Diamond atoa jibu la utata kufuatia interview ya Ommy Dimpoz

Hata ndugu wengine masnitch simshirikishi mtu labda baba na mama, na wife kwa mbaali
 
Mambo ya team achia watoto wa kike wewe, mwanume unatakiwa upende mziki wa mtu au uuchukie mziki wa mtu, sio vigezo vya kumpenda au kumchukia anaeimba. Nyie ndo mnabandika mapicha ya wanaume wenzenu kisa mie team nyoko sijui.
Point kubwa
 
Sasa kukimbia nini hapa nifah? Kwanza ni post ya saa 9:18 PM nami ndo kwanza naiona 2:54 AM; karibu saa 6 baadae na kama usingeni-mention; wala nisingeiona simply because niliona notification yako na ya atoto; nikaona hawa "wangu", ngoja ni-login nijue kulikoni... kwahiyo haina kukimbia bhana!!

Baada ya hiyo intro; nimesoma post husika... mbona naona kama ni wa kujibu ni mashabiki wa Ommy Dimpoz kuliko wa Diamond? Manake hapo Diamond kasema yake... wanaopaswa kujibu au kutetea ni mashabiki wa Dimpoz... lakini kwavile imezoeleka kwamba adui wa "adui" yako ni rafiki basi nilitarajia mashabiki wa Kiba ndio hasa wanaopaswa kujimwayamwaya kwenye huu uzi kuliko mashabiki wa Diamond!! Kwahiyo usishangae kutowaona mashabiki wa Diamond kwa sababu; hawana sababu ya kuja kwenye huu uzi na ndio maana ukiangalia... kama ni dongo la gizani aliyepigwa ni Dimpoz na yeye na watu wake ndo wanatakiwa kulia lia humu na sio mashabiki wa Diamond!!!
 
Sasa MTU kama we bora ukae kmya,sio kwamba alishindwa kutoa pesa ila kwa nn diamond apandishe dau wakat dimpoz alikuwa ashaweka dau lake isitoshe ni washkaj waliokuwa wameshibana

Hahaaaaa tangu Diamond afanye collabo na Davido, kuna wengine hawajafanya?

Na lini Diamond alisema anawalipa, mbona wengine hawalipi na huyo Davido kuna risiti kusema kamlipa?

Hiyo omy hana ubavu wa kuomba collabo sababu hana vigezo, na usisahau AY ndie aliwatambulisha Davido na Diamond sasa kwanini yeye hakupelekwa na AY pia....


Huyo anafikiri watu tunasahau, ni kiki tu.

Wote kawapumbaza na uongo leo, na wengi mmeliwa bwaaaaaaaaa

So mniambie alimwandikia Davido akasema hapa huna pesa ya kutosha? na je aliwasiliana hata na management yake?

Kama ana ubora ana angekuwa na uwezo kama wa Diamond na Davido kufaidika unafikiri asingetaka kufanya collabo nae?

Kwanza huyo omy ana nini cha kujisifia zaidi ya kutaka kurudo kupitia Diamond kama alivyofanya mwenzake?

Na bado wataisoma namba, bila Diamond wao ni bure kabisaaaaaaa

Sasa aende basi si anafikiri collabo lazima pesa, mwambieni aende Davido yupo...mfwyuuuu zao wasio na akili ya kujipaisha na kutegemea wenngine na mwisho wa siku upwupu juuu
 
Namie nashangaa kwani davido na iyanya wameacha kuimba? Si afanye hilo collabo

Yaani ndio hapo sasa, aende sasa tena kesho apige yoweeee awaite kuwa yupo ana jumba ana pesa anazopewa na wake. Tuone

Hakuna kitu hana ubavu na haikuwa hivyo, AY alihusika angemtaja huyo ila anadanganya na kutumia jina la meneja wanaemchukia kwa maendeleo yake na wao hawabebi.
 
Sina team yoyote ila kwa hizi siku 2 diamond umejishushia hadhi sana.... Halafu si kila afanikiwae huwa ni bless za jah..... Na si kila ambae hajafanikiwa hana bless za jah na haistahili kumbeza.... Mtoaji ni mungu alie hai
Issue ni kwamba, miaka nenda rudi hapa watu wamekuwa wakimwombea mabaya... tuache unafiki wa kujifanya waungwana!!Hata ukitafuta threads za kuomba mabaya hapa JF, nyingi ni za HATERS wa Diamond...!!! Kuombea mabaya ni roho za kishetani... sasa ikiwa kila wakati watu (wenye roho ya kishetani) wanahangaika kumuombea mtu mabaya lakini mabaya hayo mtu hayamkuti; there's no way kwamba mtu huyo atakuwa analindwa na nguvu za kishetani manake ni hizo hizo nguvu za kishetani zinazomuombea adondoke huku wakisahau there's ONLY ONE Protector; nae ni Mwenyezi Mungu! Tatizo lenu mnadhani fulani ndo anapaswa kubezwa; siku akisema "enough is enough" watu mnakuja na gia za "mimi sina timu yoyote!" Toeni comments kama mnavyo-feel na sio kujificha kwenye kichaka cha "sina timu yoyote" cuz' it means nothing!
 
