Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

Dhana ya udini, ukabila na ukanda wa CHADEMA

Hakuna ukabila kwenye Chadema ni maneno ya watu wavivu kufikiria. Kuna viongozi wengi wa kaskazini kwasababu kuna wabunge wengi kaskazini. Zitto mafano wakati anaingia Chadema alikuwa kijana kidogo na hakuwa na kitu hivyo sio ukabila vilevile wanaosema Chadema ni chama cha Wachagga ni wana Chama au? kwasababu huwezi kuwa kiongozi kama si mwanachama. Sugu, Msigwa, Lissu, mbunge wa Mwanza wote hawa hawajatokea kaskazini!. Kama unataka kukosoa chama jiunge kwanza huwezi kuchagua watu tu wa Lindi wakati hawako kwenye harakati.
Excellent point great thinker!Usipotee sana mkuu.
 
Kuna watu wanafurahia Mh Mbowe kuondoka kwenye nafasi ya Uenyekiti,kuna wanaotaka hata kuandamana ili aondoke,je chama ni cha kikabila kwasababu tu kwamba mwenyekiti ana kabila?Kwahiyo mwenyekiti akiwa mgogo basi cha ni cha kigogo?

Kuna anayeweza kuniambia ukabila uko wapi kwenye chama cha cdm?Je ni kweli kuwa mwenyekiti mchagga akiondoka ndo chama kitakuwa si cha wachagga?Ili linanitatiza sana tu!


JMushi nadhani kuna haja ya chadema kueleza kwa kina na kwa mijadala mipana zaidi nini haswa 'misingi ya chama'. Hapa wataalamu wanaweza kuhusishwa kwa ajili ya kutoa technical clarifications kuhusu baadhi ya issue za kitaaluma.

Kwa nini nasema hivyo. Nimesikia mara kadhaa kwenye hotuba za Mbowe akisema 'hakuna aliye juu ya chama'. Lakini pia nimeshasikia one time Mnyika alikuwa akitoa ufafanuzi juu ya sera ya mrengo wa kati wa chadema. Kuna hatuba nyingine ya Mbowe aliitoa alipokwenda USA, akaeleza kwa kirefu sana juu sera za CDM, kwamba cdm siyo chama kinacho kumbatia umaskini, kwamba cdm ni chama kinacho amini katika individual ability to develop themselves rather than waiting for the goverment, serikali iwawezeshe watu. Kwa mtazamo wangu hizi ni baadhi ya misingi ya chama. Ila katika kuongelea mambo haya, ambayo kwa mtazamo wangu yanareflect misingi ya chama, huwa haiwekwi wazi sana pale mtu anapozungumzia hakuna mtu aliye juu ya chama. Nadhani katika kauli kama hizi, ni vizuri watu wakaelezwa nini maana ya 'kutokuwa juu ya chama'.

Nikienda kiundani zaidi kuhusu misingi ya chama. Misingi ya chama ndio chama chenyewe. Na hapa mtu anapozungumzia katiba ya chama inabidi atofautishe na misingi ya chama. Katiba ya chama naweza kusema ni mwongozo tu ambao unaweza usitoe ufafanuzi kuhusu misingi ya chama. Misingi ya chama ni yale maono ya chama ambayo kwa hayo ndio chama kilianzishwa. Yanaweza kuwa ni maono ya kamati kuuu au wajumbe ambao either wameshiriki katika kuyadecifer maono hayo na kuya transfer maono hayo kwa wale wote ambao utumishi wao ni wa kutukuka katika kusimamia misingi hiyo. Na kwenye hii misingi kuna kuwa na utaratibu wakiziboresha na kuzibadilisha bila kuathiri utendaji wa chama.

