Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto na Nandy wahojiwa na Polisi kwa kusambaza video za faragha, wapewa dhamana...

Diamond Platnumz, Hamisa Mobetto na Nandy wahojiwa na Polisi kwa kusambaza video za faragha, wapewa dhamana...

Wakuuu nimesikia kuwa diamond na nandy watapelekwa mahakani Kwa kosa la maadili OK nandy najua ni kufanya ngono kinyume na maumbile tena hadharani Lakini hiii Ya diamond sijainyaka naomba kujulishwa huyu Kijana diamond kafanyaje tena?
 
''''OK nandy najua ni kufanya ngono kinyume na maumbile tena hadharani'''


mmmh hii mpya kwangu
 
Wewe ndio unatutoa kwenye reli. Hapa tunajadili msanii Naseeb kukamatwa na polisi. Hayo mambo ya CAG sijui nini anzisha uzi wake tutajadili huko.
Ndiyo uwezo wa kitanzania huo ndugu yangu,habari moja wakati mmoja.Huwa hatuwezi mambo mawili ila tunataka maendeleo.
 
Mwakyembe amesema kuna baadhi ya wasanii ambao walianza kufanya uhuni ndani ya mitandao akiwemo mwanamuziki nyota wa muziki, Diamond ambae tayari amekamatwa na Jeshi la Polisi na anahojiwa kutokana na picha alizozungusha.

Pia Mwakyembe amesema pia imebidi binti Nandy naye akamatwe kisha kuhojiwa na wanaangalia namna ya kuwapeleka mahakamani.

Mwakyembe ametoa wito kwa vijana kuwa mitandao sio kokoro la kupeleka uchafu wote ambao umezuiwa na sheria zingine na nchi ina utamaduni wake ambapo inahitajika kulindwa kizazi cha sasa na cha kesho cha Taifa hili.

Akiuliza swali, mbunge wa Ulanga, Goodluck Mlinga alitaka kujua kauli ya Serikali juu kukithiri kwa ushoga na kutukana matusi mithili ya bomu la nyuklia ambayo sio maadili ya mtanzania na team za matusi ikiwemo za Wema, Zari, Diamond na Shilole.

Mwakyembe amesema sheria ya EPOCA ilitungwa mwaka 2010 lakini zilikosekana kanuni za kubana maudhui hasa upande wa mitandao. Amesema kanuni zimeshatungwa na zimeanza kufanya kazi.

We umemuona alivyokamatwa au ni matamshi tu kama matamshi mengine kweli diamond akamatwe isipigwe ata picha moja kama evidence.?
 
Naungana na serikali wadakwe tu ule uchafu kabisa isitoshe diamond kioo cha jamii na ana familia kutwa analandana na mama yake kila kona hamuogopi mama yake yale matukio ukiacha watoto alaonao? staha kidogo iwepo hasa mama yake anaisha nae kama msela wake kosa
Amefika hapo na kuitwa 'kioo cha jamii' kwa kufanya hayo unayoyasema. Tuwashangae wanaomshangaa. Bila hayo hakuna Diamond!
 
MTU mweusi,shida sana,yaani tunapoteza rasilimali za Serikali,kushughurika na video chafu za wasanii,!!!
Hili swala ingeachiwa basata iwaite iwapige faini basi,sio swala la kuongelea mjengoni?

Kama maadili,yalikufa tangu enzi za mereremeta,kiwila,ambayo mzee baba alijimirikisha,escrow,Richmond,
Badala ya kuuliza maswala magumu kama,wasiojurikana wa Tundu lisu wapo wapo?,unauliza kuhusu kwichi kwichi za diamond,kama mnaona wivu,nendeni awapige na muhogo wa ja'ngombe,
Dar mafuriko kila kona,mikopo ya elimu ya juu haitoshi,ajira hakuna,Kilimo hakituripi,
USA anauza nyama China,sisi tunashindwa nini kuuza SA,SADC yote?
Yaani tumeshindwa hata kutatua tatizo la mafurikovJangwani,tatizo nimeanza kulisikia tangu 1990s,yaani wahandisi wote wa ujenzi,hakuna ambaye anaweza kuleta project ya kutatua shida hii,hizi story kwamba watu wamejenga kwenye mkondo wa MTO ni za kitoto,karne hii kuna inchi ilisukuma maji ya bahari ili kupata ardhi ya kufanyia kilimo,China wanajenga visiwa baharini,sisi tuna shindwa kuzuia maji yasiende kwenye makazi ya watu,
Mpaka Leo tunajiuliza tufundishe kwa kiswahili au Kiingereza,hoja sio aina ya lugha,Tatizo letu hata tukifundisha kwa swhili,kama hakuna waalimu wazuri,tutafeli tu,maana kama ishu ni lugha mama,mbona hata hicho kiswahili,watoto wanafeli tu.
Tuongeze lugha,mtoto akimaliza darasa la saba,aweze kupiga,vizuri kiingereza,kifaransa,Ki China,
Kwa ufupi hatujawahi kufundisha kiingereza vizuri kwenye shule za msingi za umma,kingefundishwa vzr,tusingepata shida watoto wakienda secondari,
Tuache kuwaza mambo ya faragha ya vijana,tuwaze mambo mazito
Duh! Umeongea kwa hasira kwelikweli
 
wasitufanye watoto, tushachoka na drama zao, watafute vitu vya maana vya kufanya
watengeneza script wao wacheza sinema wao
 
Waambie kiki yao ishabuma hawawezi kumkamata mtoto wa bashite
 
MTU mweusi,shida sana,yaani tunapoteza rasilimali za Serikali,kushughurika na video chafu za wasanii,!!!
Hili swala ingeachiwa basata iwaite iwapige faini basi,sio swala la kuongelea mjengoni?

