Amesema atahakikisha kila shule Mbagala inachimbiwa Kisima, zitapewa madawati kwa zile zenye upungufu wa madawati.
Na mabati kwa zile ambazo hazina bati,na amesema atafanya kwa pesa yake mwenyewe na utekelezaji unafanyika mwaka huu kabla haujaisha maana ndio muda wake wa kutimiza ahadi kila mwisho wa mwaka.
Hongera Diamond, japo kazi uliyojipa ni kubwa sana.
Ila kwa umaarufu wako ungeweza kuwatafuta Wadhamini wako mfano Coca-Cola na Airtel ukawaelekeza lengo lako mkajua jinsi ya kulifanikiasha.
Hata hivyo mafanikio mema kwenye mipango yako.