Dhana ya uwepo wa Mungu na mbingu

Dhana ya uwepo wa Mungu na mbingu

ndio nazijua Kuna elimu ya
Nyota na Anga,Hisabati,Uhandisi,
uchimbaji madini,Tiba,Mapambo hizo ni baadhi ya elimu kubwa ambazo watu walianza kuzifanya na kutokea Kwa Civilization kubwa Toka Hapo kale na ndio nazozifahamu!


Mimi sijakuuliza unajua elimu gani, nimekuuliza; je wewe unajua elimu ZOTE ??
 
Mzee hujawahi kusoma biology!? Sperms and Eggs zinatokana na stem cell. Au hujui hilo. Halafu sperms zinazalishwa na mwanaume eggs huzalishwa na mwanamke.
Mbona simple tu. Una swali jingine!?

Halafu sperms zinazalishwa na mwanaume eggs huzalishwa na mwanamke…. Hapa umemaliza kila kitu [emoji1666]
 
Huko ndio kunaitwa matokeo ya kufikiria ndani ya mipaka ya muda na nafasi. Mungu na Mbingu havifikiriki kwani kila kinachofikirika ni cha uwongo. Mungu na Mbingu hupatikana katika hali ya Kweli (milele)

Yatupasa kumuabudu Mungu kwa njia ya ROHO na KWELI kwa sababu Mungu ni Roho. Yohana 4: 23 -24. Kwa sababu Mungu ni Roho basi ni ishara tosha yu Rohoni. Hivi basi Rohoni ndio Mbinguni

Ufunuo 1: kuanzai mastari 9 inaonyesha Yohana akiwa anafanya ibada Rohoni akayafunua ya Mbinguni aka Rohoni. Hivyo Issa bin Mariam alifundisha namna ya kufanya ibada hii (kwa njia ya Roho na Kweli) kitu ambacho hakuna dini za kileo zinafundisha namna kufanya ibada ya kwa njia hii ya Roho.

Wakristo wanabazina kwa njia ya Maji, na kuishi kwa Imani njia ya Yohana mbatizaji iliyopitwa na wakati lakini Yesu alibatiza kwa Roho kiwapa wafuasi wake uwezo kufikia uzima wa Milele ( kwa njama za mafalisayo na Makuhani kwa kushirikiana na Petro mwanafunzi wa Yesu namna hii ya ubatizaji imefichwa na upotoshaji mkubwa kufanywa zidi ya mafundisho ya yake)

Maneno tuyanenayo kutoka vivywani mwetu baada kifikirika na akiri zetu haviwezi kumkiri Mungu wa Kweli bali Roho kwa sababu iko katika hali ya kweli inaweza kumkiri Mungu wa Kweli.

Tuombapo neema kwa Mungu kwa kutumia mwili kwa maneno na fikra zetu tuomba neema za uwongo. Na ni neema zinufaishazo nafsi yetu ya uwongo (Mwili). Mafanikio katika mali, elimu, ndoa, familia na maisha kwa ujumla ni kwa ajili ya mwili, hukoma siku ya kifo.

Zeema zote zinufaishazo uongo zinamnufaisha shetani mungu na baba wa uwongo. Ndio ule mstari unasema umemtumkia shetani maisha yako yote. Umetumia nguvu na maarifa kupendesha matakwa ya nafsi yako ya uwongo. Ambayo ni mtumwa wa shetani.

Yatupasa kuomba kwa ajili ya Roho ambayo ipo milele, ilikuwepo, ipo na itakuwepo. Nafsi ya uwongo haiwezi iombea neema nafsi ya kweli kwa sababu sio tuu haijui pia haiwezi hata kuiweka kwenye fikra.

The soul exist beyond the Mind.

Shida na Raha zote ni za muda tuu, sio za milele ndio maana ni za uwongo. Unapaswa kutafuta njia ya kuishi maisha ya KWELI ungali mwilini. Hiyo basi usitegemee maisha ya Raha duniani na hata ukiyapata bado hayakupi kutosheka kwani mahitaji mengine hujitokeza kwa sababu uwongo hujibadiri. Hakuna tajiri aliyetosheka na wala sio kila masikini hana furaha.

Pointi hapa ni kwamba huna haja kuwa na wasiwasi na maisha ya mbinguni kwani unauwezo ya kiishi na kiyaonja ungali hai duniani. Tafuta namna.

Nawasilisha.
 
Kuna wale wanakwambia ukifika huko mwanaume utapewa wanawake mabikra 70@ ili uwashughulikie na wao kazi yao ni kukulisha tu ili uwashughulikie vizuri ilihali kwenye kitabu wanachokiamini wanaambiwa usizini.
 