My point ni kwamba watu wengi haswa maccm na hta baadhi ya viongozi wa cdm kwa kushindwa kuelewa hilo wanashindwa kuelewa dhana nzima ya chadema na misingi ya kuundwa kwa chama. Ni uwazi usio na kificho kwamba katika hili misingi ya cdm ni tofauti sana na ccm. Inabidi waelewe pia Misingi ya chama pia siyo katiba ya chama. LAkini hili halijawekwa wazi sana na viongozi wa cdm. Ndo maana watu wanaropoka tuu udini, ukabila, ukanda nk. Kwa sababu hawaelewe misingi ambayo cdm inaisimamia. CCM misingi yake ilishakufa, hili swala la misingi linaweza kuwapatabu, ndo maana kwenye mambo mengi sana wanashindwa kufanya maamuzi. Muungano upo hoi, azimio la arusha limeshazikwa. CCM ni chama cha kishikajishikaji tu!! Its like a group of cannibals animals, which if they dont get food they will eat each other.

Haya mambo ya kifafanuliwa sana kwa undani kupitia makongamano, vijarida tV sessions, magazetini yatasaidia sana kufungua akili za watu kuepukana na hizi kasumba za watu waccm wanasambaza sera zao za udini, ukabila na uakanda.

Misngi ya chama ielezwe vizuri na maana ya kutokuwa juu ya chama ifafanuliwe zaidi, haswa baada ya kufukuza akina zitto.
 
Mkuu Nara,I stand to be corrected,kauli ya "hakuna aliye juu ya chama" ina maana kuwa ukivurunda,taratibu za chama zitafuatwa bila kujali umaarufu ama cheo cha mwanachama huyo.

Kwa mfano watu kama Lowassa na Chenge wako juu ya chama chao.
 
Last edited by a moderator:
Kuna watu wanafurahia Mh Mbowe kuondoka kwenye nafasi ya Uenyekiti,kuna wanaotaka hata kuandamana ili aondoke,je chama ni cha kikabila kwasababu tu kwamba mwenyekiti ana kabila?Kwahiyo mwenyekiti akiwa mgogo basi cha ni cha kigogo?

Kuna anayeweza kuniambia ukabila uko wapi kwenye chama cha cdm?Je ni kweli kuwa mwenyekiti mchagga akiondoka ndo chama kitakuwa si cha wachagga?Ili linanitatiza sana tu!

Udini kwanza ndio la msingi ndio uje ukabila, na ukanda. Ukiwa mkristo chadema utasurvive otherwise utajuta.
 
Udini kwanza ndio la msingi ndio uje ukabila, na ukanda. Ukiwa mkristo chadema utasurvive otherwise utajuta.
Unamaanisha kamati kuu ya chadema inafanya maamuzi kwa kuzingatia dini?unaweza kutoa mifano halisi ili kuprove point yako?Chadema kimeanzishwa miaka ishirini na ushee iliyopita.Ni chama ambacho bado kinajengwa.Hilo la udini unao ushahidi?
 
Chadema ni chama cha kikabila na hili liko wazi kabisa hakuna mjadala.Ni chama cha kichaga chenye lengo la kuendeleza fikra za kibaguzi za akina chief Marealle ambazo Nyerere alizikataa katakata,msitufanye watz mazezeta kuwa hatujui kilichopo nyuma ya pazia
 
Kuna watu wanafurahia Mh Mbowe kuondoka kwenye nafasi ya Uenyekiti,kuna wanaotaka hata kuandamana ili aondoke,je chama ni cha kikabila kwasababu tu kwamba mwenyekiti ana kabila?Kwahiyo mwenyekiti akiwa mgogo basi cha ni cha kigogo?

Kuna anayeweza kuniambia ukabila uko wapi kwenye chama cha cdm?Je ni kweli kuwa mwenyekiti mchagga akiondoka ndo chama kitakuwa si cha wachagga?Ili linanitatiza sana tu!

naanza na katibu wa bavicha!!sijui hata alipitaje kwenye uchaguzi wa bavicha !!ila kwa kuwa ni mpwa wa mboe akili ndogo ikashinda akili kubwa maajabu ya siasa za chadema
 
naanza na katibu wa bavicha!!sijui hata alipitaje kwenye uchaguzi wa bavicha !!ila kwa kuwa ni mpwa wa mboe akili ndogo ikashinda akili kubwa maajabu ya siasa za chadema
unaposema hujui alipitaje unamaanisha kuwa hana vigezo vya kuwa kwenye nafasi hiyo?unaweza kufafanua ni kivipi unaona kwamba hafai kuongoza?Hapo unaposema hujui alipitaje ni kauli tata tu ambayo huwezi hata kuitetea.
 
