Diamond usiwapuuze wanaokuandama sasa, hao sio shilawadu au Konde Gang. Chukua hoja zao

Sasa kwanini usimkamate umpeleke rumande kuliko hii kuzunguka zunguka kama kuku anataka kutaga?
Mimi polisi mpaka nimkamate, mbona wao wenyewe polisi na watu wa usalama wanajuwa na ndiyo maana wanamtumia tu kwenye kampeni zao.
 
Mjomba ebu tuwe wawazi kidogo!
Kulingana na hali ilivyo hapa nchini kwetu Tanzania (kiutawala), ungekuwa wewe ni Diamond, serikali ya CCM ingekufuata uiunge mkono ungekataa?
Ungekemea maovu ya serikali? Ungeweza kuwa mwanamziki na wakati huohuo kuwa mwanaharakati?
Chukulia ungekuwa Diamond!
 
Ndo maana nasema hata ss hivi angekuja na kusema jamani wale mashabiki zangu wa CCm mnipigie kura. Asingelifanya la kitaifa. Sababu sehemu nyingine za uzalendo na Utaifa anajificha
 
Mwache tu hajui kwamba hao hao waliompandisha ndio watakaomshusha.
Hii statement nimeanza kuisikia kabla huyo dogo hajatoa wimbo wake wa 'number one', nadhani hutoka kwa wale wasiojua mashabiki zake kindakindaki ni watu wa aina gani.
Majority ya die hard fans/fanatics hawana Twitter accounts na hata JF hawamo, zaidi ya habari za udaku za Tiffa, Zari, Mobeto, Wema and the likes hakuna kingine wanachofuatilia.
Ukimkosoa Diamond wanakuchukulia ya kuwa wewe either ni Konde gang au Ali Kiba fan au just a hater mwenye wivu wa maendeleo ya mpambanaji aliyetoka kwenye maisha ya chini kabisa mpaka kuwa high flyer.
Hao activists hawana kabisa uwezo wa kumshusha na kukaa kwake kimya kunawakera kwani walitaka aongee kitu ili waweze ku-twist maneno yake, sasa huyo dogo ana washauri ambao kutetereka kwake kutaathiri maisha yao na familia zao ndiyo maana asemayo/afanyayo yako calculated.
 
Kakaa kimya mnataka aseme ... wabongo tunashida kubwa sana mtu mnamshambulia alafu mnamfundisha jinsi ya kulia?
Ndio maana ya ustaa iyo

Beyonce na ustaa wake wote kuna kundi lake linamfundisha namna ya kuishi[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]kupata ustaa ni sekunde tu ila kuumaintain ndio mziki ulipo hapo
 
Killmonger Yah nakumbuka mpaka ikawa gumzo bungeni alitakiwa alipe 400m kwa TRA
 
Kabisa mkuu kwamfn kuna mwanayanga aliwah kuvaa jezi imeandikwa simba babalao na kuna wengine wakasema Waz kuwa ni diamond pekee ndo anaweza kuwafanya wanayanga waimbe simba babalao
 
Wivu tu na umaskini unawasumbua
 
Kijana hana washauri wazuri !! mambo ya Usanii na Siasa ni kuwa makini nayo saana, watanzania wanamuhukumu kupitia mitandao.

Ningekuwa mimi, nabadilisha benchi lote la ufundi, naomba radhi naanza ukurasa mpya !!
Vunja bei nae sijui hana washauri naona amejiiingiza kwa fujo siasani.

Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…