Diamond azindua Pafyum yake ya Chibu, bei yake ni balaa

Ila watu wa JF mnaongoza kwa kukatisha watu tamaa jamani khaaa!!!

Mshauri mtu kuliko kumponda,
Kama ww huwezi kununua wengine wanaweza na chenji hawadai.
 
bora useme maana ukisema unaonekana hater nani anunue pafyumu ya chibu 105,000? yaani haitakiwi izidi elf 20 hyo parfume . soko lake ni la raia wa kawaida watu wenye hela zao hawatanunua kamwe.kachemsha sana
Utajiskiaje siku upo mbele ya kadamnasi halafu unakuta watu kama 20 mnanukia harufu moja?
 
Umemaliza.
sumbai Iceman 3D hebu mkuje niwanuse au hamjanunua?
 
Sanaa yetu bado ina safari ndefu, almasi (Diamond) yetu imeva attire yq ki naijeria na hereni ( ya almasi siju?).

Angezindua ubani, utuli na marashi yangeuza zaidi.....
 
ha ha ha..namkumbuka mwalimu wangu wa marketing alitufundisha akasema unapoingia dukani ukasoma price tag au ukatajiwa bei ya bidhaa fulani ukajikuta moyoni unalalamika kuwa bei ni ghali ujue hapo si mahali pako,...ondoka katafute kile unachokimudu..naishi kwa hiyo kanuni hadi leo...
 
Usawa huu wa magu mbona kazi anayo

Kama target yake ni soko upande wa kina mama anaweza kupumua kidogo, sidhani kama wanaume wanaweza kupitia trouble zote za kutoa misimbazi 10+ kua na perfume Lina jina chibu
Mimi hiyo hata bure sichukui msiniulize kwa nini.!
 
Kweli maisha magumu kitu cha $48 watu wanalalamika kuna sehemu ukienda hapa DSM hata shati zuri hupati kwa dola 48 cha msingi ni kuangalia ubora wake ukoje na kama ni wa dubai lazima itakuwa katika kiwango cha juu...yeye hajatarget watu wa instagram/facebook wengi wao ni jobless hawana faida yeyote zaidi ya kupiga blah blah tu mungu amsaidie dogo azidi kufika mbali kwenye kazi zake.
 
Kusema kweli chibu na mkubali sana lkn perfume duu, hebu fikiria kidogo kupunguza. Ila sitoshangaa, zikifanya vizuri sokoni kwani kila mtu na mfuko wake, so usiseme watu hawana ela, sema mimi sina ela, Kuna watu watazinunua tu.
Bora alivyofanya hivyo bila hivyo huoo mtaani kila mtu akipita mnanukia harufu moja
 
Mkuu kama mtu mtupiaji na unajijali hiyo laki na elfu tano ni ndogo sana labda uwe na pesa za kuunga unga

Pia kitendo cha kuuza kwa bei ya chini huko mtaani pasingekarika hata mabeki tatu wangenukia harufu moja na mabosi zao.
 
Kwani hakuna size ya vichupa vidogo (vile vya jerojero gulioni)
Na je hawauzi ya kupima au ya paketi ndogo kama viroba.?
Ahghh..! Kumbe mmesema perfume mie nlikuwa sijaelewa vizuri!
 
[emoji13] [emoji13] [emoji13]
 
True mkuu.. Unakuta mtu analalama kuhusu bei huko ni kutaka kulazimisha maisha amabayo si ya saizi yake..Kama huna hela akatafute vya saizi yake. KWa tunaojua pafyumu laki moja mbona ya kawaida sana. Mbona tunalipia pafyumu za watu wa nje hela hizo kwa nini tusisapoti vya kwetu. Anayeshangaa pafyumu ya laki ina maana hiyo si ya saizi yake. Awachie wenye saizi zaoπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Huyu mtoto anajua sembe 1kg ni 2000!!! Atoe sembe ya daimond 1600 kwa 1kg tutamuelewa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…