Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Dhambi ambazo huwezi tubu peke yako bila kushirikisha watumishi wa Mungu

Neema ni mlango mgumu kuliko hata Ule wa SHERIA ya Musa.

Anania na Saphira waliishi kipindi Cha neema, lakini neema hiyo haikuwapa kuishi walipomdanganya Roho mtakatifu.

Kuwapo katika kipindi Cha neema, hakikupi Ruhusa ya kuzini na mke wa mtu Kisha ukapiga kimya na kujidanganya Eti utafunikwa na neema.

Yaliyoandikwa hapo juu ni maelekezo ya Mungu kupitia Roho MTAKATIFU.
Wewe unasema neema ni mlango mgumu
Wakati Yesu alisema watu waende kwake maana nira yake ni laini na mizigo wake ni wepesi
Sasa huyo roho uliyenaye mbona kama anajipinga vile
Mimi najua ni neema pekee ndiyo inayoweza kumfanya mtu aweze kukataa hayo unayoyaita wewe kwamba ni matendo mabaya ambapo sheria ilishindwa,Warumi 8:3
 
Wewe unasema neema ni mlango mgumu
Wakati Yesu alisema watu waende kwake maana nira yake ni laini na mizigo wake ni wepesi
Sasa huyo roho uliyenaye mbona kama anajipinga vile
Mimi najua ni neema pekee ndiyo inayo weza kumfanya aweze kukataa hayo unayoyaita wewe kwamba ni matendo mabaya ambapo sheria ilishindwa,Warumi 8:3
Mbona unakwepa kujibu,

Neema inatoa Utaratibu Gani wa mtu aliyeanguka dhambini , aliyeokoka, amjuaye Mungu, Kwa kuzini na mke wa mtu?

Ni sawa tutubu chumbani pekeako na kuamini umesamehewa?

Jibu Hilo, acha chenga.
 
Mnajiiiiiiiipa presha .Nan kakwambia Mungu ana formalities za kibinadam zaid namna hii!!???

Ujue anayekuondolea hatia sio kutubu mbele za mtu. NI Holly spirit, period!!!! Hii kwenda mbele za watu imekaa kisailolojia tu ili ku bust iman yako ila hata sio lazima wala haina ukwel...

Biblia inasema nini kuhusu Roho Mtakatifu:

"Unapoituma Roho wako, vinaumbwa, nawe waufanya upya uso wa nchi. (Kutoka Biblia ya NIV, Zaburi 104:30)"

Niende wapi nijiepushe na Roho yako? Nitakimbilia wapi uso wako? (Kutoka Biblia ya NIV, Zaburi 139:7)

"Unifundishe kuyafanya mapenzi yako, kwa maana wewe ndiwe Mungu wangu; Roho yako mwema na unitongoze mahali tambarare. (Kutoka Biblia ya NIV, Zaburi 143:10)"

mistari hii inazungumza juu ya Roho kutoka kwa MUNGU Mwenyezi.

Mstari wa kwanza hapo juu, Zaburi 104:30, unakubaliana kikamilifu na Mistari Adhimu hapo juu kuhusu MUNGU Mwenyezi Akiipulizia Roho yake ndani ya matumbo ya mama zetu tukiwa fetusi.


Ikon för Verifierad av gruppen
 
Mbona unakwepa kujibu,

Neema inatoa Utaratibu Gani wa mtu aliyeanguka dhambini , aliyeokoka, amjuaye Mungu, Kwa kuzini na mke wa mtu?

Ni sawa tutubu chumbani pekeako na kuamini umesamehewa?

Jibu Hilo, acha chenga.
Kwa nini uzinzi tu lakini?
Fikiria jamaa amekukamata na akakufanya chochote hata kukuauwa, na haujapata nafasi ya kwenda kwa mchungaji wako, itakuwaje hapo? Utaenda motoni eti si ndiyo unavyo fikiria
 
Kwa nini uzinzi tu lakini?
Fikiria jamaa amekukamata na akakufanya chochote hata kukuauwa, na haujapata nafasi ya kwenda kwa mchungaji wako, itakuwaje hapo? Utaenda motoni eti si ndiyo unavyo fikiria
Acha chenga.

Naongelea uliyezini na hukukamatwa, katika kipindi hiki unachoita Cha neema,

Ni sawa kutubu pekeako kimya kimya, bila mkeo kujua ulichofanya, bila mume wa uliyezini naye kujua na kusamehe?

