Chige mkuu umenishangaza sana!Kumbe hapa ni kuwachamba mashabiki wa Kiba!Inakupaswa uelewe kuwa shabiki wa KIBA sio kumchukuia mwingine yeyote!!Chuki inakuja pale mashabiki wa Dai mnapoanza kuattack shabiki wa Kiba personally kwa maneno ya chuki,hasira na dharau!!Unategemea hawatajibu mapigo?So kumbe hata mkitoka nje ya special thread mnawaona kama maadui!Sidhani kama ushabiki unapaswa kuwa wa chuki na hisia kali kiasi iko!Ivi unajua Kiba na Dai wala hawachukiani personally kama mnavochukulia nyie!Kwa taarifa yako Kiba anasikiliza hadi ngoma za Dai wala sio ajabu!Ni sawa na kufikiri Drake hasikizi ngoma Za Chris brown!Huo mwingine utoto a
Huwezi kunikuta namponda mtu eti kwa sababu anampenda Kiba wakati hayo ni mapenzi yake yeye na yake katu hayawezi kuwa yangu na yangu hayawezi kuwa yake! Hata ukifuatilia post zangu hapa utakuta nawa-dis wale ambao wamefura kisa Diamond yupo na Zari... hapa wanataka kujionesha kwamba wana-feel very sorry for Diamond wakati wengi wao ni ama mashabiki wa Kiba au Wema ambao siku zote wanamponda! Sasa inashangaza, wale wale ambao mara zote wamekuwa wakimponda kwa kumpa majina ya kila aina leo wanabadilika na kujifanya ku-feel very sorry na ndio maana kwangu naona ni unafiki!!
Tukija suala la ku-attack, mie always msimamo wangu upo wazi na siuonei aibu kuusema! Lakini ilitokea si mara moja wala mara mbili; pale unapoelezea kuhusu nani unamkubali, wengine hiyo wanachukulia kana kwamba unamponda mtu wao... na nimeshawahi kutukanwa sana hapa lakini katika kutukanwa huko haikupata kutokea kusema kwamba Kiba si lolote si chochote ila tu kwavile unamsifia hasimu wa Kiba; hadi ikafikia siku nikasema (sorry kwa wana-UKAWA) sasa hawa mashabiki wa Kiba wanakoelekea watakuwa kama mashabiki wa UKAWA walio jukwaa la siasa!! Mfano mzuri tu, jana Baba Levo kapokea mvua ya matusi kweli kweli kwa sababu tu kaongea mambo ambayo mashabiki wa Kiba wanaona ni kama amem-dis Kiba!! To be honest, kama Levo asingekuwa karibu na Kiba nami ningesema ni kweli kam-dis lakini Kiba na Baba Levo wote ni vijana wa Kigoma, na wote ni wanamzuki... watu wala hawafahamu Kiba na Baba Levo huwa wanawasiliana vipi au matani yao yanavuka vipi. Kinyume chake, mtu ambae hata Kiba anamuona kwa mbali leo hii anataka kujifanya anamfahamu na kumpenda sana Kiba kuliko ilivyo kwa Baba Levo!!
Unfortunately, kutokana na huu ujinga ujinga tukajikuta wengi wetu tunakuwa caught off-guard... kwamba, kwavile ukimsifia fulani hata kama huna ugomvi na mwingine basi wale wengine wanakuona adui, basi unaamua ku-side na wale ambao angalau kwa namna moja au nyingine mna-share some common interests. I hate to say this, but let's call a spade a spade. Mashabiki wa Kiba wapo too insecure! Siku Diamond kasema yupo tayari kumsaidia Kiba watu wacha waje juu... lakini Kiba huyo huyo aliwahi kusema yeye ndie alim-release Diamond lakini watu yote hayo tunaona ya kawaida!! Kuna siku Misago kamuuliza Sheta ikiwa anampango wa kufanya kazi na Kiba Shetta akasema hana mpango huo,sio tu ni KIba bali na msanii yeyote wa Tanzania kwa sasa lakini cha ajabu mashabiki wa Kiba wakaja juu... mtu unakaaa unajiuliza sasa hapa watu wanakasirika nini, unashindwa kupata jibu!!!
Kuhusu Diamond and Kiba, hapa nimeshawahi kusema kwamba mashabiki ndio wanakuza "bifu" la Diamond na Kiba na nikasema wazi kwamba, ndugu wakigombana chukua jembe ukalime... Diamond na Kiba wote wanatoka KGM na kwa tabia za Kiafrika ili mradi wanatoka sehemu moja basi tutawachukulia kama ndugu. And to be honest, kama kuna misunderstanding yoyote between the guys, it's about to be resolved na ikaja kuharibika siku ya Fiesta!