Chadema ni chama cha kikabila na hili liko wazi kabisa hakuna mjadala.Ni chama cha kichaga chenye lengo la kuendeleza fikra za kibaguzi za akina chief Marealle ambazo Nyerere alizikataa katakata,msitufanye watz mazezeta kuwa hatujui kilichopo nyuma ya pazia
Sasa kama chadema kina hayo matatizo si ndo mnatakiwa mfurahie nyie ccm?Hivi mwenyekiti akiwa mgogo ndo utajiunga na chadema?wewe ni ------ kama mwenyekiti wako?unaweza kunitajia fikra moja ya kibaguzi ya marealle waliyonayo chadema?
 
Unategemea nini kama halmashauri ya ubongo wako umejaa matope sasa hili ndio umeandika nini au nyie ndio mnaamini kua bara bara zikitengenezwa basi ni mbunge katengeneza acheni ujinga manyinyiemu nyie.

Chama hiki kimejipambanua kuwa ni cha wachaga kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
1. Viongozi wakuu wa juu hawakuchaguliwa kwa sifa bali ni kwa kabila lao. M/kiti, mtunza fedha akina mnyika. Makatibu wengi wa mikoa ni akina kilewo, munisi, kiwia
2. Kati ya wabunge 25 wa kuteuliwa hakuna wanaotoka mikoa ya kusini ya mtwara na lindi kama wapo tutajie
3. Asilimia kubwa ya wabunge wa kuteuliwa ni wachaga au watu wanaousiana na big fish kama vile rose kamili, dada yake lisu n.k.
4. Kwenye chadema sio tu chama cha kikabila bali ni chama chenye mwelekeo wa kifamilia.
 
Unabisha nini wewe bila kuletwa takwimu kwa haraka tu inajulikana uozo wa cdm ulivyo kwenye ubaguzi nafurahi mpaka 214 mwezi wa sita ivi cdm itabakia huko huko kwa wachaga labda na kwa hao wauza maharahe uko mbeya maana wanaweza kuchagua hata jiwe kuliko wenye akili na busara nao sio kosa lao ni elimu tu hakuna ila wakistuka no wepesi kuchange kama kinyonga.
 
Unabisha nini wewe bila kuletwa takwimu kwa haraka tu inajulikana uozo wa cdm ulivyo kwenye ubaguzi nafurahi mpaka 214 mwezi wa sita ivi cdm itabakia huko huko kwa wachaga labda na kwa hao wauza maharahe uko mbeya maana wanaweza kuchagua hata jiwe kuliko wenye akili na busara nao sio kosa lao ni elimu tu hakuna ila wakistuka no wepesi kuchange kama kinyonga.
Chama kitajengwa na wananchi wa eneo husika.CCM ilikuwa kila mahali kwasababu enzi za chma kimoja ilikuwa ni lazima uwe na kadi ya chama.Wewe unataka sehemu ambayo haina wanachama wa kutosha wapewe mbunge wa kuteuliwa?Fimbo ya mbali haiui nyoka.Wananchi waki accept idea za chama,wakakijenga chama,watapata viongozi.Hakuna mchagga aliyeteuliwa kwenda kuongoza Singida.
 