Jibu Hilo, usilete siasa.
 
"Mbingu ipo na ndimo Mungu anamokaa"
Kwani Mungu anakaa?
Mbingu ipo na ndimo Mungu anamokaa.
Kuhusu dhambi, hakuna dhambi, zote zilichukuliwa na Yesu,
Dhambi ya kumkufuru roho ni mtu kutokuamini ya kwamba Mungu alimtoa mwanaye kama ondoleo la dhambi ili kila aaminie asife bali aishi
 
Mnajiiiiiiiipa presha .Nan kakwambia Mungu ana formalities za kibinadam zaid namna hii!!???

Ujue anayekuondolea hatia sio kutubu mbele za mtu. NI Holly spirit, period!!!! Hii kwenda mbele za watu imekaa kisailolojia tu ili ku bust iman yako ila hata sio lazima wala haina ukwel...
Exactly
 
Kwangu mimi naona dhambi kubwa kuliko zote ni ile ya kujiondoa uhai(Kujinyonga hadi kufa,kujipiga bastola nk)

Dhambi nyingine zote,mtu anakuwa na fursa ya kupatana na Mungu kwa njia ya toba(Kutubu).

Dhambi ya kujiondoa uhai inakuwa kubwa kwasababu mtu anakuwa ameondoa uhai wake mwenyewe.

Anakuwa amekiuka amri ya Mungu inayosema usiue,na wakati huohuo anakuwa amejiondolea fursa ya kuweza kutubu(Toba).
 
Anayesamehe dhambi ni Mungu.

Mtumishi wa Mungu ni chombo chake na msaada wa kukufungua pingu wewe uliye mtumwa.

Amen
Watumishi wa Mungu waadilifu wamebaki wachache siku hizi.
Wengi wanakwenda kimwili..hii inaondoa kuaminiwa na jamii.
Hili nalo hulioni?
Na Mtumishi naye akitenda dhambi,akatubie kwa nani?
Je,Biblia imeweka utaratibu gani katika Toba?
 
Salaam shalom.

INTRODUCTON.

Imeandikwa, Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.( 1 Yoh 1:9).

Dhambi ni kutotii, kwenda kinyume na maelekezo ya Mungu. Na Roho mtakatifu yupo kutukumbusha dhambi zetu Ili tuzitibie Ili tuendelee kuwa WATAKATIFU.

DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:


1. ZINAA NA UASHERATI.

UASHERATI ni kufanya Tendo la zinaa na mtu nje ya NDOA asiye mkeo au mumeo.

UZINZI ni kufanya tendo la uchafu, zinaa kabla ya Kuoa au Kuolewa.

Ukizini na mke wa mtu au mume wa Mtu, au ukiota unazini ndotoni na mtu au watu usiowafahamu, usijidanganye kuwa ukitubu sirini utasamehewa, HATIA itaendelea kuwepo Hadi uwatafute watumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. Watumishi Wana BUSARA ya kusuluhisha dhambi hiyo pande zote mbili Ili ufunguliwe.

Kuzini na mke wa mtu, faini ya juu ni kulipa Mahari aliyotoa muoaji Ili akusamehe, kushirikisha mtumishi ni kutumia BUSARA ya Mungu Ili muibiwa mke aridhie kukusamehe kutomlipa, au akupunguzie faini.

(Mithali 6:20-35,) UZINZI hufunga NAFSI, Amri ya Mungu usizini (Kumbukumbu la torati 5:1-21)

2. USHOGA.

Ikiwa uliwahi kuwa shoga, ukaamua kuacha, kamwe usitubu sirini na kuishiwa hapo, USHOGA huambatana na mapepo na kufungwa NAFSI, mfungwa kamwe hawezi jifunguanpingu mwenyewe, unawahutaji watumishi wa Kweli Ili UOMBEWE na kuwekwa huru, sadaka ni LAZIMA Ili itolewe huko. ( Mwanzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke makusudi Ili asizae na mke aliyepewa.

3. USAGAJI.

Mwanamke pia aliyewa kufanya dhambi hiyo, huwezi kufunguliwa na Utumwa na HATIA hiyo pekeako Kwa kutubu sirini, nenda Kwa watumishi wa Kweli, Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. mwanzo 38:9-10, Onani aliuwawa Kwa dhambi hiyo, ( kumbukumbu la torati 5:1-21) Amri za Mungu Usiue.

