Diamond kwa nyimbo hizi mbili mpya: Hata ukistaafu Mziki leo sina cha kukudai Kamanda, hebu sikiliza na wewe.

nimepata nafasi ya kusikiliza nyimbo mbili za diamond ni zakawaida sana sikutegemea baada ya kuona nyuzi nyingi hapa za kusifia ni vinyimbo fulani ni kama wasanii wachanga wale wanaokuja kwenye gemu
Yaani unaandika utadhani tulizisikiliza wote....[emoji47] [emoji47]
 
Kwahiyo ulitarajia nyimbo ziwe za kutisha....[emoji12] [emoji12]
 
Kwan lazima kuipenda kazi ya kila mmoja duniani ile ni kazi anajua jinsi ya kujiingizia kipato... ww km unapenda kufuga kuku huwez lazimisha na mwingine afuge ..chuki zitatumaliza watz
 
Za kawaida lkn ukienda YouTube inashika namba moja kwa kutrend (sikomi) na hiyo audio sio video na nyimbo zimetoka bila promo wala kiki apo na hizi nyimbo zote diamond platnumz, kafanya kama freestyle zipo hivyo Je angeongeza userious kidogo si ingekuwa hatari, kwako nyimbo ni za kawaida ila wenzako walio wengi wanazipenda na ndio maana zinatrend YouTube na nyimbo hazina hata siku tatu
 
Eti za kawaida sana....

Hata mwenyewe Diamond anafahamu hizo sio sehemu ya zile alizokusudia kuwa big hits kwake... zile ni matunda ya mtu ukiwa na studio! Unarekodi muda wowote ukijisikia na kuachia bila kuwa kwenye program au ratiba maalumu!!!

Look, Diamond nyimbo zake huwa anatanguliza videos... hivi hushangai zile kaanza na audio! Tena sio wasafi.com kwamba tungesema anataka kuuza lakini kaachia Youtube!!!

Sio hivyo tu, Diamond ni bingwa wa promo!!! Umeshaona anazifanyia promo yoyote zile ngoma?! Hata huko Instagram hajazi-post!!! Ni kawaida ya Diamond hiyo?!

Lakini ilivyo ni kwamba, ngoma is about taste. Msanii anaweza asiwe serious na track husika lakini watu wakaipenda... haidhuru hata kama wewe huzipendi!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…