Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Umwombe radhi muibiwa Tena… you can’t be serious 🧐
Ndo maana ya kumwambia zipo dhambi huwezi tubu pekeako,

Soma (Mathayo 5:25), yasema patana na mshitaki wako muwapo njiani kabla hajakupeleka Kwa kadhi, kadhi akakupeleka Kwa liwali, ukatupwa GEREZANI.

Dhambi ya UZINZI ni Moja wapo inayomfanya aliyeitenda kuwa gerezani.

Maana ya kuwa gerezani ni ugumu uliouongelea wa mazingira ya kumalizana na kupata msamaha Kwa uliyemuibia Mume, Mungu anataka umwombe radhi akusamehe ndipo Mungu akusamehe.

Ukitubu pekeako unajidanganya, ndomana ninashauri TUMIA mtumishi wa Mungu asaidie kukupatanisha upate msamaha wake.

Tofauti na hapo, ukitubu bila kufanya hivyo, dhambi hiyo haikuondoki, na ukifa ni Kuzimu direct.

Amen
 
Salaam shalom.

INTRODUCTON.

Imeandikwa, Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.( 1 Yoh 1:9).

Dhambi ni kutotii, kwenda kinyume na maelekezo ya Mungu. Na Roho mtakatifu yupo kutukumbusha dhambi zetu Ili tuzitibie Ili tuendelee kuwa WATAKATIFU.

DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:


1. ZINAA NA UASHERATI.

UASHERATI ni kufanya Tendo la zinaa na mtu nje ya NDOA asiye mkeo au mumeo.

UZINZI ni kufanya tendo la uchafu, zinaa kabla ya Kuoa au Kuolewa.

Ukizini na mke wa mtu au mume wa Mtu, usijidanganye kuwa ukitubu sirini utasamehewa, HATIA itaendelea kuwepo Hadi uwatafute watumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. Watumishi Wana BUSARA ya kusuluhisha dhambi hiyo pande zote mbili Ili ufunguliwe.

Kuzini na mke wa mtu, faini ya juu ni kulipa Mahari aliyotoa muoaji Ili akusamehe, kushirikisha mtumishi ni kutumia BUSARA ya Mungu Ili muibiwa mke aridhie kukusamehe kutomlipa, au akupunguzie faini.

(Mithali 6:20-35,) UZINZI hufunga NAFSI, Amri ya Mungu usizini (Kumbukumbu la torati 5:1-21)

2. USHOGA.

Ikiwa uliwahi kuwa shoga, ukaamua kuacha, kamwe usitubu sirini na kuishiwa hapo, USHOGA huambatana na mapepo na kufungwa NAFSI, mfungwa kamwe hawezi jifunguanpingu mwenyewe, unawahutaji watumishi wa Kweli Ili UOMBEWE na kuwekwa huru, sadaka ni LAZIMA Ili itolewe huko. ( Mwanzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke makusudi Ili asizae na mke aliyepewa.

3. USAGAJI.

Mwanamke pia aliyewa kufanya dhambi hiyo, huwezi kufunguliwa na Utumwa na HATIA hiyo pekeako Kwa kutubu sirini, nenda Kwa watumishi wa Kweli, Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. mwanzo 38:9-10, Onani aliuwawa Kwa dhambi hiyo, ( kumbukumbu la torati 5:1-21) Amri za Mungu Usiue.

4. PUNYETO/ KUJICHUA.

Ikiwa uliwahi kujichua, ukaamua kuacha, unahitaji kwenda Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi Ili ufunguliwe, Mpiga PUNYETO ni mfungwa, ni mke au mume wa Roho chafu katika Ulimwengu wa Roho, hivyo kufunguliwa ni LAZIMA utoe sadaka, uvunje NDOA chafu hiyo ya kiroho na hati ya NDOA chafu ya kiroho iondolewe, usipofanya hivyo, unajidanganya. Mbinguni huingii ng'o!! (Mwanzo 38:1-25) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke Ili asizae na mke wa marehemu kaka yake.
Neno Hilo hapo juu ni ROHO. Amen.

5.MWANAMKE KUOA MWANAMKE/MWANAUME KUOA MWANAUME MWENZIE.

Kutubu dhambi hii sirini bila watumishi wa Mungu ni kujidanganya. Chukua sadaka, nenda Kwa mtumishi, Sema Kweli Ili UOMBEWE na kufunguliwa, NDOA haramu ivunjwe na ufungwa wako kiroho uondolewe. ( Mwanzo 38:9-10, (Mithali 6:20-35)Amen.

