIKA KITABU CHA UZIMA, NINAOMBA UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, NIWEZESHE NIISHI MAISHA MATAKATIFU.
Ameen
Dhambi tajwa hapo juu, maelekezo ni kumshirikisha Mtumishi wa Mungu wa Kweli.labda huko kwa ISAKA ila kwa Ishmael tunaambiwa TUTUBU NA TUACHE BASI.inakuwa umesamehewa.
Mwenyezi mungu anasema yeye ni MSAMEHEVU ANA SAMEHE MADHAMBI MAKUBWA NA MADOGO.
na anawapenda wanaomba msamaha na kuacha
Sent from my SM-A042F using JamiiForums mobile app
Nimemjibu mtu humu ready, pitia comments.Tupe
Tupe reference ya maandiko
Mada inaongelea baadhi ya dhambi ambazo ni LAZIMA kushirisha mtumishi.Yesu alipokufa pale msalabani pazia la hekaru lilipasuka maana yake ametoa mpaka kati ya Mungu na mwanadamu hivyo tukiwa na shida ikiwemo kutubu sio lazima kwenda kwa mchungaji sisi wenyewe anatusikia
Labda kuvunja maagano ya giza muda mwingine mtu peke yako huwezi! Inakubidi umuombe mchungaji msaada!
Ya UZINZI Kwa Mfano, ni Siri wewe na Mungu wako?Dhambi ni Siri baina yako wewe na Mungu wako.
Barikiwa.Chochote unachofanya kuuharibu mwili ni dhambi.
Tumepewa kazi ya kuvuta oxygen sio bangi na sigara.
Hii principles inafungu moja lenye kukusanya vitu vyote vya aina hii.
Dhambi Haina usawa, hupaswi kumtangazia binadamu matendo yako maovu. Ukitaka kutubu piga goti ulie mbele ya Mungu lakini sio kupitia kwa binadamu mwenzako.Ya UZINZI Kwa Mfano, ni Siri wewe na Mungu wako?
Lete ushahidi/uthibitishi japo mdogo tu wa kimaandiko. Vinginevyo, haya yatahesabika kuwa ni mawazo binafsi tu ya mtu ambayo watu watakuwa na uhiyari wa kuyatii au kutotii.
Aaiseee wewe ni muongo wa wazi kabisa mambo ya walawi inasema mtu shahawa zikitoka unakuwa najisi kwa siku nzima sharti ni uoge (ujitakase) na hiyo hatia inaondokaSadaka niliyoiongelea Si sadaka ya kufanyika mbadala Ili usamehewe dhambi, HAPANA.
Mtu anayejichua Kwa Mfano, awe kwenye NDOA au nje ya NDOA,
Ukijichua, katika Ulimwengu wa Roho umefunga NDOA kabisa katika Ulimwengu wa Roho.
Na ndoa hiyo, lazima Mahari imetolewa na mapepo, hivyo ajichuaye, ni mfungwa kamili.
Kuondoa hati ya NDOA ya NDOA ya kiroho, kuondoa sadaka hiyo na Mahari hiyo, lazima ukomboe na sadaka na Damu ya Yesu.
Unahitaji kufundishwa na Roho mtakatifu.
Pia maandiko yapo, nikikuletea maandiko utaamini?