Huyu ndio Diamond ninayemjua mimi.
Hii nyimbo imemrudisha asili ya nyimbo zake.
Japo amekuwa akipiga nyimbo za kibiashara na burudani zaidi.
Lakini hii amerudi katika ile ladha yake ya nyimbo zake za awali
kama 'kamwambie', 'Mbagala', nk.
Hii ni hit ya 'rohoni' itawashika sana wale watu
wa sauti za kumtoa nyoka pangoni.
Hatari ya sauti iliyotumika (Ajemi) ikatokea amekufa
kisha watu wakawa wanasikiliza huu wimbo itakuwa
ni kuvirudisha vilio upya, tena vya kwikwi kubwa!!.
sijajua kama huyu kijana anazijua hizi sauti na asili yake.