Diaspora Hawatoi connection?

Jamaa yangu kashindwa kunitumia hela dola 80 elfu nimalizie ujenzi.Anadai serikali ya jimbo idara ya uhamiaji kitengo cha kuzuia utakatishaji fedha imemzuia,sababu waliyompa ni hela nyingi mno kutuma mpaka awe na maelezo ya kujitosheleza mkuu.
 
Mwanangu kafeli mwezi sasa kunitumia fungu anadai kuna idara wanamkwamisha bila sababu za msingi.
 
Nilimwambia atoe ushahidi wa mimi kuwasiliana nae kabla ya leo kaishia kuranda randa tu na kubwabwaja nonsense.

Hivi kuna visa special ya mashoga? Mambo mengine ni uzwazwa hata kuyawaza tu, they don't add up.
Mwana alilalamika kichizi kua ulimpa maneno""Kuntu"""kisa kaomba umwelezeee baadhi ya detail's tu😂😂😂😂.
 
Sisi tumesaidiwa, tunasaidia na watu wanaendelea kusaidiwa. Nani aliyefika hakupewa msaada unless alikua na mambo ya hovyo. Kuna mambo watu mnajiongelea tu au mnataka tukisaidiana tuwe tunapost?
Mkuu kuna watu ni walalamishi ajabu! wakiona unafanya mipango ya kutoka ndio hao hao wanaanza kukukatisha tamaa.
Ukitoka wanageuka kuanza kukuomba connection. Mfano mzuri ni mimi, ni juzi tu niliandika nyuzi humu kuhusiana na safari yangu ya Marekani.
Lakini ukilinganisha negative comments na positive, negative ni nyingi zaidi. Kama hiyo haitoshi mbali na yote nimepambana kivyangu (kipesa) hadi kufika.
Sikuwahi kumuomba mwanajukwaa yeyote humu hata senti 5, ikiwa naongopa ajitokeze yeyote niliemuomba na sikuwa na kitu kabisa.
Kikubwa sana ambacho nashukuru ni kuwa watu walinisaidia sana hasa ushauri wewe ukiwa mmoja wao.
Lakini baada ya kuwa nimefika huku umegeuka msaada mkubwa kupita maelezo kwangu, umekuwa zaidi ya ndugu, ninapokwama unanisaidia sana hadi nimewahi kuweka thread humu.
Ajabu mbali na yote niliyoandika kuna watu wananifata DM wananiuliza ulifikaje huko,ukiwaambia wasome nilichoandika tangu naanza harakati hadi nafika hawarudi tena.
Ushauri, ndugu zangu kama wewe ni kijana una ndogo za kufika nje, fanya commitment mwenyewe, utasaidiwa ikiwa unaonyesha juhudi na nia ya unachokipigania mbali na hapo ni ngumu sana.
Jikusanye taratibu tu ila kwa akili sana na mipango madhubuti, fanya mambo yako mwenyewe bila msaada wa agents bila hivyo utatapeliwa na kuishia kukata tamaa.
Ukifika nje amin utasaidiwa tu, mimi ni shahidi wa haya, Bufa amenisaidia sana, Mungu ambariki sana.
 
[emoji16][emoji16]
 
Hii inafikirisha sana aisee, wengine tumeingia hatumjui yeyote zaidi ya Mungu tu.
 
Jamaa yangu kashindwa kunitumia hela dola 80 elfu nimalizie ujenzi.Anadai serikali ya jimbo idara ya uhamiaji kitengo cha kuzuia utakatishaji fedha imemzuia,sababu waliyompa ni hela nyingi mno kutuma mpaka awe na maelezo ya kujitosheleza mkuu.

Jamaa yako anakufunga kamba. Tushatuma zaidi ya hizo zimefika bila shida yeyote.

Kiwango kama hicho afanye wire transfer aende bank yake wanatuma right way to your bank account maana taayri wanajua zimeingiaje otherwise wasingezipokea.

Kama haiwezekani kutuma hela bongo hizo remittances za over 500M USD a yr diaspora tunazotuma kila mwaka tunatumaje? Jamaa yako muongo no more, no less.
 

Kaka, I'm humbled. Nashukuru 🙏🙏🙏
 
Hivi ukiacha jamaa kuwa muongozo USD 80,000/= mtu anatumaje kizembe tu uende Matako bar Kujenga heshima? Kwani Wabongo hatujuwani.

Mimi mshijaji wangu baada ya kupata green card after 10 years ndio akaja Bongo kukaa miezi mitatu asimamie mwenyewe nyumba yake.

Imagine alituma pesa ijengwe servant kota kwanza ili afikie lakini bado hata hiyo servant kota akakuta ni madudu mtupu inabidi afumuwe fumuwe.

Kwahiyo Mimi nawatetea sometimes ukiona mtu kutuma pesa nyingine anakuwa mzito siyo mjinga.

Mimi nitamlaumu mshkaji wangu diaspora kama kweli Nina shida genuine na akashindwa kunisaidia amount kama USD 100 hapo ndio naweza kumlaumu mwamba ana roho mbaya.

Lakini Ki ukweli Wabongo hatuko honestly kabisa.

Tena Sasa hivi Chris Lukosi akituliza akili Wabongo wa Marekani watamtumia sana kuwanunulia hizo Range Rover UK na anazitowa mwenyewe bandarini Dar, gari INA kwenda kufungiwa nyumbani ukirudi Bongo unanunuwa betri mpya tu unachomeka unawasha unapiga misele yako tu fresh, ukiondoka unalifungia garage unachomowa betri.
 

I agree mkuu. Labda jamaa kampiga chenga tu kashindwa kumwambia ukweli. Kwenye swala la honesty bongo ni sifuri.
 
I agree mkuu. Labda jamaa kampiga chenga tu kashindwa kumwambia ukweli. Kwenye swala la honesty bongo ni sifuri.
Mimi naelewa sana, sometimes nakuwa na mwanangu Bongo akiishiwa cash anatumia line yangu ya airtel kuivuta pesa kutoka Marekani namtolea maisha yanaendelea, kuna system inakubali laini ya airtel tu.

Kwahiyo Mimi mtu anidanganyi, ukiona mtu anasita kufanya transfer ya pesa anahofia usalama na honesty tu ya mtu anayekutumia, wengi wameumizwa na ndugu zao kabisa.
 

I couldn't agree more mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…