Alaf watu wengine wajinga kweli, uzalendo wa taifa? Aliyeshnda tuzo ni diamond na sio taifa! Eti kalitangaza taifa, guys tuna mlima Kilimanjaro, tuna Serengeti, tuna Ngorongoro.. Kwakifupi Tanzania inajitangaza haitaji kutangazwa na mtu!!
Inaelekea hufahamu vizuri haya mambo! Ule Mlima Kilimanjaro hata ukisimama Tanga huwezi kuuona, je unadhani watu wa Ulaya, America, Asia na kadhalika wanauona Mlima Kilimanjaro kutokea huko huko waliko? The same applies to hivyo vivutio vingine ulivyotaja!
Sasa basi, hivyo vivutio ulivyotaja havijitangazi vyenyewe bali vinapaswa kutangazwa... kwa bahati kabisa, kutangaza vivutio vya nchi zinazojulikana duniani ni rahisi kuliko kutangaza vivutio kutoka kwenye nchi zisizofahamika duniani! WHY? Tuchukulie South Africa kwa mfano! Majority duniani wanafahamu kwamba kuna nchi inaitwa South Africa wasichofahamu ni nini kinapatikana South Africa! Hivyo basi, assume Mt. Kilimanjaro ipo South Africa... tangazo la la sekunde 15 CNN kwa maneno "Visit South Africa, the Land of Mount Kilimanjaro, The Highest Mountain in Africa with Ice cap...!" Hilo tangazo peke yake linatosha kumfanya mtu atembelee SA kwa ajili ya Mount Kilimanjaro kwavile tangu zamani alikuwa anafahamu kwamba kuna SA lakini alichokuwa hafahamu ni nini atakuta akija SA!
Kinyume chake, chukua tangazo hilo hilo na kuwa:""Visit
Tanzania, the Land of Mount Kilimanjaro, The Highest Mountain in Africa with Ice cap...!" Swali litakalofuata kwa audience ni "
where the hell is Tanzania?"
Sidhani kama pia ulikuwa ufahamu kwamba moja ya mambo yanayoitangaza nchi ni muziki! Majority duniani wanaifahamu Jamaica kwa ajili ya Reggae music hususani kipindi cha Bob! DRC inafahamika Afrika mzima kwa ajili ya muziki! Kwa kifupi, baadhi ya mambo yanayotangaza nchi ni sanaa na michezo na lazima wawepo watu wa kuifikisha hiyo sanaa na michezo kwenye dunia ya nje!
Kwahiyo, you're 100% very wrong kudhani eti Tanzania inajitangaza yenyewe!!!