Kama maadili,yalikufa tangu enzi za mereremeta,kiwila,ambayo mzee baba alijimirikisha,escrow,Richmond,
Badala ya kuuliza maswala magumu kama,wasiojurikana wa Tundu lisu wapo wapo?,unauliza kuhusu kwichi kwichi za diamond,kama mnaona wivu,nendeni awapige na muhogo wa ja'ngombe,
Dar mafuriko kila kona,mikopo ya elimu ya juu haitoshi,ajira hakuna,Kilimo hakituripi,
USA anauza nyama China,sisi tunashindwa nini kuuza SA,SADC yote?
Yaani tumeshindwa hata kutatua tatizo la mafurikovJangwani,tatizo nimeanza kulisikia tangu 1990s,yaani wahandisi wote wa ujenzi,hakuna ambaye anaweza kuleta project ya kutatua shida hii,hizi story kwamba watu wamejenga kwenye mkondo wa MTO ni za kitoto,karne hii kuna inchi ilisukuma maji ya bahari ili kupata ardhi ya kufanyia kilimo,China wanajenga visiwa baharini,sisi tuna shindwa kuzuia maji yasiende kwenye makazi ya watu,
Mpaka Leo tunajiuliza tufundishe kwa kiswahili au Kiingereza,hoja sio aina ya lugha,Tatizo letu hata tukifundisha kwa swhili,kama hakuna waalimu wazuri,tutafeli tu,maana kama ishu ni lugha mama,mbona hata hicho kiswahili,watoto wanafeli tu.
Tuongeze lugha,mtoto akimaliza darasa la saba,aweze kupiga,vizuri kiingereza,kifaransa,Ki China,
Kwa ufupi hatujawahi kufundisha kiingereza vizuri kwenye shule za msingi za umma,kingefundishwa vzr,tusingepata shida watoto wakienda secondari,
Tuache kuwaza mambo ya faragha ya vijana,tuwaze mambo mazito

imagine
hawana kazi za kufanya hawa mawaziri, wanakula kodi zetu bure,sijui tumelogwa na nani, wako wanapoteza muda ku discuss chupi ya Nandy na video za Dai
 
Kabla ya kuwalaumu hao wanao jiita ma celeb nadhani tujilaumu sisi kwanza. Tunapenda kutoa airtime kwenye mambo ya kijinga kuliko mambo ya maana na ndio maana watafuta kiki nao wanapitia kwenye hayo hayo ya kijinga ili wapate airtime. Jiulize Jana Diamond kapost matukio kama mawili nayo weza kuyaita makubwa. La kwanza ni hili la kupost ujinga na la pili ni kuonyesha kuwa wallnafanya mazungumzo na startimes nadhani kuhusiana na mambo ya wasafi TV. Sasa jiulizeni kati ya hayo matukio mawili ni lipi limepewa promo na RAIA kuliko jingine? Lipi ni la maana kuliko jingine? Umaarufu alio upata Nandy(japo kwa njia mbovu) baada ya tukio lake na alio kuwa nao kabla ni vitu viwili tofauti. Kwa hiyo wakati wao wanafanya huo ujinga ma sisi ni either kwa kujua auu kuto kujua tuna kuwa tuna support kwa promo tunayo wapa kwenye mitandao.

Note: siungi mkono matendo yao wanayo yafanya.

Ili kukomesha hizi tabia inabidi kupotezea ujinga wowote wanao ufanya. Mfano MTU akipost video chafu watu wasimsambaze kwa kuwa kwakufanya hivyo wanamuongezea umaarufu(japo wa kijinga) inapelekea wengine kuiga . Huo ni mtazamo wangu
 
Ndo maana suala la kusema Diamond anabeba bendera ya Tanzania, Diamond ni kioo cha jamii, wengine tuliipinga kwa udi na uvumba.

Matatizo ya vi nchi vichanga visivyojielewa. Chriss Brown au 50 cent akienda kutumbuiza UK wamarekani hawasemi amebeba bendera ya Marekani au ni kioo cha jamii ya Marekani. Mnakabidhi bendera halafu siku akitoa picha la pono mnafanyaje, mtasema pono ni reflection ya utamaduni wetu?
 
Labda kosa ni kuvaa kufuli oversize.
[emoji13] [emoji13] [emoji13] [emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji377] [emoji377] [emoji377] [emoji124] [emoji125] [emoji125]
 
Back
Top Bottom