4. PUNYETO/ KUJICHUA.

Ikiwa uliwahi kujichua, ukaamua kuacha, unahitaji kwenda Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi Ili ufunguliwe, Mpiga PUNYETO ni mfungwa, ni mke au mume wa Roho chafu katika Ulimwengu wa Roho, hivyo kufunguliwa ni LAZIMA utoe sadaka, uvunje NDOA chafu hiyo ya kiroho na hati ya NDOA chafu ya kiroho iondolewe, usipofanya hivyo, unajidanganya. Mbinguni huingii ng'o!! (Mwanzo 38:1-25) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke Ili asizae na mke wa marehemu kaka yake.
Neno Hilo hapo juu ni ROHO. Amen.

5.MWANAMKE KUOA MWANAMKE/MWANAUME KUOA MWANAUME MWENZIE.

Kutubu dhambi hii sirini bila watumishi wa Mungu ni kujidanganya. Chukua sadaka, nenda Kwa mtumishi, Sema Kweli Ili UOMBEWE na kufunguliwa, NDOA haramu ivunjwe na ufungwa wako kiroho uondolewe. ( Mwanzo 38:9-10, (Mithali 6:20-35)Amen.

6. ORAL SEX.

Ikiwa uliwahi kushiriki oral sex, kunyonya au kuramba Kwa mdomo sehemu za Siri za mwanamke au Mwanaume na ukatambua ni DHAMBI, ukaacha, Bado u kifungoni.

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli wa Mungu ufunguliwe na Mungu.

(1 Wakorintho 6:9-11), (Ufunuo wa Yohana 21:8) (Mzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda Tendo la NDOA kinyume.

7. ABORTION./ UTOAJI MIMBA/ KUFUNGA UZAZI/ KUTUMIA VIDONGE VYA KUPANGA UZAZI.

Kimbia haraka Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli ,beba sadaka kulingana na uwezo wako, UOMBEWE ufunguliwe.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Usiue ni Amri ya Mungu.

Ukipuuza Utakataliwa GETI la Mbinguni.

9. IKIWA ULIWAHI TUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME/ KIKE.

(Mwanzo 38-9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda kinyume na Utaratibu wa Tendo la NDOA na taratibu za UZAZI alizoweka Mungu.


Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.

10. MAUAJI.

Ikiwa uliwahi kuua bila kukusudia ,ukahukumiwa JELA ukatoka, ikiwa uliua Kwa Siri na hukubainika, ikiwa ulishiriki kuua, usijidanganye kuwa unaweza kutubu sirini, HATIA Ili ikuondoke uwe na Amani, Tafuta kiongozi wa Mungu wa Kweli mwenye BUSARA za Mungu, akuongoze Cha kufanya, utoe pia sadaka ya Ukombozi. ( Acts 9:3-6) Sauli alikuwa mwuaji, Yesu alimwelekeza aende Kwa mtumishi.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Mungu ameamrisha " Usiue".

11. IBADA ZA SANAMU, KUSHIRIKI IBADA ZA WAFU NA KUTOA SADAKA KWA MIZIMU KIMILA NK NK.

Kushiriki Ibada za KIMILA na Kutoa sadaka Kwa Roho za kishetani za Mababu, ni DHAMBI pia, ni kufungwa ni Utumwa ambao huwezi kujifungua pekeako.

(Mithali 6:20-35) kifungo Cha NAFSI sababu Ibada ya sanamu ni UZINZI kiroho mbele za Mungu, ( UFUNUO 21:8, (1 korinthians 6:9-11) watendao uchawi na Ibada ya sanamu watatupwa Jehanum.

Ukiamua kuacha na kuokoka, hatua inayofuata ni kushirikisha watumishi kukusaidia kukutenga na madhabahu hizo.

Sadaka ni LAZIMA, sababu, Ulimwengu wa Nuru na Giza sadaka ni inevitable. Amen

HITIMISHO.

Dhambi nilizotaja hapo juu, ni baadhi tu ya dhambi ambazo huwezi tubu pekeako, zimetajwa sawasawa na Ruhusa ya Roho mtakatifu Kwa mtumishi wake sawasawa na ufunuo wake apendavyo.