Habari wakuu,

Huu mjadala ni mpana sana na upo tangu miaka mingi sana, nitaeleza nadharia ya uwepo wa mbingu na Mungu jinsi ulivyoibuka, nitatumia mifano ya sasa na ya kale ili niweze kueleweka,

Nitaanza na concept ya mbingu. Fikiria maisha jinsi yalivyo magumu, fikiria changamoto za kimaisha unazopitia mfano huna ajira, huna shughuli yeyote, biashara ngumu, huna uwezo wa kununua chakula, unaumwa huna pesa ya kwenda lutibiwa hospitali, umebambikiziwa kesi na wanasiasa, hujapata mtoto, umelima mazao yamepigwa ukame hakuna utakacho vuna, umepata msiba wa mtu unayempenda kafariki ghafla n.k majanga ni mengi

Kumbuka upo Tanzania, bara la Afrika sayari ya tatu iitwayo dunia wengi mnaiita duniani,

Sasa unaambiwa kuna nchi inaitwa mbinguni lakini haijulikani ilipo, Raisi wa hiyo nchi ni mungu, mawaziri ni malaika na kwenye hiyo nchi hakuna changamoto zozote za kimaisha yaani vyakura vipo vya kutosha, mazingira ni mazuri, kuna bustani nzuri, kuna hewa safi, hakuna magonjwa na ukiwa huko hauwezi kufa, huitaji ajira wala kufanya biashara ili uweze kujikimu yaani bata zote ni bureeee ,

Lakini ili uingie kwenye hiyo nchi ni lazima ufe kwanza kisha siku ya mwisho utafufuliwa utafanyiwa interview kwa kuangalia experience ya matendo yako, kama ulitenda mema utaingia huko kama ulitenda mabaya hutaingia kwenye nchi ya mbinguni yaani bata utazisikia tuu na utapewa adhabu ya kuchomwa moto na kufa mara ya pili ila inasemekana kabla hujachomwa utafungwa minyororo miaka elfu moja kwanza ndio uchomwe mpaka kufa.,

kabla raisi wa mbinguni ambaye ni mkombozi atakachokifanya muda mfupi kabla ya zoezi la kuwafufua wafu na kuwafanyia interview

assume siku ya tukio ni mwaka 2021 december. Wale watakao kuwepo siku hiyo wataungana na watakaofufuliwa kwenye kufanyiwa interview ya kuingia katika nchi yenye asali na maziwa na bata zote

Hiki ndicho kinachofanya watu tunasali usiku na mchana ili tupate tiketi ya kuingia mbinguni.​
December 2021 ndo hii
 
Anaepinga hakuna Mungu ajitokeze hapa na aseme kwa herufi kubwa ili tuone....
 
Haya ni maelezo ya kitoto sana ni ya level ya darasa la saba.
Hakuna kitu kinachotokea tu bila ya kuwa na chanzo.
Mfano ukiona Samsung Galaxy pale Kariakoo au Land Rover vogue,au system ya whatsaap,utakuwa ni mjinga kuamini hivi vitu vimetokea tu kibahati bahati!! Hakuna aliyevitengeneza!!
Sasa iangalie Dunia,na ulimwengu,angalia mwanadsmu na mifumo yake ya ubongo,kupumua,moyo,damu,hivi vitu haviwezi kutokea tu!!kwa akili ile ile,lazima Kuna super power Ili design hii mambo!!hiyo super power ndio Mungu
Mkuu nimekupata vizuri sana kwenye mifano yako na Hoja yako imebase kwenye point ya hakuna kitu kinatokea tu bila kuwa na chanzo right? Tuanzie hapo

Umetolea mfano wa simu aina ya Samsung Galaxy pale kariakoo haiwezi kuwa imetokea tu from no where lazima kutakuwa na mtu amefanya yake, which is true

Umetolea mfano ukiangalia science ya mwili wa binadamu na system zake, ukiangalia dunia ilivo ni wazi kuwa kuna chanzo cha uwepo wake, ambayo ni super power ambayo tuna ita Mungu, which is true

Tuje kwenye hoja ya Kila kitu kina mwanzo wake au kina chanzo chake, je akiangalia uundaji wa Samsung Galaxy pale kariakoo na ushajua kuwa kuna mtu ambae ana akili sana nyuma yake ndio alikuwa mtengenezaji, je ukiambiwa huyo mtu/fundi alietengeneza Samsung Galaxy yeye hana chanzo/mwanzo wa kupatikana kwake utaamini?

