Diamond alamba mamilioni ya CAF, Kutumbuiza uzinduzi wa AFCON 2017

Diamond alamba mamilioni ya CAF, Kutumbuiza uzinduzi wa AFCON 2017

hizo avatar mnazoweka mnawaaibisha wahusika wa hizo picha.

Yaani unakuta mtu kapost kitu
ukiangalia avatar na kitu alichoPost hata haviendani..

nakushauri umuondoe huyo mtu
hapo humtendei haki.. siamini kama angeona picha inatumiwa na mtu kama kama angekuangalia tu!
Iondoe wewe na kiperepere chako
 
Kiba ni mkubwa kuliko hizo tuzo za AFCON!
Kweli Kabisa AFCON haijawahi toa timu ikacheza walau nusu fainali ya kombe la dunia achilia fainali na kuchukua kombe.CAF limejaa rushwa ya akina Hayattou na kupendelea timu za waarabu.Bora aliyeimba na R Kelly,ana nafuu.
 
Huyu jamaa anatisha kwakweli, ana juhudi sana kumlinganisha na wabongo fleva wengine ni kumkosea heshima .Yeye amekaa kimataifa wengine kitaifa that's all.
 
Huyu dogo sasa alikofikia ni kubaya, yaani amenunua hadi CAF hawa ndio wajuzi wa soka wote wamenunuliwa, kweli huyu ni msanii wa ujanja ujanja.
 
yani diamond anatutoa kimasomaso sana...
mimi king'amuzi changu cha zuku kikikata salio, huwa wanaonyesha station za West, central Africa...
nikiweka GYAN TV au RTN GABON
playlist zao hukosi MAKE ME SING, NANA , Alive je Utanipenda... mpaka raha!!!!
Diamond katufikisha mbali jamani tumuheshimu.
 
Shirikisho la soka barani africa CAF limemchagua diamond platnumz na kumlipa mamilioni kutumbuiza kwenye sherehe za uzinduzi wa michuano ya mataifa africa yatakayofanyika nchini Gabon maarufu kama Afcon2017
Michuano hiyo itafanyika mapema mwakani 2017
Uganda ndo taifa pekee ya africa mashariki lililofanikiwa kufuzu
Akiongea kwenye kipindi cha Times Fm manager wa diamond sallam ameongeza kuwa diamond tayari ana booking mpaka julai 2017. Kama unamtaka inabidi usubiri hadi julai
Naskia wameahirisha,walikosea kumtangaza diamond,sasa hivi Show kapewa Kiba....
 
Kweli ukweli hauchelewi..kuna jamaa mmoja kitu chake kilikuwa kimechafuka anasema. Nahisi Habari hii kitachafuka zaidi.
 
Kwani waliomwita wamempa show baada ya kusikia anachoimba au wamemwita ili wakaanze kuangalia kama ana cha kuimba!??
Ila ni Jambo zuri hata kuitwa
inaleta picha nzuri ya mafanikio

ni mtanzania mwenzetu ndio jambo ninaloona ni jema zaidi kwa upande wangu
 
Back
Top Bottom