NB: Si DHAMBI zote zinahitaji kuona mtumishi wa Kweli kukusaidia kufunguliwa pingu za dhambi, ni baadhi ya dhambi ambazo Zina vifungo na attachment na maagano ya kipepo na kishetani.

ANGALIZO: Sadaka tutoazo Si Kwa ajili ya kununua Muujiza, au kununua Msamaha wa Mungu, Yesu msalabani alikwisha maliza yote Kwa Damu yake msalabani. Sadaka tunatoa kama shukrani tu na kuonyesha Upendo Kwa Yale Mungu alikwisha tutendea.

Mungu awabariki.

Source: Nabii Justine Ibrahim, U-Tube., Promover Tv channel U-Tube.

Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wako, fuatisha Sala hii,

EE YESU, NINAKIRI KWAKO KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU,ULIANDIKE KATIKA KITABU CHA UZIMA, NINAOMBA UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, NIWEZESHE NIISHI MAISHA MATAKATIFU.

Ameen
mkuu
Katika kutafuta toba kwa Mungu hakuna masharti zaidi ya kumuamini Bwana Yesu Kristo kwamba alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na kupitia toba ya kumaanisha kuacha dhambi tunasamehewa dhambi zetu.

Hayo ya kusema baadhi ya dhambi lazima Mtumishi wa Mungu ndo akutubishe ama akuongoze ni sawa na kuweka Lango jipya zaidi ya Yesu Kristo ili kumfikia Baba kwa minajili ya ondoleo la dhambi.

Yesu aliweka category mbili za dhambi,
  1. Dhambi zote atendazo mwanadamu dhidi ya mwanadamu -- Hizi zote zinasameheka kwa toba ya kumaanisha kuziacha
  2. Dhambi atendayo mwanadamu dhidi ya Mungu nayo ni Kumkufuru ROHO MTAKATIFU -- Hii HAISAMEHEKI hata ufanye toba ya kuongozwa na mitume na manabii. Pia hii mpaka uifanye unakuwa umefungua mageti mengi sana kumsogelea Mungu na kuzijua siri za Mbinguni na kuishi katika tumaini la Roho Mtakatifu. Hivyo ukimsaliti unakuwa fungu moja na ibilisi muasi ambaye tayari adhabu yake imewekwa tangu kale
Tunachohitaji kutoka kwa Watumishi yaani mitume na manabii ni muongozo namna ya kukisogelea Kiti cha Enzi cha Mungu Baba kwa unyenyekevu, kujikana, kujuta na kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi.
 
Watumishi wa Mungu waadilifu wamebaki wachache siku hizi.
Wengi wanakwenda kimwili..hii inaondoka kuaminiwa na jamii.
Hili nalo hulioni?
Na Mtumishi naye akitenda dhambi,akatubie kwa nani?
Je,Biblia imeweka utaratibu gani katika Toba?
Upo Sahihi

Ikumbukwe yule Towashi aliyekutana na Philipo alifanya maamuzi yake binafsi baada ya kusikia Neno na siyo kuongozwa kutubu. Alisema, hapa kuna maji kwa nini nisibatizwe? Yusufu akamjibu kuwa Ukiamini kwa moyo wako wote... naye akasema Naamini kwamba Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu. Akabatizwa.

Kila mmoja ana style yake ya kujileta kwa Mungu.

Kuna wakati Yesu akiwa kwenye Sinagogi (msikiti) anafundisha na watu wamemsonga sana. Familia fulani walitaka ndugu yao aliyepooza aponywe, walichofanya ni kuondoa sehemu ya paa la Sinagogi na kumshusha mgonjwa na kitanda chake kwa kamba. Yesu bila kupepesa alimwambia mgonjwa MWANANGU UMESAMEHEWA DHAMBI ZAKO.... Hii kauli ina maana kubwa sana kwenye ulimwengi wa Kiroho na pia ni maelekezo rasmi kwamba uponyaji pia ni matokeo ya kusamehewa dhambi. Na ukiangalia yule mgonjwa hakutubu wala kuongozwa na Yesu kukiri imani. Ambapo haina tofauti na yule mwanamke aliyeletwa kwa Yesu akituhumiwa Uzinzi. Hakupewa nafasi na washtaki wake kujutia makosa yake bali kwa sababu Roho wa Mungu uliwaconvict washtaki wake wakakimbia. Yesu alimwambia USITENDE DHAMBI TENA......