Tuje kwenye uumbaji wa dunia na vyote vilivyomo pamoja na binadamu mwenyewe, refer uliposema hakuna kitu kinatokea tu bila chanzo au mwanzo ba jinsi mwanadamu alivoumbwa lazima kuna nguvu ambayo imetumika kukamilisha hilo swala, swali linakuja

Sasa kama uumbaji wa mwanadamu ni kiashiria kwamba kuna nguvu imetumika ya uumbaji ambayo ni Mungu, je hujiulizi kama kuumba dunia na mwanadamu kulihitaji super power kubwa sana je uumbaji wa alieumba dunia na binadamu ye alihitaji super power kiasi gani katika uumbwaji wake?

Kwa akili ya kawaida kabisa, ukiangalia baiskeli ilivotengenezwa basi unatoa pongezi wa mgunduzi, kwamba huyo mtu alikuwa na Akili sana, ukiangalia mwanadamu alivoumbwa lazima utasema aliemuumba ye ni Smart kuliko mwanadamu alivo,ukija kwa Mungu sifa unatoa kwa nani? Coz tushakubaliana hapo mwanzo kuwa Kila kitu kina mwanzo wake

Kama unaamini kuwa Mungu ye hajaumbwa Wala hajazaliwa sasa unatoa wapi nguvu ya kupinga mtu akisema dunia na vyote vilivyomo vimetokea tu from no where kama ilivo kwa Mungu? Kama ukiangalia Samsung Galaxy unasema kuna mtu kafanya yake hapo Kwanini ukiangalia uwezo wa Mungu usiseme dahhh aliefanya Mungu akawa na huu uwezo sijui yeye ana uwezo kiasi gani.....!

Kwa upande wangu naweza kuamini kwamba dunia na vyote vilivyomo vilihitaji Architecture wake ili vitokee ila linapokuja swala la kusema huyo Architecture pamoja na ubora wake na ukamilifu wake eti hana chanzo hapo ndio utata unapoanzia, shikilia msimamo wako wa kwamba hakuna kitu kinatokea tu bila chanzo, kwa kitu chenye uwezo kama wa Mungu hakiwezi kutokea tu from no where brother
 
Hii nadharia ilianzia huko nchini israel walikuwa kila wakipigana vita hawashindi, sababu waliamini kuwa wanashindwa vita kwa sababu ya matendo yao mabaya hivyo basi wakaanza kuamini kuwa mkombozi wao atakuja kuwakomboa endapo watatenda mema, na huyo mkombozi wao waliamini ananguvu zisizo za kibinadamu na ndiye atakaye kuja kuwa mfalme wa israel,

Baada ya ujio wa yesu na matendo yake mema na ya kijasiri ya kutokuogopa chochote, raia wengi wakaanza kuamini kuwa huyo ndiye mkombozi wao aliyetabiliwa, kumbuka wakati huo israel ilikuwa chini ya utawala wa kirumi yaani raia wote ni mateka wanaitumilia serikali ya warumi,

Basi taarifa zikamfikia kiongozi wa kirumi hapo israel aliyekuwa akiitwa HERODE (jina silikumbuki vizuri) herode akaona ampasie kesi PONSIO PILATO, huko yesu akahukumiwa kuteswa mpaka kufa,

Kumbuka nchi nzima walikuwa wanaamini yesu ndio mkombozi wao na walijua hatakufa maana ndiye aliyetabiliwa,

Baada ya yesu kuteswa na kufa wakawa suprised kwamba mbona amekufa? Maana yake sio yeye aliyetabiliwa!

Basi hapo ndipo alipoibuka jamaa mmoja aitwaye PAULO, huyu akaja na nadharia kuwa mkombozi aliyetabiliwa ni huyo huyo yesu aliyekufa, ila kilichokufa ni mwili na tayari amekwisha enda ktk nchi itwayo mbinguni huko ili mtu aende inabidi afe kwanza kisha siku ya mwisho atafufuliwa na kwenda huko, ila kikubwa matendo ya mhusika yawe mema ndio tiketi yake ya kuingia huko. Waisrael wote wakaanza kuamini hivyo kuwa mkombozi wao ndio yesu na wao watamfuata huko kwenye nchiaa ya mbinguni.​
no...waisraili hawamwamini YESU,wana dini yao inaitwa jiduism,na hawatumii biblia,na sehemu zao za kuabidiwa zinaitwa masinagogi na si makanisa wala misikitikt na kiongozi wao anaitwa rabbi na wala sio mchungaji,padri,shekh wala askof,na wana pia kiongozi mwingine akiitwa kuhani....
 
Back
Top Bottom