MTU mweusi,shida sana,yaani tunapoteza rasilimali za Serikali,kushughurika na video chafu za wasanii,!!!
Hili swala ingeachiwa basata iwaite iwapige faini basi,sio swala la kuongelea mjengoni?
Kama maadili,yalikufa tangu enzi za mereremeta,kiwila,ambayo mzee baba alijimirikisha,escrow,Richmond,
Badala ya kuuliza maswala magumu kama,wasiojurikana wa Tundu lisu wapo wapo?,unauliza kuhusu kwichi kwichi za diamond,kama mnaona wivu,nendeni awapige na muhogo wa ja'ngombe,
Dar mafuriko kila kona,mikopo ya elimu ya juu haitoshi,ajira hakuna,Kilimo hakituripi,
USA anauza nyama China,sisi tunashindwa nini kuuza SA,SADC yote?
Yaani tumeshindwa hata kutatua tatizo la mafurikovJangwani,tatizo nimeanza kulisikia tangu 1990s,yaani wahandisi wote wa ujenzi,hakuna ambaye anaweza kuleta project ya kutatua shida hii,hizi story kwamba watu wamejenga kwenye mkondo wa MTO ni za kitoto,karne hii kuna inchi ilisukuma maji ya bahari ili kupata ardhi ya kufanyia kilimo,China wanajenga visiwa baharini,sisi tuna shindwa kuzuia maji yasiende kwenye makazi ya watu,
Mpaka Leo tunajiuliza tufundishe kwa kiswahili au Kiingereza,hoja sio aina ya lugha,Tatizo letu hata tukifundisha kwa swhili,kama hakuna waalimu wazuri,tutafeli tu,maana kama ishu ni lugha mama,mbona hata hicho kiswahili,watoto wanafeli tu.
Tuongeze lugha,mtoto akimaliza darasa la saba,aweze kupiga,vizuri kiingereza,kifaransa,Ki China,
Kwa ufupi hatujawahi kufundisha kiingereza vizuri kwenye shule za msingi za umma,kingefundishwa vzr,tusingepata shida watoto wakienda secondari,
Tuache kuwaza mambo ya faragha ya vijana,tuwaze mambo mazito