Haya mambo ya kujiaminisha kuwa mitume na manabii ndiyo walioshika funguo za kuelekea toba ni fundisho la mwovu shetani
 
mkuu
Katika kutafuta toba kwa Mungu hakuna masharti zaidi ya kumuamini Bwana Yesu Kristo kwamba alikufa kwa ajili ya dhambi zetu na kupitia toba ya kumaanisha kuacha dhambi tunasamehewa dhambi zetu.

Hayo ya kusema baadhi ya dhambi lazima Mtumishi wa Mungu ndo akutubishe ama akuongoze ni sawa na kuweka Lango jipya zaidi ya Yesu Kristo ili kumfikia Baba kwa minajili ya ondoleo la dhambi.

Yesu aliweka category mbili za dhambi,
  1. Dhambi zote atendazo mwanadamu dhidi ya mwanadamu -- Hizi zote zinasameheka kwa toba ya kumaanisha kuziacha
  2. Dhambi atendayo mwanadamu dhidi ya Mungu nayo ni Kumkufuru ROHO MTAKATIFU -- Hii HAISAMEHEKI hata ufanye toba ya kuongozwa na mitume na manabii. Pia hii mpaka uifanye unakuwa umefungua mageti mengi sana kumsogelea Mungu na kuzijua siri za Mbinguni na kuishi katika tumaini la Roho Mtakatifu. Hivyo ukimsaliti unakuwa fungu moja na ibilisi muasi ambaye tayari adhabu yake imewekwa tangu kale
Tunachohitaji kutoka kwa Watumishi yaani mitume na manabii ni muongozo namna ya kukisogelea Kiti cha Enzi cha Mungu Baba kwa unyenyekevu, kujikana, kujuta na kutubu kwa kumaanisha kuziacha dhambi.
Tupe mfano wa category ya pili
 
Tupe mfano wa category ya pili
Mkuu
Kama umeshindwa kuelewa description yake basi hata mfano hautasaidia kukuelewesha.... Na bahati mbaya hakuna mfano kwenye Maandiko unaoelezea binadamu aliyemkufuru Roho Mtakatifu baada ya Yesu Kupaa kwenda Mbinguni lakini kuna waasi wa kwanza katika Agano Jipya ambao haijasemwa kama walimkufuru Roho Mtakatifu lakini waliadhibiwa vikali sana na Mungu. Mkumbuke Anania na mkewe Safira


Kila kitu nimeweka humo kwa lugha nyepesi sana kueleweka.
 
In life what you believe is what you get,km kichwani mwako inasema huwezi mpk mchungaji ajue umezini that’s you kwakua mchungaji sio mungu ilaunapotubu unaongea na mungu wangu wako and read a correct mistari ya kutubu sidhani km hutasamehewa your mind is your driver
 
Salaam shalom.

INTRODUCTON.

Imeandikwa, Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na haki, hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.( 1 Yoh 1:9).

Dhambi ni kutotii, kwenda kinyume na maelekezo ya Mungu. Na Roho mtakatifu yupo kutukumbusha dhambi zetu Ili tuzitibie Ili tuendelee kuwa WATAKATIFU.

DHAMBI AMBAZO KAMWE HATIA YAKE HAITAKUONDOKA HADI USHIRIKISHE WATUMISHI WA MUNGU ILI UOMBEWE UKIAMBATISHA NA SADAKA YA UKOMBOZI NI ZIFUATAZO:


1. ZINAA NA UASHERATI.

UASHERATI ni kufanya Tendo la zinaa na mtu nje ya NDOA asiye mkeo au mumeo.

UZINZI ni kufanya tendo la uchafu, zinaa kabla ya Kuoa au Kuolewa.

Ukizini na mke wa mtu au mume wa Mtu, au ukiota unazini ndotoni na mtu au watu usiowafahamu, usijidanganye kuwa ukitubu sirini utasamehewa, HATIA itaendelea kuwepo Hadi uwatafute watumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. Watumishi Wana BUSARA ya kusuluhisha dhambi hiyo pande zote mbili Ili ufunguliwe.

Kuzini na mke wa mtu, faini ya juu ni kulipa Mahari aliyotoa muoaji Ili akusamehe, kushirikisha mtumishi ni kutumia BUSARA ya Mungu Ili muibiwa mke aridhie kukusamehe kutomlipa, au akupunguzie faini.