6. ORAL SEX.

Ikiwa uliwahi kushiriki oral sex, kunyonya au kuramba Kwa mdomo sehemu za Siri za mwanamke au Mwanaume na ukatambua ni DHAMBI, ukaacha, Bado u kifungoni.

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli wa Mungu ufunguliwe na Mungu.

(1 Wakorintho 6:9-11), (Ufunuo wa Yohana 21:8) (Mzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda Tendo la NDOA kinyume.

7. ABORTION./ UTOAJI MIMBA/ KUFUNGA UZAZI/ KUTUMIA VIDONGE VYA KUPANGA UZAZI.

Kimbia haraka Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli ,beba sadaka kulingana na uwezo wako, UOMBEWE ufunguliwe.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Usiue ni Amri ya Mungu.

Ukipuuza Utakataliwa GETI la Mbinguni.

9. IKIWA ULIWAHI TUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME/ KIKE.

(Mwanzo 38-9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda kinyume na Utaratibu wa Tendo la NDOA na taratibu za UZAZI alizoweka Mungu.


Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.

10. MAUAJI.

Ikiwa uliwahi kuua bila kukusudia ,ukahukumiwa JELA ukatoka, ikiwa uliua Kwa Siri na hukubainika, ikiwa ulishiriki kuua, usijidanganye kuwa unaweza kutubu sirini, HATIA Ili ikuondoke uwe na Amani, Tafuta kiongozi wa Mungu wa Kweli mwenye BUSARA za Mungu, akuongoze Cha kufanya, utoe pia sadaka ya Ukombozi. ( Acts 9:3-6) Sauli alikuwa mwuaji, Yesu alimwelekeza aende Kwa mtumishi.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Mungu ameamrisha " Usiue".

11. IBADA ZA SANAMU, KUSHIRIKI IBADA ZA WAFU NA KUTOA SADAKA KWA MIZIMU KIMILA NK NK.

Kushiriki Ibada za KIMILA na Kutoa sadaka Kwa Roho za kishetani za Mababu, ni DHAMBI pia, ni kufungwa ni Utumwa ambao huwezi kujifungua pekeako.

(Mithali 6:20-35) kifungo Cha NAFSI sababu Ibada ya sanamu ni UZINZI kiroho mbele za Mungu, ( UFUNUO 21:8, (1 korinthians 6:9-11) watendao uchawi na Ibada ya sanamu watatupwa Jehanum.

Ukiamua kuacha na kuokoka, hatua inayofuata ni kushirikisha watumishi kukusaidia kukutenga na madhabahu hizo.

Sadaka ni LAZIMA, sababu, Ulimwengu wa Nuru na Giza sadaka ni inevitable. Amen

HITIMISHO.

Dhambi nilizotaja hapo juu, ni baadhi tu ya dhambi ambazo huwezi tubu pekeako, zimetajwa sawasawa na Ruhusa ya Roho mtakatifu Kwa mtumishi wake sawasawa na ufunuo wake apendavyo.

NB: Si DHAMBI zote zinahitaji kuona mtumishi wa Kweli kukusaidia kufunguliwa pingu za dhambi, ni baadhi ya dhambi ambazo Zina vifungo na attachment na maagano ya kipepo na kishetani.

ANGALIZO: Sadaka tutoazo Si Kwa ajili ya kununua Muujiza, au kununua Msamaha wa Mungu, Yesu msalabani alikwisha maliza yote Kwa Damu yake msalabani. Sadaka tunatoa kama shukrani tu na kuonyesha Upendo Kwa Yale Mungu alikwisha tutendea.

Mungu awabariki.

Source: Nabii Justine Ibrahim, U-Tube., Promover Tv channel U-Tube.

Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wako, fuatisha Sala hii,

EE YESU, NINAKIRI KWAKO KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU,ULIANDIKE KATIKA KITABU CHA UZIMA, NINAOMBA UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, NIWEZESHE NIISHI MAISHA MATAKATIFU.

Ameen
Kumbe tangazo la biashara ya Nabii feki Justine...
 
nimekufatilia tangu mwanzo wa uzi wako nilitegemea nitaona umetoa fungu la biblia linalokusapot twende kuombewa kwa mtumishi, lakini naona porojo za kupiga sadaka tu
Rudi kusoma,

KATIKA Kila category nimeambatisha na vifungu vya maandiko ya BIBLIA.
 
Kah maokoto yamezingatiwa sana aisee eti Mungu alimtoa mwanae
 
Ikiwa Mungu alimtoa mwanawe wa pekee Yesu kristo awe sadaka ya kutukomboa,

Nani wewe usitoe sadaka. Sadaka ni Kwa ajili Yako, usidhani unamfaidisha Mchungaji.