Naona unamwaga mapovu... hata huyo Yesu alikuwa na maadui, unashangaa kwa Diamond! Yaani bila aibu unamtaja Jokate na Wema kwenye hili?! Si ndo hao hao mlikuwa mnawashangilia kila walivyokuwa wanamkashifu jamaa... siku kapiga kombora moja tu kwa Jokate; basi hadi kesho haachi kulia lia...!!!
 
Hapo ndipo mnapokosea watu... hivi KABISA KABISA ulitarajia Dimpoz angesema "nilikuwa na-mind sana mshikaji alivyokuwa anapiga hatua?" Did you expect that? Nakubaliana na minji moja kwa moja and from my experience! One of my favorite song dunia hii ni "Machoni Kama Watu!" Do you know why?

Hakuna asiyejua kwamba kwenye suala la views Dimpoz kamlenga Chibu; kwenye kufanya muziki kiujanja ujanja kamlenga Chibu; kwenye suala la muziki mbaya kamlenga Chibu... lakini kwavile Radioni kaongea kinafiki huku akijifanya too innocent; majority mmeingia king! Matokeo yake leo hii Diamond anaonekana mbaya kuelezea mafanikio yake... lakini ana haki hiyo: "mimi sijui kuimba; mnajua nyinyi; mimi nanunua views na views za ukweli mnapata nyinyi; mimi nina sauti mbaya; na wenye sauti mzuri ni nyinyi.... sasa inakuaje tena huyo huyo ambae ni mbaya kila eneo lakini ndie anafanya vizuri?" Huu ndo ukweli ambao hamtaki kuusikia kwavile mmetekwa na "fake innocency" ya Ommy Dimpoz! To be honest inakera... mtu una-fight usiku na mchana hadi wapuuzi wengine wanafikia kusema anamtia mama ake... halafu anatokea mpuuzi anakuambia unafanya muziki wa kiujanja ujanja!" Watu wanafahamu moja ya mafanikio makubwa ya Diamond ni video zilizoenda shule... mle hamna uchawi zaidi ya ku-invest millions of shillings... ukifanya vizuri; anatokea mtu anasema unafanya muziki kiujanja ujanja... kwanini usimtukane ukikumbuka mateso unayopata!!

Unless uwe mnafiki ndo unaweza kuvumilia or else; utafyatuka tu!!! Na hata katika hili; is all about what is best for you: UNAFIKI AU REALITY!

Na msisahau kwamba, hadi mambo yanakuja mitandaoni yanaanza chini chini! Na aliyeyaleta huku mitandaoni ni huyo Dimpoz mnayemtetea baada ya kusema "watu wananunua views" huku watu wakijifanya hawajui kamlenga nani!!! Ni mwendelezo ule ule wa "kununua tuzo....!"
 
To be honest. hata kama dogo ni punga ila kichwani yupo vizuri kuliko mond. na kuwa na mafanikio haina maana una busara au akiri wakati mwingine mtu unakutana na zari unabonyeza right button at the right time basi. unamshukuru mungu anayenyesha mvua kwa wema na wabaya
 
Kwa maneno Diamond aliyoandika ameonyesha jinsi alivyo insecure anaishi kwa kunusa nusa kila kila kinachoongelewa juu yake na lazima ajibu.Kwa stage aliyofikia angetakiwa kuwa mstaarabu na kumeza mambo.....Kuwa na kifua .Lakini yeye anataka kila siku asikike tu.Namuonea huruma kwa sababu watu sasa wanamsubiria atetereke tu kimafanikio waanze kushangilia.Ni kama vile wanasema aliyejuu mngoje chini uhangaike naye.Diamond anatakiwa abadilike afanye kazi zake tu ....nafikiri hata huyu Salaam ni manager ambaye mpenda masifa tuu .
 
Wewe akili huna Inaonyesha Hata vitu unavyonunua huwa hausomi maelekezo vizuri
Hujakosea.. ndio maana nimesema unaweza kuwa mchawi umejuaje sisomi malelezo ya bidhaa zangu ambazo nanunua? Umepatia kabisa huwa sisomi..kwakuwa sijui kusoma..
 
Hahaha hana akili kwa kweli amesahau wacha mungu kama ayubu walivyofanyiwa kwa mapigo kumi,

Halafu wasio mcha mungu kama mafreemason wanavyoteka dunia ya leo..

Jamaa kakosa akili
 
Aaaaah chige acha siasa zako wewe.

Sijaongelea hii post (majibu ya diamond kuhusu alichokisema Ommy ktk interview)
Bali namaanisha sakata hili kwa ujumla.
Tokea hili sakata limeanza (na lilikolezwa juzi baada ya chibu kuitwa xxl kueongelea hili) umekuwa kimya sana.
Nilitamani kuona busara zako ktk hili [emoji12] lakini sijakuona kabisa ukilizungumzia ilhali upo jambo ambalo sio kawaida yako kabisa.
 
Mbona nimeshawahi kuongea kwa posts chache sema kwavile nipo tight; naingia JF nanusa; kisha huyoo!! Na kwa taarifa tu, nimeandika thread sasa hivi, hii hapa kuhusu huyo Dimpoz manake kaka enu anazidi kunitia mashaka...!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…