(Mithali 6:20-35,) UZINZI hufunga NAFSI, Amri ya Mungu usizini (Kumbukumbu la torati 5:1-21)

2. USHOGA.

Ikiwa uliwahi kuwa shoga, ukaamua kuacha, kamwe usitubu sirini na kuishiwa hapo, USHOGA huambatana na mapepo na kufungwa NAFSI, mfungwa kamwe hawezi jifunguanpingu mwenyewe, unawahutaji watumishi wa Kweli Ili UOMBEWE na kuwekwa huru, sadaka ni LAZIMA Ili itolewe huko. ( Mwanzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke makusudi Ili asizae na mke aliyepewa.

3. USAGAJI.

Mwanamke pia aliyewa kufanya dhambi hiyo, huwezi kufunguliwa na Utumwa na HATIA hiyo pekeako Kwa kutubu sirini, nenda Kwa watumishi wa Kweli, Ukiwa na sadaka ya Ukombozi. mwanzo 38:9-10, Onani aliuwawa Kwa dhambi hiyo, ( kumbukumbu la torati 5:1-21) Amri za Mungu Usiue.

4. PUNYETO/ KUJICHUA.

Ikiwa uliwahi kujichua, ukaamua kuacha, unahitaji kwenda Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli Ukiwa na sadaka ya Ukombozi Ili ufunguliwe, Mpiga PUNYETO ni mfungwa, ni mke au mume wa Roho chafu katika Ulimwengu wa Roho, hivyo kufunguliwa ni LAZIMA utoe sadaka, uvunje NDOA chafu hiyo ya kiroho na hati ya NDOA chafu ya kiroho iondolewe, usipofanya hivyo, unajidanganya. Mbinguni huingii ng'o!! (Mwanzo 38:1-25) Mungu alimwua Onani Kwa kumwaga shahawa nje ya uke Ili asizae na mke wa marehemu kaka yake.
Neno Hilo hapo juu ni ROHO. Amen.

5.MWANAMKE KUOA MWANAMKE/MWANAUME KUOA MWANAUME MWENZIE.

Kutubu dhambi hii sirini bila watumishi wa Mungu ni kujidanganya. Chukua sadaka, nenda Kwa mtumishi, Sema Kweli Ili UOMBEWE na kufunguliwa, NDOA haramu ivunjwe na ufungwa wako kiroho uondolewe. ( Mwanzo 38:9-10, (Mithali 6:20-35)Amen.

6. ORAL SEX.

Ikiwa uliwahi kushiriki oral sex, kunyonya au kuramba Kwa mdomo sehemu za Siri za mwanamke au Mwanaume na ukatambua ni DHAMBI, ukaacha, Bado u kifungoni.

Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli wa Mungu ufunguliwe na Mungu.

(1 Wakorintho 6:9-11), (Ufunuo wa Yohana 21:8) (Mzo 38:9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda Tendo la NDOA kinyume.

7. ABORTION./ UTOAJI MIMBA/ KUFUNGA UZAZI/ KUTUMIA VIDONGE VYA KUPANGA UZAZI.

Kimbia haraka Kwa mtumishi wa Mungu wa Kweli ,beba sadaka kulingana na uwezo wako, UOMBEWE ufunguliwe.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Usiue ni Amri ya Mungu.

Ukipuuza Utakataliwa GETI la Mbinguni.

9. IKIWA ULIWAHI TUMIA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME/ KIKE.

(Mwanzo 38-9-10) Mungu alimwua Onani Kwa kutenda kinyume na Utaratibu wa Tendo la NDOA na taratibu za UZAZI alizoweka Mungu.


Chukua sadaka, mwone mtumishi wa Kweli UOMBEWE na kufunguliwa.

10. MAUAJI.

Ikiwa uliwahi kuua bila kukusudia ,ukahukumiwa JELA ukatoka, ikiwa uliua Kwa Siri na hukubainika, ikiwa ulishiriki kuua, usijidanganye kuwa unaweza kutubu sirini, HATIA Ili ikuondoke uwe na Amani, Tafuta kiongozi wa Mungu wa Kweli mwenye BUSARA za Mungu, akuongoze Cha kufanya, utoe pia sadaka ya Ukombozi. ( Acts 9:3-6) Sauli alikuwa mwuaji, Yesu alimwelekeza aende Kwa mtumishi.