Sasa kama chadema kina hayo matatizo si ndo mnatakiwa mfurahie nyie ccm?Hivi mwenyekiti akiwa mgogo ndo utajiunga na chadema?wewe ni ------ kama mwenyekiti wako?unaweza kunitajia fikra moja ya kibaguzi ya marealle waliyonayo chadema?

wewe si ni walewale tu, unatetea ujinga wakati jibu unalo. Sera ya kibaguzi ya majimbo chadema imetoka wapi unajua? Tanzania moja acheni ubaguzi
 
wewe si ni walewale tu, unatetea ujinga wakati jibu unalo. Sera ya kibaguzi ya majimbo chadema imetoka wapi unajua? Tanzania moja acheni ubaguzi

Sera ya majimbo ni ya kibaguzi kvipi?na uchaggani kungekuwa na rasilimali kama mafuta na madini si ndo mngechonga sana na uongo kuukolezea?Ujinga ni kuhakikisha rasilimali zinawanufaisha wananchi wanaotokea maeneo hayo?Sera ya majimbo kwa maoni yangu ni kama kurudisha madaraka kwa wananchi.
 
Chama hiki kimejipambanua kuwa ni cha wachaga kwa kuzingatia mambo yafuatayo:
1. Viongozi wakuu wa juu hawakuchaguliwa kwa sifa bali ni kwa kabila lao. M/kiti, mtunza fedha akina mnyika. Makatibu wengi wa mikoa ni akina kilewo, munisi, kiwia
2. Kati ya wabunge 25 wa kuteuliwa hakuna wanaotoka mikoa ya kusini ya mtwara na lindi kama wapo tutajie
3. Asilimia kubwa ya wabunge wa kuteuliwa ni wachaga au watu wanaousiana na big fish kama vile rose kamili, dada yake lisu n.k.
4. Kwenye chadema sio tu chama cha kikabila bali ni chama chenye mwelekeo wa kifamilia.

Fanya tafiti ujue wabunge wa viti maalum wanapatikana vipi ndani ya vyama vya siasa.
 
Wewe unataka tuseme halafu utusababishie ban tu kwani nini ambacho hujui juu ya hoja yako hii.
 
wewe si ni walewale tu, unatetea ujinga wakati jibu unalo. Sera ya kibaguzi ya majimbo chadema imetoka wapi unajua? Tanzania moja acheni ubaguzi

Unaongea tu hujui hata mifumo ya majimbo inayounda federal state inaendeshwa vipi na manufaa yake ni yapi.

Nchi zote zilizoendelea zina mfumo wa shirikisho na kama hazina basi ni nchi zenye utawala unaozipa mamlaka za chini.

Sisi watanzania mfano wewe tunaendekeza rasilimali na hatufikilii vitu vingine. Italy haina rasilimali kama sisi lakini inatupa msaada.

Utawala wa majimbo una manufaa sana mfano mikoa ambayo haina rasilimali ingekuwa inaongoza kwa viwanda, mashule na kilimo. Yote ingefanyika kuhakikisha wanapata bajeti ya kuendesha serikali ya jimbo.

Nikupe mfano marekani majimbo mengine yalijikita kwenye elimu kama Massachusets, mengine kwenye tafiti kama california wana silicon valley, north carolina wana research triangle park. Makampuni makubwa unayoyasikia yako kwenye hivyo vituo.

Wengine walijukita kwenye afya, nk.

Msome mifumo ya shirikisho si kukaa kuogopesha watu na ubaguzi. Kuwa na serikali moja ilikuwa msumali wa mwisho kwa mweusi ulioachwa na wakoloni wakati nchi zao walizianzishwa kwa kuungana kama majimbo.
 
Sasa kama chadema kina hayo matatizo si ndo mnatakiwa mfurahie nyie ccm?Hivi mwenyekiti akiwa mgogo ndo utajiunga na chadema?wewe ni ------ kama mwenyekiti wako?unaweza kunitajia fikra moja ya kibaguzi ya marealle waliyonayo chadema?
Mkuu jmushi1 wewe kiwango chako ni cha juu nashangaa unabishana na hawa mateja ya lumumba yenyewe yana komaa ili ya pate buku7 kwaajili ya unga jioni
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom