Diamond kamuomba Gwajima yaishe

Diamond kashapoteza mashabiki akiwemo mimi... na nikikuchukia ujue nimekuchukia jumla.....!
Taratibu mkuu ngoja tuone hii muvi itaishia wapi ndio tutoke na hitimisho!
 
Kanikwazaa!
Angemuacha tu huyo mbwa kichaa kesho abweke tu
Kelele zake za kuongeza idadi ya sadaka tumezizoea
Wewe Dada acha kushabikia Watumishi wa Mungu kuchafuliwa. Hajawahi toa sadaka kwake zinakuuma nini?
 
Siku Dhambi kubwa ambayo nitaifanya na haitahitajii msamahaa ni kuja kuingia kwenye Kanisaa la Gwajimaa.... hiyo kwangu itakuwa dhambi kubwa sanaaa!! Hata dunia nzima Abakie yeye Nitaabudu vitu vingine alivyo umba Mungu ila sio kuingia kanisani kwake
So upo tayari kutenda dhambi kubwa ya kuabudu vitu/miungu ila sio mungu. Ndio maana kina zero brain wanaongoza nchi ludia kusoma ulichoandika
 
Mungu ni mwenye huruma kwa wote wamchao, wanaomwangukia na wanaomtegemea. Ni Mungu huyo huyo mwenye huruma ndiye atakayewatupa jehanamu wote watendao maovu na wakafa katika uovu wao.

Ni Mungu huyo huyo wa huruma ndiye aliyemwondolea uhai Anania na mkewe kwa kumdanganya mtumishi wake Paulo. Ni huyo huyo Mungu wa huruma ndiye aliyewaangamiza Wamisri ndani ya bahari ya Sham.

Kuyasoma maandiko ni rahisi lakini kuyaelewa maandiko inahitaji roho ya Mungu. Huruma ya Mungu hupatikana kwa toba.

Mkristo ni yule afuataye mfano wa Kristo ambaye alijifanya mtu ili aje kuwaonesha watu namna wanavyotakiwa kuishi. Kristo alisistiza kusamehe lakini kusamehewa kunaendana na toba ya kweli. Hatuwezi kuishi kwa udhalimu bila ya kutubu halafu tutegemee kuiona huruma ya Mungu.

Pia mtume Paulo anasema panapostahili kuonya, onya hata kwa ukali. Mtumishi wa Mungu anaweza hata kutumia maneno makali kwa nia ya kuonya.

Kwa wakatoliki, (wanaoamini uwepo wa Watakatifu), Mtakatifu Padre Pio, binadamu anayetajwa kuwa mmoja wa wanadamu wawili (mwingine ni Francis) waliotenda miujiza mingi kuliko mwingine yeyote baada ya mitume, aliwahi kuwafukuza baadhi ya watu walioenda kutubu dhambi wakati walikotoka wameacha mazingira ya dhambi kuendelea. Aliwafukuza, aliwakaripia na kuwagombeza.

Watumishi wa Mungu wanaweza kukaripia, kukemea na kulaani pia. Ndiyo maana Yesu alisema, 'mtakaowafungia dhambi Duniani na mbinguni wamefungiwa ......). Lakini pia alieleza namna ya kuwaonya, na wakikataa, wanafungiwa. Ni tafsiri mbovu kudai kuwa mkristo anatakiwa kumsamehe kila mtu, hata ambaye hakuomba kusamehewa.
 
Mimi naamini Pastor anapata kipato chake kihalali kwan hata serikali imejiridhisha na hilo. Kwa watu kwenda kuambudu kwake hilo siwezi lisemea ni imani na utashi wa mtu na ni uhuru wake. Mondi naye naamini kabisa anajipatia kipato chake kihalali na kwa juhudi zake na serikali naamini imejiridhisha na hilo.
Mondi anauhuru wakutoa mawazo yake kwa njia yeyote ile na ni haki yake kama watanzania wengine, kama alivyo Gwajima pia. Mondi kaamua kutumia muziki ambayo ni kazi yake na Gwajima anaamua kutumia madhabahu ambayo ni kazi yake. Mpaka hapo sijaona tatizo! Tatizo linakuja pale unaposikia Mondi anahofu juu ya lile Gwajima atakaloongea... kwanini uwe na hofu? Kisheria sidhani kama Mondi kavunja kipengele chochote ila ukiwa na wasiwasi juu ya mtu fulani kujibu pale ulipo mtaja ndipo tunapoanza fikiria kuna nini?
 
ASKOFU TUMUACHIE ATAJUA LA KUFANYA.NAKATAA HUU WIMBO SI WA KUMLILIA ROMA .
 
We basi ndo hivyo tena Mimi unaeneza neno la mungu kumbe hata ya shetani yamo.
 
Na ubabe wake wote asijaribu kumpandishia askofu hilo wenge lake ndipo atakapoona makanisa nayo yanaungana kumpinga kama vilivyoungana vyombo vya habar...
Kwa huyu askofu bora mkuu awe mpole tu vingnevyo atajipaka mavi kwa mikono yake mwenyew kumbuka na wwnyew wanaisoma namba kwa namna yao hvyo wakipata sababu ya kulipuka utaandaliwa waraka na baraza la maaskofu utasomwa parokian na usharika zoooote hapo atakua amejiweka pabaya zaid...
Tunajua hapend kukosolewa lkn asilete shobo kwa jumuiya ya wakristo
 
Na huyo Gwajima kwanini ajipatie umaarufu kwa kuongea maisha ya watu. Alimkejeli askofu Pengo na JK akampelekesha puta. Matokeo yake kaona anayo haki ya kuwa hakimu wa maisha ya watu.

Inaboa sana kuona kiongozi wa kiroho anaamua kuiishi fitina ambayo ni mlango mkubwa wa shetani. Haya mambo ya wachungaji kuingia kwenye vita za maneno na raia wasio na platform au wasiopenda majibizano, sio ustaarabu wala utamaduni wa kitanzania.
 
Mkuu huyo askofu anaringia watu , lakini mkuu kabisa ndiye mwenye nchi.

Ni vituko vya mwaka kuamini kwamba Gwajima anao uwezo wa kujibizana na mamlaka ya juu kabisa ya nchi. Mkuu hii ni afrika sio Marekani wala dunia nyingine ya kwanza, viongozi wa nchi hizi wanazo powers kubwa sana kushinda huo umaarufu wa wachungaji.
 
Safi cana wa Kiristo wasikuhizi huendeshwa kwa mihemko ..hawaongozwi kwa neno la uzima..inasikitisha kuona wakiristo wanawanyooshea vidole watumishi wakiloho bila woga..biblia ina mipaka na inasema muonyaneni ninyi kwa ninyi ...hapo paulo alikua akiwaambia viongozi wenzie
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…