Elia alilishwa na Mungu kupitia kunguru, usidhani watumishi wa Mungu wanategenea sadaka zako.

Na usijidanganye ukaenda Kutoa sadaka ya wizi, au ya kutapeli madhabahuni, utaondoka na LAANA.

Ubarikiwe.
Tukirudi kwenye uhalisia wa kutubu na kusamehewa, uhalali wa kwamba lazima ukatubu pamoja na mtumishi unatoka wapi?.

Maana kufa kwa Yesu msalabani kulipunguza formalities nyingi sana, kipindi cha Torati watu waliishi kwa sheria, bali sisi tunaishi kwa neema.

Yesu alisema hakuja kuivunja torati bali kuitimiliza. Tafsiri yake kuna mambo yaliwekwa sawa baada ya yeye kuja duniani kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu.

Mwisho kabisa, yule mwanamke aliyezini na wakataka kumpiga mawe na akaletwa mbele ya Yesu, embu tuambie, alipelekwa kwa kuhani gani ambaye alimuombea ili dhambi zake zisamehewe?
 
Tukirudi kwenye uhalisia wa kutubu na kusamehewa, uhalali wa kwamba lazima ukatubu pamoja na mtumishi unatoka wapi?.

Maana kufa kwa Yesu msalabani kulipunguza formalities nyingi sana, kipindi cha Torati watu waliishi kwa sheria, bali sisi tunaishi kwa neema.

Yesu alisema hakuja kuivunja torati bali kuitimiliza. Tafsiri yake kuna mambo yaliwekwa sawa baada ya yeye kuja duniani kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu.

Mwisho kabisa, yule mwanamke aliyezini na wakataka kumpiga mawe na akaletwa mbele ya Yesu, embu tuambie, alipelekwa kwa kuhani gani ambaye alimuombea ili dhambi zake zisamehewe?
Mwanamke aliyezini aliletwa Kwa Yesu Ili Yesu atoe HUKUMU.

Mahakama Ile ikifanyika wazi mchana kweupe, Yesu akamsamehe na kumwambia usifanye dhambi tena.

Paulo alipotokewa na YESU na kupigwa upofu, aliambiwa nenda mjini utamkuta mtumishi atakuombea,

Wakati Paulo anaambiwa hayo, tayari lilikuwa kipindi Cha neema.

Mchawi Kwa Mfano, Unadhani anaweza kutubu mwenyewe chumbani anaweza kuvunja mikataba ya kichawi aliyofunga na shetani?

Leo ukizini na mke wa mtu, unaamini unaweza kutubu pekeako chumbani, mwenye mume akakusamehe na Mungu akakuondolea HATIA moyoni?

Kizazi hiki mbona hamtaki kuambiwa Kweli ya Mungu?
 
Mwanamke aliyezini aliletwa Kwa Yesu Ili Yesu atoe HUKUMU.

Mahakama Ile ikifanyika wazi mchana kweupe, Yesu akamsamehe na kumwambia usifanye dhambi tena.

Paulo alipotokewa na YESU na kupigwa upofu, aliambiwa nenda mjini utamkuta mtumishi atakuombea,

Wakati Paulo anaambiwa hayo, tayari lilikuwa kipindi Cha neema.

Mchawi Kwa Mfano, Unadhani anaweza kutubu mwenyewe chumbani anaweza kuvunja mikataba ya kichawi aliyofunga na shetani?

Leo ukizini na mke wa mtu, unaamini unaweza kutubu pekeako chumbani, mwenye mume akakusamehe na Mungu akakuondolea HATIA moyoni?

Kizazi hiki mbona hamtaki kuambiwa Kweli ya Mungu?
Haya mafundisho ya lazima ukatubu kwa mtumishi mnayatoa wapi kiongozi?.

Huyo mtumishi yeye akifanya dhambi anatubu mbele ya nani?. Mwanadamu ni nani mpaka atumike kama daraja la kusamehe dhambi?.

Yesu mwenyewe alisema tukiomba kwa jina lake, hiyo ndo connection tuliyonayo kati ya Mungu na Mwanadamu.

Sipingi watumishi kuombea watu, ila siaminj katika kauli ya dhambi fulani haisameheki isipokuwa kuwe na intervention ya mwanadamu katikati.
 
Haya mafundisho ya lazima ukatubu kwa mtumishi mnayatoa wapi kiongozi?.

Huyo mtumishi yeye akifanya dhambi anatubu mbele ya nani?. Mwanadamu ni nani mpaka atumike kama daraja la kusamehe dhambi?.