(Kumbukumbu la torati 5:1-21) Mungu ameamrisha " Usiue".

11. IBADA ZA SANAMU, KUSHIRIKI IBADA ZA WAFU NA KUTOA SADAKA KWA MIZIMU KIMILA NK NK.

Kushiriki Ibada za KIMILA na Kutoa sadaka Kwa Roho za kishetani za Mababu, ni DHAMBI pia, ni kufungwa ni Utumwa ambao huwezi kujifungua pekeako.

(Mithali 6:20-35) kifungo Cha NAFSI sababu Ibada ya sanamu ni UZINZI kiroho mbele za Mungu, ( UFUNUO 21:8, (1 korinthians 6:9-11) watendao uchawi na Ibada ya sanamu watatupwa Jehanum.

Ukiamua kuacha na kuokoka, hatua inayofuata ni kushirikisha watumishi kukusaidia kukutenga na madhabahu hizo.

Sadaka ni LAZIMA, sababu, Ulimwengu wa Nuru na Giza sadaka ni inevitable. Amen

HITIMISHO.

Dhambi nilizotaja hapo juu, ni baadhi tu ya dhambi ambazo huwezi tubu pekeako, zimetajwa sawasawa na Ruhusa ya Roho mtakatifu Kwa mtumishi wake sawasawa na ufunuo wake apendavyo.

NB: Si DHAMBI zote zinahitaji kuona mtumishi wa Kweli kukusaidia kufunguliwa pingu za dhambi, ni baadhi ya dhambi ambazo Zina vifungo na attachment na maagano ya kipepo na kishetani.

ANGALIZO: Sadaka tutoazo Si Kwa ajili ya kununua Muujiza, au kununua Msamaha wa Mungu, Yesu msalabani alikwisha maliza yote Kwa Damu yake msalabani. Sadaka tunatoa kama shukrani tu na kuonyesha Upendo Kwa Yale Mungu alikwisha tutendea.

Mungu awabariki.

Source: Nabii Justine Ibrahim, U-Tube., Promover Tv channel U-Tube.

Ikiwa hujampokea Yesu kuwa BWANA na Mwokozi wako, fuatisha Sala hii,

EE YESU, NINAKIRI KWAKO KUWA MIMI NI MWENYE DHAMBI, NINAOMBA UNISAMEHE, ULIFUTE JINA LANGU KATIKA KITABU CHA HUKUMU,ULIANDIKE KATIKA KITABU CHA UZIMA, NINAOMBA UWEZO WA KUSHINDA DHAMBI, NIWEZESHE NIISHI MAISHA MATAKATIFU.

Ameen
Ila nyie watumishi kausha damu ni shida Sana. Kumbe ndo mnadanga watu huko Ili mpate sadaka
. Tuwekee mafungu ya uliyoyandika hapa. Mimi nitakutumia sadaka laki 2. Unitumie no ya mpesa.
 
Kuna dhambi ambazo kwame Mungu awezi kuzisamehe ata ukitubuni pamoja na uchafu (ushoga,kumdhihaki nk )
 
Mkuu uko sahihi kabisa! Lakini hata hivyo Sadaka ya Ukombozi ni ile iliyopatikana pale Msalabani,yaani damu ya Yesu,si vinginevyo,
(Mathayo26:28)
Hakuna Sadaka nyingine inayoweza kumridhisha Mungu atusamehe zaidi ya hiyo iliyopatikana pale Msalabani,
(Waebrania10:6-10)
Chakuzingatia tu kwa kuwa Sadaka hiyo ilitolewa mara moja mara mtu anapaswa kutubu dhambi zake kwa KUMAANISHA KUZIACHA hata kama dhambi hiyo ni kubwa kiasi gani mf.Kuua,Kuzini,Kulawiti,kubaka,kunyanganya,nk atasamehewa tu,
(Isaya1:18) (Mithali28:13)
HATARI iliyopo ni pale mtu ambapo ametubu dhambi,harafu baada ya kujifunza Kweli ya Neno la Mungu kwa muda mrefu ikatokea AKAFANYA DHAMBI KWA KUKUSUDIA huku akijua ni dhambi mf.ni mtumishi wa Mungu,askofu,nk pale anamhuzunisha Roho Mtakatifu! Kusamehewa siyo rahisi hivi hivi,ni shughuli kweli kweli,(Waebrania10:26-29)
 
Back
Top Bottom