Yesu mwenyewe alisema tukiomba kwa jina lake, hiyo ndo connection tuliyonayo kati ya Mungu na Mwanadamu.

Sipingi watumishi kuombea watu, ila siaminj katika kauli ya dhambi fulani haisameheki isipokuwa kuwe na intervention ya mwanadamu katikati.
Nimekuuliza mchawi anaweza kujifungia ndani akatubu pekeake na kujitenga na mikataba ya kichawi pekeake?

Nimekuuliza, ukizini na mke wa mtu, ukijifungia ndani pekeako ukatubu bila kumwomba msamaha mwibiwa mke Kwa msaada wa watumishi wa Mungu unaamini Mungu atakusamehe?

Hivi m asomaga maandiko na kuyaelewa Kweli?

Ujuaji unakusaidia nini kuondoa Giza kichwani mwako?
 
Mnajiiiiiiiipa presha .Nan kakwambia Mungu ana formalities za kibinadam zaid namna hii!!???

Ujue anayekuondolea hatia sio kutubu mbele za mtu. NI Holly spirit, period!!!! Hii kwenda mbele za watu imekaa kisailolojia tu ili ku bust iman yako ila hata sio lazima wala haina ukwel...
Picha linaanza kushindwa kutofautisha kati ya uzinzi na uasherati
 
We umezaliwa na mwanamke tu huwezi kujifanya huna dhambi na hao watumishi pia wana dhambi ova
 
Huu ni upuuzi kiwango cha juu kbs karne hii ya sayansi na technology, hao unaewambia dhambi hizo nao wanazitenda. Wao wenyew wanahamasisha ushoga we uende ukawaungamie, amkeni acheni ujinga na upumbavu.
 
Mwanamke aliyezini aliletwa Kwa Yesu Ili Yesu atoe HUKUMU.

Mahakama Ile ikifanyika wazi mchana kweupe, Yesu akamsamehe na kumwambia usifanye dhambi tena.

Paulo alipotokewa na YESU na kupigwa upofu, aliambiwa nenda mjini utamkuta mtumishi atakuombea,

Wakati Paulo anaambiwa hayo, tayari lilikuwa kipindi Cha neema.

Mchawi Kwa Mfano, Unadhani anaweza kutubu mwenyewe chumbani anaweza kuvunja mikataba ya kichawi aliyofunga na shetani?

Leo ukizini na mke wa mtu, unaamini unaweza kutubu pekeako chumbani, mwenye mume akakusamehe na Mungu akakuondolea HATIA moyoni?

Kizazi hiki mbona hamtaki kuambiwa Kweli ya Mungu?
Kwani Kutubu ni nini?
 
Kwanza tunatakiwa Tuanze hapo kwenye neno Kutubu,
Kutubu ni kugeza mtazamo
Wayahudi siku zote waliamini katika torati na mafundisho ya Musa kwamba yangewapatia haki mbele za Mungu Lakini haikuwezekana
Yesu anakuja anawaambia, Matthew 4v17 watubu yaani waigeukie injili, habari njema (waachane na torati ambayo si njema) ambayo kwa hiyo injili wataingia kwenye ufalme wa Mungu yaani watahesabiwa haki
Kwa hiyo KUTUBU ni kuacha TORATI na kuiamini INJILI kwa mujibu wa bibilia
 
Kwanza tunatakiwa Tuanze hapo kwenye neno Kutubu,
Kutubu ni kugeza mtazamo
Wayahudi siku zote waliamini katika torati na mafundisho ya Musa kwamba yangewapatia haki mbele za Mungu Lakini haikuwezekana
Yohana mbatizaji anakuja anawaambia, Matthew 4v17 watubu(waigeukie injili, habari njema waachane na torati ambayo si njema) ambayo kwa hiyo injili wataingia kwenye ufalme wa Mungu yaani watahesabiwa haki
Kwa hiyo KUTUBU ni kuacha TORATI na kuiamini INJILI kwa mujibu wa bibilia
Neema ni mlango mgumu kuliko hata Ule wa SHERIA ya Musa.

Anania na Saphira waliishi kipindi Cha neema, lakini neema hiyo haikuwapa kuishi walipomdanganya Roho mtakatifu.

Kuwapo katika kipindi Cha neema, hakikupi Ruhusa ya kuzini na mke wa mtu Kisha ukapiga kimya na kujidanganya Eti utafunikwa na neema.

Yaliyoandikwa hapo juu ni maelekezo ya Mungu kupitia Roho MTAKATIFU.
 
Back
Top Bottom